#COVID19 Siku 60 zijazo Tanzania inaweza kuwa zaidi ya India kwenye suala la COVID-19

2019

JF-Expert Member
Dec 31, 2018
2,980
4,451
Tanzania nchi ya mzaha mzaha kwenye kila kitu. Watanzania wengi ni watu wasiojali, yani hawajali chochote kiwe hatari au faida.

Watanzania hao hao kwenye kualalamika wanaongoza baada ya kupata madhara tayari ila ni wazito sana kufanya maamuzi.

Pamoja na wizara ya afya kutangaza idadi ya waathirika wa covid bado kama vile hakuna kilichotokea, lakini je kutangaza idadi ya wagonjwa ndio itawachochea watu kuchukua tahadhari? Jibu ni HAPANA.

Kwani mwanzoni ikiwezekana vipi? Hapa nampa sifa sana Makonda akiwa RC wa Dar. Tunakumbuka hatua alizotangaza zilisaidia sana.

Kwa sasa raia ana mkutano na taasisi fulani kajaza watu zaidi ya 100 hakuna umbali wa kukaa barakoa sio lazma afu unawaambia "jihadharimi na corona, ipo na tuna wagongwa" nani anakusikiliza? Makanisa yanajaa kama kawaida, misikiti kama dawa, vikao mikutano kwenye usafiri hakuna tahadhari inayochukuliwa mnategea nini baada ya siku 60?

Wekeni alama huu uzi mtakuja kunikimbuka
 
Tuache kutishana By grace of God, Our country is corona free. Tuache kutishana achana na wanasiasa wanaotaka kupleese watoa misaada kwa kutuhusisha na mambo yasotuhusu. Sisi wengine tutaendelea kuchangamana zero distance na imani yetu itatuponya Kama tulivyoponywa toka corona ya kwanza
 
Tuache kutishana By grace of God, Our country is corona free. Tuache kutishana achana na wanasiasa wanaotaka kupleese watoa misaada kwa kutuhusisha na mambo yasotuhusu. Sisi wengine tutaendelea kuchangamana zero distance na imani yetu itatuponya Kama tulivyoponywa toka corona ya kwanza
Kwa hiyo @santoshi Mungu ni mbaguzi sio, Tanzania ndio inapendwa zaidi
 
Mola atupishilie mbali maana kama ni maonyo na miito ya tahadhari, lipi halikusemwa?

 
Serikali yako yenyewe ina utani na ugonjwa huu, sasa wananchi wafanye nini? Mfano, bila ku-impose marufuku ya kujaza abiria kwenye daladala, dereva gn au mfanyabiashara gn atajali kuweka level seat kwenye gari yake.

Kingine, nachoona ni move tu ya serikali yako kujaribu kuwapooza mabeberu ili waone tuko pamoja. Kama tumevuka first, second, sijui mpaka third wave ya mlipuko wa Covid19, hii fourth wave (delta variant) wana maajabu gani?

Tusisasahau kutumia juice ya limao/ndimu. Na tuondoe hofu pia.
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom