Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
wapendwa,
niko chumani kwangu saa hizi na nahisi pumzi zinataka kukauka. nina mchanganyiko wa wasiwasi na matumaini, japo najiamini kwa hili ninalotarajia kulifanya, lakini tashwishi na mchecheto vinanizinga, nimeona niwashirikishe huenda nikapata tafu japo kidogo!!
ni kwamba baada ya siku 30 zijazo yaani jumatano ya tarehe 1 june 2011, nitamuarifu rasmi kijana mmoja kuwa nimemteua kuwa mchumba wangu!!!
ni uamuzi mgumu na mzito sana kwangu mimi binafsi. kijana huyu nimemfahamu tangu mwaka 2006 alipoanza kunitaka mapenzi, tumezunguka naye sana katika mitaa ya mapenzi huku nikihakikisha kuwa anaupata moyo wangu kikamilifu japo mwili wangu sikumruhusu kuufunua. kwa kweli tumehangaika naye sana na tumewahi "kukosana" naye mara kadhaa kisha tunarudiana. natumaini mnanielewa vyema ninaongea nini hasa ninaposema "kukosana"
baada ya misukosuko yote, hatimaye alinielewa vyema nami nikamuelewa, sasa kila kilichokuwa kinazuia sisi kuwa mwili mmoja kimeondoshwa kwa neema za Mungu. nimeamua kuwa June mosi nitamthibitishia kuwa ndiye mume wa ndoto zangu. naam, mume wa ujana wangu! kama hatakuwa na objection, siku ya jumamosi ya tarehe 4 June, nitamtambulisha nyumbani kwetu na kumtaka naye apange siku ya kunipeleka na kunitambulisha kwao. kama mambo yataenda kama ninavyoomba, ndoa itafungwa mwezi october au novemba 2011!!
sasa nadhani mnaweza kuuhisi wakati niliomo ni wa aina gani.
naomba maombi yenu wote tuweze kuvuka salama. mimi naanza maombi mazito mfululizo kumkabidhi Mungu siku hizi zote 30 (and beyond) aziratibu mwenyewe kwa kadiri ya wingi wa rehema na fadhili zake
Mungu awabariki sana
mpenzi wenu Miss Judith (Mrs mtarajiwa)
Glory to God!
Judith Mungu nimwema na fadhili zake ni za milele ingawa nimechelewa kuiona hii bado nina kanafasi cha uwakilishi hata kama sio Nec
Ndugu mpendwa Mungu awatie nguvu chochote mlichopanga kikafanikiwe ila safri ni ndefu sana sana na unaitaji divine intervation kwenye ndoa yako mungu akasimame nayo..kuna madada wametembea na huyo mtarajiwa na awajaolewa samhan yawezekana na wewe ulikuwa na umpendae ukamwacha zile zote ni roho na zinasema na pale zinapoongea ama kunungunika ma dear zina function.....sijui dini gan ila simama na Mungu sana sana ,Ndoa ni mpaka mwisho ...mnapokubaliana kuna kaka mmoja alihisi amelowa kanisan pale mkewe mtaraji alipokataa atoweza kuwa nae maisha yote na ndoa aikufungwa mpendwa..sio yeye ingawa baadae alijuta na kusema akujua alichosema lakini kwa Mungu imekula kwake daima...so hata wanaume nimefurah kama ajakuchezea bado maana kuna wengi wanaingia na gea za ndoa kumbe wanakufanya mpira wa kona kujaribishia siza za uume wao kwenye mwili wako na kukimbia mwisho unakuwa juza wa mapenzi........simama na Mungu sana sana zipo roho zinalia ulipotamka hili hadharani unaolewa na kwa kukusaidia jifunze kuwa msiri kwenye mafanikio yako sikukatazi kwa nini umetujuza la hasha akuna asiependa mafanikio yako vile vile sio wote wanaopenda uitwe MRS..
Kwenye baibo kuna mifano mingi tu ya watu waliotangaza baraka zako wakageuka watumwa Yussuf alioteshwa atakuwa waziri mkuu akaenda kwa ndugu na wazazi wake kumwambi mnajua mtakuwa chini yangu akuna aliekubali wala kumuelewa mwisho wa siku aliishia kuuzwa kabla ya kusudi la Mungu kutimia pengine asingesema ovyo wasingemtenda nduguze....jaribu kusoma neno la MUNGU sana kila wakati utaona mabo mengi katika ndoa ;ndoa si kipindi cha kibonde clouds unacheka siku imepita unasubiri kingine la hasha kuna mengi kwenye ndoa ntajaribu kukuttmia maandiko ya baibo kukusaidia hili
Yapo Mambo ya Kulaani na kukataa kabla ya ndoa yako
1)KUACHIKA AMA KUACHANA
Wengi wanaingia kwenye ndoa wakiwa na furaha ya ajabu lakini baada ya muda si mrefu wanaanza akufaraganyika na mwisho kuishi maisha ya ajabu amapo mmoja waoa anaona mwisho tangu mwanzo kwa kuamua kuacha kila kitu na kuanza maisha upya..nasema hivi sikutishi lakini si mpango wa Mungu kuachana ila kutokana na ufahamu wetu tunaishia kuachana...efe 4:6 Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa...mwombe mungu akupe marifa ujue jinsi ya kuishi na mumeo utakaekuwa nae...Pili sasa hivi usikimbilie just ndan ya siku 30..nampa mtu moyo wangu hapanakuweka wazi
OMBA KUSUDI LA MUNGU KWENYE NDOA YAKO LITIMIE;;
USIONE UMEKAA NAE TANGU 2006 KUNA NDOA IMEVUNJWA WIKI 2 ZILIZOPITA WAMEKAA TANGU 1999 NIKIWA CHUO WAKAOANA MWAKA 2006....SO MUDA SIO TATIZO KABISA .MWAMBIE MUNGU AKUONYESHE KAMA ANAFAA KUWA NA WEEWE...INATAKIWA UMPATE MUME ATAKAEKUWA NA KUSUDI LA MUNGU JUU YAKE;;UNAWEZA KUOMBA JUST MUME UKAPATA YOYOTE GAFLA AKAKWAMBIA NIMEKWAMBIA SITAKI KUSIKIA KWENDA KANISAN HATA SIKU MOJA;;UNARUDI KWA WAZAZI OOH HUYU KUMBE ALIKUWA SHETAN SHETAN WEWE ULIEMWINGIZA MYONI MWAKO NA KUMPA SIKU 30 ZA KUJIANDAA KUCHEZEA MOYO WAKO ...KWENYE BABIBO UTAONA KUSUDI LA NDOA NI FURAHA NA AMANI NA MUMTUKIE MUNGU;;MIMI NILITENDWA SANA KABLA YAA KUOA NA NIKAKUTANA NA MTU NIKAONA HUYU ANAFAA KUKLIKO WOTE DUNIAN BAADA YA MAMA WA YESU..NIKAMWOMBA MLOKOLE MMOJA ANIOMBEE ANYWAY KIPINDI HIKO SIKUWA NIMEOKOKA..NIKAMWOMBA BABA MWAKASEGE ANIOMBE AKANIPA MISTARII AKANI ALERT KWENYE MAOMBI KUNA MAWILI MI NAOMBA KUSUDI LA MUNGU NA SIOMBI JUST UOE OK??NIKAMWAMBIA SAWA MWISHO ALIONGEA NIKAUMIA AKASEMA KWENYE MAOMBI HAYA YAWEZEKANA UNA MWANAMKE UNAMWONA HUYO NDIE WAKO KAMA SI MAPENZI YA MUNGU ANAKWENDA KUPANGUA UHUSIANO NA HUTOKAA UMWONE MILELE..DUH..NIKAKAA WIKI NIKIJIULIZA NIMWAMBIE NINA HUU NIMEMPENDA AMA LAH...AKIWA MAOMBINI NDUGU USIMGUSE MUNGU MWEZI WA KWANZA WA PILI YULE BINTI AKAPATA VISA YA MAREKAN BILA HATA KUNJULISHA ANAONDOKA BAAYA YA WIKI AKANIFWATA HNY NAELEKEA USA SIJUI KAMA NTARUDI ILA NTAJARIBU TUANGALIE UJE SIWEZI BILA WEWE LAKINI MUNGU AKASEMA UTAWEZA UKIWA NA MIMI...NDUGU IKUMWONA TENA NIKAJA KUSOMA OPEN UNIV..NIKIWA NATOKA KWENYE MTIHAN NIKAWA NIMEPAKI NA BINTI PEMBEN GARI YAKE IMEARIBIKA AIWAKI NI MTUNDU WA MAGARI KIDOGO...NIKACHUKUA WAYA NIKAMWOMBA MTU ASHIKE UPANDE WA PILI NIKAWASHA GARI..UWEZI AMINI USIKU ULE AKAWA ANAFIKIRIA JINSI YA KWENDA KWAO KIPUNGUNI..NIKAMWAMBIA UTAENDESHA HII YANGU M NTAENDESHA YAKE MPAKA TUKAFIKA ..NIKIWA NJIAN ROHO WA MUNGU AKASEMA NIOMBE UPATANISHO NAE NA HUYO NDIE MKE WANGU MTARAJIWA NIKAWA NAJIONA KAMA CHIZI...NIAKAANZA KUSALI KWENYE ILE GARI MPAAKA NAFIKA NIKALILIA KUSUDI LA MUNGU...NIKAOMBA APPOINTMENT BAADA YA PAPER....NIKAJA KUKUTA NI BINTI AMEOKOKA ANAJIHESHIMU NA YEYE AKANIPA STORY ZAKE TUKAMLILIA MUNGU NA SASA NI MAMA WA MTOTO WANGU ,..SO KUNA MAMBO MENGI TU UNAKUMBANA NAYO UKITANGAZA NDOA MUNGU AKUREJESHHEE MUME WA UJANA WAKO
BE BLESSED!!!