GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Siku 21 za Ngeleja: Taifa linaelekea Gizani Rasmi
Nashtushwa sana na mbinu za serikali kuendelea kulifanya suala la upatikanaji wa Nishati ya Uhakika ya Umeme kuwa la kisiasa zaidi kuliko kupata ufumbuzi wa kdumu na kuwaeleza watanzania nafasi yake na uwezo tulionao katika kushughulikia tatizo hili.
Tunaendelea kukwama kwa kasi ya ajabu kwa kuendelea kutegemea kudra ya Mungu kuendesha Nchi, huku kasi ya maovu nayo ikishamiri. Kwa mtaji huu wa maovu mengi kuliko mema kudra za Muunba zinatoka wapi kwa kizazi kilichomuasi? Huu ni mchezo wa kuigiza na ndotoza alinacha kuukwaa utajiri kwa mauzo ya kapu la vioo.
Serikali inasisitiza kuwa haitasimamisha uzalishaji wa Umeme katika bwawa la Mtera kama ilivyofanya mwaka 2006, haya yanazungumzwa huku kiwango cha chini cha uzalishaji umeme katika bwawa hilo kinapigania roho kwa poniti zaidi ya 90 zilizosalia katika uwezo wake wa juu wa 698.50 mpaka kiwango cha chini cha 690 na ujazo wa hivi karibuni ni mita za ujazo 690.74.
Vyanzo vyetu vingine ambavyo vinazalisha umeme vyote vipo taaban na vinafanya kazi chini ya kiwango na katika hatua zake za lala salama kabla ya kusitisha shughuli zake kutokana na kutokuwa na maji ya kutosha na hii ni kwa kiwango cha karibu zaidi ya asilimia 100 chini ya kiwango cha kawaida
Kihansi kwa sasa ni MW 90 badala ya MW 180, Kidatu MW 40 badala ya 204, New Pangani MW 20 badala ya MW168 na Nyumba ya Mungu ni MW3.5 badala ya MW 8.
Mamlaka ya Hali ya hewa haijatabiri kuwepo na Mvua katika chanzo chochote kati ya vyanzo vinavyokusanya maji kuelekea mabwawa haya si Ruaha Mkubwa wala Ruaha Mdogo na Kisigo wakati ambavyo hukusanya maji mengi kwa ajili ya bwawa la Mtera wakti wa kipindi cha masika.
Sipati picha kwa kasi hii ya ongezeko la ukame ambao unashamiri tuna miujiza gani ya kupata nishati ya uhakika na ambayo haitakuwa inaelekea kukoma kabisa ndani ya siku 21 za Waziri Ngeleja alizopewa kusahihisha mapungufu yake katika Bajeti ya Nishati na Madini.
Nashawishika kabisa kuamini kuwa baada ya kipindi si kirefu tunaelekea gizani jumla kama taifa hakuna cha mgawo wala jenereta kutoka vituo vya TANESCO kanda ambayo mengi kati ya hayo yamesimama muda mrefu kutokana na hitilafu za kiufundi na kukosekana kwa vipuri vya kuyakarabati.
Tunaomba Neema za Muumba Mvua zinyeshe katika vyanzo hivi Taifa lisifike huko, maana kama tutafika huko. Mimi na wewe hatujui nini hasa itakuwa hatima ya Taifa letu.
ADIOS
Nashtushwa sana na mbinu za serikali kuendelea kulifanya suala la upatikanaji wa Nishati ya Uhakika ya Umeme kuwa la kisiasa zaidi kuliko kupata ufumbuzi wa kdumu na kuwaeleza watanzania nafasi yake na uwezo tulionao katika kushughulikia tatizo hili.
Tunaendelea kukwama kwa kasi ya ajabu kwa kuendelea kutegemea kudra ya Mungu kuendesha Nchi, huku kasi ya maovu nayo ikishamiri. Kwa mtaji huu wa maovu mengi kuliko mema kudra za Muunba zinatoka wapi kwa kizazi kilichomuasi? Huu ni mchezo wa kuigiza na ndotoza alinacha kuukwaa utajiri kwa mauzo ya kapu la vioo.
Serikali inasisitiza kuwa haitasimamisha uzalishaji wa Umeme katika bwawa la Mtera kama ilivyofanya mwaka 2006, haya yanazungumzwa huku kiwango cha chini cha uzalishaji umeme katika bwawa hilo kinapigania roho kwa poniti zaidi ya 90 zilizosalia katika uwezo wake wa juu wa 698.50 mpaka kiwango cha chini cha 690 na ujazo wa hivi karibuni ni mita za ujazo 690.74.
Vyanzo vyetu vingine ambavyo vinazalisha umeme vyote vipo taaban na vinafanya kazi chini ya kiwango na katika hatua zake za lala salama kabla ya kusitisha shughuli zake kutokana na kutokuwa na maji ya kutosha na hii ni kwa kiwango cha karibu zaidi ya asilimia 100 chini ya kiwango cha kawaida
Kihansi kwa sasa ni MW 90 badala ya MW 180, Kidatu MW 40 badala ya 204, New Pangani MW 20 badala ya MW168 na Nyumba ya Mungu ni MW3.5 badala ya MW 8.
Mamlaka ya Hali ya hewa haijatabiri kuwepo na Mvua katika chanzo chochote kati ya vyanzo vinavyokusanya maji kuelekea mabwawa haya si Ruaha Mkubwa wala Ruaha Mdogo na Kisigo wakati ambavyo hukusanya maji mengi kwa ajili ya bwawa la Mtera wakti wa kipindi cha masika.
Sipati picha kwa kasi hii ya ongezeko la ukame ambao unashamiri tuna miujiza gani ya kupata nishati ya uhakika na ambayo haitakuwa inaelekea kukoma kabisa ndani ya siku 21 za Waziri Ngeleja alizopewa kusahihisha mapungufu yake katika Bajeti ya Nishati na Madini.
Nashawishika kabisa kuamini kuwa baada ya kipindi si kirefu tunaelekea gizani jumla kama taifa hakuna cha mgawo wala jenereta kutoka vituo vya TANESCO kanda ambayo mengi kati ya hayo yamesimama muda mrefu kutokana na hitilafu za kiufundi na kukosekana kwa vipuri vya kuyakarabati.
Tunaomba Neema za Muumba Mvua zinyeshe katika vyanzo hivi Taifa lisifike huko, maana kama tutafika huko. Mimi na wewe hatujui nini hasa itakuwa hatima ya Taifa letu.
ADIOS