Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Uongozi wa nchi si suala wala jukumu dogo. Ni jukumu la kila mwezi, kila wiki, kila siku, kila saa, kila dakika na kila sekunde kwa kipindi cha miaka mitano!! Utendaji wa kiongozi unapimwa hivyo hivyo. Kuna mafanikio ya muda mrefu na muda mfupi.
Mafanikio ya JK kama Raisi yalitajwa sana wakati wa kampeni zake za uraisi. Aliyoshindwa yalitajwa sana na wagombea wengine wa upinzani. Wakati wa kampeni JK alitaja zaidi mafanikio yake wapinzani wakataja zaidi aliyoshindwa. Kampeni zimeisha, uchaguzi umemalizika. WanaJF hawaombwi kura, ni watu wenye uelewa na wanaishi katika jamii ya watanzania. WanaJF wana nafasi ya 'kumhukumu' kwa haki JK.
Kwa kutambua uelewa, umakini na nafasi ya JF katika jamii namleta kwenu JK mumtolee hukumu ya haki. Kwa siku 1900+ tangu achaguliwe kuwa Raisi amefanikiwa nini? Ameshindwa nini?
Hukumu ya wanaJF katika mfumo wa tathmini ya mafanikio au kushindwa kwake katika Elimu, Afya, MIUNDOMBINU, KILIMO, USALAMA WA RAIA, AJIRA, MICHEZO, RUSHWA N.K itasaidia kutoa mwanga tunatoka wapi na tunaelekea wapi kama nchi. Pia itasaidia kujua tunatakiwa tufanye nini kama wanaJF. Tushauri, tukosoe na tutoe suluhisho.
CCM wasijitetee, CDM na vyama vingine wasikosoe pekee. Lengo liwe kutoa suluhisho la kudumu kwa matatizo ya nchi yetu au kutoa msukumo zaidi kwa yale yaliyofanikiwa.
Hatuwezi kusubiri mpaka 2015 kujikwamua tulipokwama au kujipongeza kwa tulipofikia. Kila sekunde, kila saa, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka ni lazima tuendelee au turudi nyuma! Umasikini au utajiri wetu unapotea au unaongezeka kwa kila sekunde sio kwa miaka 5. Miaka 5 ni majumuisho!!
Mafanikio ya JK kama Raisi yalitajwa sana wakati wa kampeni zake za uraisi. Aliyoshindwa yalitajwa sana na wagombea wengine wa upinzani. Wakati wa kampeni JK alitaja zaidi mafanikio yake wapinzani wakataja zaidi aliyoshindwa. Kampeni zimeisha, uchaguzi umemalizika. WanaJF hawaombwi kura, ni watu wenye uelewa na wanaishi katika jamii ya watanzania. WanaJF wana nafasi ya 'kumhukumu' kwa haki JK.
Kwa kutambua uelewa, umakini na nafasi ya JF katika jamii namleta kwenu JK mumtolee hukumu ya haki. Kwa siku 1900+ tangu achaguliwe kuwa Raisi amefanikiwa nini? Ameshindwa nini?
Hukumu ya wanaJF katika mfumo wa tathmini ya mafanikio au kushindwa kwake katika Elimu, Afya, MIUNDOMBINU, KILIMO, USALAMA WA RAIA, AJIRA, MICHEZO, RUSHWA N.K itasaidia kutoa mwanga tunatoka wapi na tunaelekea wapi kama nchi. Pia itasaidia kujua tunatakiwa tufanye nini kama wanaJF. Tushauri, tukosoe na tutoe suluhisho.
CCM wasijitetee, CDM na vyama vingine wasikosoe pekee. Lengo liwe kutoa suluhisho la kudumu kwa matatizo ya nchi yetu au kutoa msukumo zaidi kwa yale yaliyofanikiwa.
Hatuwezi kusubiri mpaka 2015 kujikwamua tulipokwama au kujipongeza kwa tulipofikia. Kila sekunde, kila saa, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka ni lazima tuendelee au turudi nyuma! Umasikini au utajiri wetu unapotea au unaongezeka kwa kila sekunde sio kwa miaka 5. Miaka 5 ni majumuisho!!