Siku 100 za Rais Samia naiona dhamira njema aliyonayo kwa nchi yetu

DENLSON

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
944
1,253
Ndani ya siku 100 Mh Rais ameonesha dhamira njema.
1. Uhuru wa kutoa maoni- Kwa kadili yake mwenyewe alituambia yuko tayari kukosolewa na kweli watu wanakosoa na anasikkliza mfano siku ambayo aliteua wakuu wa taasisi na watu wakasema mtu flani hafai asubuhi akatengua uteuzi. Hii inajumuisha na kuingia twitter bila VPN.

2. Demokrasia - Ameonesha dhamira njema ya kusikiliza maoni mbadala, kabla ya hapo Mbowe asingepata hata nafasi ya kuzindua ujenzi wa ofisi za chama

3. Sekta binafsi - Ameweka wazi anataka kufanya kazi na sekta binafsi na ameshakuta na wafanyabiashara na wawekezaji kuhusu hili.

4. Uhuru wa Mihimili ya Serikali - Hatujasikia kuna mhimili uliojichimbia chini sana. Mahakama inatoa hukumu angalau bila kulalia upande wowote.

5. Kodi - ameweka wazi hataki mapato ya dhulma.

6. Ajira na Mishahara - amesema ataongeza mishahara mwakani huku akijitahidi kuongeza ajira kwa kadri ya uwezo wa Selikari kwa sasa.

7. Uhusiano wa kimataifa - amefanya mabadiliko makubwa kwenye wizara pamoja na kurudisha uhusiano na mataifa jirani.

9. COVID-19 ameweka wazi msimamo wake ingawa haupendwi na wafuasi wa chama chake ila ndio ukweli wenyewe. Sisi sio kisiwa.

10. Uendelezaji wa miradi - anajitahidi kwa kadri awezavyo miradi ambayo tayari hela imetumika ikamilike ili fedha za Watanzania zisipotee.

Kwa kweli naiona DHAMIRA NJEMA ya Mh Rais na mimi kama mlinzi wa zamu sitanyamaza kumkumbusha Mungu kuhusu wewe mpaka atakapoifanya imara nchi hii ili kupitia yeye tupate KATIBA MPYA na kupitia yeye ule mshikamano na umoja wa Watanzania uonekane tena.
 
Dhamira njema ya kutuletea chanjo ya corona? Mungu kamletea ujumbe kupitia kupokelewa kuvaa barakoa huku kitaa. Mfalme Beltashazari aliletewa kwa kiganja kilicho uaandika ukuta. Kutaka kuonesha approach ya kumtegemea Mungu haikuwa sahihi!!! Mungu atajidhihirisha tu.
 
Nilikuwa namsikikiza DG wa TPA na TRL hawa mabwana ni mafundi wa maneno yenye vision .....nahisi wakiwa Team wanaweza fanya jambo positive.

DG wa TPA anasema kasi ya upakuaji mizigo imekuwa kubwa mnoo kulinganisha na 5 yrs back.

Anasema ameunda Pic (port improvement committe) ambayo inasimamiwa /ongozwa na wadau wa bandari contrary to 5 yrs back ambapo iyo PIC ilikuwa inaongozwa na DG wa TPA.

😆😆😆 That gentlemen (DG TPA) is so smart eh?
 
Dhamira njema ya kutuletea chanjo ya corona? Mungu kamletea ujumbe kupitia kupokelewa kuvaa barakoa huku kitaa. Mfalme Nebukardezari aliletewa kwa kiganja kilicho uaandika ukuta. Kutaka kuonesha approach ya kumtegemea Mungu haikuwa sahihi!!! Mungu atajidhihirisha.
ww ulichoona ni chanjo tu? mbona lishaweka wazi. anaetaka atapata asietaka hatopata.. hakuna mtu analazimishwa.
Oh Mungu kamleyea ujumbe.. ujumbe gani?
 
Dhamira njema ya kutuletea chanjo ya corona? Mungu kamletea ujumbe kupitia kupokelewa kuvaa barakoa huku kitaa. Mfalme Nebukardezari aliletewa kwa kiganja kilicho uaandika ukuta. Kutaka kuonesha approach ya kumtegemea Mungu haikuwa sahihi!!! Mungu atajidhihirisha.
Magufuli is gone.
 
Nilikuwa namsikikiza DG wa TPA na TRL hawa mabwana ni mafundi wa maneno yenye vision .....nahisi wakiwa Team wanaweza fanya jambo positive

DG wa TPA anasema kasi ya upakuaji mizigo imekuwa kubwa mnoo kulinganisha na 5 yrs back

Anasema ameunda Pic (port improvement committe) ambayo inasimamiwa /ongozwa na wadau wa bandari contrary to 5 yrs back ambapo iyo PIC ilikuwa inaongozwa na DG wa TPA

😆😆😆 That gentlemen (DG TPA) is so smart eh ?
Yupo vizuri brother Eric Hamis hata Kadogosa hizi ni aina za vichwa vya kupewa nafasi za kuleta mageuzi ya kiutendaji ndani ya hizi mamlaka nyeti.
 
ww ulichoona ni chanjo tu? mbona lishaweka wazi. anaetaka atapata asietaka hatopata.. hakuna mtu analazimishwa.
Oh Mungu kamleyea ujumbe.. ujumbe gani?

Endelea kufuka tu! Lakini Watanzania wamekataa barakoa ni ujumbe tosha kwako na unayetaka kumlaghai asiuone huu ukweli na abadilike. Alishindwa kumpaka bull dozzer oil chafu sembuse Mungu wa Mbinguni.
 
Dhamira njema ya kutuletea chanjo ya corona? Mungu kamletea ujumbe kupitia kupokelewa kuvaa barakoa huku kitaa. Mfalme Nebukardezari aliletewa kwa kiganja kilicho uaandika ukuta. Kutaka kuonesha approach ya kumtegemea Mungu haikuwa sahihi!!! Mungu atajidhihirisha.
Tatizo lako una mchungaji mpumbavu halafu unamwamini.
 
Dhamira,

Vipi kuhusiana na washauri na maamuzi yanayofanyika ??

Je ni mema??
 
3. Sekta binafsi- Ameweka wazi anataka kufanya kazi na sekta binafsi na ameshakuta na wafanyabiashara na wawekezaji kuhusu hili.
Una maana gani na "skta Binafsi"?

Ya walanguzi na wachuuzi? Wezi wanaoiharibu serikali isifanikishe kazi za kuwahudumia waTanzania kwa ufanisi?

Wakulima siyo sekta binafsi, mbona hakuna kitu huko?

Hadi hapa alipofikia, mama amejitambulisha wazi kwamba yeye ni mhudumu wa kundi hilo lililomteka akili na si kuwatumikia umma wa waTanzania kwa manufaa ya Tanzania.

Muhimize apunguze kasi ya kuiuza nchi hii kwa bei chee.
 
Una maana gani na "skta Binafsi"?

Ya walanguzi na wachuuzi? Wezi wanaoiharibu serikali isifanikishe kazi za kuwahudumia waTanzania kwa ufanisi?

Wakulima siyo sekta binafsi, mbona hakuna kitu huko?

Hadi hapa alipofikia, mama amejitambulisha wazi kwamba yeye ni mhudumu wa kundi hilo lililomteka akili na si kuwatumikia umma wa waTanzania kwa manufaa ya Tanzania.

Muhimize apunguze kasi ya kuiuza nchi hii kwa bei chee.
Kuwatumikia umma unataka awe anawapikia chai asubuhi na chakula cha mchana?.

Dunia hii ukijifungia ndani imekula kwako.
 
JPM ameshaondoka kutoka juu ya uso wa dunia na huyu Mama ni mpaka 2025 hivyo tuwe wapole. Ramli chonganishi hazina tija.
Mbona unamlilia huyo JPM wako, ni wapi umeona nikimtaja popote?
Huyu ni lazima nimtaje sana hata kama nyinyi vikaragosi vyake mtatokwa machozi ya damu kwa kumtetea. Huo ni wajibu wangu kwa Tanzania, kama ilivyo wajibu wangu kumsifu atakapofanya vizuri katika kuitumikia Tanzania.
 
Back
Top Bottom