Sikiliza wimbo huu kisha utoe comment...

Mrimi

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
1,691
633
Nilikuwa nasikiliza wimbo huu,mpaka unaisha nikakosa cha kusema.
Sijui wanajamii nyie mna maoni gani.
 

Attachments

  • Ambulance_mbuzi_wa_kafara.mp3
    4.4 MB · Views: 1,558
tuonee huruma na bando zetu za kuunga-unga.
tupia mashairi tujadili mambo.
 
Nilikuwa nasikiliza wimbo huu,mpaka unaisha nikakosa cha kusema.
Sijui wanajamii nyie mna maoni gani.
Duuhh, lazima wamtafute kuanzia mtunzi aliyerekodi na yule anayesambaza na atakayesikiliza nikiwemo mimi... NAJARIBU KUWAZA HIVI AKIKUTANA NA ROMA MKATOLIKI WATAIMBA NINI? MAANA CONTENT NAISIKILIZA HUKU NAJIONEA HURMA.... Eti twiga wameenda kutibiwa.... mweeeeeeeeee...
 
tuonee huruma na bando zetu za kuunga-unga.
tupia mashairi tujadili mambo.

Naongea na nyinyi mliosomeshwa bure wakati wa nyerere,halafu saa hizi wanachuo wakiandamana waongezewe mikopo,nyinyi mnatuma kikosi waogeshwe pilipili,eh..

No one can stop me,Only God..

Rest in peace Mwaikusya,pole baba Mwandosya,
Nini walichokupa,Mwakyembe ukanyonyoka,
Ulimboka ukowapi,ukweli hutaki kuananika,
Ulisema unawajua,serikalini ni vibopa,
Ni kiasi gani umepewa,mpaka domo umefunika,
Mtaani inasadikika,iko ulaya unakula bata,
Kibanda wamemtoa jicho,hivi mna nini na wanyakyusa?
Madai ya madaktari,yameishia msitu wa Pande,
Msihangaike kunitafuta,kama mnataka mnichinje,
Natoka Milima ya Rungwe,ulizeni kwa Mwasanje,
Nako kuna misitu,sio mpaka mnipeleke kwenye misitu ya Pande,
Mnasena nchi haina udini,basi mwacheni Yohana naye ng'ombe wake amchinje,
Nilijua ukubwa dawa,ndio maana sikuchachawa,
Akili mmenyimwa,mmeshindwa kutuweka sawa,
Ona haya mambumbu,kuku anataga bila jogoo eti wanamshuru mzungu,
CHADEMA na nyinyi jaribuni kujipanga,
Nani aliyewatuma,mtoe namba za Anna Makinda?
Hayo matokeo mabovu,tatizo sio Kawambwa,
Walimu wana stress,wanadaiwa mikopo kwenye kila taasis,
Na walipolalamika,mlisema acheni kazi,
Mishahara ndio tatizo,ya nini tume ya uchunguzi?
(Wapuzi)

CHORUS x 4
We ni nani unaongea?
Mimi ni mbuzi wa kafara,
Huogopi kupotea?
Mi nimbuzi wakafara,

Hii nyimbo inapopigwa lia,usicheze kiduku,
Tambiko langu ni mtu,we nenda ukachinje kuku,
Maneno yangu si luku,hapa hatii mguu kasuku,
Mnasema sheria msumeno,mbona kwingine haina meno?
Vigogo inashindwa kata,au nimtaje Zombe ili awe mfano?
Kama walikuonea,mbona hukudai fidia na jela ukatumikia?
Waheshimiwa vipi,twiga walioenda kutibiwa?
Hivi wamezidiwa,mbona taarifa hatujapewa?
Mmezidisha wizi,mpaka mnamzunguka mkubwa,
Ikulu haijui mchongo,KIA ndege anapanda twiga..

(CHOUS X 4)

Mwizi akiondoka,si kuna kuwa na nafuu?
Lowasa mmemtoa,na umeme unapanda juu,
Lowasa hakuwa fisadi,kumbe ni siasa tu,
Mikataba mlisaini wote,vipi ajiuzulu peke yake?
Nakumbuka msafara,alipotembelea watu wake,
Kwenye majanga hakwenda ulaya,Lowasa tulilia wote,
Tofauti na mwenzake,kazi yake kukata utepe,
Siasa ni mchezo mchafu,nimeelewa maana yake,
Lowasa mmempaka tope,mzalendo na chama chake,
Mnawapa watu sehemu nyeti,kwa sababu mlisoma wote,
Heheheheee.. acha nicheke!
Nchi yetu ina ukimwi,na CD4 zimeshuka,
Panapofuka moshi,si ndio moto utakapowaka?
Vitambulisho vya taifa,ni proposal na mashaka,
Soda zina madhara,mbona onyo hamjaweka?
Hivi jamani,mna nini nyie mamburura,
Kijijini hakuna maji,eti mnataka kuchimba bomba la gesi kutoka Mtwara!
Hivi ni kipi,tutakachojivunia jamani?
Madini ni yetu,chapa ni ya mjerumani,
Dini zimeletwa na wageni,nyinyi mnagombania nini?
Wajinga mapanga tupeni,Afrika tujenge amani,
Dawa za kuongeza siku,hilo sio jibu letu,
Sogea nikung'ate sikio nikujuze mwanakwetu,
Wanatengeneza magonjwa ili watuuzie madawa,
Amani kwa babu yangu Nyika,na mzee Nyagawa,
Alitunza muarovera,hakupenda hizi dawa,
Alifahamu madhara,ndio maana hakuzipa power,
Mpenda haki hapendwi,na msema kweli anauliwa,
Nauli wamekuchangia mjomba,mbona umekula bata?
Hata pesa mkinipa hili domo sio zito kamwe sitolifunika,
Baada ya kuongea haya,lolote lawezanifika,
Kwa lolote nitakukumbatia,nitazidi kukulilia Afrika..

(CHORUS X 4)

Enheee.. Damu ya Mwangosi ipo kwenye uso wa nchi..

What goes around,what comes around.. Hiki kikombe hakiepukiki..

Sugu vita mlianzisha wengi,vipi vipi umejisalimisha peke yako brother? Hehe.. Au mgao usingetosha?! Hahaha..

Mmelifungia gazeti la Mwanahalisi,udaku yanaonesha matusi.. Hihihi.. kweli hii nchi nona..!!

Haha..

Nimejaribu kwa uwezo wangu kwa kadiri nilivyoweza ila hapo kwenye red sina hakika sana,labda kwa waliosikiliza wimbo huu vizuri wanaweza wakahariri.Ila kiukweli dogo ameamua kutupia mawe kizani,tunasuri kusikia kelele kwa yeyote likatayempata!
 
Kweli huyu ni Mbuzi wa Kafara ila sidhani kama huu wimbo utakuja sikika kwenye Radio station yoyote.
 
Nilikuwa nasikiliza wimbo huu,mpaka unaisha nikakosa cha kusema.
Sijui wanajamii nyie mna maoni gani.

We mkali nigeisikia wapi hii bila JF, haitapigwa Radio yoyote TZ.

"Kijijini hakuna maji,eti mnataka kuchimba bomba la gesi kutoka Mtwara"
 
Kweli huyu ni Mbuzi wa Kafara ila sidhani kama huu wimbo utakuja sikika kwenye Radio station yoyote.

Uko sahihi mkuu.
Huu wimbo ni mzuri sana na ungeweza kupata airtime ya kutosha,tatizo ni pale alipofumba mcho na kutupia mawe kizani.Kwa uzani,huu wimbo hautofautiani sana na Miss Tanzania wa Solo Thang ambao nao kama kawaida haukupewa airtime kabisa.

Anyway,naamini ipo siko watu watamwelewa tu dogo
 
We mkali nigeisikia wapi hii bila JF, haitapigwa Radio yoyote TZ.

"Kijijini hakuna maji,eti mnataka kuchimba bomba la gesi kutoka Mtwara"

Hizi tunaita revolutionary songs.
Kwa kawaida hizi huwa hazipigwa redioni,wanasema zina uchochezi.
 
haamini mtu ni kasuku,

Nimejaribu kwa uwezo wangu kwa kadiri nilivyoweza ila hapo kwenye red sina hakika sana,labda kwa waliosikiliza wimbo huu vizuri wanaweza wakahariri.Ila kiukweli dogo ameamua kutupia mawe kizani,tunasuri kusikia kelele kwa yeyote likatayempata!

"Hapo kwenye Red" Hatii mguu kasuku!!!

Yaaani Kasuku hafui dafu.

Ila best na we mkali uling'amua haya yote kwa kusikiliza tu? Duh...
 
Usiogope bana kitu kiko i-tune yaani kama page moja ya karatasi kodaunilodi, haya mwanangu mashahiri ndo hayo!

Kazi kwako!

Hata akisoma hayo mashairi,hawezi kupata ile ladha ya wimbo wenyewe.
 
Hivi nnavyokwambia nshaichoma nakamua tu kwa gari yangu!

Sijuwi niiweke ringitoni?

Hebu subiri!
Hehehehehe naona wewe umeamua kuwa ''kuku wa shughuli'' embu iweke ringtone halafu kesho ukutane na wazee wa kung'oa kucha na meno pasipo na ganzi ''Utajuuuuta''.
 
Hehehehehe naona wewe umeamua kuwa ''kuku wa shughuli'' embu iweke ringtone halafu kesho ukutane na wazee wa kung'oa kucha
na
meno pasipo na ganzi ''Utajuuuuta''.
Mimi t
ayari nimeiweka kama ringtone. Unasema wazee wa kucha wamefanyaje? Hilo jina inaelekea wamelipenda japo sioni uzuri wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom