Sijutii kuacha kazi, Mshahara wa Tsh. 450,000 usingenitosha na majukumu niliyokuwa nayo

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,013
1,634
Miaka minne nyuma niliamua kuacha kazi na kujitosa rasmi kwenye kilimo, ufugaji wa kuku, kupindi hicho nilikua nachukua mshahara 400,000 ukitoa makato mengine ilikua inabaki around kwenye 350000.

Niliamua kujitesa kwa mshahara huo nikawa na save na kuwekeza kwenye kilimo cha mahindi na machungwa na pia nilikuwa najishugulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji, baada ya kuingia kwenye ndoa niliona tu huko mbeleni maisha yatakua magumu sana kama nitaendelea na hii kazi yangu.

Nikachukua maamuzi magumu ya kuacha kazi na pia nikaua biashara ya ufugaji wa kuku na kufungua biashara ya uwakala wa mitandao ya simu.

Nilipata changamoto nyingi za kukimbiwa na marafiki na ndugu hawakunielewa, na kupunguza ukaribu kwangu kwani waliniona nitakua mzigo kwao.

Nilimueleza mke wangu umuhimu wa haya maamuzi yangu alinielewa na kuniunga mkono. Sasa ni miaka minne imepita tokea nichukue maamuzi magumu.

Wale wenzangu ambao wapo kazini naambiwa mshahara umefikia 450,000 kabla ya makato lakini mimi binafsi mshahara huo usingenitosha kwa maisha ya sasa.

MAFANIKIO
~ Biashara ya huduma za kifedha inaniingizia hicho kiwango cha Mshahara au zaidi.
~ Kilimo cha machungwa now kinaniingizia mpaka milioni 4 kwa mwaka na kitaongezeka mbeleni.
~ Kilimo cha mahindi mwaka jana kiliniingizia milioni 2 mwaka huu nimejipanga zaidi.

HITIMISHO
Ukitaka kufanya yako fanya usikatishwe tamaa na mtu, mimi kwa uwezo wa Mungu naiona kesho yangu nzuri.
 
Miaka minne nyuma niliamua kuacha kazi na kujitosa rasmi kwenye kilimo, ufugaji wa kuku, kupindi hicho nilikua nachukua mshahara 400,000 ukitoa makato mengine ilikua inabaki around kwenye 350000.

Niliamua kujitesa kwa mshahara huo nikawa na save na kuwekeza kwenye kilimo cha mahindi na machungwa na pia nilikuwa najishugulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji, baada ya kuingia kwenye ndoa niliona tu huko mbeleni maisha yatakua magumu sana kama nitaendelea na hii kazi yangu.

Nikachukua maamuzi magumu ya kuacha kazi na pia nikaua biashara ya ufugaji wa kuku na kufungua biashara ya uwakala wa mitandao ya simu.

Nilipata changamoto nyingi za kukimbiwa na marafiki na ndugu hawakunielewa, na kupunguza ukaribu kwangu kwani waliniona nitakua mzigo kwao.

Nilimueleza mke wangu umuhimu wa haya maamuzi yangu alinielewa na kuniunga mkono. Sasa ni miaka minne imepita tokea nichukue maamuzi magumu.

Wale wenzangu ambao wapo kazini naambiwa mshahara umefikia 450,000 kabla ya makato lakini mimi binafsi mshahara huo usingenitosha kwa maisha ya sasa.

MAFANIKIO
~ Biashara ya huduma za kifedha inaniingizia hicho kiwango cha Mshahara au zaidi.
~ Kilimo cha machungwa now kinaniingizia mpaka milioni 4 kwa mwaka na kitaongezeka mbeleni.
~ Kilimo cha mahindi mwaka jana kiliniingizia milioni 2 mwaka huu nimejipanga zaidi.

HITIMISHO
Ukitaka kufanya yako fanya usikatishwe tamaa na mtu, mimi kwa uwezo wa Mungu naiona kesho yangu nzuri.
Maamuzi magumu nikitaka yafanya huwa sitaki ushauri hata nikiomba ushauri nakuwa nataka tu kusikia waasemaje ila uamuzi nakuwa nishauchukua.
 
Maamuzi magumu nikitaka yafanya huwa sitaki ushauri hata nikiomba ushauri nakuwa nataka tu kusikia waasemaje ila uamuzi nakuwa nishauchukua.
Usitegemee ukamilifu kutokea kwako ama kwa wenzako hakuna mwenye ukamilifu kabisa maisha yetu Ni full of uncertainties and probabilities but still watu wanataka kulazimisha kuwa kesho yao wanaijua itakuwaje
 
Usitegemee ukamilifu kutokea kwako ama kwa wenzako hakuna mwenye ukamilifu kabisa maisha yetu Ni full of uncertainties and probabilities but still watu wanataka kulazimisha kuwa kesho yao wanaijua itakuwaje
Tunaishi kwa matumaini kuwa kesho itakuwa bora zaidi ya jana na njia tunayofuata ni bora. Ukiomba ushauri watu watakutisha sana sana.
Kuna jamaa alikuwaga engineer voda kuanzia kama 2009-2015, aliacha kazi wakaenda kuanzisha kampuni yeye na rafiki yake ina deal na mambo ya minara. Hakuwaambia ndugu wala mkewe kuwa kaacha kazi aakijua lazima watamwona chizi. Alikuwa anaamka asubuhi anaenda kazini kama kawaida ila kumbe ofisini kwao. Lakini kufikia miaka 2018 hivi ile move ilikuwa imepay off kiasi kwamba kila mwezi yeye na rafiki yake wanajilipa kila mmoja mls 40. ALikuja kuwaambia ndugu na mke wake baada ya kampuni kusimama.
Believe in your instinct ukifail jaribu tena na tena.
 
Trust them smt they know more what you want. Hii logic brain inasumbua mno kila kitu inabidi u reason yenyewe inajua ku think in linear function eg if ......then thinking. Kuna mambo Ni beyond body and mind
Kabisa mkuu na hii ndio huwa inafanya watu ambao hawajasoma sana wafanikiwe katika biashara. Msomi ukitaka anzisha biashara, unaandika business plan, unaanza kuangalia scenarios kibao, una reason kila kitu mwisho unasema hapana hii biashara haiwezekani.
Muha anakuja zake tu anafungua kabiashara ili mradi anajua hapa kuna wahitaji baada ya miaka ana duka kubwa.
 
Back
Top Bottom