Sijui niache kazi! Msaada wenu ndugu

Jagarld

JF-Expert Member
Apr 7, 2011
2,515
3,042
Habari zenu ndugu wanajf wenzangu,hamjambo?

Kuna jambo moja linanitesa na kuninyima raha ndugu zangu,ningependa kuliweka wazi kwenu ili mwenye msaada wake aweze kunisaidia.

Nimekuwa na urafiki wa kawaida na dada mmoja ambaye mme wake ni boss wa kampuni moja inayojishughulisha na mambo ya kusafirisha watalii na huyu dada nae ana cheo kikubwa kwenye hii kampuni yao,urafiki wetu ulianza mwaka mmoja wakati nafanya kazi serikalini baadae akaniambia kwanini nisihamie kwenye kampuni yao na kunipa ahadi kibao,alinitaka nimpe nakala ya vyeti vyangu nami kweli nikafanya hivo,baada ya wiki tatu nikaitwa kufanya interview,siku ya interview nilihudhuria akanipigia simu niende ofisini kwake ambako tulianza kupiga stori na interview nikaambiwa imeahirishwa mpaka nitakapojulishwa.

Baada ya wiki mbili nilipokea barua ya kuitwa kazini na nikaenda tukaelewana mshahara na mambo mengine yakawa safi ikanibidi nirudi ofisini na kuandika barua ya kuacha kazi ndani ya masaa 24.

Baada ya wiki moja nikaanza kazi rasmi kwa mwajiri wangu mpya,kwa muda wa miezi minne kazi imekuwa inaenda vizuri lakini mke wake boss akaanza kama matani anataka zawadi,nikamwambia poa zawadi tu utapata wala usijali huku tunataniana.

Kuanzia wiki iliyopita amekuwa mtu wa kupiga simu muda wowote usiku baada ya boss kusafiri,anasema ametokea eti kunipenda tangu siku ya kwanza tunakutana naye ndo maana kafanya kila njia niwe karibu naye,anadai atanifanyia vitu vikubwa zaidi ata ambavyo sijafikiria maishani nikikubali kufanya na kama nitaonesha umasikini jeuri yeye atajua atakavofanya japo anadai ananipenda ana ananihurumia mwisho wangu utakuwa mbaya nikikataa,mda huu ninapoandika hii niponyumbani baada ya kuomba ruhusa kuwa naumwa.

Ndugu zangu nifanyaje?
 
we kubali yaishe sababu utapoteza vyote kule kazi umeacha cha kufanya hapo ni kula kisailensa we ni mtoto wa kiume hicho ni kitu kidogo sana kudeal nacho yapo mambo makubwa sana ya kuumiza kichwa sio hilo kwanza nakushangaa kujifanya unaumwa huyo dawa yake piga mzigo huku ukitafta ajira sehemu nyingine ukipata tu unasepa otherwise we kula lakini kimya kimya bosi asijue
 
duh!!! ulipokosea ni pale demu kukupigia pande kupata kazi mwana...iwe fundisho kwa wanaume wengine dnt ever ever let mwanamke akupigie pande...wewe kama vyeti vyako vimekalika ya nini kubebeka.
sasa mwana hapo huna jinsi wewe itabidi tuu umege huyo dada...na tena umpige dozi kamilifu mpaka adate kweli kweli huku ukijua kabisa hapo ngoma nje nje. wewe mwana vitu atakavyotaka kukufanyia hakikisha hela zinajaaa benk account yako maana itabidi uanze kutumia ARV toka ulaya maana bongo wameshachakachua. pole sana
 
Habari zenu ndugu wanajf wenzangu,hamjambo? Kuna jambo moja linanitesa na kuninyima raha ndugu zangu,ningependa kuliweka wazi kwenu ili mwenye msaada wake aweze kunisaidia.
Nimekuwa na urafiki wa kawaida na dada mmoja ambaye mme wake ni boss wa kampuni moja inayojishughulisha na mambo ya kusafirisha watalii na huyu dada nae ana cheo kikubwa kwenye hii kampuni yao,urafiki wetu ulianza mwaka mmoja wakati nafanya kazi serikalini baadae akaniambia kwanini nisihamie kwenye kampuni yao na kunipa ahadi kibao,alinitaka nimpe nakala ya vyeti vyangu nami kweli nikafanya hivo,baada ya wiki tatu nikaitwa kufanya interview,siku ya interview nilihudhuria akanipigia simu niende ofisini kwake ambako tulianza kupiga stori na interview nikaambiwa imeahirishwa mpaka nitakapojulishwa.
Baada ya wiki mbili nilipokea barua ya kuitwa kazini na nikaenda tukaelewana mshahara na mambo mengine yakawa safi ikanibidi nirudi ofisini na kuandika barua ya kuacha kazi ndani ya masaa 24.
Baada ya wiki moja nikaanza kazi rasmi kwa mwajiri wangu mpya,kwa mda wa miezi minne kazi imekuwa inaenda vizuri lakini mke wake boss akaanza kama matani anataka zawadi,nikamwambia poa zawadi tu utapata wala usijali huku tunataniana. Kuanzia wiki iliyopita amekuwa mtu wa kupiga simu mda wowote usiku baada ya boss kusafiri,anasema ametokea eti kunipenda tangu siku ya kwanza tunakutana naye ndo maana kafanya kila njia niwe karibu naye,anadai atanifanyia vitu vikubwa zaidi ata ambavyo sijafikiria maishani nikikubali kufanya na kama nitaonesha umasikini jeuri yeye atajua atakavofanya japo anadai ananipenda ana ananihurumia mwisho wangu utakuwa mbaya nikikataa,mda huu ninapoandika hii niponyumbani baada ya kuomba ruhusa kuwa naumwa. Ndugu zangu nifanyaje?

Kimbia, hilo ni pepo. Imagine huyo bwana ajue kama date na mkewe? Pili kama ni dili wamechonga kufanya hivyo unajuaje? Achana nae bwana. Usiache kwazi kwa ajili ya mpuuzi mmoja. Keep her sms akilete zengwe kwenye kazi yako unamwonyesha mumewe.
 
oh alafu naomba kabisa uhakikishe iwe iweje huyo unamla tigo!!! taha way atleast u got sumthing against her
 
we kubali yaishe sababu utapoteza vyote kule kazi umeacha cha kufanya hapo ni kula kisailensa we ni mtoto wa kiume hicho ni kitu kidogo sana kudeal nacho yapo mambo makubwa sana ya kuumiza kichwa sio hilo kwanza nakushangaa kujifanya unaumwa huyo dawa yake piga mzigo huku ukitafta ajira sehemu nyingine ukipata tu unasepa otherwise we kula lakini kimya kimya bosi asijue

ahsante mkuu lakini shetani hana aibu kabisa dah,ata mwaka haujaisha nimetoka serikali leo yameanzaa!
 
Kimbia, hilo ni pepo. Imagine huyo bwana ajue kama date na mkewe? Pili kama ni dili wamechonga kufanya hivyo unajuaje? Achana nae bwana. Usiache kwazi kwa ajili ya mpuuzi mmoja. Keep her sms akilete zengwe kwenye kazi yako unamwonyesha mumewe.

nashukru sana kwa ushauri wako da Caroline danzi nitajitahidi
 
Last edited by a moderator:
mkuu kuwacha kazi sikazi but kupata kazi nikazi. kula mzigo taratibu but kumbuka kupima HIV muimu kiongozi. mwambie hakupe manoti ya kutosha ndiyo umpe madude.

Wewe msomeshe kwamba kazi unapenda na pi unaheshimu ndoa yao! usikubali mwambie unampenda ila kwa kuwa tayari ameolewa ni ngumu! wakati huo tafuta tape recoder kutunza ushahidi. Then endeleaa kumshauri akubaliane nawe wakati huo we chapa kazi hakikisha unafanya kazi kwa ufanisi wako wote. Piea mweleze madhara kama atatakakukuharibia!

then uwe mwaminifu na mfungie vioo kiana ili uwe na sura ya kazi! ikitokea amekuharibia mface hubby wake na mwambie ukweli wa mambo na pia mpe ushaidi utarudisha kazi na ikishindikana atafanya lolote ili uwe na kazi kwa kuwa umelinda ndo yake!

Usijaribu kula tunda! ukifanya hivyo hautaacha utanogewa na itafika 40 mambo yatakuwa mabaya na unaweza kupoteza maisha yako hata kwa kuuawa! mke/mume wa mtu mavi!!!!

usisilize mambo ya kupiga mzigo then unatafuta pengine! no utanogewa! na je kama ameathirika?? si ndo umeukwaa! tena mtu wa jinsi hiyo basi ujue kuna wengi anawapa! shauri yako!!! nenda kazini chapa kazi, hakuna cha kukuharibia wala nini!!!:israel:

Usitende dhambi ya uzinzi na mke wa mtu itakurudia! kama sisi kukamatwa basi na wa kwako atatembelewa hapo baadaye! gangamaa kijana!!!!! usiogope kazi tunapewa na Mungu yamkini hapo si mpango wake kwanza umeingia kimapenzi mapenzi tu!
 
Usijaribu....usijaribu.....wala usijaribu kuhusiana na huyo mke wa boss, hatari iliyo mbele ni kubwa kuliko maamuzi ya sasa. "Mapenzi yanapoanza usiku unaonekana mchana ila yakikolea mchana unaonekana usiku" Ndio maana hakuna walioweza kuyaficha mapenzi hata mwanamuziki Fresh Jumbe akayafananisha mapenzi na KIKOHOZI....Uwe makini ndg hapo unaipoteza nafsi yako.
 
Unanikumbusha utani wa Mmakonde alipomwona mwizi wa nazi zake juu, kwamba "njomba uchipande wala uchichuke, uchiruke wala uchibaki hapo, ukifanya hivyo njomba nchale".

Kaka haupo salama, whether ummege au umpotezee. Cha kufanya acha kazi hapo, siyo salama kwako, na kesho au kesho kutwa usirudie kosa hili!
 
Dah mtihani huu!!! Ila kwa yote jua mke wa mtu ni sumu na mumewe akijua atakuua kabisa!!! Tena kirahisi mno!! Chezea pesa na kila kitu ila si mke wa mtu!! Mwogope kama ugonjwa usiotibika!!!
 
Back
Top Bottom