Sijisikii Fahari kuhusishwa na Mbunge wala Bunge la Tanzania

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Kuna wakati nilidhani pengine iko siku nitagombea ubunge, niwe mbunge wa bunge la Jamhuri ya Tanzania

Nafurahi tamaa hii imepotea kwa kuwa Ubunge na Bunge letu vimekosa hishima na uadilifu mbele ya jamii ya Kitanzania na duniani kiasi kwamba sitamani kuhusishwa navyo.

Kuna nyakati wahalifu fulani walikuwa wanajisikia fahari kuwa wahalifu au kuhusishwa na kundi fulani la uhalifu. Pale Magomeni mapipa paliwahi kutokea kundi linaitwa vijana wa Yoso, ambao walikuwa waporaji na wabakaji maarufu wanaojisikia fahari kufanya vitendo hivyo pamoja na kujulikana kwamba wao ni Yoso.

Bunge letu
linakula rushwa
limeshindwa kuwajibisha serikali kuhusu ufisadi na mikataba mibovu
limeshindwa kusimamia serikali kukuza uchumi na kushusha inflation
limeshindwa kusimamia serikali uporaji wa mashirika na viwanda vya umma
linapitisha sheria za misamahaa ya kodi kwa wawekezaji na wafanya biashara kubwa
limeshindwa kusimamia serikali kukusanya kodi kikamilifu
limeshindwa kusimamia serikali kuboresha huduma za jamii (elimu, afya, maji, etc)
linatumika na serikali kukandamiza haki
linajilimbikizia mali na pesa za umma
linatunga sheria kudhulumu wananchi
limeshindwa kuwatetea walimu na madaktari waliogoma
linapitisha bajeti za kifisadi
linajitukuza kuzidi wananchi
limegeuka kuwa uwanja wa mipasho na majungu


Wabunge wetu
wanakula rushwa, ni mafisadi
wameshindwa kudhibiti mafisadi
wameshindwa kusimamia mikataba yenye tija kwa taifa
wanajiongezea mishahara wakati wafanyakazi hawaongezewi
wameshindwa kuwatetea walimu na madaktari waliogoma
hawalipi kodi katika mishahara na posho zao
hawaungani kutetea maslahi ya wananchi bali maslahi yao
wanapitisha sheria za dhuluma kwa wananchi
wanapitisha bajeti kifisadi
wanajitukuza
wanapika majungu na mipasho

Sijisikii fahari kuhusishwa na Mbunge wala Bunge la Jamhuri ya Tanzania
 
Toka walivyopitisha sheria ya kipuuzi ya SSRA sitamani kusikia kitu kinaitwa bunge wala wabunge,
labda nitabadilisha msimamo wangu siku sheria hii ikibadilishwa.
 
Kuna wakati nilidhani pengine iko siku nitagombea ubunge, niwe mbunge wa bunge la Jamhuri ya Tanzania

Nafurahi tamaa hii imepotea kwa kuwa Ubunge na Bunge letu vimekosa hishima na uadilifu mbele ya jamii ya Kitanzania na duniani kiasi kwamba sitamani kuhusishwa navyo.

Kuna nyakati wahalifu fulani walikuwa wanajisikia fahari kuwa wahalifu au kuhusishwa na kundi fulani la uhalifu. Pale Magomeni mapipa paliwahi kutokea kundi linaitwa vijana wa Yoso, ambao walikuwa waporaji na wabakaji maarufu wanaojisikia fahari kufanya vitendo hivyo pamoja na kujulikana kwamba wao ni Yoso.

Bunge letu
linakula rushwa
limeshindwa kuwajibisha serikali kuhusu ufisadi na mikataba mibovu
limeshindwa kusimamia serikali kukuza uchumi na kushusha inflation
limeshindwa kusimamia serikali uporaji wa mashirika na viwanda vya umma
linapitisha sheria za misamahaa ya kodi kwa wawekezaji na wafanya biashara kubwa
limeshindwa kusimamia serikali kukusanya kodi kikamilifu
limeshindwa kusimamia serikali kuboresha huduma za jamii (elimu, afya, maji, etc)
linatumika na serikali kukandamiza haki
linajilimbikizia mali na pesa za umma
linatunga sheria kudhulumu wananchi
limeshindwa kuwatetea walimu na madaktari waliogoma
linapitisha bajeti za kifisadi
linajitukuza kuzidi wananchi
limegeuka kuwa uwanja wa mipasho na majungu


Wabunge wetu
wanakula rushwa, ni mafisadi
wameshindwa kudhibiti mafisadi
wameshindwa kusimamia mikataba yenye tija kwa taifa
wanajiongezea mishahara wakati wafanyakazi hawaongezewi
wameshindwa kuwatetea walimu na madaktari waliogoma
hawalipi kodi katika mishahara na posho zao
hawaungani kutetea maslahi ya wananchi bali maslahi yao
wanapitisha sheria za dhuluma kwa wananchi
wanapitisha bajeti kifisadi
wanajitukuza
wanapika majungu na mipasho

Sijisikii fahari kuhusishwa na Mbunge wala Bunge la Jamhuri ya Tanzania

Mkuu kuna kitu hujakitafakari vizuri. Nionavyo mimi, tatizo kubwa lipo kwa wabunge wengi wa ccm kwani wanaendeleza maslahi ya chama chao ndani ya serikali. kIla kitu kwao ni NDIYOOOOOOOO!!!! halafu hii sheria YA marekebisho ya mifuko ya jamii ya ssra baadhi ya wabunge wa upinzani wamezungumza hadharani na kudai hicho kipengele cha umri hakikuwepo wakati wanaijadili. sasa hapa inaonekana KILICHOMEKWA juu kwa juu na serkali ya magamba kwa sababu wazojua wao. ndo maana mi nilipendekeza kama kuna uwezekano tujikumbushe kwa hansard za bunge tujiridhishe hasa ilkuwaje.
USHAURI WANGU: watanzania tujihusisheni sana na siasa. wanasiasa wana maamuzi nyeti sana yanayohusu mustakabari wa maisha yetu, wao ndo wanapitisha bajeti ambayo ndani yake kuna MISHAHARA, HUDUMA ZA KIJAMII mf MAJI, DAWA, BEI ZA VITU, UDHIBITI WA RASILIMALI ZETU n.k. tukiwaachia wanasiasa mambo nyeti kama haya, halafu bahati mbaya wakawa wahuni, hakyanani watatuchuuza mchana kweupe. Watanzania tujipangeni tuiondoe ccm ili tujipange kivingine. ccm haina jipya na haioneshi dalili za kubadilika. mafisadi ndo tena wanapewa uenyekiti wa kamati za fedha na uchumi, unategemea nini hapo?????????
 
Kinachonishangaza ni kwamba hata wabunge niliokua nao chuoni enzi zile uanafunzi wakijifanya wanaharakati,wapigania haki makamanda majina kibao wamebadilika na kuiacha misimamo yao. Hivi wamerogwa au ilikua njaa?
 
Back
Top Bottom