CONTROLA
JF-Expert Member
- Sep 15, 2019
- 6,935
- 22,915
Kuna vitu huwa najaribu vifikiria kwenye maisha najipa majibu tu kuwa sitoweza,maana kama ni kujaribu kuvaa nimeshajaribu kuvaa pete za urembo za kawaida tu muda mrefu ila nimeshindwa. Sasa nikija kufikiria pete ya NDOA ambayo nasikia ile pete ikishaingia kidoleni kuvuliwa ni kwenye special case tu, sijioni kama nitafanikisha hilo.
Huwa nanunua pete za kawaida za urembo natia kidoleni ila kiukweli huwa ile pete sifiki nayo jioni lazima ntajikuta nimeitoa nimeiweka mfukoni mana nahisi kama vidole vyangu vinakereketwa.
SWALI MLIO KWENYE NDOA:
Huwa nanunua pete za kawaida za urembo natia kidoleni ila kiukweli huwa ile pete sifiki nayo jioni lazima ntajikuta nimeitoa nimeiweka mfukoni mana nahisi kama vidole vyangu vinakereketwa.
SWALI MLIO KWENYE NDOA:
- Kuna shida yeyote kama nimeoa na nikatoka kwenda kazini au popote bila pete ya ndoa kidoleni?
- Sitofikiriwa vibaya na jamii?
- Hili swala ni la uamuzi binafsi au inapasa nipate kibali cha kutovaa pete kutoka kwa mke wangu?
- Naombeni kujua nyie mlio kwenye ndoa kuanzia mwaka wa pili na kuendelea hizo pete hapo. Vipi kwa upande wenu?