Nyakwaratony
JF-Expert Member
- Dec 21, 2011
- 573
- 140
Asalaam Aleikum!
Bwana Yesu asifiwe!
Nilimpenda sana kaka mmoja aliyekuwa mwalimu wangu, kumbe na yeye kwa wakati huo alikuwa ananipenda ila hakutaka kuniambia. Tuliheshimiana sana pia tulikuwa marafiki sana. Baada ya kumaliza chuo niliondoka mkoan hapo lakini nawasiliano yaliendelea, hapo ndipo alipoanza kusema lake la moyoni.
Woooh, nilifurahi sana na kujisemea moyoni ulikuwa wapi? mawasiliano yaliendelea kuwa mazuri zaidi na zaidi, baada ya mwaka nilikwenda kumtembelea ila sikufika anapoishi kwani nilihisi kwa jinsi ninavyomfeel na yeye anavyonifeel tunawezajikuta tumeishia kubanjuja. Nilifanya hivyo kila mwaka nilipopata likizo kwa kipindi cha miaka mitatu.
Tulizungumza mambo mengi hasa kuhusu kuanzisha familia na alionekana kukubali,mwaka wa nne tulianza mapenzi rasmi nikiamini kuwa tunaelekea kuanzisha familia kwani ni muda tosha wa kusomana tabia (hayo ndio yalikuwa mawazo yangu) baada ya miezi minne ya mapenzi motomoto alianza kubadilika, mara hapatikani siku nzima ukimuuliza anadai simu haikuwa na charge, mara line iliblock na sababu chungu nzima.
Kwa vile sikuwahi kufika kwake niliamua kufunga safari na kwenda mpaka ofisini kwake, nilichoambiwa ni kwamba kasafiri kwenda mkoani anakaribia wiki, kabla ya hapo alikuwa na wiki nzima hapokei wala kujibu sms zangu na hatukuwa tumegombana. Nilichukia na kumuandikia sms kali ya kusitisha uhusiano. Nahisi alishukuru sana kwani hakujibu kabisa. Na uhusiano tulikuokuwa tumeudumisha kwa muda wa miaka minne ukaishia hapo....
Ilikuwa ni mwezi wa tano tangu nimeachana na huyo kaka. Ilipofika mwezi wa nane nilipigiwa simu na kaka mwingine niliyesoma nae course flani miaka ya nyuma, wakati tunasoma alinidatilia sana ila sikumkubalii. Alinikaribisha kwake nikamuhaidi ningeenda wiki iliyofata, kweli nilienda tuliongea mambo mengi hatimaye tukaanza uhusiano, baada ya mwezi tukapeana maraha. Kiukweli ndani ya mwezi kabla ya ku-do alinicare sana. Outing kibao, shopping za kufa mtu n.k.
Ila baada ya ku-do tu mapenzi yalipungua hatimaye nilimchukia sana na mapenzi yakaisha. Huyu wa mwisho sasa yeye nilimzungusha kwa muda wa miezi sita baadaye nikaamua kujilipua nikampa tundi... Weee yan yeye alikuwa akijisikia ndio ananitafuta "wewe uko wapi nikufate" akinifata ni direct kwake ku-do tu. Baada ya hapo anaweza asipokee simu au asijibu sms. Na ikitokea kajibu jua kuwa anahitaji. Ukisema basi tutoke tukazungumze kuhusu mahusiano yetu anadai yupo busy.
Je nifanyeje, mapenzi kwangu yamekuwa shubiri, ni miezi miwili sasa mawasiliano yamekatika baina yangu na boyfriend wangu wa mwisho. Je nimekuwa rahisi sana? Lakini mbona nachukua muda mrefu kukubali kutoa tundi labda ungesema ni Easy Going? Msaada wenu ni muhimu kwangu. Samahani kwa maneno mengi. Ahsanteni.
Bwana Yesu asifiwe!
Nilimpenda sana kaka mmoja aliyekuwa mwalimu wangu, kumbe na yeye kwa wakati huo alikuwa ananipenda ila hakutaka kuniambia. Tuliheshimiana sana pia tulikuwa marafiki sana. Baada ya kumaliza chuo niliondoka mkoan hapo lakini nawasiliano yaliendelea, hapo ndipo alipoanza kusema lake la moyoni.
Woooh, nilifurahi sana na kujisemea moyoni ulikuwa wapi? mawasiliano yaliendelea kuwa mazuri zaidi na zaidi, baada ya mwaka nilikwenda kumtembelea ila sikufika anapoishi kwani nilihisi kwa jinsi ninavyomfeel na yeye anavyonifeel tunawezajikuta tumeishia kubanjuja. Nilifanya hivyo kila mwaka nilipopata likizo kwa kipindi cha miaka mitatu.
Tulizungumza mambo mengi hasa kuhusu kuanzisha familia na alionekana kukubali,mwaka wa nne tulianza mapenzi rasmi nikiamini kuwa tunaelekea kuanzisha familia kwani ni muda tosha wa kusomana tabia (hayo ndio yalikuwa mawazo yangu) baada ya miezi minne ya mapenzi motomoto alianza kubadilika, mara hapatikani siku nzima ukimuuliza anadai simu haikuwa na charge, mara line iliblock na sababu chungu nzima.
Kwa vile sikuwahi kufika kwake niliamua kufunga safari na kwenda mpaka ofisini kwake, nilichoambiwa ni kwamba kasafiri kwenda mkoani anakaribia wiki, kabla ya hapo alikuwa na wiki nzima hapokei wala kujibu sms zangu na hatukuwa tumegombana. Nilichukia na kumuandikia sms kali ya kusitisha uhusiano. Nahisi alishukuru sana kwani hakujibu kabisa. Na uhusiano tulikuokuwa tumeudumisha kwa muda wa miaka minne ukaishia hapo....
Ilikuwa ni mwezi wa tano tangu nimeachana na huyo kaka. Ilipofika mwezi wa nane nilipigiwa simu na kaka mwingine niliyesoma nae course flani miaka ya nyuma, wakati tunasoma alinidatilia sana ila sikumkubalii. Alinikaribisha kwake nikamuhaidi ningeenda wiki iliyofata, kweli nilienda tuliongea mambo mengi hatimaye tukaanza uhusiano, baada ya mwezi tukapeana maraha. Kiukweli ndani ya mwezi kabla ya ku-do alinicare sana. Outing kibao, shopping za kufa mtu n.k.
Ila baada ya ku-do tu mapenzi yalipungua hatimaye nilimchukia sana na mapenzi yakaisha. Huyu wa mwisho sasa yeye nilimzungusha kwa muda wa miezi sita baadaye nikaamua kujilipua nikampa tundi... Weee yan yeye alikuwa akijisikia ndio ananitafuta "wewe uko wapi nikufate" akinifata ni direct kwake ku-do tu. Baada ya hapo anaweza asipokee simu au asijibu sms. Na ikitokea kajibu jua kuwa anahitaji. Ukisema basi tutoke tukazungumze kuhusu mahusiano yetu anadai yupo busy.
Je nifanyeje, mapenzi kwangu yamekuwa shubiri, ni miezi miwili sasa mawasiliano yamekatika baina yangu na boyfriend wangu wa mwisho. Je nimekuwa rahisi sana? Lakini mbona nachukua muda mrefu kukubali kutoa tundi labda ungesema ni Easy Going? Msaada wenu ni muhimu kwangu. Samahani kwa maneno mengi. Ahsanteni.