Sijakamatwa wala kushikiliwa na mtu yeyote!

Status
Not open for further replies.

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Wakuu,

Imebidi nitafute internet kukanusha taarifa ya kukamatwa kwangu. Bahati mbaya nimekuta ile thread husika imeshafungwa na imebidi nianzishe mpya.

Ni hivi, sijahojiwa, sijakamatwa wala kushikiliwa na mtu yeyote. Pamoja na matatizo mengi ya kiuongozi ya serikali yetu, siamini kwamba kuna mtu kule serikalini anaweza kuthubutu hata kufikiri kumkamata mtu kwa sababu ya kuuliza swali ambalo halipendi.

Sielewi nia hasa ya taarifa hii. Ama ni mwendelezo wa vitendo vya kujaribu kuichafua JF ili tuonekane sisi ni wazushi ili watu waache kuamini taarifa zetu za hapa hasa kuhusu ufisadi, au ni mwendelezo wa woga ambao umejikita miongoni mwa baadhi ya watanzania katika kuogopa vivuli vyetu (fear of unknown).

Kama ni kwa ajili ya woga, napenda kuwatia moyo watanzania popote walipo kuwa viongozi wetu wakiwatembelea popote mlipo msisite kuwauliza maswali magumu au yanayowakera kwa kuhofia kukamatwa. Kama unaogopa sana kukamatwa, hakikisha huvunji sheria za nchi yetu na nchi nyingine uliopo au utakayotembelea.

Poleni sana kwa wale waliopata usumbufu kwa taarifa hii.

Once again, I assure you that I am safe and well, and I am on my way home in Southampton.


Ni mimi mwanachama mwenzenu,

Kitila.
 
Thanks Kitila, will leave this here for now and merge the two later on. Thank you, by the way, well done for raising EPA issue at the forum yesterday. Have a good day !
 
Wakuu,

Imebidi nitafute internet kukanusha taarifa ya kukamatwa kwangu. Bahati mbaya nimekuta ile thread husika imeshafungwa na imebidi nianzishe mpya.

Ni hivi, sijahojiwa, sijakamatwa wala kushikiliwa na mtu yeyote. Pamoja na matatizo mengi ya kiuongozi ya serikali yetu, siamini kwamba kuna mtu kule serikalini anaweza kuthubutu hata kufikiri kumkamata mtu kwa sababu ya kuuliza swali ambalo halipendi.

Sielewi nia hasa ya taarifa hii. Ama ni mwendelezo wa vitendo vya kujaribu kuichafua JF ili tuonekane sisi ni wazushi ili watu waache kuamini taarifa zetu za hapa hasa kuhusu ufisadi, au ni mwendelezo wa woga ambao umejikita miongoni mwa baadhi ya watanzania katika kuogopa vivuli vyetu (fear of unknown).

Kama ni kwa ajili ya woga, napenda kuwatia moyo watanzania popote walipo kuwa viongozi wetu wakiwatembelea popote mlipo msisite kuwauliza maswali magumu au yanayowakera kwa kuhofia kukamatwa. Kama unaogopa sana kukamatwa, hakikisha huvunji sheria za nchi yetu na nchi nyingine uliopo au utakayotembelea.

Poleni sana kwa wale waliopata usumbufu kwa taarifa hii.

Once again, I assure you that I am safe and well, and I am on my way home in Southampton.


Ni mimi mwanachama mwenzenu,

Kitila.
Kitila,
Happy to know you are safe. I hope the leaders answered the question you asked,what was it about(I mean the way you coined it) and how did they respond?
 
Heshima kwako mkuu,
Kwa kweli nilisikitika kupata taarifa mbaya kiasi hicho.Mkuu,umefanya jambo la busara sana kuja hapa kukanusha, i wish wanasiasa wetu wangekua realistic namna hii i mean kuweka mabo sawa wakati wananchi wanakuhitaji ufanye hivyo.


Ila sasa na huyu ndugu yetu brazameni aje aseme ni nani aliyempa hizi taarifa ili tujue ni nani anaetaka kushusha heshima ya kijiwe hiki.ni vizuri kujua wenye nia mbaya na hili jamvi.

Pia hongera sana kwa kuuliza swali muhimu.Well done bro!
 
Mkuu Kitila amani iwe juu yako! Na pole kwa disturbances ambazo familia, marafiki na ndugu zako wanaweza kuwa wamezipata kutokana na uzushi huu!@!!!
 
Brazamen, sasa ni zamu yako kutueleza nani alikupa taharifa hizo mana tunataka kujua ukweli nani anataka kutuaribia kijiwe ambacho kinaonekana sasa ni nguzo ya watanzania. Tunasubiri mkuu
 
Wakuu,

Imebidi nitafute internet kukanusha taarifa ya kukamatwa kwangu. Bahati mbaya nimekuta ile thread husika imeshafungwa na imebidi nianzishe mpya.

Ni hivi, sijahojiwa, sijakamatwa wala kushikiliwa na mtu yeyote. Pamoja na matatizo mengi ya kiuongozi ya serikali yetu, siamini kwamba kuna mtu kule serikalini anaweza kuthubutu hata kufikiri kumkamata mtu kwa sababu ya kuuliza swali ambalo halipendi.

Sielewi nia hasa ya taarifa hii. Ama ni mwendelezo wa vitendo vya kujaribu kuichafua JF ili tuonekane sisi ni wazushi ili watu waache kuamini taarifa zetu za hapa hasa kuhusu ufisadi, au ni mwendelezo wa woga ambao umejikita miongoni mwa baadhi ya watanzania katika kuogopa vivuli vyetu (fear of unknown).

Kama ni kwa ajili ya woga, napenda kuwatia moyo watanzania popote walipo kuwa viongozi wetu wakiwatembelea popote mlipo msisite kuwauliza maswali magumu au yanayowakera kwa kuhofia kukamatwa. Kama unaogopa sana kukamatwa, hakikisha huvunji sheria za nchi yetu na nchi nyingine uliopo au utakayotembelea.

Poleni sana kwa wale waliopata usumbufu kwa taarifa hii.

Once again, I assure you that I am safe and well, and I am on my way home in Southampton.


Ni mimi mwanachama mwenzenu,

Kitila.

SONGELA ZIGIZIGI MUNTUWA WANE
 
Brazamen, sasa ni zamu yako kutueleza nani alikupa taharifa hizo mana tunataka kujua ukweli nani anataka kutuaribia kijiwe ambacho kinaonekana sasa ni nguzo ya watanzania. Tunasubiri mkuu


Nilisha onya juu ya akina Brazamen, Kada na wenzake kwa kuwa makini kuandika hapa na kuacha kukurupuka kwa hisia .Ninaonya tena kwamba hawa jamaa wanachafua Chama chao cha CCM kwa uzushi kama huu na kutuchafulia jina kama JF na kutuchonganisha na Serikali yetu .Tutasimamia issues na si majungu .Unaweza kuacha kuandika kama huna cha kusema lakini si kuzusha issues .Tabia hizi za uongo za akina shy , na sasa Brazamen ni mbaya na hatari sana .

Hatuna chuki na serikali wala Nchi yetu ila tunasimamia issues.Nilisema na Kitila kabla sijalala na sasa naamka nakuta uongo huu.Unaidhalilisha Serikali kuonekana kwamnab iko low kiasi hiki .Mimi nadhani shitaji clarification toka kwa huyu jamaa .
 
Hivi wanausalama wa Tanzania wana jurisdiction ya kumkamata mtu nje ya nchi? Nadhani tungeishuku hii stori toka mwanzoni.
 
Brazaman

Wewe mbona unaingilia mambo ya huku wakati kule mambo ya kikubwa kunakushinda, usilete UDAKU tena hapa tafadhali. Serikali ya UK hawawezi kufanya ujinga kama huo hapa watu ni makini sana upuuzi kama huo hutokea Zimbabwe na Sehemu nyingine nyingine ambazo bado democacy ni ndoto. Nimeimgia just about an hour lakini nilianza kufuatilia ili kujua whats going on nilitilia mashaka sana habari yako.

Mkumbo keep it up brother.
 
Mkuu Kitila tunashukuru uko salama salimini na umejitokeza kukanusha uzushi uliotokea na zaidi hongera kwa "kumkoma nyani mchana kweupee" mkuu, well done sir!
 
Mkuu Kitila,

Asante sana kwa kuelezea kwamba uko salama. Niliposoma habari ya Brazamen kweli sikuamini, nikachukua simu ili nimpigie balozi moja kwa moja, bahati nzuri upande mwingine ukanisimamisha na kunishauri nipate info zote kabla ya kukurupuka. Ndio nikakumbana na ujumbe wa Lunyungu.

Kitendo cha Brazamen sio kizuri kabisa na kingeweza kukosanisha hata watu. Kumkamata mtu kwa kuuliza swali tena nje ya nchi, ingelikuwa imepita hata yale anayofanya Mugabe. Kwa kweli nilikuwa tayari kushusha imani na huyo mama mpaka sifuri.

Lengo nafikiri ni kuichafua JF ili tuonekane wazushi. Tuwe macho na waangalifu kama tunataka hiki chombo kiendelea kuwa na nguvu.

Nimeandika mara nyingi, adui mkubwa wa JF ni wanachama wake. Kuna wanachama watakuja kuiua JF kwa makusudi au bila makusudi. Lazima tujiandae kuwakabili mapema kuhakikisha hawatumii JF kuendeleza matatizo na frustrations zao binafsi.
 
Nilisha onya juu ya akina Brazamen, Kada na wenzake kwa kuwa makini kuandika hapa na kuacha kukurupuka kwa hisia .Ninaonya tena kwamba hawa jamaa wanachafua Chama chao cha CCM kwa uzushi kama huu na kutuchafulia jina kama JF na kutuchonganisha na Serikali yetu .Tutasimamia issues na si majungu .Unaweza kuacha kuandika kama huna cha kusema lakini si kuzusha issues .Tabia hizi za uongo za akina shy , na sasa Brazamen ni mbaya na hatari sana .

Hatuna chuki na serikali wala Nchi yetu ila tunasimamia issues.Nilisema na Kitila kabla sijalala na sasa naamka nakuta uongo huu.Unaidhalilisha Serikali kuonekana kwamnab iko low kiasi hiki .Mimi nadhani shitaji clarification toka kwa huyu jamaa .

..imeeleweka!
 
brothamen jamani kapotelea wapi? aje kutuambia alizipata wapi??

HUYU NDIE BRAZAMEN

BRAZAMENI

Re: Unaifahamu Jambo Forums?
________________________________________
FIRST RULE OF JAMBO FORUMS, WE DO NOT TALK ABOUT JAMBO FORUMS

SECOND RULE OF JAMBO FORUMS,WE DO NOT TALK ABOUT JAMBO FORUMS
__________________
women DO NOT reward sensitivity and loyalty with sex....be friendly but don't be her friend...


http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=10165
 
HUYU NDIE BRAZAMEN

BRAZAMENI

Re: Unaifahamu Jambo Forums?
________________________________________
FIRST RULE OF JAMBO FORUMS, WE DO NOT TALK ABOUT JAMBO FORUMS

SECOND RULE OF JAMBO FORUMS,WE DO NOT TALK ABOUT JAMBO FORUMS
__________________
women DO NOT reward sensitivity and loyalty with sex....be friendly but don't be her friend...


http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=10165

Mimi nilianza kumdharau tangia nilipo ona jina lake .Mtu wa maana na akili nzuri hawezi kujiita la ajabu ila mtu wa ajabu mwenye maajabu atajiita jina la ajabu .
 
Brazameni,

Hadhi na heshima yako imeshuka kama ya Watawala wetu, na itakuchukua muda mrefu na pengine haitwezakana kurudi tena!

Mod, nadhani huyu Brazameni anastahili kemeo (karipio kali) kama si kufungiwa kwa muda kwa sababu zifuatazo:-

Moja, Brazameni ni miongoni mwa watu ambao kwa 'kutupeleka sokoni' kupitia JF ni kuidhalilisha JF na sisi Wanachama wake;

Mbili, ameipaka matope Serikali yetu tukufu na Taasisi yake muhimu ya Usalama wa Taifa;

Mbili, kwa makusudi kabisa anataka kuifanya JF kuwa kijiwe cha wahuni na watu wasio na kazi wakati sisi tuna uchungu sana na nchi yetu kuliko Chama Tawala (CCM) na baadhi ya Viongozi wetu wa nchi akiwemo Mhe. Rais (bado nina imani naye)wakati ni hapa hapa JF ndipo tulipoanza kuvalia njuga suala la Richmond na BoT kabla hata Bunge halijaingilia kati.

NAOMBA KUTOA HOJA!
Nne
 
Brazameni, najua ulitoa habari kama fununu tu, lakini ni bora u clarify mambo au uombe msamaha hapa hapa mshirika...
 
Brazameni, najua ulitoa habari kama fununu tu, lakini ni bora u clarify mambo au uombe msamaha hapa hapa mshirika...

Honestly speaking, Brazameni should come foward and atlist give some few words!!

What exaclty transpared on his side.

Smone cant just come and giv such sensitive news...with no any motivations!

Brazamen tukusikie..labda sisi ndio hatukuelewi au kuna tunachokukusea...!!

Lakini kimia kizito hakitakuwa dalili njema kwako na kwetu pia!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom