onjwayo
JF-Expert Member
- Apr 8, 2020
- 1,346
- 1,303
Juzi CCM walioonekana kukaa meza moja na familia ya Baba wa Taifa, Mama Maria pamoja watoto wake Makongoro na Madaraka. Dhumuni bado sijaelewa, ila tu kwa sababu ya kampeni nilijua ni kupata huruma ya familia hii. Katika kipindi hiki vihoja na vingi na bila kutokuwa makini unaweza ukafanya mengi mno ya hovyo na mengine ya msingi.
Haijapita hata muda wajumbe wa hiyo hiyo CCM iliwakataa watia nia toka familia hiyo kwa kuwapa jumla ya kura saba tu. Kwa namna nyingine wajumbe wa CCM hawawataki hiyo familia kuwa miongoni mwa wanaongoza katika serikali iwe kwa kura au kwa kuteuliwa. Kwa kuongezea ushahidi, Makongoro alipogombea ubunge wa Afrika Mashariki aliangukia pua licha ya kudumu kipindi cha nyuma alipochaguliwa kwa kuwa ndugu yake Vincent Kiboko alikuwepo bungeni hivyo alishawishi upande mwingine uwapitishe.
Kwa kuhitimisha, ni kwa nini mwenyekiti asingeweza kupindua meza na kuwateua kuwa wagombea kama alivyofanya kwa kina Silinde, Katambi, Gwajima na wengine? Hivi mlimsikia vizuri Mama Maria? Usemi wake ni kuwa walimlazimisha kuongea na hata kuja pale ni kuongeza tu idadi.
Jamani, naomba kama ni kumuenzi Nyerere naye mtendeeni haki kama kina Karume na Mwinyi. Familia hii ibaki kuwa Royal kwa kuheshimiwa na si kutumika katika kampeni tu. Lala pema Baba wa taifa.
CCM mnamchafua Baba wa Taifa
Haijapita hata muda wajumbe wa hiyo hiyo CCM iliwakataa watia nia toka familia hiyo kwa kuwapa jumla ya kura saba tu. Kwa namna nyingine wajumbe wa CCM hawawataki hiyo familia kuwa miongoni mwa wanaongoza katika serikali iwe kwa kura au kwa kuteuliwa. Kwa kuongezea ushahidi, Makongoro alipogombea ubunge wa Afrika Mashariki aliangukia pua licha ya kudumu kipindi cha nyuma alipochaguliwa kwa kuwa ndugu yake Vincent Kiboko alikuwepo bungeni hivyo alishawishi upande mwingine uwapitishe.
Kwa kuhitimisha, ni kwa nini mwenyekiti asingeweza kupindua meza na kuwateua kuwa wagombea kama alivyofanya kwa kina Silinde, Katambi, Gwajima na wengine? Hivi mlimsikia vizuri Mama Maria? Usemi wake ni kuwa walimlazimisha kuongea na hata kuja pale ni kuongeza tu idadi.
Jamani, naomba kama ni kumuenzi Nyerere naye mtendeeni haki kama kina Karume na Mwinyi. Familia hii ibaki kuwa Royal kwa kuheshimiwa na si kutumika katika kampeni tu. Lala pema Baba wa taifa.
CCM mnamchafua Baba wa Taifa