Ruhazwe JR
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 3,403
- 920
Tukiwa kwenye majonzi juu ya mwenzetu aliyetolewa uhai na waporaji wa pumzi, ambao sisiti kuwaita watekaji wa demokrasia watumiwao na kundi la watu wachache wenye kujiharalishia madaraka kwa nguvu ya mtutu, mtutu ambao umenunuliwa kwa kodi ya sisi walala hoi,naona ni vema nirudi kwa upande wa Channel Ten.
Nimekua nikifatilia taarifa zao za hivi karibuni wanaonekana hawako kiuhalisia hasa pale linapokuja swala la uozo wa serikali.Mfano ni ile habari juu ya kifo cha Ally kilichosababishwa na Polisi mjini Morogoro.Walionekana kutoa taarifa kwa kuipendelea polisi na kuikandamiza CHADEMA,lakn siku si nyingi polisi wamepiga hodi kwao tena hodi ya kishindo.
Mimi sisiti kuwaambia na kuwashauri,wakae chini watafakari,kama kuna hongo walipokea kutoka CCM ili wawe wanapotosha kweli na kua ongo basi ni wakati wao hata hili la Iringa wapotoshe.Kama wamekua wakifanya vile kwa sababu ya woga basi wanapaswa waamke sasa nakuchukua hatua kwa vitendo.
Binafsi simjui mmiliki wa channel 10 lakin kama ni kigogo wa CCM nawashauri ndugu zetu wanaofanya kazi huko kuwa maisha ni popote,wakati wao umefika wakimbie mapema.
Narudia tena sifurahii kifo,ila kwa hili mnapaswa kukaa upya na kutafakari.
Nimekua nikifatilia taarifa zao za hivi karibuni wanaonekana hawako kiuhalisia hasa pale linapokuja swala la uozo wa serikali.Mfano ni ile habari juu ya kifo cha Ally kilichosababishwa na Polisi mjini Morogoro.Walionekana kutoa taarifa kwa kuipendelea polisi na kuikandamiza CHADEMA,lakn siku si nyingi polisi wamepiga hodi kwao tena hodi ya kishindo.
Mimi sisiti kuwaambia na kuwashauri,wakae chini watafakari,kama kuna hongo walipokea kutoka CCM ili wawe wanapotosha kweli na kua ongo basi ni wakati wao hata hili la Iringa wapotoshe.Kama wamekua wakifanya vile kwa sababu ya woga basi wanapaswa waamke sasa nakuchukua hatua kwa vitendo.
Binafsi simjui mmiliki wa channel 10 lakin kama ni kigogo wa CCM nawashauri ndugu zetu wanaofanya kazi huko kuwa maisha ni popote,wakati wao umefika wakimbie mapema.
Narudia tena sifurahii kifo,ila kwa hili mnapaswa kukaa upya na kutafakari.