Sifa nyingine ya Augustine Mahiga: Yeye ndiye "Shahidi Y" kwenye kesi ya Uhaini ya mwaka 1982/83

Hans Pope (senior) alikuwa Regional Police Commander, Iringa, kabla ya kupelekwa Mkoa wa Ziwa Magharibi (West Lake Region) ambao sasa ni Kagera. Nakumbuka picha yake ilipochapishwa magazetini hapa nchini, 1972, baada ya kuuawa na askari wa Amin waliomteka Mutukula.

Katika picha ile, mwili wake ulivimba sana. Amin alisema jeshi letu lilikuwa na Wachina na Hans Pope ulikuwa ndiyo ushahidi huo. Hans Pope alikuwa na damu ya Kijerumani, siyo ya Kichaina, ingawa sura yake katika picha ile ilikuwa kama ya "Kichaina" kwa sababu ya kuvimba sana. Naikumbuka sana picha ile. Ilikuwa ukurasa wa kwanza magazetini.

Watoto wake ndiyo hao wawili Zacharia na Harry waliohusika na mpango wa kumpindua Nyerere, 1982, pamoja na wanajeshi wengine.

Zacharia alikuwa captain kikosi cha mabomu na Harry (RIP) alikuwa rubani wa Airwing. Walishawishiwa kuingia kwenye uhaini kwa hisia kuwa Nyerere kumsababisha kifo cha baba yao kwa kumpeleka kuwa RPC Wes Lake Region .
Duh! Na utajiri kautolea wapi wakati alikuwa mtumishi wa serikali? Na huyo Harry yupo hai?
 
Mayalla kama ulikuwa unapendelea kufuatilia kesi unikumbushe kesi ya MTU mmoja anaitwa
(1) Thomas Nzangira alikamatwa kwa kesi ya uhaini kama sio ujasusi nimesahau
(2) dereva taxi muhando aliyewachomekea kesi kina maghee alikuwa anapaki taxi yake Kilimanjaro hotel
Yes nilikuwa napenda kufuatilia kesi, hiyo kesi ya uhaini ya Juma Thomas Zangira pia niliifuatilia.
Ilizungumzwa hapa na humu kuna nyuzi nyingi tuu za kesi hii,
Pamoja Na Ufisadi Wake Wote, Chenge is One of Best Brains Kwenye Bunge Full of Ignorants - JamiiForums

Kesi yenyewe kamili imeripotiwa hapa
Juma Thomas Zangira: Mtanzania wa kwanza kushitakiwa kwa ujasusi - JamiiForums

P
 
Inasemekana Baba yako alikuwa mtu mwena na mwenye akili sana na hata mama yako pia naye alikuwa na uwezo mzuri sana kichwani (Hizi ni habari za wambea). Lakini mbona wewe umekuwa ni mtu wa ajabu na hovyo-hovyo kihivi, au vinasaba vya akili vya wazazi wako vimekuruka wewe na kwenda kwa wajukuu ? Man you're a disappointment.....

NO HARD FEELINGS...........
Mkuu Kataskopos a.k.a MalikomuLumumba,
it's very true, wazazi wangu wote wawili baba, Mzee Andrew Mayalla (RIP) alikuwa ni mtumishi mtiifu wa Idara na mama still alive ni retired now lakini bado ni well taken care na Idara pia ni mtumishi mtiifu wa Idara, but very unfortunately mimi mtoto wao, I'm not!.

Ila sasa baada ya kuitwa kuhojiwa Dodoma na Kamati ya Bunge, sasa nimejitambua na namtafuta Polepole ili nami niunge rasmi juhudi
P
 
Mkuu Kataskopos, it's very true, wazazi wangu wote wawili baba, Mzee Andrew Mayalla (RIP) alikuwa ni mtumishi mtiifu wa Idara na mama still alive ni retired now lakini bado ni well taken care na Idara pia ni mtumishi mtiifu wa Idara, but very unfortunately mimi mtoto wao, I'm not!.

Ila sasa baada ya kuitwa kuhojiwa Dodoma na Kamati ya Bunge, sasa nimejitambua na namtafuta Polepole ili nami niunge rasmi juhudi
P
Sasa baba, kwanza samahani nakuita baba coz wewe kwangu ni baba tu kulingana na umri wako.
Kwanini usiitetee maslahi ya watanzania bali unataka uungane tena na watu wanaotuumiza watanzania?
 
Duh...!.
P
Najuwa ni ngumu sana kueleza namna ambavyo umeweka maamzi kichwani mwako ila jitahidi basi hata kututetea sisi watanzania tunalia sana na vitu vingi mno ambavyo vinatumiiza sana lakini pia nakumbuka mbali sana siku ile unamuuliza rais maswali najuwa kabisa unajuwa ni kwa jinsi gani kuna mambo yanafanyika kinyume na utaratibu ila una vunga tu
 
Mkuu Kataskopos, it's very true, wazazi wangu wote wawili baba, Mzee Andrew Mayalla (RIP) alikuwa ni mtumishi mtiifu wa Idara na mama still alive ni retired now lakini bado ni well taken care na Idara pia ni mtumishi mtiifu wa Idara, but very unfortunately mimi mtoto wao, I'm not!.

Ila sasa baada ya kuitwa kuhojiwa Dodoma na Kamati ya Bunge, sasa nimejitambua na namtafuta Polepole ili nami niunge rasmi juhudi
P
Sawa kaka mkubwa, mimi mdogo wako nikutakie kila la kheri.
 
Stuxnet,

Kwa maoni yangu, upande wa UTETEZI ndiyo uliotia fora ukiongozwa na Wakili MURTAZA LAKHA.

Kwa kweli Murtaza Lakha alikuwa na maswali ya kuwachachafya sana mashahidi wa upande wa mashtaka.

Upande wa mashtaka ulikuwa na wakili anaitwa William Sekule ambaye alifanya kazi nzuri sana ktk kuhitimisha kesi na kuchambua ushahidi na kuuunganisha na washtakiwa.

cc Nguruvi3, Pascal Mayalla
Tunaomba sofy copy ya hiyo kesi jamani.
 
Tunaomba sofy copy ya hiyo kesi jamani.

..kwa bahati mbaya sinayo.

..ila ninaitafuta, na nikiipata lazima niilete hapa JF.

..hata hotuba ya baba wa taifa alipotangaza vita vya uganda niliileta hapa JF baada ya kuipata.
 
..hiki kipande nimekitoa ktk Eulogy aliyoandika Attilio Tagalile kuhusu Agustine Mahiga.

" It was under Dr Mahiga as Director General of the Intelligence and Security that the 1983 abortive coup against Mwalimu Julius Nyerere was foiled. That abortive coup would have been a fait accompli, had 'Daily News' Editor, Reginald Mhango (who has since passed on) not cautioned Abdallah Mhando for not reporting to the authorities what he had heard from his passenger.

When he said he did not know whom he could report to, Mhango linked him with Charles Kizigha who was close to Dr Mahiga and from their own, it was taken over by the Intelligence. The alleged coup leaders were rounded up and later arraigned and after a two-year trial under Principal Judge, Nassoro Mzavas some of the alleged coup plotters were discharged and others were convicted. " -- Attilio Tagalile
 
Kuna mshtakiwa mmoja katika kesi ile ambaye ni miongoni mwa wale tisa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha, Bwana Eugene Maganga(Sasa ni marehemu) aliwahi kumuelezea sana Mzee Mahiga

Alisema kama kuna mtu mmoja unayeweza kusema aliishika kesi, akaipeleleza vizuri, akakusanya ushahidi usioacha hata kivuli cha shaka dhidi yao na kupelekea washtakiwa kutiwa hatiani basi ni Shahidi Y! Alikua mtu mahiri wa kazi yake, mwenye kumbukumbu, anayejua kujieleza na very smart. Walikua wakimhomfia wakati wote wa kesi lakini pia walikua wakim admire kwa uwezo wake

Nilikua nje ya jengo la Mahakama Kuu siku ya hukumu yao 1986. The atmosphere kwa walioachiwa ilikua so emotional.. kuna waliotoka mbio, kuna waliokimbilia kanisani. Sara Banyikwa alinitoa machozi. Alipotoka nje ya jengo la Mahakama alilakiwa na ndugu na jamaa miongoni mwao ni mwanae mdogo wa kike aliyekua na miaka chini ya kumi. Alijaribu kumbeba mwanaye huyo lakini masikini hakuweza!!! Alikua amedhoofu sana na aliishia kumkumbatia kwa muda mreefu sana

Wengi ya waliohukumiwa wamefariki baada ya kuachiwa kwa msamaha wa Rais 1993 akiwemo Hatibu Gandhi(Hatty McGhee), Captain Suleiman Matusela "Commando" na Captain Eugene Maganga. Hata aliyetakiwa kua mshtakiwa namba moja kabda ya kutoroka, Pius Mutakubwa Lugangira au "Father Tom" ambaye pia alikua ndio mastermind na paymaster wa huo mpango naye alifariki (natural death) akiwa nchini Uingereza

Wakati ule pamoja na kua na nyenzo duni "kitengo" kilikua na watu wenye weledi wa hali ya juu sana kwasababu kwanza vetting kwa maofisa wake ilikua fair na yenye kuzingatia mahitaji halisi ya nafasi anayopaswa muhusika kuitumikia
 
Sasa baba, kwanza samahani nakuita baba coz wewe kwangu ni baba tu kulingana na umri wako.
Kwanini usiitetee maslahi ya watanzania bali unataka uungane tena na watu wanaotuumiza watanzania?

If you can't beat them, join them.​

 
Je, Augustine Mahiga ndiye "Shahidi X" kwenye kesi maarufu ya uhaini ya mwaka 1983?

Yasemekana alikuwa na kumbukumbu mujarab zilizowezesha kuwasambaratisha washtakiwa.

Kitabu cha Kesi ya Uhaini kilitoka mwaka 1985 kilichokuwa kimeandikwa na Marehemu Mnenge S. Suluja. Mhusika mkuu wa washtakiwa alikuwa Thomas Lugangira au ‘Uncle Tom’. Wenzake walikuwa ni Hatibu Gandi au ‘Hatty Mac Ghee’, Kapteni Mohammed Tamim, Kapteni Mbogoro, Kapteni Christopher Kadege, Luteni Badru Rwechungura Kajaja na Kapteni Mapunda.

Wengine walikuwa ni Banyikwa na mkewe, Christopher Ngaiza, Zacharia Hans Pope, Kapteni Rodrick Rosham Robert, na Eugene Maganga. Kingine kilichokuwa very interesting kwenye kesi ni baadhi ya wana usalama kutumia Alphabet kuji-indetify badala ya majina yao yaani walikuwa Mr. X Kama Mabere Marando, Dr. Hassy Kitine, na Mr Y Dr Augustine Mahiga, nadhani pamoja na Mizengo Pinda nk.

Washtakiwa 9 Kati ya 16 Walihukumiwa kifungo cha maisha. Na Jaji Nassoro Mzava. Mwaka 1993 Walitoka kwa Sababu ya Tanzania kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi hivyo wafugwa wa kisiasa walipaswa kutoka Lakini Hatty MCghee alitoka akiwa mahtuti na akafariki Hospital MCghee aliwahi kutoroka pamoja na Uncle Tom lakini akadakiwa Horohoro Tanga. Mawakili Waliotia Fora ni Hussein Muccadam(RIP) Murtaza Larkha, Jadeja Wote walikuwa wa Asia.
Kitabu kinapatikana wapi?
 
Back
Top Bottom