Sifa nyingine ya Augustine Mahiga: Yeye ndiye "Shahidi Y" kwenye kesi ya Uhaini ya mwaka 1982/83

Juma Thomas Zangira alikuwa mtu wa intelligence miaka ya mwanzo ya Uhuru wetu wa Bendera, na alikuwa karibu sana na Oscar Kambona. Alikuja kufungwa baadae na alipotoka ndio akawa na kibarua pale Kilimanjaro Hotel enzi hizo.
Alihukumiwa kwa kesi ya espionage au uhaini, kwa makosa ya kuwasiliana, kukusanya taarifa za siri kati ya mwaka 1971-1977 na mzungu John Wilson kuhusu msimamo wa Tanzania ktk nchi za Rhodesia na mtazamo wa Nyerere ktk maswala ya uchumi wa nchi.

Huyo mzungu John Wilson alikuwa (alijifanya) mfanyabiasha. Hata hivyo hukumu yake ya miaka 20 jela ilitenguliwa na majaji Nyalali, Kisanga, Lugakingira wa Mahakama ya Rufaa hadi miaka 13. Sababu walishindwa kuproove kimaandishi maelezo aliyokuwa akimtumia huyo John Wilson. Zilipatikana barua za huyo mzungu tu wala si JWTZ. Na yeye alisema aliyokuwa akimwambia ni mambo ambayo hata vyombo vya habari magazeti, radio vilikuwa vikiripoti. Ukaonekana ni ushahidi then kifungo kikapungua ila alionekana ni tishio kwa usalama wa taifa, Tanzania law report 1980.
Nashukuru sana kwa hii stori maana enzi zile nilikuwa darasa la tatu na gazeti lilikuwa Uhuru naishia kusomaa habari za chakubanga basi
 
Mkuu Joka Kuu umenikumbusha mbali!

Tulikuwa tunaishi Drive In Estate, mafleti next to Banyikwas, nyumba zimeungana na kutenganushwa na ukuta. Mzee wa Kihangaza, mke Mhangaza, alikuwa na mabinti 4 bomba sana!, Hope, Daines, Betty na Ngola na kaka yao mmoja Mzomu. Hapo ndipo vikao vilipo fanyikia!.

Kesi hiyo ilikuwa na similarities nyingi na Kesi ya Mauaji Mwanza, Mzee wangu, Andrew Mayalla ndio alikuwa RSO wa Mwanza, Jaji alikuwa Nassor Mzavas, DPP alikuwa William Sekule, Mzee wangu alitetewa na wakili Murtaza Lakha, ndie pekee alichomoka, wengine wote walikula mvua nyingi!.

Murtaza Lakha alinifanya nitamani kuwa wakili, by then ukikosa 1st class forget law, ndio nika-opt journalism, he was the best na mpaka sasa bado sijaona wakili yoyote Tanzania aliye vaa viatu vyake!.
P
JokaKuu katika kesi ya uhaini mimi nilikuwa mshabiki wa Hussein Muccadam(RIP).
Nilikuwa navutiwa sana na ujenzi wake wa hoja. Lakha of course alikuwa ni kiboko na hao ndio walioamsha watu wengi kuhusu ''taaluma ya uwakili'' na umuhimu wao katika kesi.

Bado sijaona wa kiwango cha Marhum Muccadam au Murtaza Lakha. Hawa walikuwa 'next level'
 
JokaKuu katika kesi ya uhaini mimi nilikuwa mshabiki wa Hussein Muccadam(RIP).
Nilikuwa navutiwa sana na ujenzi wake wa hoja. Lakha of course alikuwa ni kiboko na hao ndio walioamsha watu wengi kuhusu ''taaluma ya uwakili'' na umuhimu wao katika kesi.

Bado sijaona wa kiwango cha Marhum Muccadam au Murtaza Lakha. Hawa walikuwa 'next level'

..Hawa mawakili walikuwa wanatetea washtakiwa tofauti ktk kesi ile.

..Kwa hiyo ni vizuri wenye kumbukumbu wakatuhabarisha kuhusu timu ya mawakili wa utetezi na washtakiwa waliokuwa wakiwatetea.

..Lakini pia kuna umuhimu wa kuwajua mawakili wa upande wa mashtaka kama William Sekule, Johnson Mbwambo, Kulwa Masaba, na wengine.
 
JokaKuu jambo la kushangaza ni kuwa kesi ilikuwa wakati wa chama kimoja, RTD, Mzalendo, Sundy News, Daily News, Uhuru na Mfanyakazi.

Gazeti kinara lilikuwa Mfanyakazi, liliandika kila neno kutoka mahakamani.
Nilishangazwa sana na uwazi kiasi kwamba hata mambo mengine nyeti yalikuwa yanaandikwa.

Nani anawakumbuka wahariri na waandishi wa Mfanyakazi! Timu ya habari ilikamailika.

Bado sikumbuki vizuri Tamim aliuawa vipi. Sijui kama ilikuwa ukomandoo au walim-set
 
JokaKuu jambo la kushangaza ni kuwa kesi ilikuwa wakati wa chama kimoja, RTD, Mzalendo, Sundy News, Daily News, Uhuru na Mfanyakazi.

Gazeti kinara lilikuwa Mfanyakazi, liliandika kila neno kutoka mahakamani.
Nilishangazwa sana na uwazi kiasi kwamba hata mambo mengine nyeti yalikuwa yanaandikwa.

Nani anawakumbuka wahariri na waandishi wa Mfanyakazi! Timu ya habari ilikamailika.

Bado sikumbuki vizuri Tamim aliuawa vipi. Sijui kama ilikuwa ukomandoo au walim-set

..kuhusu Mohamed Tamimu.

..nadhani alikuwa Captain jeshini.

..kwa kumbukumbu zangu alifuatwa na wanausalama mahali alipokuwa anaishi.

..kama sikosei alipotoka mlangoni kuwaona waliomfuata akaamua kukimbia na kuruka ukuta wa uani alipokuwa akiishi.

..wanausalama walianza kumkimbiza na yeye alielekea eneo la barabara ya Morocco.

..alipofika barabarani akadandia gari lililokuwa limebeba bia ambapo alianza kuwarushia chupa za bia jamaa waliokuwa wakimkimbiza.

..wanausalama walimrushia risasi na kumjeruhi. Inasemekana alikimbizwa hospitali na alipofika huko alikuwa amekwisha kufa.

..kuna wanaosema Tamimu alitoroka jeshini akiwa Uganda na aliingia nchini kinyemela toka Kenya na kuanza kupanga mipango ya mapinduzi.

..Taarifa nyingine zinasema Tamimu alikuwa mlinzi wa Raisi Professor.Yusuf Kironde Lule na taarifa zake zilikuwa zinajulikana na wakubwa zake jeshini.
 
JokaKuu jambo la kushangaza ni kuwa kesi ilikuwa wakati wa chama kimoja, RTD, Mzalendo, Sundy News, Daily News, Uhuru na Mfanyakazi.

Gazeti kinara lilikuwa Mfanyakazi, liliandika kila neno kutoka mahakamani.
Nilishangazwa sana na uwazi kiasi kwamba hata mambo mengine nyeti yalikuwa yanaandikwa.

Nani anawakumbuka wahariri na waandishi wa Mfanyakazi! Timu ya habari ilikamailika.

Bado sikumbuki vizuri Tamim aliuawa vipi. Sijui kama ilikuwa ukomandoo au walim-set
Kulikuwa uwazi wa kuandika habari na uhuru wa Mahakama kuliko sasa hivi.

Japo ilikuwa Serikali ya chama kimoja Majaji hawakuingiliwa na aliyewateua
 
JokaKuu katika kesi ya uhaini mimi nilikuwa mshabiki wa Hussein Muccadam(RIP).
Nilikuwa navutiwa sana na ujenzi wake wa hoja. Lakha of course alikuwa ni kiboko na hao ndio walioamsha watu wengi kuhusu ''taaluma ya uwakili'' na umuhimu wao katika kesi.

Bado sijaona wa kiwango cha Marhum Muccadam au Murtaza Lakha. Hawa walikuwa 'next level'
True, hawa wote walikuwa na asili ya India, wapo tunao kina Prof Issa Gullam Hussein Shivji. Murtaza Lakha na Hussein Muccadam walibobea kwenye criminal litigations Shivji amebobea kwenye Katiba.

P
 
..Hawa mawakili walikuwa wanatetea washtakiwa tofauti ktk kesi ile.

..Kwa hiyo ni vizuri wenye kumbukumbu wakatuhabarisha kuhusu timu ya mawakili wa utetezi na washtakiwa waliokuwa wakiwatetea.

..Lakini pia kuna umuhimu wa kuwajua mawakili wa upande wa mashtaka kama William Sekule, Johnson Mbwambo, Kulwa Masaba, na wengine.
Mkuu JokaKuu,
Hao mawakili wa serikali upo sawa kasoro huyo Mbwambo siyo .
Ni Johson Mwanyika ndiye aliyekuwa wakili.
Mbwambo ni mwanahabari.
 
Nani anawakumbuka wahariri na waandishi wa Mfanyakazi! Timu ya habari ilikamailika

Kama sikosei mhariri wa gazeti la mfanyakazi wakati huo alikuwa marehemu HAMID NZOWA na huyu marehemu Richard Ndassa pia akifanya kazi kwenye gazeti lile!!
 
Mkuu Joka Kuu umenikumbusha mbali!

Tulikuwa tunaishi Drive In Estate, mafleti next to Banyikwas, nyumba zimeungana na kutenganushwa na ukuta. Mzee wa Kihangaza, mke Mhangaza, alikuwa na mabinti 4 bomba sana!, Hope, Daines, Betty na Ngola na kaka yao mmoja Mzomu. Hapo ndipo vikao vilipo fanyikia!.

Kesi hiyo ilikuwa na similarities nyingi na Kesi ya Mauaji Mwanza, Mzee wangu, Andrew Mayalla ndio alikuwa RSO wa Mwanza, Jaji alikuwa Nassor Mzavas, DPP alikuwa William Sekule, Mzee wangu alitetewa na wakili Murtaza Lakha, ndie pekee alichomoka, wengine wote walikula mvua nyingi!.

Murtaza Lakha alinifanya nitamani kuwa wakili, by then ukikosa 1st class forget law, ndio nika-opt journalism, he was the best na mpaka sasa bado sijaona wakili yoyote Tanzania aliye vaa viatu vyake!.
P
Ukikosa first class kwenye nini?
 
Stuxnet,

Kwa maoni yangu, upande wa UTETEZI ndiyo uliotia fora ukiongozwa na Wakili MURTAZA LAKHA.

Kwa kweli Murtaza Lakha alikuwa na maswali ya kuwachachafya sana mashahidi wa upande wa mashtaka.

Upande wa mashtaka ulikuwa na wakili anaitwa William Sekule ambaye alifanya kazi nzuri sana ktk kuhitimisha kesi na kuchambua ushahidi na kuuunganisha na washtakiwa.

cc Nguruvi3, Pascal Mayalla

Kiongozi Jokakuu, nadhani William Sekule alikuwa ndiye DPP kwa wakati huo. Hv sasa ni jaji mstaafu. Nadhani sijakosea.
 
Kumbe Mizengo ni kitengo?
Pinda yupo apo
tapatalk_1588448418303.jpeg
 
Ni kweli Mahiga alikuwa ni hazina kubwa sana ktk Nchi yetu ya TZ katika masuala ya Diplomasia.Ila sielewi kwa nini Mhe.Rais alimbadilisha Wizara.
Wizara ina safari nyingi sana ile na mzee wetu tayari alianza kuonesha kuchoswa na maradhi
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom