Nashukuru sana kwa hii stori maana enzi zile nilikuwa darasa la tatu na gazeti lilikuwa Uhuru naishia kusomaa habari za chakubanga basiJuma Thomas Zangira alikuwa mtu wa intelligence miaka ya mwanzo ya Uhuru wetu wa Bendera, na alikuwa karibu sana na Oscar Kambona. Alikuja kufungwa baadae na alipotoka ndio akawa na kibarua pale Kilimanjaro Hotel enzi hizo.
Alihukumiwa kwa kesi ya espionage au uhaini, kwa makosa ya kuwasiliana, kukusanya taarifa za siri kati ya mwaka 1971-1977 na mzungu John Wilson kuhusu msimamo wa Tanzania ktk nchi za Rhodesia na mtazamo wa Nyerere ktk maswala ya uchumi wa nchi.
Huyo mzungu John Wilson alikuwa (alijifanya) mfanyabiasha. Hata hivyo hukumu yake ya miaka 20 jela ilitenguliwa na majaji Nyalali, Kisanga, Lugakingira wa Mahakama ya Rufaa hadi miaka 13. Sababu walishindwa kuproove kimaandishi maelezo aliyokuwa akimtumia huyo John Wilson. Zilipatikana barua za huyo mzungu tu wala si JWTZ. Na yeye alisema aliyokuwa akimwambia ni mambo ambayo hata vyombo vya habari magazeti, radio vilikuwa vikiripoti. Ukaonekana ni ushahidi then kifungo kikapungua ila alionekana ni tishio kwa usalama wa taifa, Tanzania law report 1980.