Uchaguzi 2020 Sifa Bora alizonazo Tundu Lissu zitakazomfanya kuwa Rais wa JMT

Aangalia tu idadi ya comments na views za mada zinazuhusu Lisu utagundua kuwa chadema iko Death bed.Angalia hata hii tu
Mmh! Unajipa moyo kwa idadi feki za duplications za wana fc lumumba?? Mitandaoni tunaongoza, mitaani ndio usipime. Mnaishia kusema ooh wapinzani wa mitandaoni.
 
Tundu Lissu sio tu ni jasiri bali pia ana uwezo mkubwa wa kiakili. Ana utulivu wa moyo na akili. Ana uwezo wa negotiation na hashindwi. Haamini ktk visasi na malipizo ya mabomu, bunduki, mapanga na aina nyingine za mateso na manyanyaso.
Umemaliza .
 
Kama wewe ni mfatiliaji wa siasa za Tanzania na Afrika utakubaliana na mimi kuwa kwa muda mrefu sasa tumekuwa tukikosa kiongozi bora wakuongoza watanzania kwa maslahi ya taifa na wala sio vyama na wanaompa vyeo.

Tulipata janga kama taifa baada ya kuongozwa na Mh Rais Magufuli ambaye aliokota urais kama embe chini ya mnazi kwa kupewa na wale wanaoitwa wenye nguvu.

Matokeo yake nchi imekuwa ni vilio vitupu, hali mbaya ya uchumi na uliopo kuwa wa makaratasi tu. Hali mbaya ya amani, upendo kufifia na hofu kutawala nchini.

Sasa kila mtu anahaha namna ya kumwondoa huyu aliyeshika mizizi pasipo kuwa na mvuto kwa watanzania. Mwaka 2015 nchi yetu iliingia katika janga la kiurais kwa kumpata Rais asiyekuwa na uwezo wa kudumisha utawala wa kisheria, kuheshimu katiba na uhuru wa kisisasa, Kiuchumi na kijamii.

Baada ya kilio cha miaka 5 sasa, mwenyezi Mungu anatuletea rais bora kabisa mwenye sifa zifuatazo. Na ana uwezo wa kurejesha matumaini ya watanzania.

Si mwingine ni Tundu Antiphas Mugwai Lissu mbobevu ktk fani ya sheria, mwenye upendo na uzalendo wa kweli ktk nchi yake.

Sifa zifuatazo zitampa Urais TL kwani watanzania wote wanamjua na kumfahamu vizuri asiyekubaliana nazo ana lake binafsi.

1. Ni kiogozi shupavu na jasiri, hili litamwezesha kufabya maamuzi magumu na yenye tija kwa taifa. Wananchi wanaamini hataishia maneno ya majukwani tu bali atatenda kwavitendo na sio maigizo kama ya Rais Mafufuli.

2. Ana uzoefu unaohitajika kuwa Rais. Watanzania wanajua Mh Tundu Lissu ana uzoefu na serikali zote zilizopita kuanzia ya Mwinyi hadi ya Magufuli. Madhaifu ya kiuongozi ni yale yale miaka yote. Na hakuwahi kubadilika ktk misimamo yake ya kusimamia utawala bora, haki na wajibu.

3. Uwezo wa kutuvusha kiuchumi. Mhe Tundu Lissu anafahamika vyema kama mpambanaji wa maslahi kwa wananchi. Anajua vyema changamoto za maisha ya wananchi. Sio kujenga fly over ya mita 500 ubungo na kwenda kuimbia nyimbo tandahimba! INAHUSU!!

4. Yupo tayari kuwa amiri jeshi mkuu wa Tanzania. Kama anavyofahamika vema kwa vyombo vyote vya dola kuwa ni kiongozi shupavu. Asiyeyumbishwa na siasa za chuki, uhasama na kuburuzana. Ni mwanasheria aliyebarikiwa kuitendea haki taaluma yake. Ni mfano bora kwa wote wanaovutiwa kusoma taaluma ya sheria. Hata hivyo ni kiongozi mwema na mwenye ushirikiano, heshima, busara na utulivu wa kiakili kama sifa bora ya kuwa amiri jeshi mkuu.

5 . Ni msema kweli. Hili ni sifa bora kabisa ktk utawala wa dunia ya kwanza zilizoendelea. Hawezi kusema kuwa tatizo halipo kwa kulificha. Mdororo wa uchumi na uhusiano wa kimataifa umekuwa ndio wimbo wake siku zote kiasi mahasimu wake wasiopenda ukweli kumwinda na pengine kutaka kuondosha uhai wake. Lisu ni mpenzi wa Mungu kweli kweli.

Karibu Mh Tundu Lissu wewe ni yule ajaye Unayesubiliwa kwa miaka nenda Rudi.
6 msaliti wa taifa
 
Cheyo, kwa herufi kubwa, aeleza sifa mbaya aliyonayo T.A.L.
Cheyo ni kipimo bora kabisa cha mzee mpumbavu. Kama anamkubali magu kwa kiwango hicho sii ajiunge kabisa na ccm?
Unamsifu MTU hadi mwenyewe unayemsifu anakuona mpuuzi! Uzee wa aina hii ni bora MTU usiufike ujifie tuu kuliko kupeleka mvi zako kwa aibu kaburini.
 
Cheyo= CCM hana jipya huyo mzee.Mpaka sasa anakufa maskini alikubali siasa za kutumika.
Mwenzake huyu hapa
FB_IMG_1594573587894.jpg
 
Unalishwa maneno nawe unayala tuu bila kutafakari. Huo ni upumbaf kwa binadamu mwenye ubongo kufanya
Hawana hoja hata moja ya kumpinga Lissu. He is very clean. Wamebaki kuokoteza vimaneno vya jumlajumla tu.
 
TUNDU LISSU NI MGONJWA WA AKILI,KWELI AWE RAIS WA TANZANIA!?,.HUYU LISSU MBABAISHAJI NA MPIGA POROJO?!, LABDA AWE RAIS WA YANGA AU WA SIMBA,KUWA RAIS WA TANZANIA,NI NDOTO ZA MWENDAWAZIMU,
 
Hiyo ni myth. Jpm alipata urais kutokana na mizengwe iliyokuwepo kati ya Membe na Lowasa. Aliuangukia tu kwa bahati. Muone anavyojifanya mjanja lakini hana lolote
Sasa hivi anatumia hela nyingi na kujipendekeza kwa wasanii ili wamuimbe akidhani ndio atakubalika. Anachofanya ni kuwaharibia tuu hao watoto vipaji na nyota zao.
Siasa za kisanii au usanii wa kisiasa haujawahi kumuacha MTU salama. Kumbuka kina Mallow, Msechu nk
 
Back
Top Bottom