Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Niko katika mahusiano ya kimapenzi na mdada mmoja kwa takribani mwaka mmoja na nusu sasa. Na kwa kweli tangu niwe na huyu mpenzi wangu hatujawahi kutatizana sana na pia ni mtu tunayependana sana. Ndugu na jamaa kwa pande zote wanaelewa uhusiano wetu. Kutokana na mipangilio yangu nilipanga kumu-engage huyu mpenzi wangu tarehe 24 July mwaka huu tena kwa kum-surprise, nilipanga tarehe hii kwa makusudi kabisa kwani kwangu mimi ni tarehe inayobeba matukio mazito na muhimu katika maisha yangu. Lakini kwa muda wa mwezi mmoja sasa nimekuwa katika dilema kiasi kwamba nahisi kama ahadi ya kumu-engage huyu mpenzi wangu naweza kuifuta muda wowote.
Sababu kubwa ni kuwa nimekutana na binti mwingine ambaye sina jinsi ya kumuelezea hapa nikaeleweka.Tulikutana katika mkutano wa kikazi Arusha na nikajikuta navutika kwake. Kifupi kwa vigezo vyangu ni mzuri wa sura na umbo, yuko hot kimapenzi nakosa wa kumfananisha naye, ana akili ya maisha ni mshauri wa aina yake. Kifupi katika muda mfupi niliokuwa naye amenifanya nipagawe.
Kumbuka nina mtoto wa kike wa miaka 9 niliyezaa na mwanamke mwingine yuko shule grade 4 hapa Dar na huyu dada amenishawishi tumtafutie shule moja ya boarding Arusha na hata ada yuko tayari kulipa kwani kwa habari nilizopata hiyo shule hata fee yake ni ndefu pia. Najikuta nayumba sana ingawa mchumba wangu mtarajiwa bado hajagundua kinachoendelea lakini nahisi muda si mrefu yatasanuka tu. Maana kinachonitokea ni kama napoteza hisia kwa huyu mchumba mtarajiwa. Mimi ni mtu wa misimamo sana lakini katika hili najiona nimepigwa bao sielewi ni mapenzi tu au kuna zaidi ndani yake. ameniomba kama niko tayari kuwa naye kwa karibu afanye mpango wa kupata uhamisho wa kikazi ili aje huku Dar...sijampa jibu ingawa ndio hivyo simu kila siku kutwa mara 4, are you ok sweet, umekula nini leo mchana, umeshalala au uko wapi unafanya nini na nani? Ili mradi mambo kedekede..
Sababu kubwa ni kuwa nimekutana na binti mwingine ambaye sina jinsi ya kumuelezea hapa nikaeleweka.Tulikutana katika mkutano wa kikazi Arusha na nikajikuta navutika kwake. Kifupi kwa vigezo vyangu ni mzuri wa sura na umbo, yuko hot kimapenzi nakosa wa kumfananisha naye, ana akili ya maisha ni mshauri wa aina yake. Kifupi katika muda mfupi niliokuwa naye amenifanya nipagawe.
Kumbuka nina mtoto wa kike wa miaka 9 niliyezaa na mwanamke mwingine yuko shule grade 4 hapa Dar na huyu dada amenishawishi tumtafutie shule moja ya boarding Arusha na hata ada yuko tayari kulipa kwani kwa habari nilizopata hiyo shule hata fee yake ni ndefu pia. Najikuta nayumba sana ingawa mchumba wangu mtarajiwa bado hajagundua kinachoendelea lakini nahisi muda si mrefu yatasanuka tu. Maana kinachonitokea ni kama napoteza hisia kwa huyu mchumba mtarajiwa. Mimi ni mtu wa misimamo sana lakini katika hili najiona nimepigwa bao sielewi ni mapenzi tu au kuna zaidi ndani yake. ameniomba kama niko tayari kuwa naye kwa karibu afanye mpango wa kupata uhamisho wa kikazi ili aje huku Dar...sijampa jibu ingawa ndio hivyo simu kila siku kutwa mara 4, are you ok sweet, umekula nini leo mchana, umeshalala au uko wapi unafanya nini na nani? Ili mradi mambo kedekede..