Sidanganyiki - Leo ndio mnajua Tanzania inahitaji katiba mpya?

Mzee Mzima Mwanakijiji, habari zaasubuhi??

Vipi, nyumbani kwema??? Maana naona bado ni asubuhi hata kukusingizia jamaa atakua kalewa naona aibu hata kusema. Hizi kisrani na ufanano kati yako na Malaria Sugu na kwa muda ule ule mzee eehhh?? Au hizi ID zote mbili ni za kwako mzee.

Busara zinatuelekeza hivi, ukiona swala wakitimka katika kundi kubwa wakitoka porini walikojizoelea huku wakijaribu kunyang'anyana mlango na wewe nyumbani kwako WALA HUHITAJI KUULIZA KUNANI HUKO KWAO PORINI. Cha msingi na wewe timkia tu ndani mara moja ukingoja sasa SIMBA huenda akakugeuza kitoweo. Ndani ya chama kilichokua salama yetu sote Tanzania kumeingiliwa na MDUDU WA AJABU mzee. Ndio maana unaona hata na wazee wetu Mzindakaya Majiyatanga ambao kisiasa bado ni Vijana wadogo tu wamejiamulia kujitunzia heshima zao kwa kwenda nyumbani mapema. Hivi MM pamoja na MS niseme nini ndio tuelewane hapa???

Mada ya katiba yaliopamba moto hivi sasa wala halina jina nyingine bali ni kwamba Tanzania TUMETIWA AIBU KUBWA kimataifa na wanasiasa waroho na MAFISADI ambao kila kitu mali hakiwapiti mbali. Hebu angalia sasa hivi wanavyohangaika KUTAFUTA FEDHA ZA KUJA KUNUNULIA UCHAGUZI WETU 2015 yaani ni fedheha tupu na hawawezi kuyazuia tena kuonekana wazi mezani kwa sababi ni kwamba walishayasuka hivyo ni kuendelea kufumuka tu machoni mwetu.

Mwanakijiji swali lako halimtii shaka sana mwenye ananeemeka na CCM- Mafisadi ya sasa hivi. Lakini ukumbuke kwa CCM-Uadilifu wote tunawafahamu hadi dakika hii na ile CCM-Yatima ambayo nayo ni sampuli nyingine ya mafisadi ila tu wamefungiwa nje kwa sasa kwa sababu hawana vinasaba na wanamtandao nao pia tunawatambua bila kujali dini zao, Ubara wala Visiwani!! MM, Mwizi ni mwizi tu hata Lowassa hawezi kujificha nyuma ya madhabahu na tukamkubalia kamwe. Nitakushangaa sana, sawa sawa na ninavyomshangaa rafiki yangu MS ambaye pia nahisi ni wewe wewe hapo, kwamba badala ya kuona madai ya katiba kwa sasa ni matokeo ya wizi uliokithiri kila pembe ya nchi, kiburi cha sokwe mtu na dalili za mzaha kwa mambo ya msingi, yeye akawa anaona madai ya mabadiliko kwetu sisi vijana kwa sasa chini ya mawani ya udini - HOW MYOPIC here mzee??

Mwisho, ninalo swali rahisai tu, je huwa kuna KIPINDI FULANI KATIKA MAJIRA HIZI ZA MWAKA ambazo mtu au watu wakidai katiba ndio sahihi?? Ukumbuke wewe unahisi kana kwamba huenda umeshiriki kudai sana katiba kwa kalamu yako kipindi kirefu sasa lakini hilo tu peke yake haikupi uhalali wa kuhoji hata kidogo Mtanzania yeyote atakayejiamulia kudai katiba mpya hata kuanzia wiki ijayo.

Nadhani tuko pamoja rafiki yangu mwana-JF mwenzangu.
guuuuuud. nilikuwa napishana maneno na mmoja kati ya waandishi wa gazet la MWANAHALISI hili toleo la tarehe 08/12.2010
na ugomvi wangu na yeye ni swali langu kwake kwamba (ni kweli mnadai katiba mpya kwa maslahi ya taifa au mna agenda nyingine ya kutaka kutambuliwa kama wanaharakati waliofanikisha uwepo wa katiba mpya??) alishindwa kunijibu na akahamia katika kutoa maneno machafu kwamba nami ni msujudia watawala!!!!!
hapa anachotuthibitishia MWANAKIJIJI ni ule wasiwasi wangu kuwa kuna watu wanataka waje wapate nafasi katika serikali zijazo kutokana na mchango wao katika kudai katiba mpya na mwisho wa siku waje kuwa MAFISI na MAFISADI.hawa ni mafisadi watarajiwa ambao wanaona kama wanaporwa nafasi yao ya kuwa WACHANGIAJI WAKUU katika mchakato wa kuelekea kuundwa kwa katiba mpya na hivyo wanaona kama vile malengo yao ya kisiasa(KIFISADI) YANAINGILIWA NA WATU KAMA MKAPA,JAJI MKUU NA WENGINE WENGI WATAKAOJITIKEZA.
Mwanakiji na wenzako wa aina yako mmejawa na tamaa kiasi cha kuwa tayari hata kuitupa na kuisagasaga dhamira yenu mlioipigania kwa muda mrefu(KATIBA MPYA), eti kisa tu......... mtakuwa avershadowed.
acheni ubinafsi,,, muundo mpya wa katiba ni muhimu kwa taifa zima bila kujali ni nani alifanikisha
 
Je kweli tatizo la Tanzania ni ukosefu wa katiba mpya au tuna matatizo mengine makubwa sana?

Kama nchi tuna sheria mbalimbali ambazo zimetungwa kupitia bunge. Katika sheria hizi zipo nyingi tu ambazo ni nzuri sana lakini je zimetusaidia nini sisi kama Watanzania? Kwanini tumeshindwa kuzitekeleza kwa vitendo? Kwanini tunaendelea kuwa maskini na wajinga wa kutupwa pamoja na juhudi za watu mbalimbali kujaribu kusaidia?

Mfano kuna sheria mbalimbali za rushwa ambazo hazifanyi kazi. Kuna sheria ya gharama za uchaguzi ambayo baadhi ya sisi tulioshiriki siasa za 2010 tuliona ingefaa lakini tukashuhudia hao hao walioitunga wakivua nguo zao na kuivunja bila hata aibu. Je tuna uhakika gani hiyo katiba mpya haitavunjwa hivyo hivyo?

Binafsi naamini katiba mpya sio suluhisho na wala haitatusaidia. Tupiganie elimu na uchumi bora kwani ndio vitu pekee ambavyo vitamfanya Mtanzania ajikomboe na kuwa huru hata kuona katiba aliyo nayo haimfai. Kwasasa ni wasomi wachache na wanasiasa ambao wanaona umuhimu wa katiba mpya lakini watu wetu wengi wako busy kuhangaika na watakula nini? Watatibiwa wapi? na watapeleka watoto wao wapi kusoma? Watu kama hao hata wakipata katiba nzuri sidhani kama wako katika nafasi ya kuilinda na kuhakikisha inafuatwa.

....

Kwa Tanzania, uchaguzi wa mwaka huu umeonyesha wazi wananchi wamechoshwa na uchumi duni na siasa za ubabaishaji. Wanataka mabadiliko katika maisha yao. Wanataka chakula nyumbani, wanataka hospitali, wanataka shule. Labda ni muda muafaka kuleta uhuru wa kiuchumi kwa wananchi wetu kabla hata ya kuleta katiba mpya. Labda tupiganie haki ya wananchi wetu kushiriki kwenye uchumi wao, kuhakikisha ajira zinatolewa kwa Watanzania. Kama hayo mambo hayawezi kufanyika mpaka tuwe na katiba mpya basi labda kuna haja ya hiyo katiba mpya. lakini kwa mimi naona leo hii hata tuletewe katiba iliyoandikwa vizuri namna gani, kama hatuna watu wengi ambao wako tayari kuitetea na kuilinda bado tutaendelea kukwama pale pale.

Mtanzania, shukrani kwa mchango wako.

Kuhusu suala la Katiba Mpya (KM)... umetoa hoja zako ambazo sina haja ya kuzirudia. Lakini, tunashindwa kuingiza kifungu cha uwajibishwaji wa viongozi? Maana'ke inaonekana watu wenye nyadhifa wanafanya mambo kama wanavyotaka, kwasababu wana "uhakika" kuna upuuzi kwenye Katiba yetu ambao unawalinda.

Mimi nitakupa changamoto (inaweza ikawa ni utopian kind of thinking; lakini inawezekana):

Kwa mfano, (1) Serikali ipunguze idadi ya Wizara. (2) Waziri awe ni daraja kati ya Rais na Wizara husika tu.

(3) Baada ya hapo, chini ya Waziri kuwe na Katibu wa Wizara. Hii nafasi iwe ni post ambayo kila mtu mwenye uwezo anaweza kujaribu ku-apply (Mtu unaleta CV yako na wahusika wanaamua kama utaweza kazi au la). Kisha Katibu anapewa ilani ambazo anapaswa azitekeleze ndani ya kipindi fulani (miaka mitatu hivi). Akifanya vizuri, mkataba unaongezwa na marupurupu mengine. Akiboronga katikati hapo, basi Waziri ana uwezo wa kumtimua kazi.

(4) Na watu watakaokuwa chini ya Katibu watakuwa wanapatikana kwa njia kama hiyo hapo juu.

(Wengine wanaweza wakasema hata huyo Waziri awe ni mwajiriwa tu! Kazi ya Wabunge iwe kutumikia majimbo yao tu na mawaziri ndio watakaokuwa wanawasaidia. Chaguo ni lako... Ningependa kusikia mawazo yako.)

Unadhani uzembe utaendelea kuendelea na kujirudia-rudia kila siku? Wangapi watakuwa wana-apply for ministerial post ili hali wanajua kibarua kinaweza kuota mbawa muda wowote ule?

Sidhani kama hawa maskini wengi waliochini -- wakisubiri "wakubwa" wawaletee umeme, elimu, uchumi bora n.k. -- wategemee mabadiliko yoyote yale wakati wahusika wakuu, walioshika usukani hawawajibiki. Rasilimali zitakuwa zinaishia juu kwa juu tu (kama mishahara ya walimu vile). Unadhani wezi hawajulikani?

Lakini, wanajua hata baada ya kumaliza vipindi vyao, Katiba "itawalinda". Mtu unaisabishia nchi hasara ya $ 100 mil, halafu unashutumiwa kwa "matumizi mabaya ya ofisi ya umma" tu? Jamani, tutafika? Kwa kifungo cha miaka miwili?

Jiulize, ingekuwaje kama Katiba yetu ingekuwa na kifungu cha kuwafikisha mafisadi kortini hata baada ya miaka ishirini baada ya kumaliza kazi zao Wizarani, kama ushahidi ukiwa kamili?

Ninachotaka mimi binafsi kama kijana Mtanzania, ni kuona kifungu cha uwajibishwaji wa viongozi kikiingizwa kwenye Katiba. Mwenye mawazo mbadala... ningependa kusikia.

Mtanzania, kwa kumalizia tu: Uchaguzi huu umeonesha kuwa Watanzania hawana imani na mfumo wa upatikanaji wa viongozi au hawajali; au wako hopeless? Waliojiandikia ni milioni 20; waliopiga kura ni milioni 8. Labda, wewe unatafsiri vipi hizi takwimu?
 
Mtanzania, shukrani kwa mchango wako.

Kuhusu suala la Katiba Mpya (KM)... umetoa hoja zako ambazo sina haja ya kuzirudia. Lakini, tunashindwa kuingiza kifungu cha uwajibishwaji wa viongozi? Maana'ke inaonekana watu wenye nyadhifa wanafanya mambo kama wanavyotaka, kwasababu wana "uhakika" kuna upuuzi kwenye Katiba yetu ambao unawalinda.

Mimi nitakupa changamoto (inaweza ikawa ni utopian kind of thinking; lakini inawezekana):

Kwa mfano, (1) Serikali ipunguze idadi ya Wizara. (2) Waziri awe ni daraja kati ya Rais na Wizara husika tu.

(3) Baada ya hapo, chini ya Waziri kuwe na Katibu wa Wizara. Hii nafasi iwe ni post ambayo kila mtu mwenye uwezo anaweza kujaribu ku-apply (Mtu unaleta CV yako na wahusika wanaamua kama utaweza kazi au la). Kisha Katibu anapewa ilani ambazo anapaswa azitekeleze ndani ya kipindi fulani (miaka mitatu hivi). Akifanya vizuri, mkataba unaongezwa na marupurupu mengine. Akiboronga katikati hapo, basi Waziri ana uwezo wa kumtimua kazi.

(4) Na watu watakaokuwa chini ya Katibu watakuwa wanapatikana kwa njia kama hiyo hapo juu.

(Wengine wanaweza wakasema hata huyo Waziri awe ni mwajiriwa tu! Kazi ya Wabunge iwe kutumikia majimbo yao tu na mawaziri ndio watakaokuwa wanawasaidia. Chaguo ni lako... Ningependa kusikia mawazo yako.)

Unadhani uzembe utaendelea kuendelea na kujirudia-rudia kila siku? Wangapi watakuwa wana-apply for ministerial post ili hali wanajua kibarua kinaweza kuota mbawa muda wowote ule?

Sidhani kama hawa maskini wengi waliochini -- wakisubiri "wakubwa" wawaletee umeme, elimu, uchumi bora n.k. -- wakati wahusika wakuu, walioshika usukani hawawajibiki. Rasilimali zitakuwa zinaishia juu kwa juu tu (kama mishahara ya walimu vile). Unadhani wezi hawajulikani?

Lakini, wanajua hata baada ya kumaliza vipindi vyao, Katiba "itawalinda". Mtu unaisabishia nchi hasara ya $ 100 mil, halafu unashutumiwa kwa "matumizi mabaya ya ofisi ya umma" tu? Jamani, tutafika? Kwa kifungo cha miaka miwili?

Jiulize, ingekuwaje kama Katiba yetu ingekuwa na kifungu cha kuwafikisha mafisadi kortini hata baada ya miaka ishirini baada ya kumaliza kazi zao Wizarani, kama ushahidi ukiwa kamili?

Ninachotaka mimi binafsi kama kijana Mtanzania, ni kuona kifungu cha uwajibishwaji wa viongozi kikiingizwa kwenye Katiba. Mwenye mawazo mbadala... ningependa kusikia.

Mtanzania, kwa kumalizia tu: Uchaguzi huu umeonesha kuwa Watanzania hawana imani na mfumo wa upatikanaji wa viongozi au hawajali; au wako hopeless? Waliojiandikia ni milioni 20; waliopiga kura ni milioni 8. Labda, wewe unatafsiri vipi hizi takwimu?

Mkuu,

Nakuelewa kabisa hapo juu kwamba dawa ni kuweka kila kitu kwenye katiba ili rais au kiongozi mwingine asiwe na uwezo wa kufanya tofauti. Lakini tatizo la hapo ni kwamba hata siku moja katiba haiwezi kutaja kila jambo maana vinginevyo itakuwa kubwa kuliko biblia na watu wengi watashindwa kuielewa.

Katiba nzuri ni ile ambayo mwananchi hata wa kawaida anaielewa na anaweza kuitetea na kuilinda. Tatizo kwa Tanzania ni kwamba ukiachia sisi wachache ambao tunaona umuhimu wa katiba. Walio wengi wanaona umuhimu ni mkate kwao na familia zao. Nina wasiwasi hawa viongozi wetu hata tuwe na katiba nzuri kiasi gani bado wataweza kuipuza na kufanya yao na kwasababu wananchi wengi hawajaona umuhimu wa hilo na hakuna kitakachofanyika. Ndio maana nikatolea mfano wa sheria ya gharama za uchaguzi. Watu wamevunja hiyo sheria akiwemo rais wa nchi lakini wale waliopewa madaraka ya kuchukua hatua wakakaa kimya.

Labda wananchi wetu wakielemika na kuwa na uchumi ambao angalau unawahakikishia kula, huenda watakuwa na uwezo wa kuitaka, kuitetea na kuilinda katiba mpya. Kwasasa naona inaweza kuishia kama ile ya vyama vingi vya siasa jambo ambalo mpaka leo watu wengi bado wanachukulia kama utani au wanaona kama ni uadui. Ni kama hatuelewi maana ya dhana nzima vya kuwepo vyama vya upinzani.

Narudia, kama katiba mpya itaweza kutibu haya matatizo yetu, basi na tuipiganie. Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kama culture ya Watanzania ya uwizi, uzembe na ujinga kutoka kwa wananchi wa chini mpaka juu haitabadilika bado tutaendelea kuwa duni hata katiba ibadilike vipi.
 
Narudia, kama katiba mpya itaweza kutibu haya matatizo yetu, basi na tuipiganie. Lakini mimi nina wasiwasi kwamba kama culture ya Watanzania ya uwizi, uzembe na ujinga kutoka kwa wananchi wa chini mpaka juu haitabadilika bado tutaendelea kuwa duni hata katiba ibadilike vipi.

Ndio hapo sasa. Matatizo ya Tanzania na Watanzania wengi ni kuwa karibia yote yanahusiana. Huwezi kuzungumzia elimu bila kutaja umaskini, uongozi mbovu, uzembe, uwizi n.k..

Kuhusu Katiba kuwa ndefu, nadhani kama watu walivyosema hapo juu, Katiba mara zote inatakiwa kuakisi na kujaribu kutatua matatizo yaliyo kwenye jamii husika. Ukiona kitu fulani kinajirudia miaka nenda rudi, ujue kuna mushkeri. Ubadhirifu wa mali za umma ulianza tokea tupate Uhuru (imagine, wakati mama yangu yuko shule ya msingi!!), lakini hadi leo tunaimba ufisadi... Na mimi nitashikilia bango hili suala la viongozi kutowajibishwa; no accountability whatsoever katika ngazi zozote zile!

Halafu, tusiseme kama haiwezekani; angalia nchi chache za Afrika ambazo zinawawajibisha viongozi wao. Wako wapi sasa hivi? (Botswana ni lulu, Bondeni... unakumbuka lile sakata la mkurugenzi wa polisi? Au kile chama cha wafanyakazi?)

Pia, kumbuka, hivi vifungu vyote vinaweza vikatajwa kwa kifupi kwenye Katiba, halafu sheria zile za mahakama ndio zikazijadili kwa kina. Sijui umenipata? Kwa hiyo, ingawa naheshimu mawazo yako, bado nasita kukubaliana na ishu ya Katiba kuwa ndefu. Cha muhimu ni kuondoa hili tatizo sugu la ubadhirifu wa mali za umma.

Ulizia Dar, kupiga "matukio" kwenye benki ni jambo la kawaida... Je, huko kwenye Wizara za madini itakuwaje? Maisha sasa hivi ni kutajirika fasta-fasta kabla hujaanza kuota mvi. Sasa, tulifumbie macho hili? Na Serikalini pia?

Juzi hapa Magufuli kapiga kelele kidogo tu, watu tukamuona kama Messiah... wakati ile kitu inatakiwa kuwa ni kawaida. Yaani, barabara ya Nelson Mandela ilianza kujengwa mwaka 2004. (Nadhani kwasababu jina la barabara yetu lina uzito wake, basi labda TanRoads walikuwa wamepanga kumaliza ujenzi baada ya miaka 27! Kuenzi tu juhudi za Madiba. Sisi wasanii; tuna ubunifu.)

Sasa, nikirudi kwa MM... Mi' nadhani "wahusika" wanataka washike usukani kwenye kusuka Katiba Mpya. Maana'ke ile ishu wakipewa vichaa, kuanzia mwanzo hadi mwisho, basi wataweka vifungu vya kuwawajibisha wazee. Kama nilivyojadilia kwenye post iliyopita.

Ni hayo tu kwa leo.
 
Mwanakijiji,

The simple answer, kwa swali lako "kwa nini sasa na sio kabla ya uchaguzi" Kuna INVISIBLE HAND
ambayo inasukuma both within Tanzania(wananchi less powerful) na outside (very powerful).

Hivyo kuwaambia wakiri hadharni ni halitawezekana kamwe
 
Binafsi naamini katiba mpya sio suluhisho na wala haitatusaidia. Tupiganie elimu na uchumi bora kwani ndio vitu pekee ambavyo vitamfanya Mtanzania ajikomboe na kuwa huru hata kuona katiba aliyo nayo haimfai. Kwasasa ni wasomi wachache na wanasiasa ambao wanaona umuhimu wa katiba mpya lakini watu wetu wengi wako busy kuhangaika na watakula nini? Watatibiwa wapi? na watapeleka watoto wao wapi kusoma? Watu kama hao hata wakipata katiba nzuri sidhani kama wako katika nafasi ya kuilinda na kuhakikisha inafuatwa.

Ni sawa na uhuru, watu wengi walianza kudai uhuru miaka mingi sana nyuma lakini sio wote walioelewa umuhimu wa uhuru mpaka miaka ya 60 na matokeo yake wananchi wengi walikuwa tayari kuutetea na kuulinda uhuru wao huo. Hivyo hivyo vyama vingi kwa Tanzania.

Kwa Tanzania, uchaguzi wa mwaka huu umeonyesha wazi wananchi wamechoshwa na uchumi duni na siasa za ubabaishaji. Wanataka mabadiliko katika maisha yao. Wanataka chakula nyumbani, wanataka hospitali, wanataka shule. Labda ni muda muafaka kuleta uhuru wa kiuchumi kwa wananchi wetu kabla hata ya kuleta katiba mpya. Labda tupiganie haki ya wananchi wetu kushiriki kwenye uchumi wao, kuhakikisha ajira zinatolewa kwa Watanzania. Kama hayo mambo hayawezi kufanyika mpaka tuwe na katiba mpya basi labda kuna haja ya hiyo katiba mpya. lakini kwa mimi naona leo hii hata tuletewe katiba iliyoandikwa vizuri namna gani, kama hatuna watu wengi ambao wako tayari kuitetea na kuilinda bado tutaendelea kukwama pale pale.

Katiba ndio sheria mama inayotoa maelekezo katika ngazi ya juu kabisa. hapo ndipo mamlaka yote yanaelezwa. Matatizo yako aina nyingi: kuna matatizo ya kimfumo, kuna ya kisera kuna ya kiutekelezaji, nk. unapozungumzia Katiba, unazungumzia mfumo, ambapo katika mfumo huo utajenga sera mbalimbali. katika katiba tunaeleza sisi tunamwelekeo gani kama nchi. katiba yetu ya sasa inasema tu kwamba hii ni nchi ya ujamaa ... lakini ukilinganisha mwelekeo wetu hivi sasa na ule wa miaka 30 iliyopita, kuna tofauti kubwa sana. katiba itaeleza mahusiano ya uzalishaji katika nchi yetu. haya yamebadilika sana na yanahitaji kuainishwa. katiba ya sasa inatoa mamlaka mengi kwa rais, ambayo inatoa mwanya kwa udikteta. ukizungumzia elimu bora, katiba itaainisha msingi yake. kutoka hapo utaweza kutunga sheria zitakazowezesha rasilimali za nchi kutumika kweli kwa ajili ya elimu bora kwa wote. bila hivyo hilo haliwezekani! katiba ya sasa inatoa nafasi kwa kikundi kidogo cha wajanja kujirundikia mamlaka na kuyatumia kwa maslahi yao na jamaa zao. wanapewa nafasi kutumia rasilimali za taifa kwa manufaa yao binafsi, na wanafanya yote hayo kwa mujibu wa katiba mbovu ya sasa! wanapewa mamlaka na katiba.

Katiba nzuri itawezesha kuwajibisha wala rushwa ngazi yoyote. kama ngazi za juu wanakula rushwa, haiwezekani kupiga vita rushwa huku chini. kwa hiyo usibeze kabisa umuhimu wa kuwa na katiba nzuri na inayoangalia maslahi ya taifa.
 
............Lakini sasa siyo wapinzani tu hata viongozi wengine wa serikali na hata wa CCM wanaanza kudai Katiba Mpya. Kilichonishangaza ni kuwa Rais Mkapa anadai naye Katiba Mpya! Really? I mean Really? Alikuwa Rais kwa miaka 10; alisimamia mabadiliko ya Katiba ya 2005 - lakini hakutaka Katiba mpya then? .................

Mbona washangaa!
Nami ninakushangaaa; kwani si ni wewe Mwanakijiji uliyewashauri kuwa ccm kama haitaki kuachwa nyuma basi idadindie treni ya Katiba Mpya! (Rejea Makala zako magazetini wiki hii)
 
Mzee Mwanakijiji,
kwa kweli ni jambo la hatari kabisa unapomsikia simba akihubiri kwamba ni dhambi mnyama mmoja kumla mwingine! ipo namna hapo. na inawezekana kwamba hawa walioanza kutoa kauli hizi wanapima kimo cha maji, kabla wengine hawajajitosa. Mimi sidhani kwamba katiba mpya anayozungumzia Mkapa ni ile inayotakiwa na Watanzania walio wengi, inayokidhi maslahi ya taifa lao. wanachotaka kufanya ni kukamata hii hoja na kuiongoza kule wanakotaka wao. Watanzania wataridhika kwamba wamepata katiba mpya, lakini wao watashangilia kwamba wamepata walichotaka: katiba inayolinda maslahi ya kikundi kidogo cha "watawala".

Ni vema kuwa na hadhari na kupinga kwa nguvu zote mielekeo kama hii. ni vema watu waadilifu na wakweli wasimame na kutetea hoja hii, ili kuimarisha umoja wa watanzania katika kudai katiba mpya, lakini ni muhimu pia kuweka tangu mwanzo nini hasa tunaongelea tunaposema katiba mpya. Kama serikali inachelewesha "kuridhia" ni vema wengine wakaanza kuainisha misingi ya katiba hiyo, angalau kueleza tunaipataje katiba mpya. hatuwezi kufanya kama An-nuur, "kuandika katiba", maana unaandika kutoka misingi ipi?
 
Tuache udwanzi jamani..Hoja ya maana hapa ni kwamba tunahitaji katiba mpya au mabadiliko ya katiba ili kuvest matakwa na mahitaji ya sasa..habari ya nani kasema nini is immaterial.

Mimi ninavyoweza kutafsiri hii attitude kama ya Mwanakijiji ni kwamba, watu (wapinzani na Mwanakijiji types) hawako interested in Katiba Mpya so much as walivyo interested na ujiko kwamba wao ndio wameleta katiba mpya. Na sasa wanaona kwa vile kina Mkapa na officials wengine wanaanza kusema wanataka katiba mpya nao, hawa wapinzani wanaona kama vile ule ujiko wa kwamba wao ndio wana push na kuleta katiba mpya utapotea.

Kuna jenerali mmoja wa jeshi US, nafikiri Patton, alisema, watu wakiacha kuangalia nani anapata credit kwa kazi gani na ku focus kwenye kufanya kazi tu, kazi kubwa inafanyika. Hizi habari nyingine za nani ndiye authentic na nani msanii zitatupotezea lengo tu.

I understand the need to be wary of deceiving politicians, lakini kwa mtu ambaye anajua umuhimu wa kubadili katiba huu si muda wa kuanza kupoteza momentum ya kudai katiba mpya kwa kuanza kushambulia forces mpya zilizojitokeza katika kudai katiba mpya.

Huu ni muda wa kuiambia serikali na CCM, angalieni, hata Mzee wenu Mkapa sasa anasema wazi katiba mpya ni muhimu, mna excuse gani sasa?
 
Mimi ninavyoweza kutafsiri hii attitude kama ya Mwanakijiji ni kwamba, watu (wapinzani na Mwanakijiji types) hawako interested in Katiba Mpya so much as walivyo interested na ujiko kwamba wao ndio wameleta katiba mpya. Na sasa wanaona kwa vile kina Mkapa na officials wengine wanaanza kusema wanataka katiba mpya nao, hawa wapinzani wanaona kama vile ule ujiko wa kwamba wao ndio wana push na kuleta katiba mpya utapotea.

Ndicho nilichokiona hapa, taabu kwelikweli!!
 
naona watu mnashindwa kupata pointi yenyewe na kama kawaida mnaanza kuuliza kama niko bado na akili zangu timamu. Mnapenda mno mazingaombwe kiasi cha kushangilia mkiona sungura katolewa kwenye kofia na wengine wanaweza kuapa kabisa kuwa ni "muujiza". Sasa leo watu wanaanza kuimba "katiba mpya" basi watu wanatakiwa kushangilia:

Hawawaambii tatizo la Katiba ya sasa ni nini? - of course tunatakiwa tuwe tunajua sote
Hawasemi kwanini sasa hivi na haikuwa kabla- tunaambiwa ni muda tu
Hawasemi wanataka nini hasa - yale yale "katiba mpya" - upya wa nini?
Hawasemi ni vitu gani viboreshwe? Je wakibadilisha tu Tume ya Uchaguzi watu wataridhika? Kwanini isiwe kufanyia mabadiliko vipengele vinavyolalamikiwa halafu tukamaliza kwani hilo halihitaji siku nyingi hata kikao cha bunge kinaweza kufanya hivyo.
Ati Katiba iliyopita haikuandikwa na sisi - well kwani kuandika sisi wenyewe kunatuhakikishia vipi Katiba nzuri? Leo hii miaka 49 ya kujitawala mbona baadhi yetu hatujivunii kuoona tunavyojitawala? kwanini tuamini ati kwa vile tutaandika Katiba sisi wenyewe basi itakuwa nzuri? Jamani, kwani vyama vingine vilirudishwa vipi na leo watu hawafurahii wakati tulishirikishwa kuvirudisha?

Katiba Mpya? kwa manufaa ya nani? Siyo wote wanaosema "nyeupe" wanamaanisha "nyeupe pe" wengine wanamaanisha "rangi ya maziwa!"

Mwanakijiji:

Nimesoma katiba ya Marekani. Nimesoma katiba ya Tanzania. Katiba ya Marekani pamoja na kuwa na zaidi ya miaka 200 ni rahisi kuisoma na kueleweka hata kwa mtu mwenye kiwango kidogo cha elimu. Mchukue mtoto wa miaka 16 wa Marekani na muulize mambo gani yaliopo kwenye Tangazo la uhuru na katiba, atakupa jibu.

Kwa Tanzania katiba ya nchi ni kitabu cha mwanasheria. Hivyo hata sisi tuliosoma siasa hatukupitia kitabu hicho. Hata baba wa taifa alikuwa anatembea na vitabu viwili tu: azimio la Arusha na Biblia. Hivyo kwa miaka mingi, katiba ya nchi ilikuwa si kitu cha kujivunia au kutilia maanani. Na kutokana na hayo, nchi imeendeshwa kwa mazoea tu. Na wengi wanachukulia katiba kama mfumo wa utawala. Lakini kimsingi katiba inaelezea taifa na watu wake.

Hivyo moja ya tatizo la katiba iliyopo sasa ni ugumu wake. Vitu vingi katika katiba ya sasa vimeelezewa kwa undani (in detail) na sio abstract. Hivyo tunatoa mzigo kwa vizazi vinavyokuja. Vizazi vinavyokuja ni lazima kutafsiri katiba kutokana na mazingira yao na sio ya sasa. Kwa mfano wa posti yako moja, katiba ya sasa inaonyesha mfumo wa uongozi wa serikali ya mapinduzi Zanzibar.
 
kwanini sasa hivi tunahitaji sana "katiba Mpya"? nini kimetokea ambacho hao wanaodai Katiba Mpya hawataki kukisema. Kwa sababu as a matter of fact yote wanayoyasema yalikuwa kweli kwa miaka mitano iliyopita; why now?

Ukitaka kujua kwa nini 'now' utakuwa umepata mzizi wa matatizo ya nchi hii!

Nakumbuka tulijadili sana swala la katiba na nakumbuka sana post yako number 164 hapa:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ali-na-kueleza-sera-za-chadema-hapa-jf-9.html

Swala la katiba na NEC tuliliongea sana kabla ya uchaguzi. Infact swali unaloliuliza si kwa hao jamaa tu hata hawa wapinzani wetu, wana mengi sana ya kujibu ukiwaweka kwenye mizani ya 'logical thinking' what should be done first before other things.

All I can say is

Respect!!
 
MMM

Madai yalikuwapo tokea enzi, ila binafsi nadhani kwa sasa wale hypocrites wamepewa go ahead na kiongo wao na chama chao kudai hivyo ili kudivert attention ya watanzania kama ilivyo ada... sie ni wadanganyika, tumeshasau wizi wa kura, hali ngumu ya maisha, ufisadi, bajeti shenzi kwenda kwa GBS supporters na unafiki wao walioita wapinzani kokoto

TO ME HII VIGOR YA KATIBA MPYA INAPEWA PROMO ZAIDI NA WADANDIA HOJA WA KILA SIKU (CCM)

sababu kubwa ya pili ni kwamba the wind of change has blown and any resistance will just lead to ones peril (including hao wenye vyao kwa sasa)

pamoja mkuu..walibeza wakati Dr.Slaa anazungumzia suala la katiba mpya...leo nini kimetokea wanataka katiba mpya..Kwanza waziri wa katiba wa CCM kasema katiba iliyopo ni safi kweli kweli haihitaji mabadiliko hata kidogo
 
Mimi ninavyoweza kutafsiri hii attitude kama ya Mwanakijiji ni kwamba, watu (wapinzani na Mwanakijiji types) hawako interested in Katiba Mpya so much as walivyo interested na ujiko kwamba wao ndio wameleta katiba mpya. Na sasa wanaona kwa vile kina Mkapa na officials wengine wanaanza kusema wanataka katiba mpya nao, hawa wapinzani wanaona kama vile ule ujiko wa kwamba wao ndio wana push na kuleta katiba mpya utapotea.

Kuna jenerali mmoja wa jeshi US, nafikiri Patton, alisema, watu wakiacha kuangalia nani anapata credit kwa kazi gani na ku focus kwenye kufanya kazi tu, kazi kubwa inafanyika. Hizi habari nyingine za nani ndiye authentic na nani msanii zitatupotezea lengo tu.

I understand the need to be wary of deceiving politicians, lakini kwa mtu ambaye anajua umuhimu wa kubadili katiba huu si muda wa kuanza kupoteza momentum ya kudai katiba mpya kwa kuanza kushambulia forces mpya zilizojitokeza katika kudai katiba mpya.

Huu ni muda wa kuiambia serikali na CCM, angalieni, hata Mzee wenu Mkapa sasa anasema wazi katiba mpya ni muhimu, mna excuse gani sasa?

Yes Kiranga you may take in that side ila nilivyomwelewa Mwanakiji ni kuwa kuna watu wanaosema wanataka katiba mpya ni WANAFIKI! ebu fikiria majaji, mpaka jaji mkuu, rais mstaafu, viongozi wa dini, mabalozi n.k wanasema swala la katiba wakati wanalala na kuamka nayo.They know this country in and out! wanajua katiba ni mbovu leo baada ya CDM kuanza kulisema basi nao wanacheza mdundo huo huo! ni wanafiki that is exactly they are!

Yes we need new katiba, ila swala hapa si katiba tu, bali kuwa macho na kuwa watu wa 'kuthubutu' kusema yale yanayotakiwa kusemwa na si kusema baada ya wengine kusema! this is a sign of hypocrisy, unresponsibility and coward!
Back to katiba hata chadema tuliwaonya na maandiko yetu/yangu yapo hata kususia uchaguzi, tuliishia kutukanwa tu. It is does not need a brain surgeon, Jet engineer or computer scientist to know that Katiba is/was wrong!!! It is even suprising to know PhD holder opened his eyes that something is wrong after 'loosing' in the ballot box! which seemed 'THE ONLY OPTION' to remove CCM from power. Even kids knew for sure JK will win!! they had katiba and they had NEC! what more do you need to be a president?

Leo barabara zetu ni mbovu na hazina alama nyingi za barabarani, zikitokea ajali kila mtu atasema na kutoa solution!, everywhere is not right in this country needs people to stand up ,foresee, talk and act not just to say after others!
 
Ati leo viongozi wa dini nao wanajitokeza na kudai Katiba Mpya! Mwisho wataanza kuja na wabunge wa CCM wakidai Katiba Mpya! Utani mwingine jamani!


... Kilichonishangaza ni kuwa Rais Mkapa anadai naye Katiba Mpya! Really? I mean Really? Alikuwa Rais kwa miaka 10; alisimamia mabadiliko ya Katiba ya 2005 - lakini hakutaka Katiba mpya then?

Pole Mzee mwenzangu, hoja imeshatekwa nyara na CCM na iwapo katiba mpya itaandaliwa basi wenyewe ndio watachukua sifa ya mabadiliko.
Nafikiri mmesahau jinsi walivyojitwalia agenda ya mageuzi ya vyama vingi mwaka 1992 wakati wapiganaji wenyewe akina MArando na wenzake wakisahauliwa na historia.
 
kwanini sasa hivi tunahitaji sana "katiba Mpya"? nini kimetokea ambacho hao wanaodai Katiba Mpya hawataki kukisema. Kwa sababu as a matter of fact yote wanayoyasema yalikuwa kweli kwa miaka mitano iliyopita; why now?


Mzee Mwanakijiji baada ya uchaguzi huu kila mwenye mapenzi na Tanzania yenye neema anajua cha kufanya ni nini? Amani na utulivu wetu tumeona jinsi gani uchaguzi unaweza kusababisha viwe historia, na wengi tumeona watu wanavyoshabikia mabadiliko kwa kwasi kubwa. Wanaoweza kusoma alama za nyakati wameanza kuogopa kwamba kama katiba mpya haipatikani kwa hiari basi umma unaweza kuamasishwa kuidai na ukafanikiwa. Kumbuka ushindi wa umma kama utaongozwa na vyama vya upinzani huo unawezakuwa ni mwanzo wa mwisho wa chama tawala!
 
Ni sawasawa tu Nyerere alivyodai kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi mara baada ya kutoka madarakani, nyakati zinabadilika na fikra zinabadilika hasa unapokuwa nje ya uwanja!!

Mawazo finyu! Nyerere aliacha uongozi wa taifa enzi zile za chama kimoja katika nchi nyingi za africa, na 1992, tayari upepo ulielekea vyama vingi, it was logical kufanya alichokifanya, sidhani kama alikuwa na maslahi binafsi kama huyu mtu wako
 
Pole Mzee mwenzangu, hoja imeshatekwa nyara na CCM na iwapo katiba mpya itaandaliwa basi wenyewe ndio watachukua sifa ya mabadiliko.
Nafikiri mmesahau jinsi walivyojitwalia agenda ya mageuzi ya vyama vingi mwaka 1992 wakati wapiganaji wenyewe akina MArando na wenzake wakisahauliwa na historia.

Surely, and they will make sure cdm is silent in this matter, they will keep on saying this until 2015! yet CDM will participate in another election!
 
kwanini sasa hivi tunahitaji sana "katiba Mpya"? nini kimetokea ambacho hao wanaodai Katiba Mpya hawataki kukisema. Kwa sababu as a matter of fact yote wanayoyasema yalikuwa kweli kwa miaka mitano iliyopita; why now?
Mwanakijiji, hawa jamaa wameona huu ndio muda muafaka wa kudai katiba kwa sababu iliyo wazi ya changamoto zilizopo. Uchaguzi mkuu uliopita haukuwa rahisi kwa chama tawala pamoja na kutumia misuli ya dola. Na kwa vyovyote vile inawezekana chaguzi zijazo zikawa na ushindani mkubwa kuliko huu tuliouona. Sasa kama Mwanza, Arusha etc watu walikesha kulinda wanayoyaamini ni matokeo ya kura zao kutoharibiwa, nani anajua kama uchaguzi ujao hamasa kama hiyo itaenea eneo kubwa zaidi na katika nafasi mpaka za uraisi? Huoni kama ukitokea uchakachuaji inaweza kuleta uvunjifu wa amani?
Well, sometimes in life it is easier to say "better devil you know"!!!
Mkapa amenusa harufu hiyo na hekima imemuongoza kusema aliyosema. Kuna mambo tunakosea lakini two wrong can't make right.
 
Back
Top Bottom