Siasa zafanya MTV Base Africa kusistisha tuzo za MAMAs

Mtuflani Official

JF-Expert Member
Dec 31, 2019
1,936
4,347
MTV Base Africa leo wametangaza kusitisha tuzo za MAMAs ambazo zilikua zifanyike 20 mwezi huu nchini Uganda.

IMG_8646.JPG


Ikumbukwe tarehe 14 mwezi wa kwanza Uganda ilikua na uchaguzi wa Urais ambako Museveni alishinda lakini watu walidai uchaguzi haukua wa haki.

Dj maarufu duniani ambaye ni Dj Khaled na mwanamuziki alipangwa kuwa mshereheshaji wa hizi tuzo.

IMG_8648.JPG

Cha ajabu Dj Khaled alijaribu kupost ujumbe kupitia twitter kutangaza hizo tuzo lakini wananchi wa Uganda walimjibu kwa kupost picha za watu waliouawa katika kipindi cha uchaguzi. Hii ilifanya Dj Khaled kufuta ule ujumbe na pia kufuta video zinahusiana na tuzo hizo kwenye mitandao yake ya kijamii.

Kuna mzungu anaitwa Jeffrey Smith huko twitter. Huku wengine tunamkumbuka kipindi cha kampeni za Tanzania 2020 alipokua akimshabikia Tundu Lissu huku akimpinga sana Magufuli. Jeffrey Smith alikua mstari wa mbele kupinga MAMAs kufanyika Uganda.

IMG_8649.JPG
 
Siasa and corona virus.

Tuendelee kujifukiza, barakoa, vitakasa mikono, umbali wa kijamii.

Au nawaingiza chaka waungwana wenzangu? Masihara sio masihara?
 
SIASA AND CORONA VIRUS

TUENDELEE KUJIFUKIZA, BARAKOA, VITAKASA MIKONO, UMBALI WA KIJAMII

AU NAWAINGIZA CHAKA WAUNGWANA WENZANGU? MASIHARA SIO MASIHARA?

Sio corona mkuu. Zilikua zimepangwa kama “virtual awards”. Dj Khaled alikua atasherehesha akiwa nyumbani kwake Miami.
 
mtv


Tuzo za MTV za muziki wa Afrika 'MTV Africa Music Awards (MAMAs)', ambazo zilikuwa zimepangwa kufanyika mjini Kampala mwezi huu zimehairishwa, waandilizi wa tuzo hizo wamesema.

MTV Base Africa imetangaza kupitia mtandao wa Twitter, bila kutoa sababu zilizopelekea kufikiwa kwa uamuzi huo.

“MTV Base inaahirisha Tuzo za muziki wa Afrika 2020. Tutaendelea kuwafahamisha mashabiki kadiri tunavyoendelea kupata taarifa zaidi,” ujumbe huo umesema.

Hivi karibuni, tuzo hizo zimekuwa zikipigwa vita na wanaomuunga mkono Bobi Wine, Jeffrey Smith na Robert Amsterdam, wakitaka waandalizi kufikiria tena uamuzi wao wa kuweka tamasha hilo nchini Uganda

“Kuandaa tamasha la kimataifa kwa ushirikiano na #Utawala wa Uganda wa kidikteta, @MTVBaseAfrica

“Sio tu kwamba litakuwa linafuta uhalifu uliofanywa na utawala huo, lakini pia litaathiri wasanii wote walioteuliwa,” Jeffrey Smith aliandika ujumbe huo.

Tamasha hilo maarufu kama MAMAs, ambalo lilikuwa limepangwa kufanyika Kampala, lilikuwa litaendeshwa kwa njia ya moja kwa moja mtandaoni kwasababu ya janga la virusi vya corona.

Pia ingekuwa ni mara ya kwanza tuzo hizo zinatolewa nchini Uganda.

Tuzio hizo ambazo mara ya kwanza zilifanyika 2008 mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini mwaka 2016, mwaka 2009 zilifanyika nchini Kenya iliyopo Afrika mashariki jijini Nairobi.
 
Niliwashangaa sana kuzifanyia uganda....sijui walitumia akili gan wakaacha 255 au 254
 
Sio corona mkuu. Zilikua zimepangwa kama “virtual awards”. Dj Khaled alikua atasherehesha akiwa nyumbani kwake Miami.
Tatizo lako ni nini hasa? Kama wenyewe Waganda ndiyo waliopost watu wameuawa wewe ni nani kuwapinga? Watu wana machungu halafu mnawaletea mambo ya awards?? Poor timing...
 
Back
Top Bottom