Siasa za Tanzania za vyama vyote zimefikia hali mbaya sana ya chuki, ubabe, kukomoana, kusalitiana, kutukanana, kudharauliana na hata kuuana!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,142
18,769
Hali ya siasa za Tanzania ni ya kutisha sana, na vyama vyote vya siasa vina hatia, CCM kama chama tawala na vyama vya upinzani. Imefikia mahali ambapo kuna chuki, ubabe, kukomoana, kusalitiana, kutukanana, kudharauliana na hata kuuana, sio tu kati ya chama tawala na vyama vya upinzani, bali pia ndani ya vyama vyenyewe, CCM na vyama vya upinzani.

Imefikia wakati wanasiasa wanapoongea unaona wazi maneno ya chukii, ubabe dharau nk dhidi ya wanasiasa ndani ya chama chao wenyewe au kuelekezwa kwa watu wa chama kingine, ambao ni Watanzania kama wao, na wote wanadai wapo katika siasa kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

Cha kusikitisha zaidi, ni kwamba Watanzania tumekubali kama vipofu kuongozwa na watu wa namna hii, na hata kushangilia na kushabikia pale wanapofanya au kutamka mambo ambayo yanaendeleza chuki na mengine mabaya kati yetu. Hivi tumerogwa na nini hadi kufikia hapa tulipo? Ile Tanzania ya watu wenye kupendana, walioitana "ndugu', waliosifika duniani kote kwa amani na umoja, imeenda wapi? Imefikia mahali tunaruhusu hawa wanasiasa wasababishe chuki kati yetu na wanandoa wetu, ndugu zetu wa ukoo, wapenzi wetu, jirani zetu, rafiki zetu na wala hilo hatulioni!

Watanzania ni lazima tufikie mahali tuamke, na kutambua kwamba wanasiasa wa vyama vyote nchini wameamua kuwa viongozi wenye akili iliyotawaliwa na chuki, ubabe nk katika kuendesha siasa zao. Hakuna siasa tena Tanzania, ni vurugu tupu zilizojaa ulevi tu wa kutaka kuhodhi madaraka kwa njia yeyote ile. Kinachoendelea sio tena wanasiasa kujinadi kwa ubora wa sera zao, bali ni wanasiasa kujinadi kwa kuonyesha ni jinsi gani wanasiasa fulani ndani ya chama chao au chama kingine wanapaswa kudharauliwa, kuchukiwa, kubezwa na ikiwezekana hata kuuliwa!

Enzi za nyuma hata tuliimba "Sisi tunataka kuwasha mwenge, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali ambapo pana chuki, heshima ambapo pamejaa dharau". Je ndicho wanasiasa wetu wanafanya? Tutaimbaje mwenge umulike hata nje ya mipaka yetu na kuleta mambo haya wakati hapa kwetu hayapo na wala hatuyajali tena? Karibu viongozi wetu wote wa siasa katika ngazi zote, kila wakifungua midomo yao utakachosikia ni dharau na chuki. Tumaini gani hilo wanalotupa?

Kuna vitabu vya dini vimeandika juu ya sifa za watu katika nyakati fulani, kuwa watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, watukanaji, wasio na utakatifu; wasio na ubinadamu, wasiopenda kusuluhishwa, wachonganishi, walafi, wakatili, wasiopenda mema; wasaliti, wasiojali kitu, waliojaa majivuno. KIla nikisoma maneno haya naona kama yaliandikwa kwa ajili ya wanasiasa wa Tanzania. Na haya nayaona katika wanasiasa wote wa Tanzania, kuanzia CCM, Chadema, NCCR, TLP nk, kuanzia viongozi wa juu hadi wa chini.

Hivi kweli Watanzania tumekuwa vipofu kiasi kwamba hatuoni haya katika wanasiasa wetu? Kwa nini tunakubali kuwa mashabiki wasio na akili kwa ajili ya watu wa namna hii ambao kwa unafiki wanajifanya wako katika nafasi zao kwa ajili ya kututumikia?

Watanzania wenzangu, tunahitaji mambadiliko makubwa katika nchi yetu. Tunahitaji msukumo mkubwa wa kuwakataa hawa wanasiasa wote ambao sio tu wanazidi kuwa vipofu wa kutuongoza sisi tuliokubali kuwa vipofu kama wao, bali wanaiangamiza nchi yetu. Tunahitaji tuake chini na kuwaonyesha kwamba hatutaki tena watu wa namna hii kujiita viongozi wetu. Tunahitaji kurudisha udugu wetu na amani ambayo ndizo zilikuwa sifa zetu kuu.
 
Yote yafanyike ila sio kufanywa na mtu aliyeaminiwa kuwaapisha wengine waitetee katiba halafu yeye ndio anaibaka katiba utadhani hii siyo nchi ya watu timamu. Hivi Nduguyai anaelewa thamani ya hili Taifa imepitea sana tangu awe spika wa Bunge? Eti muheshimiwa speaker ana uheshimiwa gani sasa
 
Yote yafanyike ila sio kufanywa na mtu aliyeaminiwa kuwaapisha wengine waitetee katiba halafu yeye ndio anaibaka katiba utadhani hii siyo nchi ya watu timamu. Hivi Nduguyai anaelewa thamani ya hili Taifa imepitea sana tangu awe spika wa Bunge? Eti muheshimiwa speaker ana uheshimiwa gani sasa
Mkuu hili sio suala la Ndugai wala Mbowe, ni suala la wanasiasa wote wa sasa katika kujifanya wapo kwa ajili yetu!
 
Nakumbuka kipindi cha nyuma mtu alikuwa akivaa jezi ya ccm anazomewa na kuchaniwa nguo zake sasa hii iliyopata chadema ndio laana ya wale wazee mliokua mnawafanyia vile vituko mana mlisahau siasa sio chuki ila mkapandikiza chuki kwa wafuasi wenu na mwisho zimerudi kwenu sasa
 
Mkuu hili sio suala la Ndugai wala Mbowe, ni suala la wanasiasa wote wa sasa katika kujifanya wapo kwa ajili yetu!
Msababishaji wa haya yote ni aina ya dereva aliyekabidhiwa gari awamu hii.
Katiba ya nchi ikisha anza kukiukwa na mwenye mamlaka akijiona yuko juu ya watu wote na kila kitu na kwamba hata haki ya watu kuchagua kiongozi wao hawana tena basi kinachobaki ni watu kujizira na tunapoelekea kwa sasa ni kwenye ile hali ya mtu kufanya maamuzi ya liwalo na liwe bila kujihangaisha kufikiria madhara.
Kiburi cha polisi, kiburi cha baadhi ya wakuu wa mkoa/wilaya , kiburi cha wakuu wa mihimili kinatoka wapi? kama sii kana kwamba kina baraka zote za kufanya yaliyotendwa na makaburu na kuzidi kutoka juu?
Na hata baadhi ya viongozi wa dini makanjanja wamekodishwa kufanya chuki dhidi ya kundi fulani na kuidharau kwa kejeli hekima ya kiungu ya wale wakuu wa dini waliopikwa na kuiva kuisimamia jamii na kuielekeza kwa kuishauri kiueledi.
Ni shauku yangu kuona mapenzi ya Mungu yakitimia kwa kile alichokusudia baada ya kuridhia yale yanayoendelea nchini kwa sasa kuchukua nafasi. Lakini mimi kibinafsi ni maombi yangu kwa Mungu kama alivyo omba Bwana Yesu , "ikiwezekana baba kikombe hiki kama taifa kituepuke"
Angalizo ni kwamba maombi yana mawili, ama kukubaliwa au kinyume chake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hali ya siasa za Tanzania ni ya kutisha sana, na vyama vyote vya siasa vina hatia, CCM kama chama tawala na vyama vya upinzani. Imefikia mahali ambapo kuna chuki, ubabe, kukomoana, kusalitiana, kutukanana, kudharauliana na hata kuuana, sio tu kati ya chama tawala na vyama vya upinzani, bali pia ndani ya vyama vyenyewe, CCM na vyama vya upinzani.

Imefikia wakati wanasiasa wanapoongea unaona wazi maneno ya chukii, ubabe dharau nk dhidi ya wanasiasa ndani ya chama chao wenyewe au kuelekezwa kwa watu wa chama kingine, ambao ni Watanzania kama wao, na wote wanadai wapo katika siasa kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

Cha kusikitisha zaidi, ni kwamba Watanzania tumekubali kama vipofu kuongozwa na watu wa namna hii, na hata kushangilia na kushabikia pale wanapofanya au kutamka mambo ambayo yanaendeleza chuki na mengine mabaya kati yetu. Hivi tumerogwa na nini hadi kufikia hapa tulipo? Ile Tanzania ya watu wenye kupendana, walioitana "ndugu', waliosifika duniani kote kwa amani na umoja, imeenda wapi? Imefikia mahali tunaruhusu hawa wanasiasa wasababishe chuki kati yetu na wanandoa wetu, ndugu zetu wa ukoo, wapenzi wetu, jirani zetu, rafiki zetu na wala hilo hatulioni!

Watanzania ni lazima tufikie mahali tuamke, na kutambua kwamba wanasiasa wa vyama vyote nchini wameamua kuwa viongozi wenye akili iliyotawaliwa na chuki, ubabe nk katika kuendesha siasa zao. Hakuna siasa tena Tanzania, ni vurugu tupu zilizojaa ulevi tu wa kutaka kuhodhi madaraka kwa njia yeyote ile. Kinachoendelea sio tena wanasiasa kujinadi kwa ubora wa sera zao, bali ni wanasiasa kujinadi kwa kuonyesha ni jinsi gani wanasiasa fulani ndani ya chama chao au chama kingine wanapaswa kudharauliwa, kuchukiwa, kubezwa na ikiwezekana hata kuuliwa!

Enzi za nyuma hata tuliimba "Sisi tunataka kuwasha mwenge, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali ambapo pana chuki, heshima ambapo pamejaa dharau". Je ndicho wanasiasa wetu wanafanya? Tutaimbaje mwenge umulike hata nje ya mipaka yetu na kuleta mambo haya wakati hapa kwetu hayapo na wala hatuyajali tena? Karibu viongozi wetu wote wa siasa katika ngazi zote, kila wakifungua midomo yao utakachosikia ni dharau na chuki. Tumaini gani hilo wanalotupa?

Kuna vitabu vya dini vimeandika juu ya sifa za watu katika nyakati fulani, kuwa watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, watukanaji, wasio na utakatifu; wasio na ubinadamu, wasiopenda kusuluhishwa, wachonganishi, walafi, wakatili, wasiopenda mema; wasaliti, wasiojali kitu, waliojaa majivuno. KIla nikisoma maneno haya naona kama yaliandikwa kwa ajili ya wanasiasa wa Tanzania. Na haya nayaona katika wanasiasa wote wa Tanzania, kuanzia CCM, Chadema, NCCR, TLP nk, kuanzia viongozi wa juu hadi wa chini.

Hivi kweli Watanzania tumekuwa vipofu kiasi kwamba hatuoni haya katika wanasiasa wetu? Kwa nini tunakubali kuwa mashabiki wasio na akili kwa ajili ya watu wa namna hii ambao kwa unafiki wanajifanya wako katika nafasi zao kwa ajili ya kututumikia?

Watanzania wenzangu, tunahitaji mambadiliko makubwa katika nchi yetu. Tunahitaji msukumo mkubwa wa kuwakataa hawa wanasiasa wote ambao sio tu wanazidi kuwa vipofu wa kutuongoza sisi tuliokubali kuwa vipofu kama wao, bali wanaiangamiza nchi yetu. Tunahitaji tuake chini na kuwaonyesha kwamba hatutaki tena watu wa namna hii kujiita viongozi wetu. Tunahitaji kurudisha udugu wetu na amani ambayo ndizo zilikuwa sifa zetu kuu.
Inaonesha kutokuwa wakomavu tusipoona chimbuko tukang’ang’ania matokeo. Chimbuko la hali hii ni pale ambapo Upinzani chini ya akina Zitto na Tundu Lissu walipoanza kumtukana na kumdharau, kumyanyasa na kumbeza Rais aliyechaguliwa na watu Mwaka 2015. Na hii dhambi haitatuacha salama maana hata Tundu Lissu akichaguliwa kuwa Rais 2025, CCM watafanya wenzao wanayoyafanya. Ni kosa kumkashifu, kumdharau, na kumsigina kiongozi aliye madarakani maana mnajenga mfumo wa ajabu. Cc Retired, Salary Slip, Mmawia etc
 
Nakumbuka kipindi cha nyuma mtu alikuwa akivaa jezi ya ccm anazomewa na kuchaniwa nguo zake sasa hii iliyopata chadema ndio laana ya wale wazee mliokua mnawafanyia vile vituko mana mlisahau siasa sio chuki ila mkapandikiza chuki kwa wafuasi wenu na mwisho zimerudi kwenu sasa
CCM kuanza kuwauwa na kuwapoteza Chadema hiyo ndio laana
 
Hali ya siasa za Tanzania ni ya kutisha sana, na vyama vyote vya siasa vina hatia, CCM kama chama tawala na vyama vya upinzani. Imefikia mahali ambapo kuna chuki, ubabe, kukomoana, kusalitiana, kutukanana, kudharauliana na hata kuuana, sio tu kati ya chama tawala na vyama vya upinzani, bali pia ndani ya vyama vyenyewe, CCM na vyama vya upinzani.

Imefikia wakati wanasiasa wanapoongea unaona wazi maneno ya chukii, ubabe dharau nk dhidi ya wanasiasa ndani ya chama chao wenyewe au kuelekezwa kwa watu wa chama kingine, ambao ni Watanzania kama wao, na wote wanadai wapo katika siasa kwa ajili ya maslahi ya Watanzania.

Cha kusikitisha zaidi, ni kwamba Watanzania tumekubali kama vipofu kuongozwa na watu wa namna hii, na hata kushangilia na kushabikia pale wanapofanya au kutamka mambo ambayo yanaendeleza chuki na mengine mabaya kati yetu. Hivi tumerogwa na nini hadi kufikia hapa tulipo? Ile Tanzania ya watu wenye kupendana, walioitana "ndugu', waliosifika duniani kote kwa amani na umoja, imeenda wapi? Imefikia mahali tunaruhusu hawa wanasiasa wasababishe chuki kati yetu na wanandoa wetu, ndugu zetu wa ukoo, wapenzi wetu, jirani zetu, rafiki zetu na wala hilo hatulioni!

Watanzania ni lazima tufikie mahali tuamke, na kutambua kwamba wanasiasa wa vyama vyote nchini wameamua kuwa viongozi wenye akili iliyotawaliwa na chuki, ubabe nk katika kuendesha siasa zao. Hakuna siasa tena Tanzania, ni vurugu tupu zilizojaa ulevi tu wa kutaka kuhodhi madaraka kwa njia yeyote ile. Kinachoendelea sio tena wanasiasa kujinadi kwa ubora wa sera zao, bali ni wanasiasa kujinadi kwa kuonyesha ni jinsi gani wanasiasa fulani ndani ya chama chao au chama kingine wanapaswa kudharauliwa, kuchukiwa, kubezwa na ikiwezekana hata kuuliwa!

Enzi za nyuma hata tuliimba "Sisi tunataka kuwasha mwenge, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali ambapo pana chuki, heshima ambapo pamejaa dharau". Je ndicho wanasiasa wetu wanafanya? Tutaimbaje mwenge umulike hata nje ya mipaka yetu na kuleta mambo haya wakati hapa kwetu hayapo na wala hatuyajali tena? Karibu viongozi wetu wote wa siasa katika ngazi zote, kila wakifungua midomo yao utakachosikia ni dharau na chuki. Tumaini gani hilo wanalotupa?

Kuna vitabu vya dini vimeandika juu ya sifa za watu katika nyakati fulani, kuwa watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, watukanaji, wasio na utakatifu; wasio na ubinadamu, wasiopenda kusuluhishwa, wachonganishi, walafi, wakatili, wasiopenda mema; wasaliti, wasiojali kitu, waliojaa majivuno. KIla nikisoma maneno haya naona kama yaliandikwa kwa ajili ya wanasiasa wa Tanzania. Na haya nayaona katika wanasiasa wote wa Tanzania, kuanzia CCM, Chadema, NCCR, TLP nk, kuanzia viongozi wa juu hadi wa chini.

Hivi kweli Watanzania tumekuwa vipofu kiasi kwamba hatuoni haya katika wanasiasa wetu? Kwa nini tunakubali kuwa mashabiki wasio na akili kwa ajili ya watu wa namna hii ambao kwa unafiki wanajifanya wako katika nafasi zao kwa ajili ya kututumikia?

Watanzania wenzangu, tunahitaji mambadiliko makubwa katika nchi yetu. Tunahitaji msukumo mkubwa wa kuwakataa hawa wanasiasa wote ambao sio tu wanazidi kuwa vipofu wa kutuongoza sisi tuliokubali kuwa vipofu kama wao, bali wanaiangamiza nchi yetu. Tunahitaji tuake chini na kuwaonyesha kwamba hatutaki tena watu wa namna hii kujiita viongozi wetu. Tunahitaji kurudisha udugu wetu na amani ambayo ndizo zilikuwa sifa zetu kuu.
Nitawaambia watz kitu kimoja: Nchi mkishakosea pale juu, basi huku chini kila kitu kinakwenda mrama. Kiongozi ni kichwa, kichwa kikishakuwa kibovu basi mwili wote unakwenda hovyo hovyo. Tulikosea mahali 2015.
 
Inaonesha kutokuwa wakomavu tusipoona chimbuko tukang’ang’ania matokeo. Chimbuko la hali hii ni pale ambapo Upinzani chini ya akina Zitto na Tundu Lissu walipoanza kumtukana na kumdharau, kumyanyasa na kumbeza Rais aliyechaguliwa na watu Mwaka 2015. Na hii dhambi haitatuacha salama maana hata Tundu Lissu akichaguliwa kuwa Rais 2025, CCM watafanya wenzao wanayoyafanya. Ni kosa kumkashifu, kumdharau, na kumsigina kiongozi aliye madarakani maana mnajenga mfumo wa ajabu. Cc Retired, Salary Slip, Mmawia etc
Twende taratibu:
1. Kudharau ni nini?
2. Kusigina ni nini?
3. Kukashifu ni nini?
Toa mifano kwa kila moja hapo juu ambapo uliowataja wameyafanya. (Lisu alifanya hivi, Zitto alifanya hivi etc) Twende taratibu maana naona kama wewe unataka kuwa muungwana.
 
Hizo ndio siasa tulizozichagua wenyewe hivyo tuvumilie tu, Siku tukizichoka tutabadilika.
 
Twende taratibu:
1. Kudharau ni nini?
2. Kusigina ni nini?
3. Kukashifu ni nini?
Toa mifano kwa kila moja hapo juu ambapo uliowataja wameyafanya. (Lisu alifanya hivi, Zitto alifanya hivi etc) Twende taratibu maana naona kama wewe unataka kuwa muungwana.
Huyu ni dictator uchwara, huyu ni rais ambaye hatatimiza miaka 5 madarakani etc. Mtu ambaye siwezi kumuingiza katika dhambi hii ni Mbowe ambnaye sijawahi ona anamtusi Rais. Hata nyie huwa mnamtukana katika mitandao kila kukicha. Mnajenga tabia ambayo itafanya hata nyie mkitawala akina mdude ccm wataibuka
 
Huyu ni dictator uchwara, huyu ni rais ambaye hatatimiza miaka 5 madarakani etc. Mtu ambaye siwezi kumuingiza katika dhambi hii ni Mbowe ambnaye sijawahi ona anamtusi Rais. Hata nyie huwa mnamtukana katika mitandao kila kukicha. Mnajenga tabia ambayo itafanya hata nyie mkitawala akina mdude ccm wataibuka
Mtu akiwa dictator tuseme siyo dictator? Mtu akisema utawala wa Magufuli watu wamepotea ni uongo? Yeye kajiita Jiwe, tukimuita Jiwe tunakosea?
 
Viongozi wa vyama wanapatikana 'by random sampling'. Kwa mantiki hiyo ni taswira ya jamii yetu ilivyo.

Ni kosa kudhani utapata maziwa kwenye kopo lenye maji. Tukitaka "out put' tofauti ni lazima tubadili " input". Maana yake ni ni? Tunapaswa kubadili jamii ambayo kwayo ndio viongozi hao hutokea na jamii hiyo ni mimi, wewe na anayesoma hapa.
 
Nitawaambia watz kitu kimoja: Nchi mkishakosea pale juu, basi huku chini kila kitu kinakwenda mrama. Kiongozi ni kichwa, kichwa kikishakuwa kibovu basi mwili wote unakwenda hovyo hovyo. Tulikosea mahali 2015.
Sidhani kama kwa sasa tatizo linaishia hapo tu. Siamini kwamba mabadiliko yakifanywa pale juu basi tutakuwa tumetatua tatizo lililopo
 
Inaonesha kutokuwa wakomavu tusipoona chimbuko tukang’ang’ania matokeo. Chimbuko la hali hii ni pale ambapo Upinzani chini ya akina Zitto na Tundu Lissu walipoanza kumtukana na kumdharau, kumyanyasa na kumbeza Rais aliyechaguliwa na watu Mwaka 2015. Na hii dhambi haitatuacha salama maana hata Tundu Lissu akichaguliwa kuwa Rais 2025, CCM watafanya wenzao wanayoyafanya. Ni kosa kumkashifu, kumdharau, na kumsigina kiongozi aliye madarakani maana mnajenga mfumo wa ajabu. Cc Retired, Salary Slip, Mmawia etc
Kwa mtazamo huo bado tunanyosheana vidole na haitaleta suluhisho. Pande zote zimehusika na makosa makubwa. Kumekuwa na filosofia kwamba ukikosean na mimi nakosea ili tusawazishe. Hii imefikia mahali pabaya na kueleta uozo wa ajabu. Dawa ni sisi kuwakataa wote
 
Back
Top Bottom