Siasa za nchi hii Mungu atunusuru

Sema Kweli

Member
Apr 12, 2013
53
20
Ndugu wana jamvi leo nimeona niseme tu kuwa kwa jinsi siasa zza nchi hii zinzvyo kwenda ni MUNGU peke yake anae weza kutunusuru na janga hili lililo mbele ya WATANZANI.

Leo nilikuwa nafuatilia siasa na jinsi watu mbali mbali wanavyo wanadi wagombea hapa Arusha,ila kilicho nitisha ni jinsi kiongozi wa ccm mwigulu anavyo endesha siasa zake siamini kama ana lengo jema na nchi hii.

Kwa sasa mwigulu anafanya siasa za aina ya ajabu sana,kwa kiongozi kama mwigulu kufanya siasa chafu kama hizi ni aibu nasema ni aibu na kama sio aibu basi ni hatari sana kwa mstakabali wa nchi yetu

Hapa naomba kuwakumbusha watanzania kuwa vyama vyote vitapita ila tanzania itaendelea kuwepo hata kama kuna watu kama kina mwigulu ambao nachelea kusema wana nia mbaya sana na taifa hili.

Nashangaa sana na sijui mwigulu anataka kuwaaminisha nini watanzania haswa pale anapo fikiri kuwa kutumia matukio kama ya ambayo sijui ni kwa nini chadema hawakupelekwa mahakamani kama ni wahusia ila sasa imekuwa kama ndo hoja ya kutafutia kura za huruma kwa wananchi ili tu kuwaaminisha kuwa haya ndio matukio ya chadema.

Ndugu zangu watanzani naomba tuiulize kama wenye serikali ambao tuliwapa utawala maana yake watulinde sisi na mali zetu nao wanalalamika nani sasa wakutulinda,kina mwigulu ni serikali hawapaswi kulalamika bali wanapaswa kutulinda na kutuhakikishia usalama wetu lakini leo hawezi nao wanalalamika na wanalalamika ili hali wanawajua wanao waumiz watanzani wenzetu tutachaje kufikiri kuwa wao ndio wanao wamwagia tindi kali na kujipendekez kuwati ili waje kuwatumia katika kampeni kama wanavyo fanya sasa?Nchi yetu imejikuta ikishuhudia matukio mbali mbali ambayo mpaka leo tumebakia gizani hatuji nini hatma yetu kwani leo ni huyo ila kesho unawez kuwa wewe kwa kuwa hakuna tena ulinzi na usalama wa raia na mali zao katika Nchi hii.

Ndugu zangu tuangalie aina hii ya siasa kwani siasa hizi hazina nia njema na Nchi hii zaida sana ni kutaka kututumbukiza katika vita na sio kama mwigulu anavyo fikiri,huwezi kuendelea kuwachonganisha watanzania ili hali ukijidai una uchungu nao ni vyema tukarudi katika msingi wa taifa letu tusipende kujidai tunahubiri amani wakati kiukweli ninyi wenyewe ndio mnao hatarisha amani ya Nchi hii.

Namalizia kwa kusema kwa watanzania wenzangu kama kuna mtu ambae anaweza kulitumbukiza taifa letu kwenye janga kubwa basi si mwangine bali ni mwigulu mchemba ni vyema sana tukachukua tahazari pale tunapo msikiliza kwani siasa za ndugu huyu ni za hatari kuliko hata ukimwi.

SISI NI WATANZANIA NA TUTAENDELEA KUWA WATANZANIA HATA KAMA TUKITOFAUTIANA ITIKADI ZETU.
TUKIFAHAMU HILO TUTAJUA NA KWA JINSI GANI TUTUMIE NDIMI ZETU ILI KULILINDA TAIFA LETU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.:A S-fire1:
 
hakuna la maana uliloandika,ni upuuzi tu.Sema mwigulu kafanya nini na siyo pumba nyingi.Sisi ambao hatuko arusha tutaaminije? Siasa majitaka ni shida sana aisee
 
sio mwigulu peke yake bali ni CCM yote anayoyafanya yamepitishwa na kubarikiwa na Jakaya Kikwete -Mwenyekiti
Philip Mangula -Makamu mwenyekiti
Abdurhaman Kinana-Katibu Mkuu
Nape NNauye-Katibu Mwenezi
Zakhia Meghji-Fedha
Asha Rose Migiro-CCM Mambo ya nje wenyeviti wa CCM,mikoa,wilaya,kata na vijiji ni mtandao huyo kijana walimwagia tindikali makusi ili waweze kumbanika kama samaki kwenye majukwaa
Anazunguka naye nchi nzika kwa ubani wa laki moja kila akionyeshwa na huku akitoa udenda,yeye Mwigulu hajali kwa sababu polisi wametaja kule singida alituma vijana na kuwanyesha viroba ndago-Iramba,yule mmuaji aliyemchinja mwenyekiti wa chadema Arumeru alimtorosha Mwigulu ni shetani na laana iko juu ya kichwa chake na kizazi chake chote
 
Sijui TUME yetu ya uchaguzi kama inaliona hili na kulifanyia kazi.Wasipoonywa hawa kwa sauti kubwa watatufikisha pabaya.
 
Ebu acha uchama. Siasa za cdm, ccm na vyama vingine zinafanana tu sio kusema Mwigulu tu.
 
Kwa yeyote mwenye mawazo kama yako anaweza ita upuuzi, ila kwa yule anae ona jinsi mwigulu anavyo yanya kwenye siasa zakeataelewa ninacha zungumza.umenitaka niseme mwigulu kafanya nini,ni sawa ila najua wewe pia uko humu na umeona video ya mkutano wake pale ngulelo,hauwezi kutumia matukio ambayo huna hakika kama unao watuhumu ndio wahusika ukafanya kuwa ndio mtaji wako wa kuombea kura.

Haiwezekani ninyi mna serikali halafu mshindwe kuwalinda watanzania matokeo yake mnatafuta wa kumbebesha lawama,
Leo hii kama sio kufilisika unadhani kuwa watu wa Arusha watabadilika kwa kuwa mnasema chadema wauwaji?
Tatizo mmeshindwa kujua nani adui yenu badala yake mnawekeza kwa chadema kuwa ndie adui yenu wakati sio.

wizi,ufisadi,dhuluma,rushwa,uhujumu uchumi,huduma mbovu za kijamii,kutokusikiliza walio waweka madarakani,Mngewekeza katika hayo wala kusingekuwa na tatizo ila kwa sababu waswahili walisha sema sikio la kufa siku zote halisikii dawa na ndio nyie ccm mlivyo.
 
Back
Top Bottom