usatrumpjr
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 2,237
- 2,897
Mkutano kuhusu madiwani wanaohama CHADEMA kwenda CCM kumhunga mkono Rais Magufuli.
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari amesema madiwani waliojiuzulu na kuhamia CCM na kupandishwa jukaani jana na kusema ni kumuunga mkono Rais Magufuli wanadanganya, wamefanya hivyo kuunga mkono rushwa.
Ameendelea kusema ana ushahidi wa madiwani hao wakipokea rushwa na alikuwa nao tangia zamani ila alikuwa anasubiri itokee ilivyotokea jana ili kusema ana ushahidi huo
Ameongezea kuwa madiwani wapya waliojiuzulu walikuwa ni wawili ila mmoja tu ndio alijitokeza jana baada ya mwingine kutafakari na kusita.
Ameongezea rushwa hiyo walipewa kwenye ofisi ya umma na yupo tayari kuupeleka kwa TAKUKURU na DCI endapo watatataka
Naye mbunge Godbless Lema amesema mkuu wa majeshi jana alisema wanajeshi wanatakiwa kukaa mbali na siasa, lakini baadae Rais akawaunganisha wanajeshi kuwa karibu na siasa
Amesema ukiona siasa zinafanyika mbele ya makamishna wa jeshi, mkuu wa majeshi, mkuu wa jeshi la polisi na mkurugenzi wa usalama wa taifa maana yake ni maelekezo huku chini kuwa vyombo vya usalama vilinde chama tawala kwa nguvu zote na kwa maana yake upinzani wana hali mbaya sana
Amesema amelaani kitendo kile cha kuchanganya kazi za jeshi ambazo kiutamaduni hufanyikia kambi za majeshi na jana ikafanyikia pale ikiwa na lengo la kuchukua madiwani wawili na walijua taarifa hizo wakiwa Nairobi
Lema ameongezea kwamba upo ushahidi wa bila shaka wa aliyekuwa anachoma shule Mkoa wa Arusha, amesema imebainika kinagaubaga ni nani alikuwa anachoma shule hizo ilikumhujumu aliyekuwepo
Amesema wataonyesha public kwenye projekta kuonyesha aliyekuwa akichoma shule
Amesema ushahidi huo walikuwa nao kitambo ila na walipanga kuutoa baada ya Lissu kupona ila tukiola jana limewatibua nyongo
Nassari ameongezea fedha walizokuwa wakihongwa zilikuwa zikitoka kwenye mifuko binafsi ya viongozi wanaowahonga na nyingine zilikuwa zikitoka kwenye mifuko ya Halmashauri
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari amesema madiwani waliojiuzulu na kuhamia CCM na kupandishwa jukaani jana na kusema ni kumuunga mkono Rais Magufuli wanadanganya, wamefanya hivyo kuunga mkono rushwa.
Ameendelea kusema ana ushahidi wa madiwani hao wakipokea rushwa na alikuwa nao tangia zamani ila alikuwa anasubiri itokee ilivyotokea jana ili kusema ana ushahidi huo
Ameongezea kuwa madiwani wapya waliojiuzulu walikuwa ni wawili ila mmoja tu ndio alijitokeza jana baada ya mwingine kutafakari na kusita.
Ameongezea rushwa hiyo walipewa kwenye ofisi ya umma na yupo tayari kuupeleka kwa TAKUKURU na DCI endapo watatataka
Naye mbunge Godbless Lema amesema mkuu wa majeshi jana alisema wanajeshi wanatakiwa kukaa mbali na siasa, lakini baadae Rais akawaunganisha wanajeshi kuwa karibu na siasa
Amesema ukiona siasa zinafanyika mbele ya makamishna wa jeshi, mkuu wa majeshi, mkuu wa jeshi la polisi na mkurugenzi wa usalama wa taifa maana yake ni maelekezo huku chini kuwa vyombo vya usalama vilinde chama tawala kwa nguvu zote na kwa maana yake upinzani wana hali mbaya sana
Amesema amelaani kitendo kile cha kuchanganya kazi za jeshi ambazo kiutamaduni hufanyikia kambi za majeshi na jana ikafanyikia pale ikiwa na lengo la kuchukua madiwani wawili na walijua taarifa hizo wakiwa Nairobi
Lema ameongezea kwamba upo ushahidi wa bila shaka wa aliyekuwa anachoma shule Mkoa wa Arusha, amesema imebainika kinagaubaga ni nani alikuwa anachoma shule hizo ilikumhujumu aliyekuwepo
Amesema wataonyesha public kwenye projekta kuonyesha aliyekuwa akichoma shule
Amesema ushahidi huo walikuwa nao kitambo ila na walipanga kuutoa baada ya Lissu kupona ila tukiola jana limewatibua nyongo
Nassari ameongezea fedha walizokuwa wakihongwa zilikuwa zikitoka kwenye mifuko binafsi ya viongozi wanaowahonga na nyingine zilikuwa zikitoka kwenye mifuko ya Halmashauri