Siasa za kilaghai za Polepole: Awamu ya Nne aliunga mkono Katiba Mpya; Awamu ya Tano alikataa, Awamu ya Sita anaitaka kwa gia ya Shule ya Uongozi

Akiwa kwenye tume ya Warioba aliwahi kusikika akisema kuna chama bila msaada wa polisi hakiwezi kushinda uchaguzi. Je ameshafikia hiyo topic kwenye shule yake?
Awamu ya tano alisimamia na kuongoza ujambazi wa kisiasa ambao haijawahi kutokea afrika mashariki na kati
 
Hata km mnamchukia sikilizeni mawazo yake
Huyo mtu ni mnafiki tu hana mawazo ya maana zaidi ya kupigania maslahi yake,wakati wa Kikwete alipoteuliwa kwenye tume ya katiba alikuwa akiongea tofauti hadi akazawadiwa u DC ,alivyoingia Magufuli alipewa uenezi CCM alianza kuongea tofauti na sasa kapigwa chini anaongea tofauti inawezekana kabisa kama angebaki madarakani hata kipindi hiki angeongea tofauti kwahiyo yupo kimaslahi zaidi.
 
Huu ulaghai wa hali ya juu unaofanywa na Polepole, alikuwa anapinga katiba mpya enzi ya mwendazake, alitumia muda mwingi kukata viuno akicheza mabolingo huku akijirekodi katika camera, alishuhudia na akawa sehemu ya tawala ya hovyo kabisa katika historia ya nchi hii,alikuwa sehemu ya tawala katili ya kiuwaji isiyojali demokrasia wala haki. Eti leo anahubiri shule ya uongozi.

Anatembea na jina la Rais wake mfukoni akiwa hana imani na Samia, anatembea huku nakule akishawishi wana CCM wamkubali mtu wake kisa alifanya kazi na JPM, na HPP alikuwa sehemu ya walioshinikiza SSH asichukue mamlaka, Mwenzie wa Kemondo katulia,yeye bado anaipima mamlaka ya nyumba kubwa, mamlaka ijibu mapigo kwa ukali wote

Namshauri huyo anayejazwa upepo na HPP asijiingize mkenge,ataisoma namba
Anayumbishwa na njaa yake. Hana njia nyingine ya kuganga njaa.
 
Back
Top Bottom