Rohombaya
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 13,055
- 10,337
Dah...wamiliki wa mabasi waliokuwa wanapandisha nauli kiholela vima yanagonga pichuKitendo cha Polepole kutumia mali ya umma ili kutafuta umaarufu kwa chama chake kilichochoka cha CCM kimewatafakarisha baadhi ya wadau wa usafiri, ambao wameweka msimamo wa kutokutumia usafiri huo abadani.
Polepole si kiongozi wa serikali wala si Ofisa wa Shirika la reli ama wizara husika, haifahamiki alikopata kiherehere cha kuingilia mipango isiyomhusu na kujichomeka kwenye kinachoitwa uzinduzi wa safari za treni Kilimanjaro - Dar, Watanzania si wajinga kiasi hicho.
Wizara ya Uchukuzi na Shirika la Reli msitumike kishamba namna hii, sasa kwa taarifa yenu wadau hawatatumia huo usafiri wenu wa kisiasa. Wameapa kuendelea kutumia Ngorika, Dar Express, Kidia one, Kilimanjaro na Sai Baba.
Sasa siku mkianza kutukanwa hadharani kwa kuchelewesha gawio msimlilie mtu, mfuateni Polepole awasaidie.