Siasa ni mchezo mchafu?

aspen

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
501
165
Kwa nini watu wenye heshima mbele ya jamii yetu wanashiriki siasa kama ni mchezo mchafu au una maana nyingine
 
Natatizika mno nikisoma posts za wanazuoni wa jf,Zinamashiko na uhalisia yakinifu.UCHAWI, UFISADI,UDINI, TINDIKALI na mengineyo yashaanza kuzoeleka kama misamiati ya siasa nchini.Je nini sababu ya haya?Watu hawa ni Mungu yupi wanamwabudu? Uadilifu uko wapi?
 
Habari za leo ndg zangu ktk jf.mie kuna haya maneno nimekuwa nikiyasikia kwa muda mrefu sasa 1.siasa ni uongo unaokaribiana na ukweli 2.siasa ni mchezo mchafu haya maneno inawezekana sio mie tu ambae nimepata kuyasikia,wakati mwingine huwa kama nayaamini hasa ninapo tambua kwamba hata sheria huwa zinatungwa na wanasiasa na wakati mwingine wanasiasa hao hao wanaweza wakavunja sheria waliyotunga,kuna msemo unasema mtunga sheria ndiye mvunja sheria,wana jf nawaombeni mnitoe tongo kwa kunipa tafsiri nzuri ya maana ya hayo maneno pia mnipe maana nzuri ya neno siasa.
 
Mkuu mbona ID yako ni ya siku nyingi.
Kwa humu JF siasa maana yake ni kuvaa gwanda, kuimba piiiipoz!!
Na usijue maana yake!
 
Kwa nini watu wenye heshima mbele ya jamii yetu wanashiriki siasa kama ni mchezo mchafu au una maana nyingine

sina maana ingine hapa nataka watu wanieleweshe,tena nahitaji wale tu ambao waliwahi kusikia maneno hayo,mie pia nahitaji kuwahoji kama ulivyo nihoji wewe.
 
Natatizika mno nikisoma posts za wanazuoni wa jf,Zinamashiko na uhalisia yakinifu.UCHAWI, UFISADI,UDINI, TINDIKALI na mengineyo yashaanza kuzoeleka kama misamiati ya siasa nchini.Je nini sababu ya haya?Watu hawa ni Mungu yupi wanamwabudu? Uadilifu uko wapi?

asante kwa kunielewa,umetazama mbali tena nahisi ukivunja ukimya nitakuwa nimetosheka kabisa.
 
Siasa ni safi ila wana ccm ndio wachafu.wezi.wauza unga,mafisadi.waongo na wanapeana vyeo kwa kujuana.mbona ulaya safi?sema wana ccm wachafu
 
Siasa ni mchezo mchafu,saa nyingine siasa ujaa fitina,ahadi za uongo kama za nyinyiemu pale jangwani,

siasa ni mchezo mchafu kwani upelekea watu kutolewa uhai wao kama walivyo mtoa uhai kamanda wetu pale arumeru.

Siasa ni mchezo mchafu,kwani upelekea watu wenye heshima kudhalilishwa kama walivyo dhalilishwa wabunge wetu na mwigulu nchemba.

Siasa mchezo mchafu kwani uzaa vibaraka wano pandikizwa kwaajili ya kuharibu siasa iliyo nzuri,kama alivyo shibuda ambaye ni kibaraka wa nyinyiemu ndani ya cdm.

Siasa ni mchezo mchafu kwani ujaa mbinu za wizi,fitina ili kutimiza malengo ya kisiasa,mbinu hizi huambata na wizi wa kura kama wanvyo fanya nyinyiemu, pia siasa huambata na fitina kama anazo ziendesha nape.
 
Siasa ni mchezo mchafu,saa nyingine siasa ujaa fitina,ahadi za uongo kama za nyinyiemu pale jangwani,

siasa ni mchezo mchafu kwani upelekea watu kutolewa uhai wao kama walivyo mtoa uhai kamanda wetu pale arumeru.

Siasa ni mchezo mchafu,kwani upelekea watu wenye heshima kudhalilishwa kama walivyo dhalilishwa wabunge wetu na mwigulu nchemba.

Siasa mchezo mchafu kwani uzaa vibaraka wano pandikizwa kwaajili ya kuharibu siasa iliyo nzuri,kama alivyo shibuda ambaye ni kibaraka wa nyinyiemu ndani ya cdm.

Siasa ni mchezo mchafu kwani ujaa mbinu za wizi,fitina ili kutimiza malengo ya kisiasa,mbinu hizi huambata na wizi wa kura kama wanvyo fanya nyinyiemu, pia siasa huambata na fitina kama anazo ziendesha nape.

kama nikweli hayo yapo basi nikweli siasa ni mchezo mchafu.
 
siasa si mchezo mchafu ila wachafu wengi wanaona ndo nyumba yao.
Dhana hii ilishaingiaga hata kwenye mziki wa kizazi kipyaa watu wengi walisema hip hop ni uhuni lakini mwisho wa siku ukweli ukafunuka !
 
....inawezekana siasa ina mlazimisha mwanasiasa kusema uongo ili afanikishe malengo.....kwamba mkinichagua mimi basi tanzania nitaifanya iwe kama paris, nitahakikisha kila mtz anamiliki gari,pia elimu kuanzia primary mpaka chuo itakuwa bure.ukiwapa tu kura wanakugeuka na kukuambia mlinukuu vibaya.
 
Ni mtizamo wa kizamani kufikiri kwamba siasa ni mchezo mchafu,mtizamo huu ulitokana na vitendo vya ulaghai a.k.a ahadi hewa na nadharia nyingi za kufikirika ambazo haziwezi tekelezeka,kwa kiswahili cha sasa longolongo kwa sana.Ukipima mafanikio hakuna kilichofanyika , na kwakuwa watanzania tulikuwa bado kwenye blanketi zito tukawa tuna waamini yaani tunaishi kwa matumaini ya kwamba siku moja watabadilika lakini wapi.Hatimae sisi watawaliwa tumebadilika na kuanza kujua tofauti ya pumba na mchele. Na hiki ndo chanzo cha mbinu mbalimbali chafu(kwa wanasiasa- watawala) kutaka ku-win mawazo ya watu ambao tayari walisha anza kustuka juu ya longolongo zao ambazo zimewapelekea kuonja mema ya uongozi na hivyo kutotaka kuachia kamwe.Achilia mbali longolongo ,rushwa ambayo wakati fulani waliibatiza jina zuri kwao la takrima,wengine wanaenda kwa Kalumanzila ili waendelee kula mema ya nchi na wengine hufitiniana (kupinga fitina) n.k. Yote hii ni kwa sababu ya kutaka kujilimbikizia mali(ubinafsi) na sio kusaidia wananchi unao watawala.Kama mtawala (mwanasiasa)alitumia pesa kupata uongozi unategemea hizo pesa alizotumia atazirudishaje, je atakubali kuachia ngazi kabla hajarudisha hizo pesa alizo tumia kumweka madarakani? Thubutu!!!.Kwa vyovyote vile lazima atafanya faulo ili abaki kwenye ulaji na hapo kudhihirisha kwamba "kweli siasa ni mchezo mchafu'
 
Back
Top Bottom