Siasa ni kazi, na waachiwe wenye kazi yao.

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
1,985
1,282
Siasa kwa mwanasiasa ni kazi, kama ilivyo biashara kwa mfanyabiashara na kilimo kwa mkulima. Zitto Z Kabwe akikaa mahabusu kwa makosa ya kisiasa ni sawa sababu ni kiongozi wa chama na siasa kwake ni kazi. Hii haina tafauti kwa mkulima kugongwa na nyoka shambani au kwa malaya kupata HIV, naam, imethibiti ajali kazini.

Mwanachama wa chama cha siasa ambaye si mwanasiasa kuwekwa rumande au gerezani kwa sababu ya siasa na kuumia na hata kufa sababu ya siasa ni ujinga ambao anatakiwa kujivua na kukaa nawo mbali, nao uwe mbali naye.

Kwa mimi mwanachama nikiwekwa ndani kwasababu ya chama ni ujinga. Kwanini nasema hivyo???

Mosi, siasa kwangu si kazi ni dhahiri nikiwekwa ndani kazi zangu zitasimama na wanaonitegemea watalala njaa. Nitawezaje kulima au kufanya biashara nikiwa rumande??? Hivi mimi nikiwekwa Rumande, Zitto au chama changu kitalisha na kutatua changamoto za familia yangu??? Kama hilo haliwezekani, kwanini sasa nifanye mambo ya kuwagharimu wanaonitegemea????

Lakini Zitto na Mbowe akiwekwa rumande au gerezani, kazi yao, ambayo ni siasa, haisimami, sababu wakiwa ndani kwa makosa ya siasa, kazi yao(siasa), ndiyo inanoga. Full kiki!!!

Pili.
Kuwa mwanachama wa chama cha siasa hakunifanyi hata kidogo niwe radhi kuweka rehani maisha yangu na wanaonitegemea.

Naweza kuweka maisha yangu rehani sababu ya siasa endapo tu:

Mosi nchi yangu ikivamiwa na nchi nyingine na uhuru wake wa kujiamulia mambo yake kuwa hatarini. Hapo sitakubali, nitapambana hadi tone la mwisho la damu yangu.

Pili, ikitokea serikali ikaninyima haki yangu ya kuchagua mtu wa kuniongoza kila kipindi cha miaka mitano au miaka ambayo tumekubaliana kama taifa kwa njia ya uwazi na ukweli, au bunge likavunjwa kinyume cha katiba, na au serikali ikikithirisha kukakaidi hukumu na maagizo ya mahakama hususani juu ya mambo yanayogusa haki za msingi za raia.

Hapa namaanisha mahakama na bunge zikiingiliwa na serikali kwa kiwango cha kuvunjwa vipengele vya katiba vilivyounda bunge na mahakama, ni dhahiri serikali hiyo inapoteza uhalali wa kisiasa na kisheria wa kuheshimiwa na kufuatwa na kila mwananchi wa nchi hii.

Serikali ya namna hiyo niko tayari kuitoa kwa jasho na damu yangu. Serikali ya CCM, kama mpinzani, nitapambana kuitoa kwa kura yangu, sababu haina sifa ya kutolewa kwa jasho na damu yangu Tukumbuke CCM haikujipeleka ikulu yenyewe, bali ni wananchi walio wengi ndiyo waliyoipeleka ikulu kwa kutumia sanduku la kura. Hata kama sikupigia kura, lakini hakufanyi wengi waliopigia kuwe si kitu na kwa kubezwa ikiwa uchaguzi huo ulifata sheria.

TANBIHI.
Niliposema kwa wanasiasa sawa kuwekwa ndani sababu ya siasa, siku maanisha ni sawa serikali kuwashikilia wanasiasa kinyume cha sheria, nilicho maanisha wao kuwekwa ndani ni suala la kawaida lakini kwa mimu nikiwekwa ndani kudhulumiwa na kujidhulumu sababu si mwanasiasa.

Kila muomba chumvi, huombea chungu chake,
Hata mtandika jamvi, hulenga ubavu wake,
Aliyeuchonga mvi, alijua windo lake,

Dotto Rangimoto
Jini Kinyonga
+255762845394 Morogoro.
0a8b12b11f090e4def7df17346b7ad82.jpg
 
Siasa kwa mwanasiasa ni kazi, kama ilivyo biashara kwa mfanyabiashara na kilimo kwa mkulima. Zitto Z Kabwe akikaa mahabusu kwa makosa ya kisiasa ni sawa sababu ni kiongozi wa chama na siasa kwake ni kazi. Hii haina tafauti kwa mkulima kugongwa na nyoka shambani au kwa malaya kupata HIV, naam, imethibiti ajali kazini.

Mwanachama wa chama cha siasa ambaye si mwanasiasa kuwekwa rumande au gerezani kwa sababu ya siasa na kuumia na hata kufa sababu ya siasa ni ujinga ambao anatakiwa kujivua na kukaa nawo mbali, nao uwe mbali naye.

Kwa mimi mwanachama nikiwekwa ndani kwasababu ya chama ni ujinga. Kwanini nasema hivyo???

Mosi, siasa kwangu si kazi ni dhahiri nikiwekwa ndani kazi zangu zitasimama na wanaonitegemea watalala njaa. Nitawezaje kulima au kufanya biashara nikiwa rumande??? Hivi mimi nikiwekwa Rumande, Zitto au chama changu kitalisha na kutatua changamoto za familia yangu??? Kama hilo haliwezekani, kwanini sasa nifanye mambo ya kuwagharimu wanaonitegemea????

Lakini Zitto na Mbowe akiwekwa rumande au gerezani, kazi yao, ambayo ni siasa, haisimami, sababu wakiwa ndani kwa makosa ya siasa, kazi yao(siasa), ndiyo inanoga. Full kiki!!!

Pili.
Kuwa mwanachama wa chama cha siasa hakunifanyi hata kidogo niwe radhi kuweka rehani maisha yangu na wanaonitegemea.

Naweza kuweka maisha yangu rehani sababu ya siasa endapo tu:

Mosi nchi yangu ikivamiwa na nchi nyingine na uhuru wake wa kujiamulia mambo yake kuwa hatarini. Hapo sitakubali, nitapambana hadi tone la mwisho la damu yangu.

Pili, ikitokea serikali ikaninyima haki yangu ya kuchagua mtu wa kuniongoza kila kipindi cha miaka mitano au miaka ambayo tumekubaliana kama taifa kwa njia ya uwazi na ukweli, au bunge likavunjwa kinyume cha katiba, na au serikali ikikithirisha kukakaidi hukumu na maagizo ya mahakama hususani juu ya mambo yanayogusa haki za msingi za raia.

Hapa namaanisha mahakama na bunge zikiingiliwa na serikali kwa kiwango cha kuvunjwa vipengele vya katiba vilivyounda bunge na mahakama, ni dhahiri serikali hiyo inapoteza uhalali wa kisiasa na kisheria wa kuheshimiwa na kufuatwa na kila mwananchi wa nchi hii.

Serikali ya namna hiyo niko tayari kuitoa kwa jasho na damu yangu. Serikali ya CCM, kama mpinzani, nitapambana kuitoa kwa kura yangu, sababu haina sifa ya kutolewa kwa jasho na damu yangu Tukumbuke CCM haikujipeleka ikulu yenyewe, bali ni wananchi walio wengi ndiyo waliyoipeleka ikulu kwa kutumia sanduku la kura. Hata kama sikupigia kura, lakini hakufanyi wengi waliopigia kuwe si kitu na kwa kubezwa ikiwa uchaguzi huo ulifata sheria.

TANBIHI.
Niliposema kwa wanasiasa sawa kuwekwa ndani sababu ya siasa, siku maanisha ni sawa serikali kuwashikilia wanasiasa kinyume cha sheria, nilicho maanisha wao kuwekwa ndani ni suala la kawaida lakini kwa mimu nikiwekwa ndani kudhulumiwa na kujidhulumu sababu si mwanasiasa.

Kila muomba chumvi, huombea chungu chake,
Hata mtandika jamvi, hulenga ubavu wake,
Aliyeuchonga mvi, alijua windo lake,

Dotto Rangimoto
Jini Kinyonga
+255762845394 Morogoro.
0a8b12b11f090e4def7df17346b7ad82.jpg
jamaa yupo chattle utapigiwa simu ya uteuzi jtatu maana umekumbuka kuweka namba yako
 
Hii ndio elimu ya siasa inayotakiwa kutolewa kwa wiki mara mbili hususani kwa vijana wenye jazba na mihemko!
 
Aya subiri teuzi. Ila hauta faidi maana tar 26 April kuna anguko kubwa linaluja
 
Sijui kama unajua ulichoandika. Hasa kwenye aya ya 9 ( ikitokea serikali ikaminya....).
Kwanza tukubaliane kwamba watu wote hatuwezi kufikiri kama ww. Hiyo jamii haipo popote duniani. Ni lazima kutakuwa na watu wenye mawazo na maamuzi ya ajabu pengine kiwango cha kutafasiriwa kama uvunjifu wa amani. Acha wakereketwa wafe kwa ajili ya vyama vyao, ww kaa pembeni. Hujui kama kuna watu mechi ya simba na yanga huwa wanapoteza maisha. Hujui kama kuna watu wanajiua kwa sababu ya kuachwa na mpenzi wake wa kike/kiume?

Kama ulivyosema kwa Zitto na Mbowe, je ni hao tu ndo wanastahili kulala selo za polisi? Vipi viongozi wa ngazi za chini. Hao waliolala selo kwa sababu ya siasa je unajua kazi zao. Huenda ni waajiriwa wa chama na hivyo wako kazini.

Acha kuamua kwa niaba ya mwenzio. Kinachotakiwa ni sheria kufuatwa tu. Anayekosea anashughulikiwa kwa kadiri ya sheria za nchi, wote tuwe sawa mbele ya sheria

Mfano wa nyoka na mkulima ni mfano wa KIJINGA KABISA. Ulitakiwa useme kama wanasiasa wanadhani wanaminywa haki zao, na kule kwa wakulima labda utumie mfano wa kwamba wananyimwa haki ya kuuza mazao yao kwenye masoko ambayo yatawalipa ili kujikwamua na umasikini.

Wanasiasa wote wawe sawa kwenye mzani wa sheria, wakulima wote wawe sawa mbele ya sheria na ww unayejitanabaisha kuwa mfanyabiashara basi uwe sawa na wenzio mbele ya sheria.
 
Back
Top Bottom