Siasa ni Ajira, kuzuia mikutano ni kunyima kundi fulani ulaji

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,864
SIASA NI AJIRA, KUZUIA MIKUTANO NI KUNYIMA KUNDI FULANI ULAJI

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Moja ya mambo ambayo nilipishana na JPM Kwenye utawala wake ni suala la kuzuia mikutano ya Kisiasa ya nje hasa Kwa wapinzani huku CCM wakiendelea na mikutano kwa mwamvuli wa kukagua miradi ya serikali iliyoandikwa kwenye ilani ya CCM.

Naona Jambo lile lile linataka kutendeka katika uongozi wa Rais Samia Suluhu.

Hii nchi Ajira zimekuwa ngumu na viongozi tayari wameshaonyesha uwezo mdogo wa kushughulikia suala hili.

Siasa ni Ajira, Siasa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine.

Wapo watu wamesoma mpaka Degree nne za masuala ya Siasa.

Siasa pia ni hobby, Siasa wakati mwingine Kwa wengine ni Mchezo na burudani.

Unazuia mikutano ya nje ya Siasa alafu unaacha mikutano ya injili, mikutano ya Wasanii ambayo huitwa matamasha ya muziki, Kwa kweli ni kuwanyima haki kundi la wanasiasa.

Wanasiasa waachwe wafanye kazi zao ikiwemo mikutano ya nje ili kujenga vyama vyao na kutafuta wanachama wapya kama ilivyo kwa mikutano ya Dini ambapo madhehebu hutumia Kueleza Imani yao ili kupata ushawishi Kwa watu na kujipatia waumini wapya.

Kuzuia mikutano ya nje ni kuzuia ukuaji wa vyama husika moja Kwa moja.

Wakati upande wa CCM inajitangaza kupitia serikali kutokana na kuwa yenyewe ndio imeunda serikali.

Nafikiri serikali iachane na mpango huo wa kubana haki ya Uhai wa vyama vingine. Kuzuia mikutano ya nje ya Kisiasa ni kuzorotesha ukuaji WA vyama husika.

Hata hivyo, mikutano mara nyingi haifanyiki nyakati za mchana ambao ni muda wa kazi. Hufanyika jioni kabisa kuanzia mida ya saa tisa mpaka saa kumi na mbili.

Sio sababu ya maana ya kuzuia mikutano ya nje ya Kisiasa labda sababu za hila na ukandamizaji.

Wengine watasema, kuruhusu kuendelea Kwa mikutano ya nje ya Kisiasa kutaathiri na kuichanganya serikali, kwani wapinzani wataishambulia na kuikosoa serikali huku wakiitoa serikali katika shabaha ya kuleta maendeleo.

Hiyo sio kweli kwa sababu serikali au CCM hakitakuwa na ulazima wa kuhofia kusikiliza hoja za upande wa pili ikiwa wao wenyewe wanafanya na kutekeleza hoja na mambo ya msingi yanayotakiwa ndani ya jamii. Lakini endapo upande wa pili utakuwa na hoja za manufaa zaidi ya CCM basi ni dhahiri shahiri hofu lazima ikae juu yao, na ndio maana wataona hatari ya mikutano hiyo.

Katiba mpya ni muhimu ikiwa bado kuna changamoto za namna hii ndani ya nchi yetu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Kinole, Morogolo
 
Sawa! Siasa ni ajira. Lakini nafikiri si ajira kama unavyofiria ww. Kwamba, kila siku watu wafanye mikutano, bila ya kujua watapata wapi pesa. Kanisani wanafanya mikutano, wanatoa sadaka. Sasa hiyo mikutano ya kumtukana Rais, wanapata wapi pesa ?Au unataka iwe nchi ya mikutano ya siasa huku, wakipewa ruzuku tu.

Hakuna kazi, nyingine. Kama ikiwa hivyo, nani atafundisha shuleni na vyuoni au nani atatibu wagonjwa hospital. Au nani atafanya shughuli nyingine? Mm nafikiri, hata tukibadilisha katiba, tuwe na kipengere kwamba siasa ni wakati wa uchaguzi tu.

Si kila siku, unaongea siasa. Eti Kwa kuwa una ruzuku. Nafikiri si sawa. Kule USA, au China au German. Naona siasa ni wakati wa uchaguzi. Huku tunakusanya vijana, badala tuwambie watafute kazi. Tunataka wafanye siasa. Hakika Afrika itachukua muda mrefu kuendelea.
 
Sawa! Siasa ni ajira. Lakini nafikiri si ajira kama unavyofiria ww. Kwamba, kila siku watu wafanye mikutano, bila ya kujua watapata wapi pesa. Kanisani wanafanya mikutano, wanatoa sadaka. Sasa hiyo mikutano ya kumtukana Rais, wanapata wapi pesa ?Au unataka iwe nchi ya mikutano ya siasa huku, wakipewa ruzuku tu.

Hakuna kazi, nyingine. Kama ikiwa hivyo, nani atafundisha shuleni na vyuoni au nani atatibu wagonjwa hospital. Au nani atafanya shughuli nyingine? Mm nafikiri, hata tukibadilisha katiba, tuwe na kipengere kwamba siasa ni wakati wa uchaguzi tu.

Si kila siku, unaongea siasa. Eti Kwa kuwa una ruzuku. Nafikiri si sawa. Kule USA, au China au German. Naona siasa ni wakati wa uchaguzi. Huku tunakusanya vijana, badala tuwambie watafute kazi. Tunataka wafanye siasa. Hakika Afrika itachukua muda mrefu kuendelea.
Umewahi kuombwa pesa na wale waliokuwa wanahudhuria mikutano ya siasa siku za nyuma? Au CCM wakifanya mikutano huwa wanakuja kwako kukuomba ugali?

Anyway, umeshaoneshwa muda wa kufanyika hiyo mikutano ya siasa, lakini bado una mawazo mgando ya kizee yaliyopitwa na wakati.
 
Wengine watasema, kuruhusu kuendelea Kwa mikutano ya nje ya Kisiasa kutaathiri na kuichanganya serikali, kwani wapinzani wataishambulia na kuikosoa serikali huku wakiitoa serikali katika shabaha ya kuleta maendeleo.
Na mm niongezee swali.

Kwani, kwa mfano serikali imeweka mkandarasi wa kujenga barabara fulani, mikutano ya hadhara itamwondoa mkandarasi site?
 
Sawa! Siasa ni ajira. Lakini nafikiri si ajira kama unavyofiria ww. Kwamba, kila siku watu wafanye mikutano, bila ya kujua watapata wapi pesa. Kanisani wanafanya mikutano, wanatoa sadaka. Sasa hiyo mikutano ya kumtukana Rais, wanapata wapi pesa ?Au unataka iwe nchi ya mikutano ya siasa huku, wakipewa ruzuku tu.

Hakuna kazi, nyingine. Kama ikiwa hivyo, nani atafundisha shuleni na vyuoni au nani atatibu wagonjwa hospital. Au nani atafanya shughuli nyingine? Mm nafikiri, hata tukibadilisha katiba, tuwe na kipengere kwamba siasa ni wakati wa uchaguzi tu.

Si kila siku, unaongea siasa. Eti Kwa kuwa una ruzuku. Nafikiri si sawa. Kule USA, au China au German. Naona siasa ni wakati wa uchaguzi. Huku tunakusanya vijana, badala tuwambie watafute kazi. Tunataka wafanye siasa. Hakika Afrika itachukua muda mrefu kuendelea.

Watafute kazi ipi wakati kazi Yao ni Siasa??

Unafikiri chama kinategemea ruzuku pekeake kujiendesha??

Unafikiri ni Jambo gani linalofanya chama kikue na kisambaa Maeneo mengine??
 
Sawa! Siasa ni ajira. Lakini nafikiri si ajira kama unavyofiria ww. Kwamba, kila siku watu wafanye mikutano, bila ya kujua watapata wapi pesa. Kanisani wanafanya mikutano, wanatoa sadaka. Sasa hiyo mikutano ya kumtukana Rais, wanapata wapi pesa ?Au unataka iwe nchi ya mikutano ya siasa huku, wakipewa ruzuku tu.
Hivi wewe naye ni miongoni mwa watanzania walio hai? Ndiyo maana nchi hii haipigi hatua aisee!

Vyama vya siasa vimeanzishwa na vinatakiwa kufanya shughuli zake kwa mujibu wa katiba.

Sasa Samia na katiba nani anapaswa kufuatwa??

Halafu pqmoja na kwamba hili ni jukwaa huru ni vema kama jambo hulijui ukaishia kulisoma tu na usitoe maoni. Mengi uliyo yaandika yanatia kinyaa.
 
Sawa! Siasa ni ajira. Lakini nafikiri si ajira kama unavyofiria ww. Kwamba, kila siku watu wafanye mikutano, bila ya kujua watapata wapi pesa. Kanisani wanafanya mikutano, wanatoa sadaka. Sasa hiyo mikutano ya kumtukana Rais, wanapata wapi pesa ?Au unataka iwe nchi ya mikutano ya siasa huku, wakipewa ruzuku tu.

Hakuna kazi, nyingine. Kama ikiwa hivyo, nani atafundisha shuleni na vyuoni au nani atatibu wagonjwa hospital. Au nani atafanya shughuli nyingine? Mm nafikiri, hata tukibadilisha katiba, tuwe na kipengere kwamba siasa ni wakati wa uchaguzi tu.

Si kila siku, unaongea siasa. Eti Kwa kuwa una ruzuku. Nafikiri si sawa. Kule USA, au China au German. Naona siasa ni wakati wa uchaguzi. Huku tunakusanya vijana, badala tuwambie watafute kazi. Tunataka wafanye siasa. Hakika Afrika itachukua muda mrefu kuendelea.
Siasa haikuwepo kipindi chote cha dictator uchwara. Kulikuwa na ajira????
Acha kuongea UONGO bhana.
Unalinganisha ujerumani na Tanzania???
 
Siasa haikuwepo kipindi chote cha dictator uchwara. Kulikuwa na ajira????
Acha kuongea UONGO bhana.
Unalinganisha ujerumani na Tanzania???
Kwa kuwa umeanzisha Uzi.Nilitegemea utajenga hoja ,kudefend Uzi wako.Lakini una majibu mepesi na matusi.Jenga hoja mahiri kutetea Uzi wako.Kwanini kuwe na mikutano.Na je mikutano itasaidia kuleta maendeleo?Na je mikutano ni kama aina ya soga tu ,zisizo na manufaa?Je ,kwannn tusiiache serikali ifanye kazi.Na sisi tuendelee na kazi zetu.Uchaguzi ukifika tufanye mikutano.Au mikutano ,itatupatia pesa ya kijikimu?
 
Hivi wewe naye ni miongoni mwa watanzania walio hai? Ndiyo maana nchi hii haipigi hatua aisee!

Vyama vya siasa vimeanzishwa na vinatakiwa kufanya shughuli zake kwa mujibu wa katiba.

Sasa Samia na katiba nani anapaswa kufuatwa??

Halafu pqmoja na kwamba hili ni jukwaa huru ni vema kama jambo hulijui ukaishia kulisoma tu na usitoe maoni. Mengi uliyo yaandika yanatia kinyaa.
Kwa hiyo ,tunaweza kuamua kufuata katiba hata kama katiba imeruhusu kitu kisicho na manufaaa?Naomba unijibu hoja zifuatazo:Je kufanya mikutano kila siku kutaweza kuwasaidia wananchi kupata pesa za kujikimu?Je ,mikutano hiyo ,ya siasa itawasaidia vijana kupata ajira?Je kwanini nchi za ulaya vyama vya siasa vinafanya mikutano wakati wa uchaguzi tu?Je ,watanzania wengi wanapenda soga kuliko kufanya kazi?
 
SIASA NI AJIRA, KUZUIA MIKUTANO NI KUNYIMA KUNDI FULANI ULAJI

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Moja ya mambo ambayo nilipishana na JPM Kwenye utawala wake ni suala la kuzuia mikutano ya Kisiasa ya nje hasa Kwa wapinzani huku CCM wakiendelea na mikutano kwa mwamvuli wa kukagua miradi ya serikali iliyoandikwa kwenye ilani ya CCM.

Naona Jambo lile lile linataka kutendeka katika uongozi wa Rais Samia Suluhu.

Hii nchi Ajira zimekuwa ngumu na viongozi tayari wameshaonyesha uwezo mdogo wa kushughulikia suala hili.

Siasa ni Ajira, Siasa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine.

Wapo watu wamesoma mpaka Degree nne za masuala ya Siasa.

Siasa pia ni hobby, Siasa wakati mwingine Kwa wengine ni Mchezo na burudani.

Unazuia mikutano ya nje ya Siasa alafu unaacha mikutano ya injili, mikutano ya Wasanii ambayo huitwa matamasha ya muziki, Kwa kweli ni kuwanyima haki kundi la wanasiasa.

Wanasiasa waachwe wafanye kazi zao ikiwemo mikutano ya nje ili kujenga vyama vyao na kutafuta wanachama wapya kama ilivyo kwa mikutano ya Dini ambapo madhehebu hutumia Kueleza Imani yao ili kupata ushawishi Kwa watu na kujipatia waumini wapya.

Kuzuia mikutano ya nje ni kuzuia ukuaji wa vyama husika moja Kwa moja.

Wakati upande wa CCM inajitangaza kupitia serikali kutokana na kuwa yenyewe ndio imeunda serikali.

Nafikiri serikali iachane na mpango huo wa kubana haki ya Uhai wa vyama vingine. Kuzuia mikutano ya nje ya Kisiasa ni kuzorotesha ukuaji WA vyama husika.

Hata hivyo, mikutano mara nyingi haifanyiki nyakati za mchana ambao ni muda wa kazi. Hufanyika jioni kabisa kuanzia mida ya saa tisa mpaka saa kumi na mbili.

Sio sababu ya maana ya kuzuia mikutano ya nje ya Kisiasa labda sababu za hila na ukandamizaji.

Wengine watasema, kuruhusu kuendelea Kwa mikutano ya nje ya Kisiasa kutaathiri na kuichanganya serikali, kwani wapinzani wataishambulia na kuikosoa serikali huku wakiitoa serikali katika shabaha ya kuleta maendeleo.

Hiyo sio kweli kwa sababu serikali au CCM hakitakuwa na ulazima wa kuhofia kusikiliza hoja za upande wa pili ikiwa wao wenyewe wanafanya na kutekeleza hoja na mambo ya msingi yanayotakiwa ndani ya jamii. Lakini endapo upande wa pili utakuwa na hoja za manufaa zaidi ya CCM basi ni dhahiri shahiri hofu lazima ikae juu yao, na ndio maana wataona hatari ya mikutano hiyo.

Katiba mpya ni muhimu ikiwa bado kuna changamoto za namna hii ndani ya nchi yetu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Kinole, Morogolo
Kama ni ajira tusubili hadi walioisomea watakapokuwa ni wanasiasa. Siyo hawa wapiga debe kwa madili ya ruzuku.
 
Kwa hiyo ,tunaweza kuamua kufuata katiba hata kama katiba imeruhusu kitu kisicho na manufaaa?Naomba unijibu hoja zifuatazo:Je kufanya mikutano kila siku kutaweza kuwasaidia wananchi kupata pesa za kujikimu?Je ,mikutano hiyo ,ya siasa itawasaidia vijana kupata ajira?Je kwanini nchi za ulaya vyama vya siasa vinafanya mikutano wakati wa uchaguzi tu?Je ,watanzania wengi wanapenda soga kuliko kufanya kazi?
Kama Kuna jambo liko kwenye katiba na halitakiwi namna pekee ya kuliondoa Ni kuibadili katiba yenyewe.

Kwa maneno yako ni dhahiri unaungana na wanaodai katiba mpya.
 
Kwa kuwa umeanzisha Uzi.Nilitegemea utajenga hoja ,kudefend Uzi wako.Lakini una majibu mepesi na matusi.Jenga hoja mahiri kutetea Uzi wako.Kwanini kuwe na mikutano.Na je mikutano itasaidia kuleta maendeleo?Na je mikutano ni kama aina ya soga tu ,zisizo na manufaa?Je ,kwannn tusiiache serikali ifanye kazi.Na sisi tuendelee na kazi zetu.Uchaguzi ukifika tufanye mikutano.Au mikutano ,itatupatia pesa ya kijikimu?

Huyo hajaanzidha Uzi Mkuu.

Naona umechanganyikiwa.

Wengine wakifanya Siasa wanaizuiaje serikali kufanya shughuli zake??

Unaijua Katiba ya nchi yako mku?
 
Back
Top Bottom