Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Siasa zote zinazofuata misingi hii katika uendeshaji wake ni siasa za kihuni na endapo sisi Watanzania tutaendelea kuzishabikia zitaiangamiza nchi yetu!!
Mtindo wa kuendesha siasa kwa kufuata misingi hii mufulisi imekuwa inashika kasi siku hata siku na inaonekana ina wafuasi wengi sana na inashabikiwa na wanasiasa uchwara ambao idadi yao kwa sasa si haba! Siku hizi si ajabu kukuta mtu anaomba nafasi ya uongozi kwa kigezo cha "mtoto wa nyumbani" huku akimnanga mpinzani wake kwa kigezo cha "wakuja"
Udini ni kitu kilichopandikizwa kwenye jamii yetu kwa maslahi ya CCM lakini nasi kama jamii tumeanza kuona kwamba ni jambo la kushabikia na kulipigia upatu. Wakristo wengi ndani ya CCM ya sasa hawajioni wako salama na waislam nao wanawatilia shaka wakristo waliomo CCM.
Kuna mvumo mkubwa sana ndani ya CHADEMA na uungwaji mkono na wakristo wanaoamini kwamba CHADEMA ni njia pekee iliyotayarishwa na Mungu "kuiokoa" Tanzania na ndiyo maana hata humu JF maneno kama "mungu wa Israel ametenda" au "Bwana atatuvusha salama" hayakosekani kutoka kwa wachangiaji wanaoamini kwamba wao ni CHADEMA damudamu!!
Ukipita kwenye baadhi ya Misikiti na kusikia shutuma zinazoelekezwa kwa CHADEMA utagundua kwamba ni kazi kwa muislamu asiye mpembuzi wa mambo kuweza kuwa mwanachama wa CHADEMA. Hata zile kauli kwamba CHADEMA ilipata kura zaidi ya CUF kwenye ule uchaguzi wa Marudio kule Zanzibar eti kwa sababu eneo la Uzini lina Wakristo wengi ni kielelezo tosha cha kuonesha ni nini kinaendelea kwenye duru za siasa hapa nchini mwetu!!
Lakini siasa hizi zinakuzwa na Rais wetu ambaye ndiye yeye kwa kinywa chake alisema kwamba kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 kulikuwa na udini bila ya kusema udini huo ulikuwa ni dhidi ya nani na yeye kama Rais wa Nchi atachukua hatua gani!!?
Kuna watu kwenye siasa zetu ni Waoga waogopao waoga walio na woga wa UKWELI. Ukweli ni kwamba haitatokea hata siku moja nchi hii ikaongozwa na dini fulani dhidi ya dini nyingine au kabila fulani dhidi ya makabila mengine. kwa pamoja kama taifa ndiyo tutaijenga nchi yetu!!
- Udini
- Ukabila
- Ubaguzi wa Jinsia na Umri
- Ubaguzi wa Rangi
- Ubaguzi wa mahali mtu atokako
- Ubaguzi wa hali ya mtu kiuchumi
Mtindo wa kuendesha siasa kwa kufuata misingi hii mufulisi imekuwa inashika kasi siku hata siku na inaonekana ina wafuasi wengi sana na inashabikiwa na wanasiasa uchwara ambao idadi yao kwa sasa si haba! Siku hizi si ajabu kukuta mtu anaomba nafasi ya uongozi kwa kigezo cha "mtoto wa nyumbani" huku akimnanga mpinzani wake kwa kigezo cha "wakuja"
Udini ni kitu kilichopandikizwa kwenye jamii yetu kwa maslahi ya CCM lakini nasi kama jamii tumeanza kuona kwamba ni jambo la kushabikia na kulipigia upatu. Wakristo wengi ndani ya CCM ya sasa hawajioni wako salama na waislam nao wanawatilia shaka wakristo waliomo CCM.
Kuna mvumo mkubwa sana ndani ya CHADEMA na uungwaji mkono na wakristo wanaoamini kwamba CHADEMA ni njia pekee iliyotayarishwa na Mungu "kuiokoa" Tanzania na ndiyo maana hata humu JF maneno kama "mungu wa Israel ametenda" au "Bwana atatuvusha salama" hayakosekani kutoka kwa wachangiaji wanaoamini kwamba wao ni CHADEMA damudamu!!
Ukipita kwenye baadhi ya Misikiti na kusikia shutuma zinazoelekezwa kwa CHADEMA utagundua kwamba ni kazi kwa muislamu asiye mpembuzi wa mambo kuweza kuwa mwanachama wa CHADEMA. Hata zile kauli kwamba CHADEMA ilipata kura zaidi ya CUF kwenye ule uchaguzi wa Marudio kule Zanzibar eti kwa sababu eneo la Uzini lina Wakristo wengi ni kielelezo tosha cha kuonesha ni nini kinaendelea kwenye duru za siasa hapa nchini mwetu!!
Lakini siasa hizi zinakuzwa na Rais wetu ambaye ndiye yeye kwa kinywa chake alisema kwamba kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 kulikuwa na udini bila ya kusema udini huo ulikuwa ni dhidi ya nani na yeye kama Rais wa Nchi atachukua hatua gani!!?
Kuna watu kwenye siasa zetu ni Waoga waogopao waoga walio na woga wa UKWELI. Ukweli ni kwamba haitatokea hata siku moja nchi hii ikaongozwa na dini fulani dhidi ya dini nyingine au kabila fulani dhidi ya makabila mengine. kwa pamoja kama taifa ndiyo tutaijenga nchi yetu!!