Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,564
- 46,109
Baada ya uchaguzi wa mwaka huu ndipo utachipuka upinzani halisi na thabiti zaidi japo utachukua muda mrefu kuwa imara. Hoja yangu imejengwa juu ya mtazamo huu
1) Kuanzia mwaka 2021 hakutakuwa tena na sababu za watu kuhama vyama vyao.Hadi kufikia mwisho wa mwaka huu wanasiasa wote maarufu katika vyama vya upinzani watakuwa wamehamia chama tawala au vyama vingine vya upinzani,pia nafasi za uteuzi kwa wahamaji vyama zitapungua kama sio kwisha kabisa.Hivyo kuanzia mwaka kesho na kuendelea kuhama vyama ni jambo litakalokosa mashiko na hamasa stahiki.
2) Kuanzia mwaka huu haitakuwa tena rahisi kwa mtu kutoka chama tawala na kupewa nafasi za juu katika vyama vya upinzani vyenye ushawishi mkubwa.Hali hii itaendelea kuimarika zaidi kuanzia mwaka 2021.
3) Wapinzani wengi waliohamia chama tawala hawatapata nafasi za kugombea ubunge au udiwani na wengi wao watapoteza kabisa umaarufu wao kisiasa na wengine wengi wataachana na siasa.
4) Minyukano ya kisiasa itakuwa ndani zaidi ya chama tawala badala ya ilivyo sasa ambapo nguvu kubwa imeelekezwa kwa upinzani unaozidi kufifia.Hali hii itaupa nguvu upinzani kupumua, kujikongoja na kujipanga upya lakini ukiwa na uzoefu wa hali ya juu na mikakati makini zaidi dhidi ya chama dola.
5) Wananchi wengi wataacha kushangilia siasa za kuhama vyama iwe ni kutoka chama tawala kwenda upinzani au kinyume chake.Kuhama vyama zitakua ni siasa zilizopitwa na wakati kwa watu wengi.
6) Upinzani utakuwa umemulikwa kiasi cha kutosha na dola na ule utakaoweza kusalia umesimama utajisahihisha na makandokando yake,utapunguza pia kutoa sababu hata ndogo za kusakamwa na kuufanya uwe imara zaidi.
1) Kuanzia mwaka 2021 hakutakuwa tena na sababu za watu kuhama vyama vyao.Hadi kufikia mwisho wa mwaka huu wanasiasa wote maarufu katika vyama vya upinzani watakuwa wamehamia chama tawala au vyama vingine vya upinzani,pia nafasi za uteuzi kwa wahamaji vyama zitapungua kama sio kwisha kabisa.Hivyo kuanzia mwaka kesho na kuendelea kuhama vyama ni jambo litakalokosa mashiko na hamasa stahiki.
2) Kuanzia mwaka huu haitakuwa tena rahisi kwa mtu kutoka chama tawala na kupewa nafasi za juu katika vyama vya upinzani vyenye ushawishi mkubwa.Hali hii itaendelea kuimarika zaidi kuanzia mwaka 2021.
3) Wapinzani wengi waliohamia chama tawala hawatapata nafasi za kugombea ubunge au udiwani na wengi wao watapoteza kabisa umaarufu wao kisiasa na wengine wengi wataachana na siasa.
4) Minyukano ya kisiasa itakuwa ndani zaidi ya chama tawala badala ya ilivyo sasa ambapo nguvu kubwa imeelekezwa kwa upinzani unaozidi kufifia.Hali hii itaupa nguvu upinzani kupumua, kujikongoja na kujipanga upya lakini ukiwa na uzoefu wa hali ya juu na mikakati makini zaidi dhidi ya chama dola.
5) Wananchi wengi wataacha kushangilia siasa za kuhama vyama iwe ni kutoka chama tawala kwenda upinzani au kinyume chake.Kuhama vyama zitakua ni siasa zilizopitwa na wakati kwa watu wengi.
6) Upinzani utakuwa umemulikwa kiasi cha kutosha na dola na ule utakaoweza kusalia umesimama utajisahihisha na makandokando yake,utapunguza pia kutoa sababu hata ndogo za kusakamwa na kuufanya uwe imara zaidi.