Siamini kama Halima Mdee anaijua Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania kumzidi Mzee Msekwa aliyeiasisi katiba hiyo mwaka 1977

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,752
139,556
Watu wenye akili wanaelewa wazi kuwa Halima James Mdee kuendelea kubishana na kamati kuu ya CHADEMA ni kupoteza muda wake bure kwa sababu swala hili limeshafika mwisho

Binafsi nimemuelewa Spika mstaafu wa Bunge ambaye sahihi yake imo kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nimeona ni kama amelitamatisha swala hili kiitifaki zaidi. Kwamba ni heri ya nusu shari kuliko shari kamili.

Kauli ya Spika mstaafu Msekwa kwamba "Daktari akipokea wagonjwa akiisha kuwatibu wanaondoka au wakifa wanaondoka" imejaa hekima kubwa ambayo unaweza usiione kwa haraka haraka.

Halima James Mdee na wenzake wakubali kuwa waliingizwa "force king" ili draft likamilike mapema na sasa mchezo umekwisha.

Mimi ni nani nimbishiye muasisi wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Maendeleo hayana vyama!
 
Japo anaweza kuwa haijui katiba zaid ya Msekwa, lkn acha amjambi.she mw/kiti na genge lake. Bora Halima Mdee kaonesha uthubutu na kugoma kuburuzwa kila siku kwa maslahi ya mtu/watu fulan ndan ya chama.
 
Screenshot_20201128-202957.png


johnthebaptist wewe ni mnafiki na msukule unaesimamia chochote ambacho kinapangwa huko ccm dhidi ya Chadema.

Kupitia mabandiko yenu na comments zenu tunajua mipango inayopangwa huko ccm pamoja na kuweweseka kwa serikali hii isiyojua isimamie kipi
 
Watu wenye akili wanaelewa wazi kuwa Halima James Mdee kuendelea kubishana na kamati kuu ya Chadema ni kupoteza muda wake bure kwa sababu swala hili limeshafika mwisho

Binafsi nimemuelewa Spika mstaafu wa bunge ambaye sahihi yake imo kwenye katiba ya JMT na nimeona ni kama amelitamatisha swala hili kiitifaki zaidi.
Kwamba ni heri ya nusu shari kuliko shari kamili.

Kauli ya Spika mstaafu Msekwa kwamba " Daktari akipokea wagonjwa akiisha kuwatibu wanaondoka au wakifa wanaondoka" imejaa hekima kubwa ambayo unaweza usiione kwa haraka haraka.

Halima James Mdee na wenzake wakubali kuwa waliingizwa " force king" ili draft likamilike mapema na sasa mchezo umekwisha.

Mimi ni nani nimbishiye muasisi wa katiba ya JMT?!!

Maendeleo hayana vyama!
Wewe una Phd ya unafiki.
 
Watu wenye akili wanaelewa wazi kuwa Halima James Mdee kuendelea kubishana na kamati kuu ya Chadema ni kupoteza muda wake bure kwa sababu swala hili limeshafika mwisho

Binafsi nimemuelewa Spika mstaafu wa bunge ambaye sahihi yake imo kwenye katiba ya JMT na nimeona ni kama amelitamatisha swala hili kiitifaki zaidi.
Kwamba ni heri ya nusu shari kuliko shari kamili.

Kauli ya Spika mstaafu Msekwa kwamba " Daktari akipokea wagonjwa akiisha kuwatibu wanaondoka au wakifa wanaondoka" imejaa hekima kubwa ambayo unaweza usiione kwa haraka haraka.

Halima James Mdee na wenzake wakubali kuwa waliingizwa " force king" ili draft likamilike mapema na sasa mchezo umekwisha.

Mimi ni nani nimbishiye muasisi wa katiba ya JMT?!!

Maendeleo hayana vyama!
Hapo si suala la ujuzi wa katiba bali ni suala la fursa na kucheza na sheria.

Kamati kuu chadema ilishapigwa hapo amini usiamini. Kesi itaenda mahakamani na wabunge watapeta mpaka 2025
 
Japo anaweza kuwa haijui katiba zaid ya Msekwa, lkn acha amjambi.she mw/kiti na genge lake. Bora Halima Mdee kaonesha uthubutu na kugoma kuburuzwa kila siku kwa maslahi ya mtu/watu fulan ndan ya chama.
Asingepolwa ubunge wake kijambazi na Gwaji boy na system,haya yangetokea?
 
View attachment 1637054

johnthebaptist wewe ni mnafiki na msukule unaesimamia chochote ambacho kinapangwa huko ccm dhidi ya Chadema.

Kupitia mabandiko yenu na comments zenu tunajua mipango inayopangwa huko ccm pamoja na kuweweseka kwa serikali hii isiyojua isimamie kipi
Comment yake ilinipelekea kujiuliza alikua nani niliyemsoma ame commment kitu hicho.
 
Comment yake ilinipelekea kujiuliza alikua nani niliyemsoma ame commment kitu hicho.
Ni hatari sana! Alafu huyu anaonekana ni mmoja wa wanaopelekewa ujumbe kuwa waandike nini kulingana na shinikizo la wananchi mitandaoni mpaka mtaani.
Records za huyu msukule zinaakisi nini kimepangwa kufanywa na serikali ikishirikiana na ccm dhidi ya wapinzani wa kweli.

Mfatilie huyu mtu utaelewa mengi mkuu
 
Hapo si suala la ujuzi wa katiba bali ni suala la fursa na kucheza na sheria.

Kamati kuu chadema ilishapigwa hapo amini usiamini. Kesi itaenda mahakamani na wabunge watapeta mpaka 2025
Nasikia ktk katiba ya CDM ukipeleka maswala ya chama mahakamani umekwisha, kama alivyo Fanya zitto na ikawa mwisho wake na akaona aende kuanzisha chama chake...

Sasa kama hao wanawake wana nguvu na ubavu basi waige ya zitto waende wakaanzishe chama chao alafu turudi ktk uchaguzi au waende haya nccr, tlp etc wataipata ya wananchi
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom