Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,512
Msimamo wangu ni huu: inashangaza sana kwa nini kuna muonekano kana kwamba jaribio la kutaka kumuua Tundu Lisu halijafanyiwa/ halifanyiwi uchunguzi na vyombo vya dola.
Neno muhimu hapo ni ‘muonekano’. Kama uchunguzi unafanyika nyuma ya pazia, basi sawa. Lakini machoni mwa wengi hakuna kinachoonekana kufanyika.
Hali hiyo inazua maswali mengi sana.
Baada ya hayo machache, tulonge sasa kuhusu ninachotaka kukijadili hapa.
Ni hivi, mimi kwa kweli siamini kabisa kama CHADEMA na washirika wao wanataka serikali ivalie njuga suala la uchunguzi wa shambulio lile.
Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu muonekano wa kutolifanyia uchunguzi shambulio lile umewapa ‘kiki’ CHADEMA.
CHADEMA sasa wamepata fimbo ya kuichapia CCM.
Mtu yeyote akianza mdahalo kidogo tu na kamanda yeyote yule, haimchukui muda kwa kamanda huyo kuleta habari za ukosefu wa uchunguzi wa jaribio la kumuua Lisu. Ukosefu wa uchunguzi huo umekuwa nongwa. Umekuwa ndo silaha [hoja] kuu ya CHADEMA.
Hata mhanga wa jaribio naye amekuwa akiitumia sana hiyo silaha kuwachapia nayo CCM.
Sasa pata picha serikali inalivalia njuga hilo suala na kufanya uchunguzi wa kweli. Hao CHADEMA watabaki na nini?
Kwanza watayakubali matokeo ya huo uchunguzi? Au watataka matokeo hayo yahitimishe tu kuwa Rais Magufuli ndiye mhusika namba moja? Nje ya hapo hawatoyakubali?
Naamini kabisa kuwa uchunguzi wa kweli ukifanyika, CHADEMA watahamisha magoli. Watakosa kabisa hoja kama vile ambavyo hoja ya ufisadi walivyoitupilia mbali baada ya kubadili gia angani.
Kwa hiyo, kwa mtaji huo, hilo shambulio dhidi ya Lissu na aftermath yake, CHADEMA wamenufaika nalo sana kisiasa. Si ajabu hata Lisu mwenyewe hajui kuwa chama chake kimenufaika kisiasa kupitia mgongo wake. Na ndo maana siamini kabisa kuwa CHADEMA iko inataka uchunguzi wa kweli ufanyike.
Siku uchunguzi wa kweli ukifanyika, CHADEMA ndo kwisha habari yake.
Neno muhimu hapo ni ‘muonekano’. Kama uchunguzi unafanyika nyuma ya pazia, basi sawa. Lakini machoni mwa wengi hakuna kinachoonekana kufanyika.
Hali hiyo inazua maswali mengi sana.
Baada ya hayo machache, tulonge sasa kuhusu ninachotaka kukijadili hapa.
Ni hivi, mimi kwa kweli siamini kabisa kama CHADEMA na washirika wao wanataka serikali ivalie njuga suala la uchunguzi wa shambulio lile.
Kwa nini nasema hivyo? Nasema hivyo kwa sababu muonekano wa kutolifanyia uchunguzi shambulio lile umewapa ‘kiki’ CHADEMA.
CHADEMA sasa wamepata fimbo ya kuichapia CCM.
Mtu yeyote akianza mdahalo kidogo tu na kamanda yeyote yule, haimchukui muda kwa kamanda huyo kuleta habari za ukosefu wa uchunguzi wa jaribio la kumuua Lisu. Ukosefu wa uchunguzi huo umekuwa nongwa. Umekuwa ndo silaha [hoja] kuu ya CHADEMA.
Hata mhanga wa jaribio naye amekuwa akiitumia sana hiyo silaha kuwachapia nayo CCM.
Sasa pata picha serikali inalivalia njuga hilo suala na kufanya uchunguzi wa kweli. Hao CHADEMA watabaki na nini?
Kwanza watayakubali matokeo ya huo uchunguzi? Au watataka matokeo hayo yahitimishe tu kuwa Rais Magufuli ndiye mhusika namba moja? Nje ya hapo hawatoyakubali?
Naamini kabisa kuwa uchunguzi wa kweli ukifanyika, CHADEMA watahamisha magoli. Watakosa kabisa hoja kama vile ambavyo hoja ya ufisadi walivyoitupilia mbali baada ya kubadili gia angani.
Kwa hiyo, kwa mtaji huo, hilo shambulio dhidi ya Lissu na aftermath yake, CHADEMA wamenufaika nalo sana kisiasa. Si ajabu hata Lisu mwenyewe hajui kuwa chama chake kimenufaika kisiasa kupitia mgongo wake. Na ndo maana siamini kabisa kuwa CHADEMA iko inataka uchunguzi wa kweli ufanyike.
Siku uchunguzi wa kweli ukifanyika, CHADEMA ndo kwisha habari yake.