Si vyema kupotosha uma kwa maneno usiyo na uhakika nayo

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454
Kuna post moja iko humu jamvini Ina potosha watu kuhusu ruzuku na vyama vya siasa na kuwa maneno haya kayasema mbowe,ni kweli alisema lakina haku maanisha hivyo kama baadhi ya watu wanavyo taka kuaminisha watu,alisema namnukuu,chadama kama chama hakitategemea fedha za ruzuku katika kampeni zake za arumeru,kwani zimekua zikilemaza vyama na kuwa tegemezi na kuwa kampeni hizo zitagarimiwa na wananchi wenyewe kwa kukichangia chama kwenye mikutano itakayo kuwa inafanyika.ndipo alipoamua kutembeza bakuli na akatoa namba za simu kwa atakae penda kutoa mchango wake.
si vizuri kumlisha mtu maneno ambayo hakusema.
 
Mkuu hakuna mtu ambaye hakumuelewa Mbowe pale uwanjani bali ni makusudi kabisa. Mbowe alikusudia siyo kwamba hawataki na hawatachukua ruzuku bali wao wametoka nje ya box kwa kuona ruzuku ndiyo chanzo cha unafiki ndani ya vyama vingi vya upinzani. Akasema kama CCM wanadhani wakikata ruzuku CDM haina chake basi wamefulia au wameingia choo cha kike.
Akaenda mbali kuwa chama kimeamua kushirikisha wananchi kwa kuanzia kampeni hizo na mambo mengine yatafuata lengo ikiwa ni kuondoa nadharia ya kuona wakati wa kampeni ni wa mavuno na kuongeza commitment kwa watu waliojitolea kutokukubali kusalitiwa kwa maana watahisi dhamana ya chama ni kila mmoja na siyo viongozi kupitia ruzuku.
 
T2015CDM mbona hawajasema Mbowe kasema mbunge mmoja wa CDM ni sawa na wabunge 30 wa magamba? Au katika hilo hakukuwa na hoja bali ukweli mtupu na akazidisha wampe Nassari ili waongeze silaha nyingine bungeni.
 
Back
Top Bottom