Si Vipapai, bali ni barabara

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Tukaambiwa wale 27 wa ajali ya Mbeya ni kafara ya saidia Taifa Stars iwafunge Machinga, Huko Singida wamefariki watatu sijui ilikuwa ndio kafara ya kumtafuta aliyemlawiti mtoto mdogo?

Waswahili tunapenda kukimbilia imani chafu panapotokea balaa. Mudhihir, Kapuya, Mwakanjuki na sasa Mama Mbatia. Si kufuru za Chadema au CUF, bali ni ubovu wa barabara zetu ulioandamana na sheria mbovu, ulafi wa wenye magari na kukosekana kwa nidhamu kwa madereva ambayo ungeambatana na mafunzo bora.

Kwa nini mpaka leo Taifa halijaanza mpango rasmi wa kupanua barabara kuu? Kwa nini kila kuna kuna matuta makubwa katika barabara kama tuta la viazi?

Ni kwa kuwa tumeachilia siasa ishikilie uhandisi na mipango bora.

Kama Serikali itakuwa makini, waache kutafuta mchawi na kufuja pesa hovyo na kuwanza kampeni rasmi ya kupanua barabara zetu, ambazo zitakua na alama bora na udhibiti wa mwendo kasi unaofanya na madereva.

Jee ile wiki ya Usalama barabarani ishakufa au ndio mtaji wa trafiki?

Kama Wabunge na viongozi wametishika, basi wapeleke mswaada wa kujenga barabara pana na zenye lami kuunganisha mikoa na si kujenga viwanja vya ndege au kununua tundege tudogo eti kuepuka ajali.

Si kipapai, kafara au malipo kwa kufuru ya ufisadi, bali ni barabara nyembamba na mbovu!

Mungu aziweke mahali pema roho za wote waliopoteza masha kwa ajali hizi na awape nguvu na afya walio majeruhi.
 
watu wanaweka siasa na kuweka kila sehemu ili wafanikiwe na nia zao zitimie ! tuweni makini na kila kinachoandikwa humu jamani !

BORA WEWE REV. UMESEMA ! ningesema mie ningeambiwa ccm wewe ! (halafu huo uanachama wamenipa wao) siasa hiyo !
 
Wanaotengeneza ni akina makamba. Unategemea nini?? Wachojua kuhubiri ni amani, umoja, mshikamano, maelewano, etc. Ukiwapeleka kwenye issue nzito kama hizo, akili zao zinakwenda likizo.
 
makamba ni kiongozi wa ccm na sio serikali ! tofautisheni vitu vingine bana !

kila kitu ccm mweeh !
 
Rev. Kishoka,

Nakubaliana na mengine yote uliyoyandika isipokuwa hilo la kupanua barabara, je utapanua kama ile barabara ya Morogoro mpaka Mbeya ili iwe na lane ngapi? Je ni economically feasible kufanya hivyo? Tuna pesa za kufanya hivyo wakati robo tatu ya nchi yetu haina barabara za maana? Je hata tukipanua tutapunguza ajali? Ukiangalia barabara nzuri TZ ndio zinaongoza kwa ajali, yaani ile ya Dar mpaka Arusha na ya Dar mpaka Mbeya. Uk

Nafikiri muhimu kwa TZ ni alama barabarani, sheria za kubana madereva wanaokimbiza magari, ubora wa magari, ubora wa barabara kwamba zisiwe na mashimo ambayo yanaweza kusababisha ajali na elimu ya kutosha kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara.
 
...

Si kipapai, kafara au malipo kwa kufuru ya ufisadi, bali ni barabara nyembamba na mbovu!

Mungu aziweke mahali pema roho za wote waliopoteza masha kwa ajali hizi na awape nguvu na afya walio majeruhi.

Nakubaliana nawe mchungaji wa kondoo wa bwana. Tatizo ni kuwa hawa jamaa wanapokuwa bungeni akili zao zinakwenda likizo. Labda wanaweza kujifunza katika hilo.

Lakini usishangae vilevile kusikia wanapendekeza bungeni kila mbunge apewe mkopo wa helikopta ili kuepuka ajali za barabarani. Hao ndio wabunge wetu.
 
Rev. Kishoka,

Nakubaliana na mengine yote uliyoyandika isipokuwa hilo la kupanua barabara, je utapanua kama ile barabara ya Morogoro mpaka Mbeya ili iwe na lane ngapi? Je ni economically feasible kufanya hivyo? Tuna pesa za kufanya hivyo wakati robo tatu ya nchi yetu haina barabara za maana? Je hata tukipanua tutapunguza ajali? Ukiangalia barabara nzuri TZ ndio zinaongoza kwa ajali, yaani ile ya Dar mpaka Arusha na ya Dar mpaka Mbeya. Uk

Nafikiri muhimu kwa TZ ni alama barabarani, sheria za kubana madereva wanaokimbiza magari, ubora wa magari, ubora wa barabara kwamba zisiwe na mashimo ambayo yanaweza kusababisha ajali na elimu ya kutosha kwa madereva na watumiaji wengine wa barabara.

Yaani tunahitaji watu kama 5 wengine wenye mtazamo kama wako, we are free to go ! maneno mazuri, yasiyo na siasa, viongozi wanakosolewa when needed, KWA KWELI NAKUPONGEZA KWA DHATI !

Pongezi zangu kwako haimaniishi serikali isikosolewe pale inapokosea, bali siasa ndio zisihusishwe na kila kitu !

Shukrani !
 
Nakubaliana nawe mchungaji wa kondoo wa bwana. Tatizo ni kuwa hawa jamaa wanapokuwa bungeni akili zao zinakwenda likizo. Labda wanaweza kujifunza katika hilo.

Lakini usishangae vilevile kusikia wanapendekeza bungeni kila mbunge apewe mkopo wa helikopta ili kuepuka ajali za barabarani. Hao ndio wabunge wetu.

mwanamalundi mbona hili limeshapendekezwa kuwa zitumike Dar kuwasafirisha viongozi kutoka uwanja wa ndege nk!

Talking about priorities!
 
Yaani tunahitaji watu kama 5 wengine wenye mtazamo kama wako, we are free to go ! maneno mazuri, yasiyo na siasa, viongozi wanakosolewa when needed, KWA KWELI NAKUPONGEZA KWA DHATI !

Pongezi zangu kwako haimaniishi serikali isikosolewe pale inapokosea, bali siasa ndio zisihusishwe na kila kitu !

Shukrani !

Kada, nami namshukuru sana ndugu Mtanzania kwa msimamo wake mzuri katika maswala ya usalama mabarabarani,(nikiwa katibu nitampa cheyo cha kusimamia hilo kama alivyo omba awali!! lol).

Kwenye wekundu hapo juu, tatizo siasa zimejipenyeza almost katika kila nyanja ya maisha ya Mtanzania... angalia na ikiwezekana toa mfano wa vitu ambavyo kama matukio ya kulalamikiwa havina links na siasa..

SteveD.
 
Kada, nami namshukuru sana ndugu Mtanzania kwa msimamo wake mzuri katika maswala ya usalama mabarabarani,(nikiwa katibu nitampa cheyo cha kusimamia hilo kama alivyo omba awali!! lol).

Kwenye wekundu hapo juu, tatizo siasa zimejipenyeza almost katika kila nyanja ya maisha ya Mtanzania... angalia na ikiwezekana toa mfano wa vitu ambavyo kama matukio ya kulalamikiwa havina links na siasa..

SteveD.

Hicho kitu hata mie nimejionea, na ndio maana nikaamua kumpongeza from the bottom of my heart !

pongezeni watu pale wanapostahili ! jifunzeni jamani its that easy !

Great for noticing the same thing steve-d !
 
makamba ni kiongozi wa ccm na sio serikali ! tofautisheni vitu vingine bana !

kila kitu ccm mweeh !

Kada, sikuelewi unaposema nitofautishe CCM na serikali. Wanaotengeneza sera (i.e., policies) ni akina nani??? kwa nini kikwete alipitia CCM ili kuingia ikulu??? Kikwete anatekeleza ilani ipi?? ni nani anatunza mafaili ya hiyo ilani??? Kada usinitie majaribuni, nikaanza kuhoji uelewa wako. Hata hivyo siamini kama ulichoandika hapo juu, ndicho ulichotaka kumaanisha. Naheshimu michango yako.
 
Kada, sikuelewi unaposema nitofautishe CCM na serikali. Wanaotengeneza sera (i.e., policies) ni akina nani??? kwa nini kikwete alipitia CCM ili kuingia ikulu??? Kikwete anatekeleza ilani ipi?? ni nani anatunza mafaili ya hiyo ilani??? Kada usinitie majaribuni, nikaanza kuhoji uelewa wako. Hata hivyo siamini kama ulichoandika hapo juu, ndicho ulichotaka kumaanisha. Naheshimu michango yako.

acha nikuulize kitu kidogo, serikali inapoamua kitu vyama vya siasa huusishwa ikiwa pamoja na ccm ? nafahamu unachosema, angalau viongozi wa ccm huwa na ilani ambayo ni kama dira yao ya kuaccomplish hizo ahadi, kumaanisha tokea wapange kwenye chama, chama hakitohusika tena katika maamuzi ya serikali.

pia kuna tofauti kubwa, si unaona mfano marehemu mama Mbatia ( Mungu amrehemu) alipokuwa anaenda nadhani kwenye shughuli za chama, lakini alitumia gari binafsi na kuiacha ya serikali serikalini !
 
Mwafrika, the two are synchronized. You can never never, never separate them. Labda kuna watu wanafikiri bado tupo primary school.

Hilo ndilo tatizo, no wonder unawaona wanaipondea JF kila siku kwa dhana kuwa watu hapa hawajui kinachoendelea. Kila siku EL anasema kuwa serikali inatekeleza sera ya sisiemu.

Leo ukiwaonyesha upungufu wa sera ya sisiemu wanasema unaleta siasa na kukuita mpinzani!

Kazi wanayo. Watabanwa hapa, watazomewa na wananchi huko mikoani hadi wakome!
 
Rev. Kishoka said:
bali ni ubovu wa barabara zetu ulioandamana na sheria mbovu, ulafi wa wenye magari na kukosekana kwa nidhamu kwa madereva ambayo ungeambatana na mafunzo bora.

Sio hilo tu, vile vile magari mengi ambayo yako barabarani Tanzania hayastahili kuwepo barabarani. Serikali imejisahau kiasi kwamba njia kuu za usafiri wa uhakika kwa raia (Mizigo yao Mazao n.k.) imeachwa ifanywe kiholela pasipo uthibiti wa kutosha.
 
Sio hilo tu, vile vile magari mengi ambayo yako barabarani Tanzania hayastahili kuwepo barabarani. Serikali imejisahau kiasi kwamba njia kuu za usafiri wa uhakika kwa raia (Mizigo yao Mazao n.k.) imeachwa ifanywe kiholela pasipo uthibiti wa kutosha.

nadhani halmashauri za wilaya zinatakiwa more responsible !
 
sasa hivi nina kila sababu ya kuanza kuiponda JF, mara ya kwanza nilikuw nawaponda mafisadi wake ! kwa nini mfute thread niliyoanzisha kumuuliza zitto maswali ?? tena nimepost tena mara 5 na mmefuta still, WHY ?????????????????

lakini sitoweka hizo chuki za moderators niichukie JF maana inalewa watoto wengi hadi yatima !
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom