Si vibaya ' tukishea ' Elimu hii pamoja ili Siku zingine Teja ' akichomoa Betri ' tusiipe Hasara Tanzania yetu.

Kuna haja mamlaka kuja na kanuni ili tankers zote zitegenezewe namna mabetri yafichwe kwenye kama "kasanduku" ka chuma na paweko na padlock.

Hii nchi wajinga wengi mno tayari nimesikia wakisema Mungu ndiye alipanga wafe kifo cha aina hiyo.

Ili muwndelee kujichotea vya watu
 
Mi naona simple kuliko zote ni kuwa makini na mtu anaye elekea kwenye kichwa cha gari,ukiona mtu wa aina hiyo kukimbia ndio utakuwa msaada wako...
 
hiyo ndo akili ya wabongo wengi tumekuwa wajinga na watu wa mihemko hasi, fatilia jamii yetu toa hata ushaur mzuri mtu atatafuta pa kukupinga ili aonekane haya ni.mambo ya ajabu sn
Nimeleta huu Uzi hapa ili tujifunze kwa faida ya baadae na sijauleta ili uanze Kunishambulia Mimi kana kwamba ndiyo Teja Mchomo Betri. Siku zingine muwe mnasoma Kwanza Uzi, Muuelewe ndipo mjibu na siyo Kukurupuka kama hivi halafu mnajikuta naanza Kuwapuuzeni. Huu ni Uzi wa Kusaidiana na siyo wa Kulaumiana kama una Stress zako za Kimaisha mlalamikie Mwenyezi Mungu na siyo Mimi sawa?
 
Sawa kuficha betr je teja akija na sigara
Kuna haja mamlaka kuja na kanuni ili tankers zote zitegenezewe namna mabetri yafichwe kwenye kama "kasanduku" ka chuma na paweko na padlock.

Hii nchi wajinga wengi mno tayari nimesikia wakisema Mungu ndiye alipanga wafe kifo cha aina hiyo.
 
nimesoma poiti zote lakini angalau https://www.jamiiforums.com/members/ngwanamangilingili.320370/ amejitahidi.


ngoma iko hivi ikitokea ajari inayoweza kuleta moto au mlipuko cha kwanza zima chanzo cha nishati.


pikipiki chomoa plagi faster, unazani mchina fala kuziweka wazi.


umeme zima main switch halaka. main switch weka sebuleni.


gari la petroli likila mweleka tu kabula ya mambo kuharibika chomoa temino za betri. tuliosoma vip tunajua. narudia, haraka sana chomoa terminal za betri. unacheza na N200?


ndipo ita fire walipige maji kisha wayanyonyeeee kwenye tenka jingine.



nb. kama limeanza kuvuja ita fayaaa haraka na uwaambie muda wowote linasambaa ili dere wa tenka anyonge kwa sipidi saaaaaaana.



byeeeee.
 
*
IMG-20190814-WA0003.jpeg
 
Kuna haja mamlaka kuja na kanuni ili tankers zote zitegenezewe namna mabetri yafichwe kwenye kama "kasanduku" ka chuma na paweko na padlock.

Hii nchi wajinga wengi mno tayari nimesikia wakisema Mungu ndiye alipanga wafe kifo cha aina haitakiwi kufichwa sana mkuu inaweza tokea hitilafu ya umeme, utatoaje Betri kama imefichwa?
 
mtu anawaka moto anakukimbilia umsaidie na wewe unamkimbia no mpige mtama aanguke chini mwagia mchanga moto unazima sasa wewe unakimbia mnakua kama vikatuni flani..
 
una haja mamlaka kuja na kanuni ili tankers zote zitegenezewe namna mabetri yafichwe kwenye kama "kasanduku" ka chuma na paweko na padlock.
Yaani weye ndo kabisa unatumaliza hata kabla hatujachota angalao lita 3 za kianzio. Box la chuma tena si betri ikijigonga pembeni ndo mlipuko kabla ya mafuta kumwagika??
Huku kitaa hali ni ngumu kishenzi. Si ulimuona mama na katoto mgongoni na dumu lake la mafuta?? Alidhani kuwa huwekwa kwenye jiko la mchina apikie mboga mchana.
Toa ushauri kuwa, angalao kodi zipunguzwe kwenye gas watu waweze kuaford kuitumia
 
Yaani weye ndo kabisa unatumaliza hata kabla hatujachota angalao lita 3 za kianzio. Box la chuma tena si betri ikijigonga pembeni ndo mlipuko kabla ya mafuta kumwagika??
Huku kitaa hali ni ngumu kishenzi. Si ulimuona mama na katoto mgongoni na dumu lake la mafuta?? Alidhani kuwa huwekwa kwenye jiko la mchina apikie mboga mchana.
Toa ushauri kuwa, angalao kodi zipunguzwe kwenye gas watu waweze kuaford kuitumia
Wizi ni tabia hata gesi ikigawiwa bure watu watachota tu maana mahitaji ya mafuta yatawepo tu kwa hiyo atauza.

Mtu mwenye bodaboda,bajaji hiyo gesi haimfanyi asihitaji mafuta.

Waboreshe tu hilo wazo langu ili betri lisiwe la kufikia tu ukizingatia hata Mbeya chanzo kilikuwa hicho hicho.
 
Kuna haja mamlaka kuja na kanuni ili tankers zote zitegenezewe namna mabetri yafichwe kwenye kama "kasanduku" ka chuma na paweko na padlock.

Hii nchi wajinga wengi mno tayari nimesikia wakisema Mungu ndiye alipanga wafe kifo cha aina hiyo.
Moto kwenye ajali kama hiyo siyo lazima usababishwe na betri tu. Petrol ni rahisi mno mno kushika moto na kitu usichotegemea kabisa kinaweza kuifanya kulipuka. Halafu hili la kusema hili lori liliwaka kwa sababu ya kuchomoa betri hakuna mwenye uhakika. Kuna shuhuda mmoja alisema baada ya wakwapuaji kufungua mifuniko, petrol ilitiririka ikakufika sehemu mama ntilie walikokuwa wanapika hivyo ikalipuka.
 
Yaani weye ndo kabisa unatumaliza hata kabla hatujachota angalao lita 3 za kianzio. Box la chuma tena si betri ikijigonga pembeni ndo mlipuko kabla ya mafuta kumwagika??
Huku kitaa hali ni ngumu kishenzi. Si ulimuona mama na katoto mgongoni na dumu lake la mafuta?? Alidhani kuwa huwekwa kwenye jiko la mchina apikie mboga mchana.
Toa ushauri kuwa, angalao kodi zipunguzwe kwenye gas watu waweze kuaford kuitumia
Bado nakataa. Kilichosababisha watu kukimbilia kuchota mafuta siyo maisha magumu. Ni tabia na utamaduni mbaya wa wizi uliojenga kwenye mioyo ya watanzania wengi. Siku hizi sehemu nyingi zenye ajali watu wanakimbilia kuiba. Imashekuwa kama sehemu ya utamaduni wetu.
 
Wizi ni tabia hata gesi ikigawiwa bure watu watachota tu maana mahitaji ya mafuta yatawepo tu kwa hiyo atauza.

Mtu mwenye bodaboda,bajaji hiyo gesi haimfanyi asihitaji mafuta.

Waboreshe tu hilo wazo langu ili betri lisiwe la kufikia tu ukizingatia hata Mbeya chanzo kilikuwa hicho hicho.
Umesema kweli. Kilichosababisha watu wengi kuungua ni tabia ya wizi na siyo umaskini. Mbona kuna watu maskini wengi na hawaibi? Na vile vile kuna tatizo la pili la watanzania kupenda kukimbilia kwenye matukio ya ajali kama wanakimbilia kwenda kuangalia movie nzuri. Hili nalo ni janga kubwa. Ila hilo la kusema waweke sijui kisanduku ni wazo fyongo. Vyanzo vinavyoweza kusababisha moto sehemu yenye petrol viko vingi sana na betri ni sehemu ndogo sana ya sababu.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom