Si rahisi kwa kiongozi wa chama cha ushindani kuwa rais tanzania!

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
.....HAIWEZEKANI kwa mazingira ya sasa mpaka haya yafanyike:
  • TUME HURU YA UCHAGUZI
  • KUKOMESHA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WALIPA KODI
  • MAREKEBISHO YA KATIBA KUPUNGUZA MADARAKA MAKUBWA YA RAIS
  • ELIMU NA UELEWA KUWAFIKIA WANANCHI

.....na mengine mengi unaweza kuongeza............
 
.....HAIWEZEKANI kwa mazingira ya sasa mpaka haya yafanyike:
  • TUME HURU YA UCHAGUZI
  • KUKOMESHA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WALIPA KODI
  • MAREKEBISHO YA KATIBA KUPUNGUZA MADARAKA MAKUBWA YA RAIS
  • ELIMU NA UELEWA KUWAFIKIA WANANCHI

.....na mengine mengi unaweza kuongeza............

NA HAYO YOTE HAYTAWEZEKANA MPAKA KIONGOZI WA UPINZANI AWE RAISI

and
It can be done, Play your part-JK NYERERE
 
subiri miujiza 31st October, maana hata Kikwete mwenyewe atampigia kura DK. Slaa.

KATIKA YEYE YOTE YATAWEZEKANA!!!!
 
Hakika HAYO YOTE hayawezekani hasa kwa watu waoga, juu ya mabadiliko ya kiuongozi, kisiasa, kifikra, kiutamaduni n.k

KIUONGOZI:
Uongozi siyo maumbile kusema kwamba haiwezekani kubadilika, au pindi yakibadilika yaweza kuleta madhara ya kudumu. (Permanent Defomation) Uongozi ni uwezo binafsi au wakati mwingine ni kipaji cha mtu alichozaliwa nacho. Hivyo inawezekana kukawa na viongozi mbalimbali tena wenye uwezo mbalimbali na mitazamo tofauti katika kuongoza na kuleta tija zaidi katika suala zima la kiuongozi. Hivyo sioni sababu ya watanzania kuwa waoga juu ya mabadiliko ya kiuongozi katika nyanja zote za kimaisha.

KISIASA:
Mabadiliko mengi katika nchi yoyote ile duniani hutokea chini ya mwevuli wa kisiasa. Hivyo siasa imekuwa ni jambo muhimu katika maendeleo ya nchi yoyote ile dunia, hivyo sii vyema kabisa kulipuuza suala la mfumo wa siasa za nchi. Hii ni kwasababu viongozi wa kisiasa ndio wasimamizi wakuu wa maendeleo na ukuaji wa uchumi wa nchi. Mambo haya yanaposhindwa kufanyika kwa ufanisi, taifa huishia kuwa duni na watu wake kuishi kwa kukosa haki zao za msingi. Hivyo pendekezo KUU na BORA zaidi kukabiliana na hili ni kubadili mfumo wa kisiasa ilikupata kie kilichokuwa kinapelea ama kukosekana kabisa.

KIFIKRA
Wapo watu wengi sana wanaoishi na fikra potofu juu ya mustakabali mzima wa maisha yao wenyewe. Ikumbikwe kuwa mafanikio ya kimaisha huanzia kwa mtu mwenyewe. Hivyo ni lazima mtu kuwa na fikra sahihi juu ya kile anachoamini au anachofikiri kukifanya. Wapo walioamini kuwa Tanzania bila Nyerere haiwezekani, lakini sasa imewezekana. Wapo wanaoamini kuwa Tanzania bila CCM haitawezekani hizi i fikra potofu maana hata vyama vilivyoleta uhuru katika nchi mbalimabali za Bara Africa, kama vile KANU na n.k havipo tena madarakani na leo hii nchi hizo zinaendelea na zipo mbele ya Tanzania Kiuchumi, kielimu na hata kimaendeleo licha ya kuwa na rasilimali finyu kuliko Tanzania. Hivyo sio sahihi kuishi chini ya fikra za Dume na za kitumwa namna hiyo.

KIUTAMADUNI
Tamaduni nzuri ni zile zinazo muacha raia katika uhuru wake. Siku hizi tunaona tamaduni za jamii husika zinaingiliwa na zikibadilishwa waziwazi na wakati mwingine hubadilishwa ili kulazimisha watu kuacha mfumo fulani na kuingizwa katika mfumo mwingine kwa maslai ya watu wachache. Ni lazima kufika sehemu na kuacha tamaduni za kiukandamzaji ili kuwa huru katika maamuzi bila kuogopa mfumo wa kisiasa, vitisho au hata watu fulani wenye nguvu kifedha au kisiasa.

Endapo watu watajua ni nini zilizo haki zao katika muhimili wa kisiasa, kimaendelea, Kijamii, kielimu au hata kiuchumi, vyote vilivyotajwa hapo katika Post #1 vinawezekana, maana uoga utawekwa kando na watu wote watainuka na kutaka mfumo wenye ubora zaidi katika maisha yao na maendeleo ya Taifa lao. Katika hili ninashawishika kuamini kwamba kuwa na mtazamo mwingine juu ya siasa za Tanzania ni jambo linalopaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania mwenye anayepumua.

Asanteni kwa leo.
 
Ustahadhi pole sana, mwaka huu lazima watanzania tumkabidhi Jk , 31.10.2010 State house leaving certificate, tumechoka kufanyiwa majaribio
 
Hakika HAYO YOTE hayawezekani hasa kwa watu waoga, juu ya mabadiliko ya kiuongozi, kisiasa, kifikra, kiutamaduni n.k

KIUONGOZI:
Uongozi siyo maumbile kusema kwamba haiwezekani kubadilika, au pindi yakibadilika yaweza kuleta madhara ya kudumu. (Permanent Defomation) Uongozi ni uwezo binafsi au wakati mwingine ni kipaji cha mtu alichozaliwa nacho. Hivyo inawezekana kukawa na viongozi mbalimbali tena wenye uwezo mbalimbali na mitazamo tofauti katika kuongoza na kuleta tija zaidi katika suala zima la kiuongozi. Hivyo sioni sababu ya watanzania kuwa waoga juu ya mabadiliko ya kiuongozi katika nyanja zote za kimaisha.

KISIASA:
Mabadiliko mengi katika nchi yoyote ile duniani hutokea chini ya mwevuli wa kisiasa. Hivyo siasa imekuwa ni jambo muhimu katika maendeleo ya nchi yoyote ile dunia, hivyo sii vyema kabisa kulipuuza suala la mfumo wa siasa za nchi. Hii ni kwasababu viongozi wa kisiasa ndio wasimamizi wakuu wa maendeleo na ukuaji wa uchumi wa nchi. Mambo haya yanaposhindwa kufanyika kwa ufanisi, taifa huishia kuwa duni na watu wake kuishi kwa kukosa haki zao za msingi. Hivyo pendekezo KUU na BORA zaidi kukabiliana na hili ni kubadili mfumo wa kisiasa ilikupata kie kilichokuwa kinapelea ama kukosekana kabisa.

KIFIKRA
Wapo watu wengi sana wanaoishi na fikra potofu juu ya mustakabali mzima wa maisha yao wenyewe. Ikumbikwe kuwa mafanikio ya kimaisha huanzia kwa mtu mwenyewe. Hivyo ni lazima mtu kuwa na fikra sahihi juu ya kile anachoamini au anachofikiri kukifanya. Wapo walioamini kuwa Tanzania bila Nyerere haiwezekani, lakini sasa imewezekana. Wapo wanaoamini kuwa Tanzania bila CCM haitawezekani hizi i fikra potofu maana hata vyama vilivyoleta uhuru katika nchi mbalimabali za Bara Africa, kama vile KANU na n.k havipo tena madarakani na leo hii nchi hizo zinaendelea na zipo mbele ya Tanzania Kiuchumi, kielimu na hata kimaendeleo licha ya kuwa na rasilimali finyu kuliko Tanzania. Hivyo sio sahihi kuishi chini ya fikra za Dume na za kitumwa namna hiyo.

KIUTAMADUNI
Tamaduni nzuri ni zile zinazo muacha raia katika uhuru wake. Siku hizi tunaona tamaduni za jamii husika zinaingiliwa na zikibadilishwa waziwazi na wakati mwingine hubadilishwa ili kulazimisha watu kuacha mfumo fulani na kuingizwa katika mfumo mwingine kwa maslai ya watu wachache. Ni lazima kufika sehemu na kuacha tamaduni za kiukandamzaji ili kuwa huru katika maamuzi bila kuogopa mfumo wa kisiasa, vitisho au hata watu fulani wenye nguvu kifedha au kisiasa.

Endapo watu watajua ni nini zilizo haki zao katika muhimili wa kisiasa, kimaendelea, Kijamii, kielimu au hata kiuchumi, vyote vilivyotajwa hapo katika Post #1 vinawezekana, maana uoga utawekwa kando na watu wote watainuka na kutaka mfumo wenye ubora zaidi katika maisha yao na maendeleo ya Taifa lao. Katika hili ninashawishika kuamini kwamba kuwa na mtazamo mwingine juu ya siasa za Tanzania ni jambo linalopaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania mwenye anayepumua.

Asanteni kwa leo.

I consider this as one of the best comments since I joined JF. You are a great person, truly you are.
 
hata mkioga, mjini hamuendi ng'oooo
achana nao hao kwanza hawafiki hata alfu,pili kama kura zao zapigwa humu maana hawako TZ,wamesahau kuwa wamefunga banda wakati farasi keshatoka wapiiiii
 
Nafikiri tunahitaji Katiba Mpya kama Kenya, Pili kuna umuhimu wa kuwa na Mabunge mawili kama Congress na Senate ili moja litazame sera na maslahi ya Taifa kama kuteua watendaji wa vyombo mbalimbali vya dola, majaji, wakuu wa vyombo vya usalama na tume huru ya uchaguzi pamoja na kuwa na uwezo wa kumfukuza Rais, wakati Congress ni kusimamia budget na kazi za kila siku za serkali?
 
.....HAIWEZEKANI kwa mazingira ya sasa mpaka haya yafanyike:

  • TUME HURU YA UCHAGUZI
  • KUKOMESHA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WALIPA KODI
  • MAREKEBISHO YA KATIBA KUPUNGUZA MADARAKA MAKUBWA YA RAIS
  • ELIMU NA UELEWA KUWAFIKIA WANANCHI


.....na mengine mengi unaweza kuongeza............

Porojo za misikitini hizi.............................
 
Back
Top Bottom