Zemanda
JF-Expert Member
- Jan 10, 2021
- 5,707
- 11,954
Kuna dada m'moja alikuwa mfua nguo, ana mtoto m'moja akawa anapitia nguo za wateja na kufua.
Nimecheka Hali!!
Kumbe sie hatoelewi sababu ya wauza vyakula?
Na wengine wanaolewa kwajili ya kuwa wapishi tu,sio upendo?
Haya vipi madobi na dada poa?
Kuna mshikaji akataka huduma zaidi, akataka na kupikiwa na kufanya usafi wa ndani jambo ambalo bi dada alikubali akawa anampikia chakula cha jioni na kumfanyia usafi.
Mwisho wa siku jamaa alihama pale akahamia sehemu nyingine. Cha ajabu yule dada akawa haonekani tena kufanya kazi za kufua za wakazi wa mitaa ile.
Sasa story iliyokuja ni kwamba jamaa aliamua kuchukua mwanamke jumla na mtoto wake akaenda kumuoa na ana ujauzito. Wadau walimuona kata nyingine huko yupo kwenye duka la jamaa ambalo alifungua ndio mkewe anakaba maokoto hapo asizunguke na mambo ya kufuliana na raia.