Itovanilo
JF-Expert Member
- Jul 30, 2018
- 2,314
- 5,138
Hello JamiiForums,
Moja kwa moja kwenye mada,ndugu zangu na mashabiki wenzangu wa mpira wa miguu (football).
Naomba basi tujifunze na kuheshimu timu zingine,tuache ile hali ya kuona kuwa hizi timu mbili za Simba na Yanga haziwezi kufungwa
Yaani mchezo wa jana kati ya Mbeya City wenyeji inaonekana kama vijana wa nyanda za juu hawakustahili kushinda.
Binafsi sikubaliani,tusikariri kwamba hizi timu zetu lazima ziondoke na point tatu hapana,lazima tujue kuwa kwanza kila timu Iko ligi kuu na inazisaka point tatu,
Pili, tumezoea ukubwa wa majina ya klabu tunasahau kuwa usajili wa uhakika nao ni muhimu ili kujihakikishia kushinda kila mechi.
Naona kwenye social media kocha Pablo analalamikiwa,anasimangwa, kejeli na dharau kibao mimi naona si sahihi kwakuwa kufungwa siyo ajabu
Ni huyo huyo katoka kuwapa zawadi ya Kombe la Mapinduzi na vijana wake akina Sakho
Najua kinachowauma ni
1. Goli limefungwa mapema kwamba ilitakiwa ifanyike juhudi lirudi haikuwa hivyo
2. Simba walipata penati ambayo haikuzaa matunda
3. Mbeya City walipungukiwa mchezaji ambapo ilikuwa advantage kwa timu pinzani lakini wapi,inauma sana
Moja kwa moja kwenye mada,ndugu zangu na mashabiki wenzangu wa mpira wa miguu (football).
Naomba basi tujifunze na kuheshimu timu zingine,tuache ile hali ya kuona kuwa hizi timu mbili za Simba na Yanga haziwezi kufungwa
Yaani mchezo wa jana kati ya Mbeya City wenyeji inaonekana kama vijana wa nyanda za juu hawakustahili kushinda.
Binafsi sikubaliani,tusikariri kwamba hizi timu zetu lazima ziondoke na point tatu hapana,lazima tujue kuwa kwanza kila timu Iko ligi kuu na inazisaka point tatu,
Pili, tumezoea ukubwa wa majina ya klabu tunasahau kuwa usajili wa uhakika nao ni muhimu ili kujihakikishia kushinda kila mechi.
Naona kwenye social media kocha Pablo analalamikiwa,anasimangwa, kejeli na dharau kibao mimi naona si sahihi kwakuwa kufungwa siyo ajabu
Ni huyo huyo katoka kuwapa zawadi ya Kombe la Mapinduzi na vijana wake akina Sakho
Najua kinachowauma ni
1. Goli limefungwa mapema kwamba ilitakiwa ifanyike juhudi lirudi haikuwa hivyo
2. Simba walipata penati ambayo haikuzaa matunda
3. Mbeya City walipungukiwa mchezaji ambapo ilikuwa advantage kwa timu pinzani lakini wapi,inauma sana