Si kwamba ufugaji wa Sungura ni utapeli, no ni uwezo wetu wa kuwaza umeisha

Naonaga watu wengi sana wanalalamika wameambiwa wafuge sungura na mwisho wa siku wanao wahamasisha wanaingia mitini.

Ufugaji wa Sungura ni kwamba wafugani wameshindwa ku tengeneza demand, wameshindwa kutengeneza soko. Watu wengi hawana utamaduni wa kula nyama ya Sungura na kuna wanao wafananisha na paka.

Sasa kinacho takiwa ni kitengeneza huo utamaduni, inawezekana kabisa kutengeneza utamaduni wa kula Sungura na watu wakawa wanawala tena sana kuliko hata kuku. Shida iko kwa wafugaji wanataka ready Market, hawataki kuumiza vichwa kabisa kutengeneza demand.

Hii nchi imejaa foreigner kibao na wana uramaduni tofauti tofauti then mtu anakuambia hakuna soko? Unazani kuna atakae kufuata shambani kwako anunue? No lazima umshawishi lazima umwambie ni kwa nini anunue nyama ya sungura.

Wafugaji wa sungura tengenezeni demand achaneni kulalamika
Wewe unaongea pumba tu, na pengine ndio wale wale waliotapeli au hujui kilichotokea..

Hao waliowauzia Mbegu ya Sungura ndio waliosema watakuja kununua Sunngura wakikua wakubwa, lakini mwishowe wakaingia mitini wasinunue, vipi tena uwatetee?
 
Kinachotakiwa ni kubadilisha zao hilo kuwa zao linalopokeleka sokoni kwa mfano ukiwa na hao sungura ukatengeneza sausage zake katika price ya kawaida utapata. Au ukachoma mishkaki yake utapata.

Au nyamanyake ya kusaga utapata. Na ngozi ukaiprocess na kuiuza na mkojo ukaugena. Utapata kidogo kidogo kwenye kila bidhaa mwisho wa siku kitakiwa kikubwa.
 
Labda kwa msaada zaidi waelezee faida za nyama ya Sungura mkuu
Kunambinu za kibiashara zinaweza tumika sungura wakatafutwa ka pesa, baadhi ya bidhaa nyingine huwa wanazipa promo watu wa lishe na madaktari baada ya kulipwa na baadhi ya viwanda/kampuni au watu,
 
Mkuu ipo hivi CHASHA FARMING
Inakuja kampuni inakuambia wanasoko la uhakika la sungura kwa bei kubwa sana ila wanataka wafugaji wawasaidie kuzalisha maana wamezidiwa na soko

Wanakupa mchanganuo wao wa biashara na unaona hapa nakua milionea

Unaingia nao mkataba wanakuuzia vifaranga vya sungura kwa bei kubwa
Watakuuzia madawa na chanjo kwa bei kubwa
Watakuuzia chakula lishe kwa bei kubwa
Na watakutoza gharama za ushauri wa kitaalamu

Utafanya haya yote na kuingia gharama kubwa kwasababu katika mkataba wao ndio wauzaji wa kila kitu na wao ndio watakao nunua hao sungura na kuwapeleka huko kwenye soko lililo wazidia(Hapa ndipo wanapo piga hela kuuza bidhaa kwa bei isio halisi na ni lazima ununue kwao)

Utamu unakuja baada ya kuwa umeingia gharama zote hizo kwa matarjio ya mkataba wa kuwauzia wao..jamaa wanaingia mitini unabaki na sungura wako

KAMA KATIKA HILI HAUONI KUNA UTAPELI BASI UNAPASWA KUJITAFAKARI UPEO WAKO WA UFAHAMU MKUU

Hivi nimekwisha danganyika hadi gharama ya sungura mmoja ameisha tumia labda zaidi ya laki moja kwa minajili ya kuja kuuza tuseme laki 2 halafu mnunuzi kapotea
Nawewe unakuja hapa jukwaani unaandika sijatapeliwa hapo na kwamba eti nitafute soko......kumbuka bei halisi ya sungura wala sio hiyo ilikua ni kunihadaa tu ili nione ntapa faida

Sasa kweli ntaweza kumuuzia mtu ambaye anamuona sungura kama paka kwa laki2 kweli jamani?

Yaani nianza kusaka soko kumshawishi mtu asinunue jogoo kwa elfu5 na kumuuzia mtu sungura kwa laki2 ili kucover hela niliotapeliwa ya vifaranga madawa chakula nk

Kumbuka tatizo kubwa la wakulima na wafugaji ni soko, jamaa wamekuhakikishia soko halafu wamesepa unarudi kule kule

Naweka hapo chini aina ya mikataba ya kitapeli
Wale ni matapeli hasa, hata wakiwanunua hawezi kurudisha gharama za uendeshaji, kingine cha kujiuliza kwanini wasifuge wao wakaajiri watu ili wakidhi hilo soko la kimataifa, hao jamaa nilishangaa kuona wananishawushi nifuge wakati wa corona wakisema wazidiwa masoko uko ulaya, wakat wanajua kipindi hicho hotel/super market zote zilikuwa zimefungwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom