Si kwa ajili ya ubaguzi, bali namshauri Rais Samia aepuke kufanya maamuzi makubwa ya muda mrefu yanayohusu upande wa Tanzania bara peke yake

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
12,396
21,976
Najua kwamba Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama Rais wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Rais Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Rais Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Rais Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na matokeo ya maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Rais Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Rais Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
 
Najua kwamba Raisi Samia ni Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama raisi wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Raisi Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Raisi Samia ajiepushe kufanya maamuzi ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Raisi Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Raisi Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Raisi Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
Sasa kama watanganyika wamelala unategemea afanye nini zaidi ya kuuza kila kitu.
 
Najua kwamba Raisi Samia ni Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama raisi wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Raisi Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Raisi Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Raisi Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Raisi Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Raisi Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
Suluhisho sahihi kwa matatizo hayo yote ni kupatikana kwa Katiba Mpya ambayo ni Nzuri.
 
Sawa, lakini kwa sasa hatuna serikali tatu, na wala hatutarajii zitakuja kesho au keshokutwa.

..usikate tamaa kudai Katiba mpya, na muungano bora kuliko huu wa sasa hivi.

..pia nakupongeza kwa hoja yako, pamoja na kwamba umekosea kwa kutoitaja TANGANYIKA.

..Nchi yetu ambayo tulidai uhuru wake, na tukaupata mwaka 1961, sio Tanzania Bara, bali TANGANYIKA.
 
Uongo mkubwa sana huu.

Suluhisho sahihi ni kupatikana kwa Katiba ya nchi ambayo ni nzuri. Katiba itakayoweka misingi imara ya kuwepo kwa Serikali moja ya kidemokrasia ambayo inawajibika kwa Wananchi, na wala siyo vinginevyo.

..Tume ya Warioba ilifanyia kazi mapendekezo ya aina mbalimbali za muungano, na ikaja na pendekezo la serikali 3.

..sasa kama unapinga findings za Tume ya Warioba inabidi utueleze chanzo cha mapendekezo ya serikali moja ni nani, na utafiti ulifanyika lini, na waliwasilisha wapi mapendekezo yao.
 
..usikate tamaa kudai Katiba mpya, na muungano bora kuliko huu wa sasa hivi.

..pia nakupongeza kwa hoja yako, pamoja na kwamba umekosea kwa kutoitaja TANGANYIKA.

..Nchi yetu ambayo tulidai uhuru wake, na tukaupata mwaka 1961, sio Tanzania Bara, bali TANGANYIKA
Legally speaking, kwa sasa hakuna nchi inaitwa Tanganyika, hivyo sijakosea kitu, nimefanya hivyo nikielewa
 
Najua kwamba Raisi Samia ni Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, lakini ni jambo lililo wazi kwamba yeye kama raisi wa Tanzania, maamuzi yake kwa zaidi ya 98% yanahusu upande wa Tanzania bara peke yake, kwa sababu upande wa Zanzibar wana raisi wao na serikali yao.

Katika hali kama hii, na ukizingatia kwamba Raisi Samia anatokea upande wa Zanzibar, ningeshauri sana kwamba Raisi Samia ajiepushe kufanya maamuzi makubwa ambayo ni ya muda mrefu (yana lock-in effect ya muda mrefu) upande wa bara peke yake. Kumekuwa na hisia zinazozidi kukua kwamba Raisi Samia anafanya maamuzi ambayo baadaye yatakuwa na athari mbaya upande wa Tanzania bara, wakati yeye amemaliza muda wake na kurudi Zanzibar, na kuwaacha Watanzania bara wakisumbuliwa na matokeo ya maamuzi yake.

Mifano ya maamuzi ambayo Raisi Samia anachukua juu ya mambo yanayohusu bara peke yake ni kama suala la mkataba wa bandari kwa DP Word ya Dubai, na hili la kuchimba madini ndani ya mbuga ya Serengeti na nyinginezo, ambapo, TANAPA, chombo cha utalii Tanzania bara, kilishalikataza sana.

Ingekuwa busara sana kama Raisi Samia angeonyesha subira na kuacha maamuzi juu ya mambo makubwa kama hayo, yenye long term lock-in effect, yafanywe wakati Rais wa Tanzania ni mtu kutoka upande wa bara. Hii itasaidia kutokuza chuki na kutoa hofu upande wa bara kwamba Raisi Samia hafanyi mambo kwa manufaa ya watu wa bara, na labda ana ajenda ya siri.
Kwa nini mnapenda kuiita TANGANYIKA , Tanzania Bara? Mbona Zanzibar hamuiiti Tanzania Visiwani?

Ukiamua kutumia Tanzania Bara ku adress inshu za Tanganyika, basi na Upande wa Pili tumia jina Tanzania Visiwani badala ya Zanzibar.
Asante
 
Uongo mkubwa sana huu.

Suluhisho sahihi ni kupatikana kwa Katiba ya nchi ambayo ni nzuri. Katiba itakayoweka misingi imara ya kuwepo kwa Serikali moja ya kidemokrasia ambayo inawajibika kwa Wananchi, na wala siyo vinginevyo.
Mkuu hoja yako ya Serikali tatu ama moja ni mzuri, lakini ni ngumu kutekelezeka; maana mshirika mmoja wa huo Muungano bado ana Nchi yake yenye hadhi ya kuwa NCHI na wakati huo huo mshiriki mwingine hana Nchi, alishaigawa kwa sababu ali iona ni kubwa mno.
 
Back
Top Bottom