Elections 2015 Si kila Mageuzi ni Mapinduzi: Wapo wapi manguli wa CCM? Na sheria zao ngeni katika utu?

Nicholas

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
25,261
7,195
Niliwahi andika hapa kwamba CCM ni Chama Cha Mapinduzi (ila si mageuzi ya usitawi)....Na Hii inatokana na ukweli kwamba CCM ni kinaenzi revolution overthrowing) na si revolution (abrupt and positive development ).. CCM kwa miaka 50 imeishi kuprogram watu kufikiri kwa namna wanayotaka, wakiwapimia watu kiasi cha kufikiri na nini cha kufikiri.

CCM kama wajamaa wengine wenye fikra duni na dhaifu sana kuweza shindana na binadamu huru wamewekeza rasilimali za nchi katika kujenga elimu ya watu wanaojiita wahaanga katika kila kitu ambacho wenzao wameweza wao wameshindwa.

Elimu ya watu wanaotaka lazimisha mafanikio ya wengine yaonekane ni unyonyaji.. ila wao wakinyonya wanyonge sana (kupitia upendeleo pekee wa viongozi wanaopenda kusema ni mapenzi ya wanyonge kwa viongozi), wao huiba kwa wanyonge kupitia ufisadi mkubwa ambao kwa ukweli ni ulafi kwani katika huo wizi huwa uwezo wao wa kuwekeza kwa faida ya jamii ni mdogo sana.

Kipindi hiki cha mageuzi ya kweli ndio kipindi cha kujiuliza maswali ya msingi:
Wapo wapi manguli wa wa siasa za
CCM waliokuwa wamejaa katika vyombo vya habari wakila vinono na kuambiwa ndio wasomi manguli katika dunia?

Wapo wapi spear zao ambao walifichwa katika upande mwingine usiofungamana na
CCM ili siku moja waibuke kama malaika au mizimu na kuiokoa CCM kwa namna ya maajabu kama tuyasomayo katika vitabu vya imani mbali mbali? Zipo wapi sheria bora za CCM? Hata zile mpya kabisa ambazo CCM kwa maono yao kwamba dunia na tanzania baadae zitakuwa na watu wenye tabia mbaya kabisa ili hizi sheria ziwasaidie?

Tuliambiwa
CCM itatawala daima? Mbona hao wasomi hawapo hata tuwaite mashujaa ,waona mbali na watuongoze katika hii daima? Vipi wamepitwa na wakati sana?

Au mabadiliko ni lugha wasioijua, lugha wasiyoipenda? Si ndio kipindi cha mapinduzi ya kijani waliyopenda tuhubiria? Si ndio kipindi cha mapinduzi ya viwanda, mapinduzi ya elimu etc.? Au wanayaogopa sana? Wapo wapi akina Shivji, Simba, Bushiru, na wengine waisaidie
CCM iwe superstars wa kizazi hiki?

Kwanini wamekubali haraka kuiacha na kuchomoka kama magurudumu mabovu/feki ktk gari imara na inayokimbia sana ktk barabara zenye changamoto? Waje waiambie dunia kwamba zile overthrowing za mataifa ya Africa (ukombozi wa Africa) haikuwa kazi ya
CCM ila ya mabepari...

Mbona sasa wanatukimbia katika mapinduzi halisi ya kilimo? Sayansi Na teknologia, mapinduzi halisi katika haki za binadamu? Wapo wapi vinara wa OAU kutoka Tz? Kwanini msubiri hadi Mwenyezi Mungu aamue mwenyewe kuruhusu Watanzania wapate nafasi ya kufanya mapinduzi bil kupinduana? Si
CCM mlikuwa wenzetu na wakombozi wetu, wakombozi si wa TZ tu ila wa Africa nzima.

Nasikitika sana kusema kufuru tuliofanya Watz chini ya mlezi
CCM. Imefikia mahali kama Watz hatutoitoa CCM Mungu sasa kafikia kukata uhai wa ushetani ktk Africa CCM..

TZ ndio palipo moyo wa si ukombozi tuu pia laana ya Africa. Mataifa tuliyodhani tumeyakomboa Mungu kayasafisha kabla yetu sisi.. Sasa ni zamu ya kutusafisha sisi..... Sheria na manguli wetu hawatoweza iponya
CCM hata watakapodhani wamefanikiwa tunayamazisha wanyonge.

Kuna Watakoendelea kula wengine ..Kabla ya kutapishwa na kutupwa ktk kisago na muumba. Kuna watakaodhani kwamba ni spare tyre (wasaliti) watavuka kabla ya kuvalishwa...

Yote kwa vile kufuru ilifika mbali sana. Yote kwa vile tulidhani tuna nguvu sana..
 
Mkuu, kama kuna taifa watu wanasali sana wakristu na waislamu na kuombea taifa ni Tanzania. wala usijali wanaondoka hawa mungu kawapa muda wa kutosha wala hawakujali wakaendelea na laana ya kula vya wajane mwaka huu watajua kuwa mungu hutumia vitu dhaifu na vilivyodharauliwa kuonyesha nguvu zake.

Lowassa walimchafua ili hata akigombea uchafu aliopakaziwa iwe sababu ya kufeli lakini Mungu kaufanya kuwa ndio namna ya kutangazwa na kujulikana kwake. Hakika CCM wanakalishwa bench mwaka huu subira yavuta
 
CCM ni ile ile kama wanvyo jinasibu wenyewe
Hata baada ya miak 100 chini yao Tz itabaki ile ile,taifa maskini na la hovyo
 
Mkuu, kama kuna taifa watu wanasali sana wakristu na waislamu na kuombea taifa ni Tanzania. wala usijali wanaondoka hawa mungu kawapa muda wa kutosha wala hawakujali wakaendelea na laana ya kula vya wajane mwaka huu watajua kuwa mungu hutumia vitu dhaifu na vilivyodharauliwa kuonyesha nguvu zake. Lowassa walimchafua ili hata akigombea uchafu aliopakaziwa iwe sababu ya kufeli lakini Mungu kaufanya kuwa ndio namna ya kutangazwa na kujulikana kwake. Hakika CCM wanakalishwa bench mwaka huu subira yavuta
Ndio mahali ccm wanapata shida sana..hawana wa kumtisha ktk haya yanayowakuta..wakitisha raia yanatokea yasiyotishwa.
 
CCM ni ile ile kama wanvyo jinasibu wenyewe Hata baada ya miak 100 chini yao Tz itabaki ile ile,taifa maskini na la hovyo
ila watu wa ccm na wengine wasio na matumaini km hawasikii vile kwamba ccm ni ile ile...au km wanafanya kusudi kwa vile wanasikia km watapiga dili vile vile.
 
Kweli Mungu ni mkuu,wamepita na kupotea ktk macho,na masikio yetu manguli wa hovyo kabisa waliosifiwa sana an CCM.
 
Niliwahi andika hapa kwamba CCM ni Chama Cha Mapinduzi (ila si mageuzi ya usitawi)....Na Hii inatokana na ukweli kwamba CCM ni kinaenzi revolution overthrowing) na si revolution (abrupt and positive development ).. CCM kwa miaka 50 imeishi kuprogram watu kufikiri kwa namna wanayotaka, wakiwapimia watu kiasi cha kufikiri na nini cha kufikiri.

CCM kama wajamaa wengine wenye fikra duni na dhaifu sana kuweza shindana na binadamu huru wamewekeza rasilimali za nchi katika kujenga elimu ya watu wanaojiita wahaanga katika kila kitu ambacho wenzao wameweza wao wameshindwa.

Elimu ya watu wanaotaka lazimisha mafanikio ya wengine yaonekane ni unyonyaji.. ila wao wakinyonya wanyonge sana (kupitia upendeleo pekee wa viongozi wanaopenda kusema ni mapenzi ya wanyonge kwa viongozi), wao huiba kwa wanyonge kupitia ufisadi mkubwa ambao kwa ukweli ni ulafi kwani katika huo wizi huwa uwezo wao wa kuwekeza kwa faida ya jamii ni mdogo sana.

Kipindi hiki cha mageuzi ya kweli ndio kipindi cha kujiuliza maswali ya msingi:
Wapo wapi manguli wa wa siasa za CCM waliokuwa wamejaa katika vyombo vya habari wakila vinono na kuambiwa ndio wasomi manguli katika dunia?

Wapo wapi spear zao ambao walifichwa katika upande mwingine usiofungamana na CCM ili siku moja waibuke kama malaika au mizimu na kuiokoa CCM kwa namna ya maajabu kama tuyasomayo katika vitabu vya imani mbali mbali? Zipo wapi sheria bora za CCM? Hata zile mpya kabisa ambazo CCM kwa maono yao kwamba dunia na tanzania baadae zitakuwa na watu wenye tabia mbaya kabisa ili hizi sheria ziwasaidie?

Tuliambiwa CCM itatawala daima? Mbona hao wasomi hawapo hata tuwaite mashujaa ,waona mbali na watuongoze katika hii daima? Vipi wamepitwa na wakati sana?

Au mabadiliko ni lugha wasioijua, lugha wasiyoipenda? Si ndio kipindi cha mapinduzi ya kijani waliyopenda tuhubiria? Si ndio kipindi cha mapinduzi ya viwanda, mapinduzi ya elimu etc.? Au wanayaogopa sana? Wapo wapi akina Shivji, Simba, Bushiru, na wengine waisaidie CCM iwe superstars wa kizazi hiki?

Kwanini wamekubali haraka kuiacha na kuchomoka kama magurudumu mabovu/feki ktk gari imara na inayokimbia sana ktk barabara zenye changamoto? Waje waiambie dunia kwamba zile overthrowing za mataifa ya Africa (ukombozi wa Africa) haikuwa kazi ya CCM ila ya mabepari...

Mbona sasa wanatukimbia katika mapinduzi halisi ya kilimo? Sayansi Na teknologia, mapinduzi halisi katika haki za binadamu? Wapo wapi vinara wa OAU kutoka Tz? Kwanini msubiri hadi Mwenyezi Mungu aamue mwenyewe kuruhusu Watanzania wapate nafasi ya kufanya mapinduzi bil kupinduana? Si CCM mlikuwa wenzetu na wakombozi wetu, wakombozi si wa TZ tu ila wa Africa nzima.

Nasikitika sana kusema kufuru tuliofanya Watz chini ya mlezi CCM. Imefikia mahali kama Watz hatutoitoa CCM Mungu sasa kafikia kukata uhai wa ushetani ktk Africa CCM..

TZ ndio palipo moyo wa si ukombozi tuu pia laana ya Africa. Mataifa tuliyodhani tumeyakomboa Mungu kayasafisha kabla yetu sisi.. Sasa ni zamu ya kutusafisha sisi..... Sheria na manguli wetu hawatoweza iponya CCM hata watakapodhani wamefanikiwa tunayamazisha wanyonge.

Kuna Watakoendelea kula wengine ..Kabla ya kutapishwa na kutupwa ktk kisago na muumba. Kuna watakaodhani kwamba ni spare tyre (wasaliti) watavuka kabla ya kuvalishwa...

Yote kwa vile kufuru ilifika mbali sana. Yote kwa vile tulidhani tuna nguvu sana..
Kichwa cha habari na ulicho andika havifanani
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom