Si halali wala haki kwa Serikali ya CCM kuwatoza wananchi fedha ili kutumia Daraja la Nyerere kwenda Kigamboni, ni ubaguzi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nimetafakari sana juu ya hii Serikali ya CCM inayodai ipo kwa ajili ya wananchi, hasa wanyonge. Na hakuna mtu anakaebisha kwamba Kigamboni kuna hao wanyonge wengi tu.

Sasa kwanini hawa wanyonge wa Kigamboni walazimishwe kutoa fedha kwa kutumia daraja la Nyerere kwenda Kigamboni? Tunajua kwamba hata ukienda Kigamboni kwa daladala bado unalipa kutumia daraja hili. Huu ni ubaguzi unaofanywa na Serikali kwa wananchi wa Kigamboni na haukubaliki hata kidogo.

Daraja la kwenda Kigamboni ni huduma ambayo serikali inapaswa kutoa kwa wananchi wake, sawa tu na kujenga daraja la Mkapa ili kuwahudumia wananchi kwenda Rufiji, au daraja la Mto Wami kwa wananchi wanaokwenda mikoa ya Kaskazini.

Sasa kama wale wanaovuka daraja la Wami kwenda Arusha, au Rufiji kwenda Lindi, au hata Ruaha kwenda Iringa - kama hawa hawatozwi fedha kuvuka haya madaraja, kwa nini wananchi wanaokwenda Kigamboni watozwe fedha?

Suala la kusema wananchi wanalipa kwa kuwa serikali inamiliki 40% na NSSF 60% halina mantiki. Serikali inapaswa kuwalipa NSSF hizo 60% ili daraja hili liwe ni mradi wa serikali ambao ulijengwa ili kuwahudumia wananchi, kama vile madaraja mengine ya Mkapa, Wami nk.

Na tusisahau kwamba katika kila lita ya petroli au dizeli tunayonunua, kuna tozo kwa ajili ya Tanroads kujenga vitu kama haya madaraja, flyover na barabara na kuzifanyia ukarabati, juu ya fedha inayotengwa na serikali na misaada kwa ajili ya miradi ya Tanroads. HUiyo basi, kuwa na tozo la daraja la KIgamboni ni sawa na kuwatoza wananchi road toll mara mbili, kinyume cha sheria za kodi.

Ninatoa wito serikali ikomoshe ubaguzi huu kwa kuwafanya baadhi ya Watanzania walipie huduma ya kutumia daraja na wengine wasilipie. Hakuna mtu anakwenda Kigamboni kwa upendezi wake (personal interest), kwa hiyo kuvuka daraja hili hakupaswi kuwa huduma ya kulipia ikiwa kutumia madaraja mengine hatulipii.
 
Nasikia Kenya wana daraja refu kuliko hata hili la kwetu barabara ya kutoka Mombasa kwenda Malindi, sehemu inaitwa Kilifi kuvuka bahari ya Hindi, lakini wanapita free hakuna kulipia. Sie tunashindwa nini?

1604399125690.png
 
Hilo daraja sio la CCM wala sio la Serikali, maana hata hiyo 40% serikaki haikuchangia kama walivyokubaliana, hivyo daraja ni la wastaafu wa mfuko wa NSSF ambao wanapaswa kurejeshewa mafao yao yaliyotumika kujenga hilo daraja. Hivyo hoja iwe, ni wapi pesa ya kuwarudishia NSSF plus interest na projected profit iki liwe mali ya serikali.
 
hili ndilo jambo la msingi linalonifanya nisivutiwe na kuenda kujenga kigamboni. sijawahi kuona iko sawa kila siku utenge kielfu mbili cha kuvukia kwenda nyumbani kwako. ikitokea siku huna huvuki.. imagine kuna siku mtu biashara au mishe zinakua ovyo unabaki na uteni tu wa kuweka mafuta kwenye gari urudi kwako
 
hili ndilo jambo la msingi linalonifanya nisivutiwe na kuenda kujenga kigamboni. sijawahi kuona iko sawa kila siku utenge kielf mbili cha kuvukia kwenda nyumbani kwako. ikitokea siku huna huvuki.. imagine kuna siku mtu biashara au mishe zinakua ovyo unabaki na uteni tu wa kuweka mafuta kwenye gari urudi kwako
NI elfu nne Mkuu, kwenda na kurudi, au?
 
Hilo daraja sio la CCM wala sio la Serikali, maana hata hiyo 40% serikaki haikuchangia kama walivyokubaliana, hivyo daraja ni la wastaafu wa mfuko wa NSSF ambao wanapaswa kurejeshewa mafao yao yaliyotumika kujenga hilo daraja. Hivyo hoja iwe, ni wapi pesa ya kuwarudishia NSSF plus interest na projected profit iki liwe mali ya serikali.
Kama serikali ina uwezo wa kupata hela za kujengea daraja jipya la Salenda ambalo hatuhitaji kwa sasa, haiwezi kushindwa kuwarudishia NSSF fedha zao kwa daraja ambalo ni la lazima kwa wananchi

Hizo fedha ambazo Magufuli alikuwa anamwambia Mfugale zipo ajenge barabara za lami kwa nini asiwarudishie NSSF?
 
hili ndilo jambo la msingi linalonifanya nisivutiwe na kuenda kujenga kigamboni. sijawahi kuona iko sawa kila siku utenge kielf mbili cha kuvukia kwenda nyumbani kwako. ikitokea siku huna huvuki.. imagine kuna siku mtu biashara au mishe zinakua ovyo unabaki na uteni tu wa kuweka mafuta kwenye gari urudi kwako
Kwa miguu na baiskeli darajani ni bure, kwa daladala wewe unalipa nauli tu, hulipii darajani, kama una gari na umeweza kutenga pesa ya mafuta, basi tenga na 3,000/= ya kuvuka.
 
Chuki ya wananchi imepanda sana, tutaona matendo mengi sana ya kigaidi nchini
Kufanya ugaidi dhidi ya nchi ya miundombinu ya nchi yako mwenyewe ni kukosa akili. Kama watu wamekasirika wanataka kufanya ugaidi wawafanyie CCM sio miundombinu ya serikali
 
Kwa miguu na baiskeli darajani ni bure, kwa daladala wewe unalipa nauli tu, hulipii darajani, kama una gari na umeweza kutenga pesa ya mafuta, basi tenga na 3,000/= ya kuvuka.
Kwa daladala hela ya kuvukia daraja haijawekwa ndani ya nauli? Nilienda Kigamboni na gari hapa juzi nililipa 2000/- kwenda na 2000/- kurudi. Inakuwaje unasema ni 3000/-

Vipi pikipiki, wanatoza?
 
Kama serikali ina uwezo wa kupata hela za kujengea daraja jipya la Salenda ambalo hatuhitaji kwa sasa, haiwezi kushindwa kuwarudishia NSSF fedha zao kwa daraja ambalo ni la lazima kwa wananchi

Hizo fedha ambazo Magufuli alikuwa anamwambia Mfugale zipo ajenge barabara za lami kwa nini asiwarudishie NSSF?
Ndio maana nikasema, hoja yako iwe ni namna gani pesa zinaweza kutengwa kwa ajili ya kuwalipa NSSF, lakini pia tambua kuna vipaumbele, kweli tuache kuboresha wodi za wamama wajawazito tuanze kutafuta bilioni 200 za kuwapa NSSF ili wewe ulieenda kuishi Kigamboni na kuacha kwingine kote kwa hiari yako, na unagari lako binafsi, usilipe 3,000/= kwa siku wakati umeweza kuweka mafuta, na kama ungepanda daladala hulipi kitu
 
Ndio maana nikasema, hoja yako iwe ni namna gani pesa zinaweza kutengwa kwa ajili ya kuwalipa NSSF, lakini pia tambua kuna vipaumbele, kweli tuache kuboresha wodi za wamama wajawazito tuanze kutafuta bilioni 200 za kuwapa NSSF ili wewe ulieenda kuishi Kigamboni na kuacha kwingine kote kwa hiari yako, na unagari lako binafsi, usilipe 3,000/= kwa siku wakati umeweza kuweka mafuta, na kama ungepanda daladala hulipi kitu
Vipao mbele? Unataka kuniambia daraja la kupita juu ya bahari Salenda ni kipaombele kuliko daraja la KIgamboni? Au unataka kuniambia zile ahadi za papo kwa papo Magufuli alikuwa anatoa kujenga barabara za lami zina kipaombele zaidi ya daraja la Kigamboni? Usiache nipendekeze tuuze Dreamliner moja tuwalipe NSSF. Corona ikiisha tutatnunua Dreamliner nyingine.
 
NImekupata Mkuu. Basi huyu jamaa lazima analipuliza, mtu mwenye akili sawa hawezi kutoa kauli kama hii
 
Vipao mbele? Unataka kuniambia daraja la kupita juu ya bahari Salenda ni kipaombele kuliko daraja la KIgamboni? Au unataka kuniambia zile ahadi za papo kwa papo Magufuli alikuwa anatoa kujenga barabara za lami zina kipaombele zaidi ya daraja la Kigamboni? Usiache nipendekeze tuuze Dreamliner moja tuwalipe NSSF. Corona ikiisha tutatnunua Dreamliner nyingine.
Ndio, vyote hivyo ni vipaumbele kwa sababu havipo bado, kigamboni bridge lipo tayari na linafanya kazi
 
Back
Top Bottom