Shy-Rose Bhanji sema ukweli wa kilichofanya ukatwe au kaa kimya

mzee wa mkeka

Senior Member
Mar 12, 2017
142
236
Habari wanajf;Tangu mgombea ubunge wa bunge la jumuia ya afrika mashariki (EALA) Shy-Rose Bhanji aenguliwa na vikao rasmi vya CCM kumekuwa na maneno yenye lengo la upotoshaji toka kwake mwenyewe. Nayaita ni maneno ya upotoshaji kwa sababu yeye binafsi anajua sababu hasa iliyofanya jina lake liondelewe licha ya kupata kura nyingi kwenye mchakato wa awali.

Kwa mwanasiasa wa kiwango chake anatakiwa atoke aseme sababu za yeye kukatwa na aweke wazi msimamo wake kuhusu hizo sababu halafu aache wananchi wachambue na waamue kati yake na CCM nani hakutendewa haki.

Shy-Rose unajua msimamo wa Tanzania kuhusu mkataba wa EPA (mkataba wa ushirikiano wa kibiashara kati ya EAC na umoja wa ulaya, EU), pia unajua msimamo mkali wa rais Maghufuli dhidi ya EPA. Pia tunajua wewe ni muumini mzuri wa EPA na namna ulivyopigana ndani na nje ya bunge la afrika mashariki kutetea mkataba huu. Tunajua hata kiasi ulichopokea kutetea EPA (hili tuliacha kwa sasa) na ulivyoshirikiana na sakretariati ya jumuia kuwayumbisha wakuu wa nchi za EAC kuhusu EPA. Pia tunajua ushirikiano wako na nchi waumini wa EPA ili kuyumbisha msimamo wa Tanzania.

Turudi kwenye common sense, Tanzania kama nchi na rais Magufuli kama mwenyekiti wa chama chako wanapinga kwa nguvu zote EPA (huu mkataba unajadiliwa toka enzi za rais mkapa) na wewe unaomba uwakilishi wa Tanzania kwenye EALA.
Ni chama na nchi gani itapeleka muwakilishi anayepingana kwa nguvu zote na msimamo wa nchi au chama? Huko EALA unataka uwakilishe chama/nchi gani?
 
Mwenyekiti wako wa CCM hajamwambia zababu zozote yeye kasema kata hilo jina tena huyo sitaki hata kumuona wala kumsikia.

Sasa Shyrose ndiyo anaomba Mwenyekiti wa CCM aweke wazi sababu za kumkata kibabe.
Anajua sana sababu zilizopelekea akaondolewa,
Kama msimamo wake kwenye suala la mkataba wa EPA ni kinyume na msimamo wa Tanzania na msimamo wa CCM yeye aende EALA kuwakilisha nini?
Ni simple logic tu kujua kwamba hata kumjadili kwenye vikao ni kupoteza muda
 
Hakuna mwenye kiti cha ubunge milele
kama uenyekiti wa cdm
huyu analialia kana kwamba alikuwa peke yake ktk nafasi hiyo!!
Wamekatwa wengi yeye pekee ndiye bora!!?

Ccm ni chama cha wanachama
si chama cha watu fulani
kila nwanachama anahaki ya kugombea
awapishe na wenzie
 
Nadhani ingekuwa jambo la Busara kwa CHADEMA kama mngetueleza mmewapataje Masha na Wenje. Suala na Shy Rose linaelezeka. Ameshaiwakilisha Tanzania sasa ni zamu ya watu wengine
Inaonekana CHADEMA inakunyima usingizi aiseeee.....yaaani umekurupuka tuuu ukacomment......soma kwanza tread uieleweee........ebo!
 
Nadhani ingekuwa jambo la Busara kwa CHADEMA kama mngetueleza mmewapataje Masha na Wenje. Suala na Shy Rose linaelezeka. Ameshaiwakilisha Tanzania sasa ni zamu ya watu wengine

Yaani wewe ni bingwa wa kukariri,hata post hujasoma umeanza na chadema as if you're sure mtoa hoja ni mpinzani wa ccm!
 
Ugonjwa wa kutohoji wagombea kabla ya kuwakata sio mzuri ..huyu angehojiwa angeambiwa yote pengine na mengine ambayo ni personal ...lakini kwa kutokumuhoji huwezi kumzuia kuongea
Kwenye siasa wagombea wanahojiwa (kiuhalisia huwa ni kumwaga sera zao) kama taratibu za uchaguzi husika zimesema kwamba mgombea atahojiwa.
Ila suala la kumpa mrejesho kila aliyeenguliwa na sababu za kumuengua halipo kiutaratibu hata kwa wagombea nafasi ya urais, sababu za kumpitisha aliyepita ndiyo huwekwa wazi.
Hii ipo kila chama, ni hoja dhaifu sana kudai hakuhojiwa.
 
Anajua sana sababu zilizopelekea akaondolewa,
Kama msimamo wake kwenye suala la mkataba wa EPA ni kinyume na msimamo wa Tanzania na msimamo wa CCM yeye aende EALA kuwakilisha nini?
Ni simple logic tu kujua kwamba hata kumjadili kwenye vikao ni kupoteza muda

Huyu dada atulie tu
 
Hakuna mwenye kiti cha ubunge milele
kama uenyekiti wa cdm
huyu analialia kana kwamba alikuwa peke yake ktk nafasi hiyo!!
Wamekatwa wengi yeye pekee ndiye bora!!?

Ccm ni chama cha wanachama
si chama cha watu fulani
kila nwanachama anahaki ya kugombea
awapishe na wenzie
Hebu ficha upu.mbavu wako kidogo! Kura alizopata zilimruhusu kuwa kwenye kinyang'anyiro, yaani alikuwa kwenye top four, jina likaondolewa akawa replaced,Why? Hapo ndo hajui sababu! The Right to be heard! Angeitwa na kuelezwa kungekuwa na shida?
 
Habari wanajf;Tangu mgombea ubunge wa bunge la jumuia ya afrika mashariki (EALA) Shy-Rose Bhanji aenguliwa na vikao rasmi vya CCM kumekuwa na maneno yenye lengo la upotoshaji toka kwake mwenyewe. Nayaita ni maneno ya upotoshaji kwa sababu yeye binafsi anajua sababu hasa iliyofanya jina lake liondelewe licha ya kupata kura nyingi kwenye mchakato wa awali.

Kwa mwanasiasa wa kiwango chake anatakiwa atoke aseme sababu za yeye kukatwa na aweke wazi msimamo wake kuhusu hizo sababu halafu aache wananchi wachambue na waamue kati yake na CCM nani hakutendewa haki.

Shy-Rose unajua msimamo wa Tanzania kuhusu mkataba wa EPA (mkataba wa ushirikiano wa kibiashara kati ya EAC na umoja wa ulaya, EU), pia unajua msimamo mkali wa rais Maghufuli dhidi ya EPA. Pia tunajua wewe ni muumini mzuri wa EPA na namna ulivyopigana ndani na nje ya bunge la afrika mashariki kutetea mkataba huu. Tunajua hata kiasi ulichopokea kutetea EPA (hili tuliacha kwa sasa) na ulivyoshirikiana na sakretariati ya jumuia kuwayumbisha wakuu wa nchi za EAC kuhusu EPA. Pia tunajua ushirikiano wako na nchi waumini wa EPA ili kuyumbisha msimamo wa Tanzania.

Turudi kwenye common sense, Tanzania kama nchi na rais Magufuli kama mwenyekiti wa chama chako wanapinga kwa nguvu zote EPA (huu mkataba unajadiliwa toka enzi za rais mkapa) na wewe unaomba uwakilishi wa Tanzania kwenye EALA.
Ni chama na nchi gani itapeleka muwakilishi anayepingana kwa nguvu zote na msimamo wa nchi au chama? Huko EALA unataka uwakilishe chama/nchi gani?
Hivi kweli tunapinga kwa nguvu zote EPA au tunaikubali baada ya marekebisho?

Hivi kutofautiana na wengine ndiyo kigezo cha kukosa sifa? Mangapi mazuri katufanyia na sasa hatuyaoni? Hivi nini maana ya kupiga kura kama ukishinda bado jina linakatwa?

Kuhusu alipewa nini kuunga mkono EPA ni kumchafua jina tu. Huku unaashiria ni fisadi na kwa kujua umeisha kumchafua na hauna hata chembe ya ushahidi unarukia eti hilo tuliache kwa sasa.

Na hao wanaopinga EPA kwa nguvu zote wamepewa nini au nalo tuliache kwa sasa?
 
Hivi kweli tunapinga kwa nguvu zote EPA au tunaikubali baada ya marekebisho?

Hivi kutofautiana na wengine ndiyo kigezo cha kukosa sifa? Mangapi mazuri katufanyia na sasa hatuyaoni? Hivi ni maana ya kupiga kura kama ukishinda bado jina linakatwa?

Kuhusu alipewa nini kuunga mkono EPA ni kumchafua jina tu. Huku unaashiria ni fisadi na kwa kujua umeisha kumchafua na hauna hata chembe ya ushahidi unarukia eti hilo tuliache kwa sasa.

Na hao wanaopinga EPA kwa nguvu zote wamepewa nini au nalo tuliache kwa sasa?

Mkataba wa EPA upo toka wakati mzee mkapa akiwa madarakani; akaja kikwete hajausign, mpaka sasa kwa magufuli.
Mjadala wake ulishika kasi sana wakati wa uongozi wa JK.
Msimamo wa tanzania upo wazi, EPA ni mkataba kinyonyaji na itauwa kabisa kidogo kinachozalishwa ndani. Huo msimamo ulishawekwa wazi na mkapa na magufuli kwa sasa
 
Hivi kweli tunapinga kwa nguvu zote EPA au tunaikubali baada ya marekebisho?

Hivi kutofautiana na wengine ndiyo kigezo cha kukosa sifa? Mangapi mazuri katufanyia na sasa hatuyaoni? Hivi ni maana ya kupiga kura kama ukishinda bado jina linakatwa?

Kuhusu alipewa nini kuunga mkono EPA ni kumchafua jina tu. Huku unaashiria ni fisadi na kwa kujua umeisha kumchafua na hauna hata chembe ya ushahidi unarukia eti hilo tuliache kwa sasa.

Na hao wanaopinga EPA kwa nguvu zote wamepewa nini au nalo tuliache kwa sasa?

Ubunge wa bunge la afrika mashariki (EALA) ni tofauti na ubunge/uwakilishi wa jimbo, jimboni unaenda bungeni kuwakilisha maoni/changamoto za wanajimbo wake.
Ila mbunge wa EALA ni muwakilishi wa bunge la jamhuri ya muungano/muwakilishi wa nchi kwenye bunge la EAC. Sasa yeye kama anamsimamo tofauti kabisa na msimamo wa serikali kuhusu EPA anaenda wakilisha nini/nani? Hiyo ndo hoja ya msingi
 
Back
Top Bottom