Shule za wenye vipaji maalumu zimezama wapi?

Kibongoto

JF-Expert Member
Aug 5, 2009
227
5
"Nasema mtachonga sana! Eti wengine wakiwemo ambao hawajasoma hata nusu darasa wanazikashifu sekondari za kata. Kisa zaidi eti ni kwa kuongoza kwa divisheni ziro katika matokeo hayo. Kuchonga wanangu ni haki yenu ya msingi, hivyo endeleeni.

Kwa hiyo mnashangalia matokeo ya sekondari za kata, mnayaacha mengine ya msingi katika sekta hiyohiyo ya elimu? Je hizo mlizoziita Shule za Wenye Vipaji Maalumu zimewafikisha wapi? Kuna cha vipaji maalumu hapa? Eti Ilboru, Mzumbe, Tabora, Kibaha hadi na Kilakala.
Naapa na hawa wa Vipaji Maalumu walibeba viroba vya divisheni 0 hivyo msishangilie sekondari za kata.Mlitegemea bado hizo ni shule maalumu? Nyo! Wanafunzi huingizwa shuleni siyo kwa matokeo maalumu, bali ni kwa vijimemo toka kwa wazito.
Mmebakia kwenye kuzitambua bado kama shule za wenye vipaji maalumu? Na St. Marian, St. Goreti, Uru Seminary zilizobeba viroba vya divisheni 1 ziwe nini? Acheni mzaha ukubwani. Kwanza mnawapotosha hao wanafunzi na kuwavimbisha vichwa buree"

Wakuu hua mnasoma nakala za huyu bwana? Jamaa hua anaandika ukweli ktk style ya maongezi,basi hua napenda sana kumsoma. Ni ukweli tupu!
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17971
 
Tatizo ni kuwa kinachotokea kama alivyonote hapo wanaokwenda kule sio maalumu kama zamani tena, umaalumu wa shule umebaki historia wazazi sasa wanafanya jitihada na juhudi kibao kumpeleka mtoto shule binafsi hasa hizi zinazofanay vizuri zaidi, na pia nahisi hata walw walimu bora wa kule maalumu hawapo tena either wamestaafu na wanaokuja kufundisha pale sio wanaostahili huko maalumu au walimu wa huko maalumu wameamua kwemda huku kwa kina Gorreti kwani maslahi ni mazuri. Mzazi siku hizi akiambiwa mtoto kafaulu kwenda Kibaha wala hashtuki hasa kwa O level kidogo bado High school wanajitahidi
 
Tatizo ni kuwa kinachotokea kama alivyonote hapo wanaokwenda kule sio maalumu kama zamani tena, umaalumu wa shule umebaki historia wazazi sasa wanafanya jitihada na juhudi kibao kumpeleka mtoto shule binafsi hasa hizi zinazofanay vizuri zaidi, na pia nahisi hata walw walimu bora wa kule maalumu hawapo tena either wamestaafu na wanaokuja kufundisha pale sio wanaostahili huko maalumu au walimu wa huko maalumu wameamua kwemda huku kwa kina Gorreti kwani maslahi ni mazuri. Mzazi siku hizi akiambiwa mtoto kafaulu kwenda Kibaha wala hashtuki hasa kwa O level kidogo bado High school wanajitahidi

nami nakubaliana na wewe mkuu
 
Ni kweli hili la vipaji maalum linatakiwa liangaliwe kwa umakini wa hali ya juu sana.It doesn't kik in my head kwamba shule za vipaji maalum kama Ilboru kuna ziro 5 na division four 26, kweli tunaandaa makapi kama siyo vibogoyo, yaani hata hizi za vipaji zimetushinda kuziendesha tuzidi kupata wanafunzi bora wanaoandaliwa na serikali mpaka tunafikia division zero kabisa, that is non sense,sasa shule za kata ambazo hazina walimu wa kutosha na vitabu, maabara wala maktaba tukipata zero 50 kunaubaya wowote jamani?
Turudi nyuma tujisahihishe na tuangalie kama bado tuko kwenye njia sahihi au tunaelekea magharibi wakati wengine wanaelekea mashariki!!!!!!
 
Utaratibu wa kuwa na shule za wanafunzi wenye vipaji vya maalum kiakili ulishafutwa toka enzi za Mungai. Hoja ilikuwa ni kuwachanganya wanafunzi wenye uwezo kiakili na walio dhaifu kiakili ili kuongeza ufanisi wa jumla na sio kwa wachache wenye uwezo kiakili waliokuwa wakitengwa na kuwekwa kwenye shule maalum.

Hivyo kwa sasa shule hizo zimebakiza tu historia, wanafunzi wanaochaguliwa kwenda shule hizo ni sawa na tu kwa vigezo vyote na wanafunzi wanaoenda kwenye shule zingine zozote za serikali nchini, katu usilinganishe kabisa matokeo ya shule hizi kwa sasa na enzi zile.
 
Tuliokuwa bora ni sisi ambao tulikwenda shule za wenye vipaji na kweli tulitokea vijijini lakini siku hizi ni wasio na vipaji ndo wananenda shule zile na kuondoka na zero.
 
Magezi hapo umenena, ni sisi vijana wa zamani angalau tulionja shule za watoto wenye vipaji. Nakumbuka tulivyokuwa tunanyanyasana darasani kupokezana namba za juu, mambo moto moto mtindo mmoja. The old good days!!!!
 
Magezi hapo umenena, ni sisi vijana wa zamani angalau tulionja shule za watoto wenye vipaji. Nakumbuka tulivyokuwa tunanyanyasana darasani kupokezana namba za juu, mambo moto moto mtindo mmoja. The old good days!!!!

Ma mdogo wee, unanikumbusha mbali - Nikiwa Kibaha pale bwana tumetoka wani karibu darasa zima- tulikuwa hatuna mchezo na shule, tulikuwa tunataniana - " umetumwa na kijiji mzee" lakini end of the day perfomance juu.

Shule zinazowika sasa ni za Private - wakati ule mtu ukisoma private unaonekana kilaza wa nguvu - tena kundi la wanaosoma shule za serikali hauwasogelei unatengwa ila kwa sasa ni opposite.

Hizi shule zitazidi kuzama as days goes on sababu serikali imepunguza fungu sababu hakuna pesa na ukizingatika matatizo ya waalimu nayo inakuwa kikwazo kingine.
 
Tatizo ni kuwa kinachotokea kama alivyonote hapo wanaokwenda kule sio maalumu kama zamani tena, umaalumu wa shule umebaki historia wazazi sasa wanafanya jitihada na juhudi kibao kumpeleka mtoto shule binafsi hasa hizi zinazofanay vizuri zaidi, na pia nahisi hata walw walimu bora wa kule maalumu hawapo tena either wamestaafu na wanaokuja kufundisha pale sio wanaostahili huko maalumu au walimu wa huko maalumu wameamua kwemda huku kwa kina Gorreti kwani maslahi ni mazuri. Mzazi siku hizi akiambiwa mtoto kafaulu kwenda Kibaha wala hashtuki hasa kwa O level kidogo bado High school wanajitahidi
Sikubaliani na wewe wanaokwenda ni maalumu,naamini mazingira mabaya yanachangia kufeli kwao
 
"Nasema mtachonga sana! Eti wengine wakiwemo ambao hawajasoma hata nusu darasa wanazikashifu sekondari za kata. Kisa zaidi eti ni kwa kuongoza kwa divisheni ziro katika matokeo hayo. Kuchonga wanangu ni haki yenu ya msingi, hivyo endeleeni.

Kwa hiyo mnashangalia matokeo ya sekondari za kata, mnayaacha mengine ya msingi katika sekta hiyohiyo ya elimu? Je hizo mlizoziita Shule za Wenye Vipaji Maalumu zimewafikisha wapi? Kuna cha vipaji maalumu hapa? Eti Ilboru, Mzumbe, Tabora, Kibaha hadi na Kilakala.
Naapa na hawa wa Vipaji Maalumu walibeba viroba vya divisheni 0 hivyo msishangilie sekondari za kata.Mlitegemea bado hizo ni shule maalumu? Nyo! Wanafunzi huingizwa shuleni siyo kwa matokeo maalumu, bali ni kwa vijimemo toka kwa wazito.
Mmebakia kwenye kuzitambua bado kama shule za wenye vipaji maalumu? Na St. Marian, St. Goreti, Uru Seminary zilizobeba viroba vya divisheni 1 ziwe nini? Acheni mzaha ukubwani. Kwanza mnawapotosha hao wanafunzi na kuwavimbisha vichwa buree"

Wakuu hua mnasoma nakala za huyu bwana? Jamaa hua anaandika ukweli ktk style ya maongezi,basi hua napenda sana kumsoma. Ni ukweli tupu!
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17971

wat about it huh??
mi ni alumni wa hapo na kwa taarifa yako tulikuwa real special students mkubwa!!
Kama mabo hayaendi vizuri sasa hivi sijui wat happened to their selections!
 
Sikubaliani na wewe wanaokwenda ni maalumu,naamini mazingira mabaya yanachangia kufeli kwao

inawezekana kabisa
unaenda pale na kipaji chako, huna mwalimu, hakuna vifaa vya kujifunzia unategemea hicho kipaji kitakua vipi kama si kudumazwa??
 
wat about it huh??
mi ni alumni wa hapo na kwa taarifa yako tulikuwa real special students mkubwa!!
Kama mabo hayaendi vizuri sasa hivi sijui wat happened to their selections!
Tatizo sio selection,BTW wanaochaguliwa kwenda hizo the so called special siku hizi ndo hao wanaokwenda St marian,St francis et al.Pia shule hazina waalimu kuna matatizo mengi sana kwenye hizo shule siku hizi si kama zamani.
 
hamna selection maalum kwa shule za vipaji these days. waliamua ku'neutralize
 
Tatizo sio selection,BTW wanaochaguliwa kwenda hizo the so called special siku hizi ndo hao wanaokwenda St marian,St francis et al.Pia shule hazina waalimu kuna matatizo mengi sana kwenye hizo shule siku hizi si kama zamani.

Hata ungekua wewe usingekubali mwanao aende akashangae madawati na kuliwa na mbu bure wakati zipo sehem ambazo anaweza kuishi maisha mazuri na taaluma iko tambalale. Tuwe wakweli tu!
 
Shule za vipaji maalum zilifutwa kwa sababu kulikuwa hakuna vigezo sahihi cha kupima kipaji cha mwanafunzi kigezo walichotumia ni ufaulu wa mwanafunzi ikagundulika kuwa kupata Dv 1au 2 si kuwa wewe una kipaji maalum hata hao wa Dv 1 waliokuwa wanakwenda pale si wote walizipata kwa kutegea akili zao walikuwa wana prove failure kwa hiyo matokeo yake hizo shule zikawa zinadidimia kielimu mwaka hadi mwaka ikafikia wakati zikawa zinafanya vibaya zaidi ya shule zingine kwa hiyo serikali kupitia kwa Mungai ikasema hakuna haja ya serikali kuendelea kugharamia shule ambazo ni sawa na shule zingine tu
 
Sikubaliani na wewe wanaokwenda ni maalumu,naamini mazingira mabaya yanachangia kufeli kwao
Hapana, mazingira hayajawahi kuwa mazuri, suala ni kuwa wakati ule tofauti na sasa wanafunzi wenye uwezo mkubwa wa kiakili ndio walikuwa wanapelekwa kwenye hizi shule, na kutokana na hilo japo walimu wengi walikuwa hovyo lakini kwa uwezo wa wanafunzi na ushindani uliokuwepo kati yao na kati ya shule moja ya special na nyingine mwisho wa siku matokeo yalikuwa yanakuwa mazuri.
 
Hapana, mazingira hayajawahi kuwa mazuri, suala ni kuwa wakati ule tofauti na sasa wanafunzi wenye uwezo mkubwa wa kiakili ndio walikuwa wanapelekwa kwenye hizi shule, na kutokana na hilo japo walimu wengi walikuwa hovyo lakini kwa uwezo wa wanafunzi na ushindani uliokuwepo kati yao na kati ya shule moja ya special na nyingine mwisho wa siku matokeo yalikuwa yanakuwa mazuri.

Nasikia wakifika huko chuo kikuu wote wanakua wanaanza moja. Tena wengine hao wa vipaji utawaonea huruma marks walizoenda nazo hapo chuo na jinsi wanavyohaha kupata makarai. Kazi kwelikweli!
 
Ilifika wakati kutokana na shule hizi kutokuwa na walimu maalum, baada ya wale waliokuwepo kustaafu kwa mujibu wa sheria na kwenda kuajiriwa katika shule za St. Goreti, Mzazi akiona mtoto wake amechaguliwa shule maalum kama ana uwezo kipesa, anampeleka huko huko St. Goreti ambako anakutana na Mwalimu yule yule aliyefundisha shule maalum.
 
Back
Top Bottom