Shule za Serikali kutong'ara kwenye matokeo ya mitihani, waandishi wa habari bado hawajatimiza wajibu wao ipasavyo

Mkumbwa Jr

JF-Expert Member
Mar 23, 2016
2,370
3,148
Mara zote shule binafsi wanakua vinara katika matokeo ya mitihani aidha darasa la saba au kidato cha nne.

Sababu za matokeo yakiwa mazuri au mabaya zipo kama vile uwezo binafsi wa mwanafunzi, bidii, mazingira, rasilimali vitabu,walimu bora, maabara za kisasa, maslahi bora ya watumishi, mbinu mbalimbali za ufikishaji mada, msukumo wa familia na jamii inayomzunguka mwanafunzi.

Nikijikita zaidi kwenye hoja nikwamba waandishi wa habari walio wengi wamejikita zaidi kuwahoji waliofaulu na kufaulisha.

Wanawahoji wanafunzi walioingia kumi bora. Mfano jana Tanzania One amehojiwa akifuatiwa na mzazi wake na leo asubuhi Channel Ten wamewahoji washindi wawili walioingia kumi bora ambapo wamemhoji mshindi wa tano na mshindi wa kumi.

Ingekua bora zaidi kama wangehojiwa wasimamizi wa zile shule kumi za mwisho pia, baadhi ya waliofeli (kama wakitaka kutoa ushirikiano). Wazazi wa wanafunzi ili changamoto zijulikane, maafisa elimu na hata waziri wa elimu. Waieleze jamii hasa changamoto nizipi na kama taifa tunapunguzaje hii aibu ya kufeli, kupoteza fedha na hasara ya muda kwa miaka minne kisha mtu apate zero

Waandishi wa habari msiishi na kufanya kazi kwa ushabiki. Kueni wachokonozi na watafiti. Mtagundua changamoto nyingi sana ambazo baadhi zingeweza kutatuliwa.

Msikae na kuwaita tu watu studioni, wafuateni huko majumbani kwao mkawahoji juu ya hii aibu ya kufeli. Wapo watakaotoa ushirikiano na MTASIKIA MLIYOKUA HAMYAJUI WALA KUYATARAJIA.

Waandishi wa habari bado hamjaamua kubalance hii story ya kufaulu na kufeli. Mnataka kujua waliofaulu wamefanyaje lakini hamtaki kujua waliofeli wameshukiwa na vitu vyenye uzito kiasi gani vichwani mwao.

Ukiachia sababu kama michujo mikali shule binafsi ikilinganishwa na shule za umma kwamba kuna walioenda kwa ana ana dooo, ninaamini kuna vitu vingine vizito na vyenye ncha kali vinavyowapiga wanafunzi kwenye shule za umma. Vitu hivyo vinaweza kua vyakwao binafsi, mazingira yanayo wazunguka au historia zao na watu wengine kama wazazi, jamii, walimu na hata serikali.

Waandishi wa habari jaribuni kufanya mizania kwenye habari msizame upande mmoja.

Mkiongozwa na hisia kama sababu za kufeli mnazijua basi hata za kufaulu hamuwezi kushindwa kujua maana hizo za kufaulu zipo wazi zaidi na zinazungumzika kila uchao na uchwa

Natoa hoja jukwaani
 
Mtihani umefeli kisha unataka upate umaarufu? Dunia haiko hivyo, tunapambania ubora tu…. ndiyo maana unamjua tajiri namba moja na sio masikini namba moja.
 
Mtihani umefeli kisha unataka upate umaarufu? Dunia haiko hivyo, tunapambania ubora tu…. ndiyo maana unamjua tajiri namba moja na sio masikini namba moja.
Jamii zilizoendelea zimekua na msuguano wa fikra.
 
Mtihani umefeli kisha unataka upate umaarufu? Dunia haiko hivyo, tunapambania ubora tu…. ndiyo maana unamjua tajiri namba moja na sio masikini namba moja.
Bado sababu za huo umaskini zimetolewa sababu na watu wanazidi kutafiti mambo kila siku.
Kama wewe umeridhika na majibu ya kila changamoto unayoijua na hutaki kujua zaidi utakua sawa na baadhi ya hao ninaoona kama hawajabalance
 
Mara zote shule binafsi wanakua vinara katika matokeo ya mitihani aidha darasa la saba au kidato cha nne.

Sababu za matokeo yakiwa mazuri au mabaya zipo kama vile uwezo binafsi wa mwanafunzi, bidii, mazingira, rasilimali vitabu,walimu bora, maabara za kisasa, maslahi bora ya watumishi, mbinu mbalimbali za ufikishaji mada, msukumo wa familia na jamii inayomzunguka mwanafunzi.

Nikijikita zaidi kwenye hoja nikwamba waandishi wa habari walio wengi wamejikita zaidi kuwahoji waliofaulu na kufaulisha.

Wanawahoji wanafunzi walioingia kumi bora. Mfano jana Tanzania One amehojiwa akifuatiwa na mzazi wake na leo asubuhi Channel Ten wamewahoji washindi wawili walioingia kumi bora ambapo wamemhoji mshindi wa tano na mshindi wa kumi.

Ingekua bora zaidi kama wangehojiwa wasimamizi wa zile shule kumi za mwisho pia, baadhi ya waliofeli (kama wakitaka kutoa ushirikiano). Wazazi wa wanafunzi ili changamoto zijulikane, maafisa elimu na hata waziri wa elimu. Waieleze jamii hasa changamoto nizipi na kama taifa tunapunguzaje hii aibu ya kufeli, kupoteza fedha na hasara ya muda kwa miaka minne kisha mtu apate zero

Waandishi wa habari msiishi na kufanya kazi kwa ushabiki. Kueni wachokonozi na watafiti. Mtagundua changamoto nyingi sana ambazo baadhi zingeweza kutatuliwa.

Msikae na kuwaita tu watu studioni, wafuateni huko majumbani kwao mkawahoji juu ya hii aibu ya kufeli. Wapo watakaotoa ushirikiano na MTASIKIA MLIYOKUA HAMYAJUI WALA KUYATARAJIA.

Waandishi wa habari bado hamjaamua kubalance hii story ya kufaulu na kufeli. Mnataka kujua waliofaulu wamefanyaje lakini hamtaki kujua waliofeli wameshukiwa na vitu vyenye uzito kiasi gani vichwani mwao.

Ukiachia sababu kama michujo mikali shule binafsi ikilinganishwa na shule za umma kwamba kuna walioenda kwa ana ana dooo, ninaamini kuna vitu vingine vizito na vyenye ncha kali vinavyowapiga wanafunzi kwenye shule za umma. Vitu hivyo vinaweza kua vyakwao binafsi, mazingira yanayo wazunguka au historia zao na watu wengine kama wazazi, jamii, walimu na hata serikali.

Waandishi wa habari jaribuni kufanya mizania kwenye habari msizame upande mmoja.

Mkiongozwa na hisia kama sababu za kufeli mnazijua basi hata za kufaulu hamuwezi kushindwa kujua maana hizo za kufaulu zipo wazi zaidi na zinazungumzika kila uchao na uchwa

Natoa hoja jukwaani
Na bado wanadai waongezwe mishahara, Sasa nitaongea na mama mishahara ipandishwe kwa performance ya shule tuone hao wanaoshindwa kufundisha kama bado wataendelea kufelisha na kutuletea zero na Kila mkuu wa mkoa na mbunge watakuwa wanatoa bonus kwa shule za serikali zinazofanya vizuri pekee.
 
Back
Top Bottom