Shule za sekondari za kata zitakuza zaidi tofauti za kielimu kwa waumini wa kikristo na kiislamu

Derspiegel

JF-Expert Member
May 30, 2016
285
238
Lengo si kukosoa ubora wa elimu inayotolewa kwa shule za sekondari za kata na nikiri kuwa shule hizo zimeongeza chachu kubwa kwa wananchi kuimarisha elimu na huduma nyingine za jamii katika maeneo yao ya vijijini.

Tofauti na nchi nyingine za kiafrika ambazo zimekuwa zikikabiliwa na matatizo ya udini na ukabila, Tanzania tulifanikia kwa kiwango kikubwa kukwepa changamoto hiyo. Mojawapo ya sababi kubwa ya utaifa ni wanafunzi kuchaguliwa kusoma shule za nje ya mikoa yao huku wengo wao wakipangiwa ajira zao nje ya mikoa yao.

Hata hivyo kwa sasa, hali hiyo inabadilika kutokana na kupanuka kwa elimu ya sekondari ambapo wanafunzi wengi wanachaguliwa kuendelea na masomo hayo. Tatizo hapa ni kuwa wanafunzi hao hawapati fursa ya kutembea na kujifunza utamaduni na maendeleo ya sehemu nyingine za nchi na kuwafanya wanafunzi kuwa na identity fulani kwenye fikra zao.

Yote tisa, tatizo linakuja kwenye namna ya kutoa elimu ambayo inadumisha utamaduni wa kitanzania wa moyo wa kupendana na kujaliana miongoni mwa watanzania licha ya nchi yetu kuwa heterogeneous society.

Kuna jamii ambazo zimekuwa zikifanya vyema kielimu nchini lakini nyingine zimekuwa hazifanyi vyema. Hivyo, katika mazingira haya, shule za kata zimepelekea kuongezeka kwa gap kati ya jamii zilizozoeleka kuwa za kielimu na zisizo vizuri kielimu.

Mbaya zaidi ni kuwa, kuna chance kubwa ya mtumishi aliyeajiriwa eneo asilolipenda kuhama eneo hilo kwenda analopenda na hiyo inazidisha jamii nyingine kuwa nyuma still.
 
Umeifumba sana mada yako, na hizi Swaumu sijui kama kuna kuambulia kitu.......

Anyway kwa Tanzania hakuna jamii inayoweza kutoka kifua mbele ya kuwa wamesoma zaidi ya wengine, nikiangalia yanayoendelea nchini asilimia kubwa ya wananchi ni illiterate, ni kama vile uniambie walio vi.laza ndio wengi nchini(pamoja na hiyo dini yao) na wachache ndio hao literate(na dini yao).... Ukijumlisha na hali yetu kiuchumi, IQ za watu wetu(very poor, below the average)

Nchi ambayo huwezi tofautisha professor na STD 7, big ptyyuuuuuuuuu
 
Aidha, maeneo mengi ya jamii za kikristo - Moshi, Rombo, Hai, Arumeru, Bukoba, Muleba, Ngara, Karagwe, Kasulu, Rungwe, Kyela, Ileje, Mbozi, Njombe, Mufindi, Mbinga, Nyasa, Tarime, Rorya na Ukerewe, yana kiwango kikubwa cha wasomi. Katika maeneo yanayokaliwa na waislamu yenye wasomi wengi ni Lushoto, Muheza, Morogoro, Same (japokuwa yote haya wakristo ni wengi pia).

Ukiangalia vyema utakuta kuwa utofauti wa kielimu utazidi kuongezeka sana endapo hatutakuwa na mfumo wa kuwachanganya wanafunzi katika maeneo mbalimbali ili ikiwezekana wao huko wanapopangiwa kazi.

Ukiangalia maeneo ambayo hayapafomu vyema kielimu, mengi yako katika mikoa ya kati ya nchi, pamoja na mikoa ya pwani, huku mikoa ya mipakani mwa nchi ikifanya vyema.
 
Umeifumba sana mada yako, na hizi Swaumu sijui kama kuna kuambulia kitu.......

Anyway kwa Tanzania hakuna jamii inayoweza kutoka kifua mbele ya kuwa wamesoma zaidi ya wengine, nikiangalia yanayoendelea nchini asilimia kubwa ya wananchi ni illiterate, ni kama vile uniambie walio vi.laza ndio wengi nchini(pamoja na hiyo dini yao) na wachache ndio hao literate(na dini yao).... Ukijumlisha na hali yetu kiuchumi, IQ za watu wetu(very poor, below the average)

Nchi ambayo huwezi tofautisha professor na STD 7, big ptyyuuuuuuuuu
Nashukuru sana kwa mawazo yako. Nimefanya hivyo ili kuanzia mbali ili tufike kwenye issue yenyewe - namna ya kupunguza tatizo la udini (na kwa mbali ukanda/ukabila) linalotunyemelea kwa kasi sana.
 
Lengo hasa la thread hii ni kupunguza jaziba na mihemuko ya watanzania kujadili ama kupanga jambo lolote nchini kwa misingi ya kidini.

Sasa, kamwe hatutaweza kuliondoa tatizo la udini kama hatuelewi chanzo cha jamii fulani kuwa mbele/nyuma kielimu.

Tukibakia na mawazo kuwa umasikini wetu ulisababishwa hasa na ukoloni wa wazungu waliotutawala hasa kuanzia karne ya 19 - 20, basi kamwe hatutatokea tuelewe sababu ya kweli ya utofauti wa kielimu, hivyo hatutaweza kuwaambia watu wetu chanzo cha hali hiyo. Tukubali hali yetu kwanza then tutakuta mambo yanakua mepesi kuyakubali.

Kuna nchi nyingi zilikuwa hazitaki masuala ya integration hasa kwenye michezo lakini baada ya muda ziligundua zilikuwa zinaloose ilihali zina resources ya kutosha.

Mfano sera ya michezo ya Ujerumani tangu 2000 kwa Academies kuendeleza jamii zote zikiwemo za kiafrika. Angalia tangu 2002 jinsi waafrika na wasio Wajerumani walivyo na nguvu kwenye timu hiyo.
 
Lengo hasa la thread hii ni kupunguza jaziba na mihemuko ya watanzania kujadili ama kupanga jambo lolote nchini kwa misingi ya kidini.

Sasa, kamwe hatutaweza kuliondoa tatizo la udini kama hatuelewi chanzo cha jamii fulani kuwa mbele/nyuma kielimu.

Tukibakia na mawazo kuwa umasikini wetu ulisababishwa hasa na ukoloni wa wazungu waliotutawala hasa kuanzia karne ya 19 - 20, basi kamwe hatutatokea tuelewe sababu ya kweli ya utofauti wa kielimu, hivyo hatutaweza kuwaambia watu wetu chanzo cha hali hiyo. Tukubali hali yetu kwanza then tutakuta mambo yanakua mepesi kuyakubali.

Kuna nchi nyingi zilikuwa hazitaki masuala ya integration hasa kwenye michezo lakini baada ya muda ziligundua zilikuwa zinaloose ilihali zina resources ya kutosha.

Mfano sera ya michezo ya Ujerumani tangu 2000 kwa Academies kuendeleza jamii zote zikiwemo za kiafrika. Angalia tangu 2002 jinsi waafrika na wasio Wajerumani walivyo na nguvu kwenye timu hiyo.
 
Aidha, maeneo mengi ya jamii za kikristo - Moshi, Rombo, Hai, Arumeru, Bukoba, Muleba, Ngara, Karagwe, Kasulu, Rungwe, Kyela, Ileje, Mbozi, Njombe, Mufindi, Mbinga, Nyasa, Tarime, Rorya na Ukerewe, yana kiwango kikubwa cha wasomi. Katika maeneo yanayokaliwa na waislamu yenye wasomi wengi ni Lushoto, Muheza, Morogoro, Same (japokuwa yote haya wakristo ni wengi pia).
Ukiangalia vyema utakuta kuwa utofauti wa kielimu utazidi kuongezeka sana endapo hatutakuwa na mfumo wa kuwachanganya wanafunzi katika maeneo mbalimbali ili ikiwezekana wao huko wanapopangiwa kazi.
Ukiangalia maeneo ambayo hayapafomu vyema kielimu, mengi yako katika mikoa ya kati ya nchi, pamoja na mikoa ya pwani, huku mikoa ya mipakani mwa nchi ikifanya vyema.

Nafikiri itakuwa hujasafiri mikoa ya iliyoko maeneo ya Pwani,huko huko mikoa iiyoko maeneo ya Pwani ziko shule za elimu za kiwango cha juu,na wapo watoto wengi wa hiyo dini,unayodhaniya wewe hawasomi.

Kwa mfano mkoa wa Tanga ndio,ilikuwa na secondary ya kwanza Tanganyika kabla ya Uhuru inayoitwa Old Tanga secondary school,na vile vile kuwa na shule ya kwanza baada ya Uhuru wa Tanganyika,inayoitwa Tanga School.

Na vile kuwa na shule ya Galanos,Usagara(Kareemjee).Mkwakwani Secondary,Popatlal, hizi zote ni shule maarufu sana na za mda mrefu,na ziko katikati ya jiji hilo.Kabla ya kuongezeka shule nyingine nyingi jijini hapo.

Karibia zote hizo zina mpaka kidato cha sita,na ni toka enzi za miaka ya 70,na 80, nafikiri hapo ni Old Tanga na Mkwakwani ndio hawana A level tu.
 
Mtoa mada usiandike mafumbo, humu hakuna IS wala Alshabaab. Mada iko kama fasihi.
 
Lengo si kukosoa ubora wa elimu inayotolewa kwa shule za sekondari za kata na nikiri kuwa shule hizo zimeongeza chachu kubwa kwa wananchi kuimarisha elimu na huduma nyingine za jamii katika maeneo yao ya vijijini.
Tofauti na nchi nyingine za kiafrika ambazo zimekuwa zikikabiliwa na matatizo ya udini na ukabila, Tanzania tulifanikia kwa kiwango kikubwa kukwepa changamoto hiyo. Mojawapo ya sababi kubwa ya utaifa ni wanafunzi kuchaguliwa kusoma shule za nje ya mikoa yao huku wengo wao wakipangiwa ajira zao nje ya mikoa yao.
Hata hivyo kwa sasa, hali hiyo inabadilika kutokana na kupanuka kwa elimu ya sekondari ambapo wanafunzi wengi wanachaguliwa kuendelea na masomo hayo. Tatizo hapa ni kuwa wanafunzi hao hawapati fursa ya kutembea na kujifunza utamaduni na maendeleo ya sehemu nyingine za nchi na kuwafanya wanafunzi kuwa na identity fulani kwenye fikra zao.
Yote tisa, tatizo linakuja kwenye namna ya kutoa elimu ambayo inadumisha utamaduni wa kitanzania wa moyo wa kupendana na kujaliana miongoni mwa watanzania licha ya nchi yetu kuwa heterogeneous society.
Kuna jamii ambazo zimekuwa zikifanya vyema kielimu nchini lakini nyingine zimekuwa hazifanyi vyema. Hivyo, katika mazingira haya, shule za kata zimepelekea kuongezeka kwa gap kati ya jamii zilizozoeleka kuwa za kielimu na zisizo vizuri kielimu.
Mbaya zaidi ni kuwa, kuna chance kubwa ya mtumishi aliyeajiriwa eneo asilolipenda kuhama eneo hilo kwenda analopenda na hiyo inazidisha jamii nyingine kuwa nyuma still.
Unataka kuandika nini hasa? Naona umejichanganya sana. Mara ukanda, udini, shule za kata, ukosefu wa walimu. What is it that you want to put down? Ebu fafanua. Zamani wanafunzi waliweza kusoma nchi nzima kwa kuwa shule zilikuwa chache. Sasa shule ziko kila kata. Bado unataka mwanafunzi aache shule ya kata kule Mtwara akasome shule ya kata Bukoba? Nani analipa nauli na atakaa wapi? Kumbuka shule za kata ni za dei ndo maana siyo ghali kuziendesha. Lakini mzazi mwenye uwezo bado anaweza kumtoa mwanaye Mtwara akampeleka shule ya binafsi ya bweni Bukoba.
 
Kuna sehemu kama unaiweka kando hivi ili mjadara uwe mjarabu, ongezea tu nyama kidogo ili na siye ma slow movers tuweze kuchangia mkuu.
 
Nafikiri nia mojawapo na pengine kubwa ya shule za Kata na hasa za sekondari ni kuhakikisha watoto wanaendelea na elimu katika maeneo ambayo si mbali na nyumbani kwao 'kwa gharama nafuu'. Na gharama nafuu namaanisha kuwa nje ya wilaya au mkoa ambapo mzazi atalazimika kugharamia usafiri na malazi/ chakula kwa kijana wake.

Sasa ili kuhakikisha kuwa kama taifa tunabaki na Umoja, kuingiliana/ kuchanganyika na kuondoa matabaka baina ya wilaya na wilaya, mkoa na mkoa, basi kuwe na jitihada za makusudi ya Serikali kuu na Halmashauri/ jiji na wananchi wenyewe kuhakikisha;

1 Shule za Kata za sekondari , zina mabweni na kantini.

2 Kuwe na utaratibu wa makusudi kati ya wilaya na wilaya au mkoa na mikoa mingineyo wa kubadilishana wanafunzi ambao wakiwa masomoni kutoka hizo wilaya au mikoa ya mbali na nyumbani, wanahakikishiwa si kusoma vizuri tu, bali chakula kizuri na malazi/makazi katika mazingira mazuri.
 
Mtoa mada usiandike mafumbo, humu hakuna IS wala Alshabaab. Mada iko kama fasihi.
Nimeiacha hivyo, ili kuongeza wigo wa kuijadili. Nashindwa nianzie wapi hivyo nawaombeni tujitahidi kwa pamoja kuifikiria zaidi labda tunaweza kupata solution humu jf.
Naomba nikuulize, mpaka sasa unaamini kuwa jamii fulani zinaendelea kiusomi kutokana na kwamba wakoloni walijenga kwa upendeleo miundombinu ya kielimu maeneo yao kipindi cha ukoloni? Kama ni hivyo, mbona kunaendelea kuwepo utofauti mkubwa tu kati ya maeneo yaliyoendelea tangu zamani na yasiyoendelea?
Unaweza kusema kuwa shule za kata zimepunguza kidogo utofauti huo lakini utofauti unaendelea kuongezeka kila unapopanda elimu ya juu hadi vyuo vikuu.
 
Kuna baadhi tumekuwa tukidai shule za kata hazifanyi vyema kutokana na mazingira magumu ya kimiundombinu. Sasa tujiulize mbona huko shule za msingi zenye miundombinu mizuri huwa kuna wengi kabisa unaona hazimo za darasani, sasa kwa nini wakifika sekondari tudhani kuwa wote zimo za kuhimili masomo ya sekondari?
Kama tunaamini kuwa mazingira bora ndiyo determinant mbona wanafunzi wenye asili ya mkoa wa Dar es Salaam (wazaramo) hawafanyi vyema licha ya kuwa mjini ambako mazingira yote yanaruhusu mwanafunzi kufanya vyema? Kuna kitu tu tukitafute tujue the factor behind this scenario.
 
Nafikiri itakuwa hujasafiri mikoa ya iliyoko maeneo ya Pwani,huko huko mikoa iiyoko maeneo ya Pwani ziko shule za elimu za kiwango cha juu,na wapo watoto wengi wa hiyo dini,unayodhaniya wewe hawasomi.
Kwa mfano mkoa wa Tanga ndio,ilikuwa na secondary ya kwanza Tanganyika kabla ya Uhuru inayoitwa Old Tanga secondary school,na vile vile kuwa na shule ya kwanza baada ya Uhuru wa Tanganyika,inayoitwa Tanga School.
Na vile kuwa na shule ya Galanos,Usagara(Kareemjee).Mkwakwani Secondary,Popatlal, hizi zote ni shule maarufu sana na za mda mrefu,na ziko katikati ya jiji hilo.Kabla ya kuongezeka shule nyingine nyingi jijini hapo.
Karibia zote hizo zina mpaka kidato cha sita,na ni toka enzi za miaka ya 70,na 80, nafikiri hapo ni Old Tanga na Mkwakwani ndio hawana A level tu.

Aiseeh unasema kweli kabisa wala sikusema kuwa mkla wa Tanga haupafomu. Naielewa wilaya ya Lushoto na Muheza (hata Korogwe) kuna vichwa balaa na ziko karibia sawa na nyingine zinazofanya vyema, isipokuwa tu Handeni na Pangani.
 
Us
Unataka kuandika nini hasa? Naona umejichanganya sana. Mara ukanda, udini, shule za kata, ukosefu wa walimu. What is it that you want to put down? Ebu fafanua. Zamani wanafunzi waliweza kusoma nchi nzima kwa kuwa shule zilikuwa chache. Sasa shule ziko kila kata. Bado unataka mwanafunzi aache shule ya kata kule Mtwara akasome shule ya kata Bukoba? Nani analipa nauli na atakaa wapi? Kumbuka shule za kata ni za dei ndo maana siyo ghali kuziendesha. Lakini mzazi mwenye uwezo bado anaweza kumtoa mwanaye Mtwara akampeleka shule ya binafsi ya bweni Bukoba.
Usinikasirikie bure ndugu yangu. Yote unayoyasema kila mtu anayaelewa isipokuwa haujawahi kuhisi kuwa, sasa hivi maeneo ambayo hayakuwa na miundombinu mizuri ya kielimu, yataendelea kudumaa (kulinganisha na yale yaliyoendelea) kwa kuwa wanafunzi watakuwa wakibakia maeneo yao ya asili. Lakini mbaya zaidi, walimu wengi wazuri hupendelea kurudi kwao palipoendelea ama kuhama kwao palipoendelea. Fuatilia jinsi shule zilizo katika wilaya/mikoa yenye mazingira magumu zinavyostruggle kupata walimu.
 
Nafikiri nia mojawapo na pengine kubwa ya shule za Kata na hasa za sekondari ni kuhakikisha watoto wanaendelea na elimu katika maeneo ambayo si mbali na nyumbani kwao 'kwa gharama nafuu'. Na gharama nafuu namaanisha kuwa nje ya wilaya au mkoa ambapo mzazi atalazimika kugharamia usafiri na malazi/ chakula kwa kijana wake. Sasa ili kuhakikisha kuwa kama taifa tunabaki na Umoja, kuingiliana/ kuchanganyika na kuondoa matabaka baina ya wilaya na wilaya, mkoa na mkoa, basi kuwe na jitihada za makusudi ya Serikali kuu na Halmashauri/ jiji na wananchi wenyewe kuhakikisha;
1 Shule za Kata za sekondari , zina mabweni na kantini.
2 Kuwe na utaratibu wa makusudi kati ya wilaya na wilaya au mkoa na mikoa mingineyo wa kubadilishana wanafunzi ambao wakiwa masomoni kutoka hizo wilaya au mikoa ya mbali na nyumbani, wanahakikishiwa si kusoma vizuri tu, bali chakula kizuri na malazi/makazi katika mazingira mazuri.
Yaani wewe umeamua kumeza kabisa tonge nililokuwa nimepanga kulimeza mwenyewe. Nakushukuru sana kuwa na idea hiyo. Nakuhakikishia kuwa ni vyema serikali ifanye uamuzi huo wa hizo shule za kata ziwe hata za hosteli kwa wanafunzi wote (wakiwemo wavulana) ili ziruhusu kuchukua wanafunzi angalao wa mkoa mmoja ama wilaya za karibu.
Hii ncho yetu bado hajawa homogeneous kihivyo na ni bora ukabila wetu siyo mkali kama udini unavylanza kutusumbua sasa. Na dalili zote zinaonyesha sloner or later tutajibagua kwa sifa hiyo ya udini. Tujipange kulishinda suala hilo.
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Shule za kata hazifanyi vizuri kwa sababu kisilabasi wako nyuma sana unakuta private wako silabasi ya 10 kata wako ya 5 lakini kwenye mtihani wa taifa hawajui kuwa wengine hawakufika huko maswali yanatolewa sawa .Na walimu wa shule za kata wala hawajali kama nyuma na wanajua kabisa .Ukiona mwanafunzi wa kata kafaulu vizuri ni juhudi zake mwenyewe kutafuta material sehemu mbali mbali pia tuisheni .Mimi ni shahidi kabisa maana nimesoma kata nilikuwa nahangaika sana kutafuta material pia tuition yaani kiukweli nilikuwa najituma mwenyewe kufanya hivyo mwisho wa siku nikaondoka na division 2 hata walimu wangu wa kata hawakuamini .
 
Shule za Kata haziongezi pengo la elimu kati ya Wakristo na Waislamu bali pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho!! Msiwe mnajidanganya na idadi ndogo ya Wakristo wasiofika hata 5% wanaopata zile One za Marian Girls!! Kuna Waislamu wengi sana wanaosomesha watoto wao kwenye shule zinazotoa matokeo mazuri na pia kuna Wakristo wengi sana ambao watoto wao wapo hizo shule za Kata! Determinant inapatikana hapo!

Mwakajana nilifanya research na area of study ilikuwa ni shule za Kilimanjaro na Mbeya! Niliyoyaona kwenye research ile nikajiambia endapo watu wangefahamu; wala pasingetokea jamii moja kutamba kwamba wao ni wasomi! Hata hao Wachaga ambao inaonekana ni wasomi; hao wasomi ni tone tu la maji kwenye bahari ya Wachaga wasio na tofauti na Wandengereko kielimu!

Hapa ifahamike kwamba hata huko Kilimanjaro na Mbeya; sehemu kubwa sana ya wananchi mkombozi wao ni shule za kata! Kwenye matokeo ya NECTA, majority nao huwa wanaondoka na mabuyu kama ndugu zao wa maeneo mengine!

Kilimanjaro na Mbeya kuna shule nyingi sana tena sana zinazoenda kwa staili ya St. XYZ! Majority ya hizi St.XYZ nazo ni wazalishaji wakubwa sana wa ZERO na ndizo zinabeba watoto wengi wa Kikristo!! Yaani majority ya hizi shule wala hazina tofauti na shule za wenzao Waislamu katika kufotoa mabuyu!

Ukiyafahamu hayo ndipo utajua ni namna gani hii nchi ilivyo kielimu... iwe ni kwa Wakristo au Waislamu! Ingawaje siwezi kuthubutu kuzikejeli shule za kata; lakini ukweli bado utabaki pale pale zinaongeza gap ya usomi kati ya wenye nacho na wasio nacho; na sio kati ya Waislamu na Wakristo! Ukiingia madarasa ya shule za kata za Kilimanjaro au Mbeya utakuta zimejaza Wakristo watupu na wala sio Waislamu na over 95% ya hawa huwa wanatoka na zero pamoja na IV mbovu!

NOTE: Naziunga mkono shule za Kata-- mambo mengine hayazuiliki!
 
Aidha, maeneo mengi ya jamii za kikristo - Moshi, Rombo, Hai, Arumeru, Bukoba, Muleba, Ngara, Karagwe, Kasulu, Rungwe, Kyela, Ileje, Mbozi, Njombe, Mufindi, Mbinga, Nyasa, Tarime, Rorya na Ukerewe, yana kiwango kikubwa cha wasomi. Katika maeneo yanayokaliwa na waislamu yenye wasomi wengi ni Lushoto, Muheza, Morogoro, Same (japokuwa yote haya wakristo ni wengi pia).
Ukiangalia vyema utakuta kuwa utofauti wa kielimu utazidi kuongezeka sana endapo hatutakuwa na mfumo wa kuwachanganya wanafunzi katika maeneo mbalimbali ili ikiwezekana wao huko wanapopangiwa kazi.
Ukiangalia maeneo ambayo hayapafomu vyema kielimu, mengi yako katika mikoa ya kati ya nchi, pamoja na mikoa ya pwani, huku mikoa ya mipakani mwa nchi ikifanya vyema.
Mkuu waliosoma sana wakristo wa hiyo mikoa wametusaidia nini kama taifa..? Si akina Andrew Chenge, Tibaijuka, Sumaye, Lowasa nd Co ni miongoni mwao..? Au ukiwa mjanja kuwaibia wenzio ndio kusaidia
 
Nimeiacha hivyo, ili kuongeza wigo wa kuijadili. Nashindwa nianzie wapi hivyo nawaombeni tujitahidi kwa pamoja kuifikiria zaidi labda tunaweza kupata solution humu jf.
Naomba nikuulize, mpaka sasa unaamini kuwa jamii fulani zinaendelea kiusomi kutokana na kwamba wakoloni walijenga kwa upendeleo miundombinu ya kielimu maeneo yao kipindi cha ukoloni? Kama ni hivyo, mbona kunaendelea kuwepo utofauti mkubwa tu kati ya maeneo yaliyoendelea tangu zamani na yasiyoendelea?
Unaweza kusema kuwa shule za kata zimepunguza kidogo utofauti huo lakini utofauti unaendelea kuongezeka kila unapopanda elimu ya juu hadi vyuo vikuu.
Siyo rahisi kujadili mada isiyoeleweka. Kama ulishindwa kuiweka vizuri ungeuliza walau swali. Lakini kama ilivyo ni mchanganyo mkubwa na inaelekea hata wewe huna uhakika unataka kujadili nini.
 
Back
Top Bottom