Shule za Roman Catholic si rafiki tena na masikini, Ada yao ni Zaidi ya Shule binafsi

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,753
7,075
Wandugu,

Katika hali ya kustajabisha , kanisa la Roman Catholic limekumbwa na sintomfahamu kwa kujiweka sana karibu na kila dalili za ufisadi. Jambo hili nimekutana nalo baada ya kuangaika sana kumtafutia shule kijana wangu, hasa katika shule za kanisa katoliki ili angalau apate elimu ya dini yake pamoja na masomo yake, cha kushangaza nimekuta karo zinaanzia million 2 mpaka mil 3 kwa mwaka, cha kushangaza zaidi kuna shule za watu binafsi zinaanzia laki 7 hadi 9 na zainafaulisha vizuri tu. Nikawa najiuliza hivi hawa viongozi wa makanisa wanategemea kweli mtoto wa masikini kusoma pale au wanachukulia ule msemo wa aliyenacho ataongezewa, ajabu zaidi ni pale nilipoomba form naambiwa ni elfu 30 na baada ya hapo atafanya mitihani akishinda au kushindwa hizo hela hazirudishi, Maandalizi ya form hayazidi elfu tano lakini tunalipia 30 lakini kwingine ni elfu 10 tu.

Tunakuomba sana Cardinari Pengo kufuatilia shule hizi zenye mlengo wa kuwa karibu na matajiri tu na sisi masikini watufikie , kama ilivyokuwa zamani kwamba kazi ya kueneza injili ni pamoja na kupata elimu bora kwa watu wote.

Pia kuna baadhi ya shule zinazoanza na St. Zina matatizo sana hasa za mkoa wa Morogoro, Kama vile St. Joseph Soga, shule hii imeanza kuaribika kupita kiasi, watoto wanatoroka sana, wanamiliki simu, wanaomba sana pesa kwa ndugu na jamaa sijui wanazifanyia nini. Shule nyingi hazina uzio angalau hata wa michongoma, au sengengenge jambo ambalo ni hatari sana kwa mazingira ya wanaosoma boarding, wengi wanaokuwa karibu na vijiji wanaaribika kwa bangi na vitabia vingine.

Nakuomba Tafakari na chukua hatua ili kanisa letu liwe bora kwa elimu, upendo na thamani.
 
Kama unalolisema ni kweli basi kanisa limenasa kwenye mtego wa shetani yaani limekengeuka. Yawapasa viongozi wa dini wathamini utu badala pesa. Kanisa lijitazame upya vinginevyo litajichimbia KABURI.
 
Toka lini KANISA KATOLIKI likawa karibu na maskini, KANISA katoliki miaka yote lipo kuwanyonya maskini...!

Ila akili kumkichwa uibiwe usiibiwe shauri yako lkn ukweli ndio huu...

KANISA KATOLIKI halijawahi kuacha unyonyaji toka kuanzishwa kwake
 
Toka lini KANISA KATOLIKI likawa karibu na maskini, KANISA katoliki miaka yote lipo kuwanyonya maskini...!

Ila akili kumkichwa uibiwe usiibiwe shauri yako lkn ukweli ndio huu...

KANISA KATOLIKI halijawahi kuacha unyonyaji toka kuanzishwa kwake

Kuna Mchungani Gani Ambaye Anawapenda Masikini??
 
Jaribu pia kuangalia gharama za kuendesha hiyo shule. Ni kweli shule ni za kanisa lakini shule zinahitaji pesa za kuendeshea ili ziweze kuwa na matokeo mazuri, Mwl mzuri kumpata lazima umwekee mazingira mazuri pia mshahara mzuri.Vitabu, maabara nk vyote vikiwa vizuri na matokeo yatakua mazuri. Hivyo tusilaumu tuu gharama tuangalie na kiwango cha shule na uendeshaji wake
 
Hapo sasa.. wachungaji wanaendesha hammer na helkopter..wao wanakaa juani kusikiliza mahubiri .. wakatoliki wako juu watake wasitake

Wenyewe wanapeleka Mamilioni ya Pesa kama Sadaka kisa wapate Ujauzito .... Halafu mwisho wa Siku wanajifungua MTOTO NYOKA ........

Leo Unalalamika Milioni 2 zinaliwa na Kanisa katoliki....
 
Wenyewe wanapeleka Mamilioni ya Pesa kama Sadaka kisa wapate Ujauzito .... Halafu mwisho wa Siku wanajifungua MTOTO NYOKA ........

Leo Unalalamika Milioni 2 zinaliwa na Kanisa katoliki....

Halafu anadhani gharama ya kuendesha shule ni ndogo...mtoto akae boarding. .walimu hawalipwi vipesa mbuzi...wanalipwa pesa nzuri kuwa motivate..na ndio naana watoto wanafaulu...ss mwanafunzi alipe ada laki 7...hajala...hajaoga..hajatumia umeme...huyo mwalimu alipwe sh ngapi...vitabu...??
 
Hapo sasa.. wachungaji wanaendesha hammer na helkopter..wao wanakaa juani kusikiliza mahubiri .. wakatoliki wako juu watake wasitake

Dhambi ni dhambi tu, uwe unaimba kwaya na mapambio au Uimbe Haleluya- Ukweli ni kuwa kanisa katoliki tokea kuanzishwa kwake halijawahi kuwa upande wa maskini
 
Dhambi ni dhambi tu, uwe unaimba kwaya na mapambio au Uimbe Haleluya- Ukweli ni kuwa kanisa katoliki tokea kuanzishwa kwake halijawahi kuwa upande wa maskini

Ulikuwepo tokea Mwanzo au Umejazwa Chuki Kuhusu kanisa Katoliki??

Mbona Chuoni Hamlalamiki Kuwa wana Bei kubwa.......
 
Wenyewe wanapeleka Mamilioni ya Pesa kama Sadaka kisa wapate Ujauzito .... Halafu mwisho wa Siku wanajifungua MTOTO NYOKA ........

Leo Unalalamika Milioni 2 zinaliwa na Kanisa katoliki....

Kanisa katoliki ni Kanisa la Mungu, lilitakiwa kuwa karibu na maskini kwani ndio hasa wanateseka hivyo wapewe misaada au huduma kwa gharama nafuu...hali iko tofauti
 
Makosa mawili hayahalalishi dhambi, okay...?

Sasa mbona Umeona Kosa kwa Kanisa Katoliki .. Hilo kosa la Kwanza je

Ninekuuliza tu kuwa Mchungaji Gani anaowapenda Masikini na Anawasomesha kwa Gharama ndogo
 

Gharama za uendeshaji ziko juu ndo maana ada zimekuwa juu pia

Hata hivyo kama wewe ni maskini sana kula kulingana na urefu wa kamba yako mbona hata serikalini vijana wanafaulu tu.

Kuhusu dini mnunulie vitabu vya dini awe ananisomea mwenyewe Tu si vinauzwa(katekisimu,Chuo kidogo cha sala,bible,novena eti)

Ukiona elimu gharama,jaribu ujinga.
 
Wala usijipe mawazo BRN itaziumbua shule nyingi.
Shule nyingi za private zilikuwa zinafanya ujanja ujanja ambao timu ya BRN walishautambua.

Mfano walikuwa wanatabia unaweza msomosha mtoto hadi class 5au6 mara unaambiwa mtoto wako mhamishe hajafikia wastani wanaoutaka. Hapo mzazi anaanza haha mtafutia shule nyingine. Kumbe mchezo wa hizi shule ni kuingiza necta timu bingwa tu. Sasa huu mpango wa ujanja ujanja wa ubaguzi wa watoto ambao wao wenyewe wamechangia kuwa na maendeleo mabovu umezuiliwa from class 4-6 ili mtoto arejeshwe class panahitajika kibari cha afisa elimu mkoa tena barua ya maombi ianzie kwa mzazi- mwalim mkuu-afisa elimu mkoa. Na from class 7 kurejeshwa class za chini kinahitajika kibari cha mratibu elim mkoa.

Hii itaziumbua shule nyingi sana. Stay tuned. BRN
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom