Andindile
JF-Expert Member
- Mar 18, 2009
- 304
- 16
Jina la Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Dr., mheshimiwa rais Jakaya Mrisho Kikwete limeshushwa hadhi na matokeo ya kidato cha nne ya shule ya Sekondari ya J.M. Kikwete iliyopo wilayani Mbozi nje kidogo ya mji mdogo wa Tunduma . Shule hiyo ambayo imepewa heshima ya pekee ya kutumia jina la Kikwete imefanya vibaya kwenye matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni hata kufanya jina la J.M. Kikwete likose heshima inayostahili. Nimeambatanisha matokeo ya shule husika. Kwa nini jambo kama hili liruhusiwe kutokea? Hivi rais anataarifa kuwa kuna shule inatumia jina lake? Kama taarifa anazo, amefanya jitihada gani kuhakikisha kuwa wanafunzi na walimu wa shule hiyo wanalitangaza jina lake vizuri kwa kufanya vyema kwenye matokeo ya kitaifa?