Shule wanazopitia watoto siku hizi

Swet-R

JF-Expert Member
Jul 20, 2018
5,613
8,042
Watoto siku hizi wanabebeshwa madaftari mengi yenye uzito kuzidi umri wao. Unakutana na mtoto wa darasa la kwanza kabeba mkoba una madaftari 8 mpaka 10, yote yale yenye kurasa nyingi.

Nimekutana na kisa kimoja mtoto wa darasa la pili analalamikia mgongo. Wazazi wake wakawa hawajui ni kwa nini. Baadae nikawaambia wamwangalie anapoenda shule tembea yake akibeba daftari. Ndipo ikagundulika anasumbiliwa na mgongo sababu ya uzito wa madaftari.

Watoto siku hizi wanabebeshwa daftari nyingi lakini bado elimu yetu ndio inazidi kudidimia. Watu wa elimu hawana ubunifu kabisa siku hizi, tofuati na kipindi chetu cha JACKSON MAKWETA. Enzi zetu darasa la kwanza la pili daftari 2 tu la HISABATI NA KISWAHILI. Hili la kiswahili linahusika pia kwenye mwandiko. Na Elimu enzi hizo ilikuwa bora sana.


Hili bunge linafanya nini kuvisemea vitu kama hivi. Wenzetu Kenya mtoto wa darasa la kwanza wanabeba daftari 2,3 na elimu yao iko vizuri kuliko sisi.

Kibaya zaidi watoto siku hizi hawafurahii kabisa utoto wao. Hawapewi hata muda wa kuutumia utoto wao, hawapewi muda wa michezo. Kutwa ni darasani. Mtoto anaanza kwenda shule kama mzaha hivi anapelekwa akashinde na wenzie kuanzia miaka mitatu anapelekwa chekechea, wengine miwili. Hapo akianza tu, ndio ujue imetoka hiyo mpaka chuo kikuu. Mtoto anaamushwa saa 11 anaandaliwa. Basi la shule linamchukua anasinzia humo kwenye gari mpaka kufika shule na kuingia darasani saa 2 anakuwa amechoka kabla hajaanza masomo. Ukitoka darasani anaenda tuition mpaka saa 1 usiku tena anaingia nyumbani akiwa amebeba daftari nyingi, anakuwa amechoka mno.

Wabunge waingilie kati hili. Kizazi kijacho kinapotea mapema kabisa. Ni kama hawaoni hivi

Kuna watu watakuja hapa kusema ndio mtoto akomae. Anakomaa huku elimu ikishuka kwa kasi. Fikiria wewe uliesoma miaka ya 90,mazingira yale na sasa. Na elimu ilivyokuwa bora enzi hizo.
 
Kipindi cha nyuma Elimu haikuwa bora kipindi hiko ila sisi ndio tulikuwa bora kwani hatukuwa tumechanjwa chanjo yoyote na uwezo wetu wa kufikiria ulikuwa mkubwa kuliko kizazi hiki cha chanjo. Wana IQ ndogo sana. Angalia tu hata humu JF ya 2000's na uilinganishe na ya sasa ya 2020"s utaona wanaongelea na kutukanana kuhusu kutoana marinda tu. Mungu awasaidie kwa kweli.
 
Tena uku kwenye shule zetu za st.kayumba ni mtihani kwa kweli dogo wa dalasa la nne hajui Tanganyika ilipata Uhuru mwaka gani
Hajui ata iyo Tanganyika yenyewe ni nini
 
Kipindi cha nyuma Elimu haikuwa bora kipindi hiko ila sisi ndio tulikuwa bora kwani hatukuwa tumechanjwa chanjo yoyote na uwezo wetu wa kufikiria ulikuwa mkubwa kuliko kizazi hiki cha chanjo. Wana IQ ndogo sana. Angalia tu hata humu JF ya 2000's na uilinganishe na ya sasa ya 2020"s utaona wanaongelea na kutukanana kuhusu kutoana marinda tu. Mungu awasaidie kwa kweli.
Kumbe eti. Unaweza kuwa sahihi mkuu. Umeniongezea jambo
 
Acha kabisa mimi mwanangu yupo la nne masomo kumi madaftari wanatumia makaunta tena kwaya mbili yan ule mzigo wa begi anaobeba ni huruma tupu bado ujachanganya darasan wanaingia saa kumi na mbili asubuhi na kutoka saa kumi na mbili jioni
 
Kabisaa...

Mi huwa na lia na Ma Profesor wetu Ma dkt na hata wana vyuonii..
Wameshindwaa mazimaa kubadili mitaala yetu na kufanya iendane na Elimu ya kisasa...

Nasema tena wasomi wetu wame chemkaa
Nasema tena wamechemkaa wana kimbilia nakusubiri teuzi tuu waje wawe wanasifia serikali na kutembelea V8 na kusain mikataba ya hovyo.

Elimu yetu nisawa na kichwa cha mwendawazimu.
Mtoto anamaliza form 4 anapata Dvn 2 lakini hajui kuandika vizuri na kupanga kazi jamaniii.
 
Watoto siku hizi wanabebeshwa madaftari mengi yenye uzito kuzidi umri wao. Unakutana na mtoto wa darasa la kwanza kabeba mkoba una madaftari 8 mpaka 10, yote yale yenye kurasa nyingi.

Nimekutana na kisa kimoja mtoto wa darasa la pili analalamikia mgongo. Wazazi wake wakawa hawajui ni kwa nini. Baadae nikawaambia wamwangalie anapoenda shule tembea yake akibeba daftari. Ndipo ikagundulika anasumbiliwa na mgongo sababu ya uzito wa madaftari.

Watoto siku hizi wanabebeshwa daftari nyingi lakini bado elimu yetu ndio inazidi kudidimia. Watu wa elimu hawana ubunifu kabisa siku hizi,tofuati na kipindi chetu cha JACKSON MAKWETA. Enzi zetu darasa la kwanza la pili daftari 2 tu la HISABATI NA KISWAHILI. Hili la kiswahili linahusika pia kwenye mwandiko. Na Elimu enzi hizo ilikuwa bora sana.


Hili bunge linafanya nini kuvisemea vitu kama hivi
Wenzetu Kenya mtoto wa darasa la kwanza wanabeba daftari 2,3 na elimu yao iko vizuri kuliko sisi.

Kibaya zaidi watoto siku hizi hawafurahii kabisa utoto wao. Hawapewi hata muda wa kuutumia utoto wao,hawapewi muda wa michezo. Kutwa ni darasani. Mtoto anaanza kwenda shule kama mzaha hivi anapelekwa akashinde na wenzie kuanzia miaka mitatu anapelekwa chekechea,wengine miwili. Hapo akianza tu,ndio ujue imetoka hiyo mpaka chuo kikuu. Mtoto anaamushwa saa 11 anaandaliwa. Basi la shule linamchukua anasinzia humo kwenye gari mpaka kufika shule na kuingia darasani saa 2 anakuwa amechoka kabla hajaanza masomo. Ukitoka darasani anaenda tuition mpaka saa 1 usiku tena anaingia nyumbani akiwa amebeba daftari nyingi,anakuwa amechoka mno.

Wabunge waingilie kati hili. Kizazi kijacho kinapotea mapema kabisa. Ni kama hawaoni hivi

Kuna watu watakuja hapa kusema ndio mtoto akomae. Anakomaa huku elimu ikishuka kwa kasi. Fikiria wewe uliesoma miaka ya 90,mazingira yale na sasa. Na elimu ilivyokuwa bora enzi hizo.
Naitetea serikali na wabunge unaowanyooshea kidole,hicho unachopigania wawe na daftari tatu ndicho kilichopo mashuleni toka 2014 tulipobadili mtaala.

Tuna Somo la kusoma, kuandika na kuhesabu.
Pia tuna Afya na Mazingira na Sanaa (haya masomo yanafundishwa kwa vitendo).
Kwa siku wanasoma masomo matatu tu na daftari tatu tu.
USHAURI: Beba hayo madaftari nane nenda kwa mwalimu mkuu atamwita mwalimu wa darasa akupe maelezo ya kutosha
 
Kipindi cha nyuma Elimu haikuwa bora kipindi hiko ila sisi ndio tulikuwa bora kwani hatukuwa tumechanjwa chanjo yoyote na uwezo wetu wa kufikiria ulikuwa mkubwa kuliko kizazi hiki cha chanjo. Wana IQ ndogo sana. Angalia tu hata humu JF ya 2000's na uilinganishe na ya sasa ya 2020"s utaona wanaongelea na kutukanana kuhusu kutoana marinda tu. Mungu awasaidie kwa kweli.

Kweli kabisa,
Kuna jamaa yangu mmoja nilikua nikimwambia kila siku kuwa,watoto wa sasa akili yao tofauti na utoto wa kipindi cha nyuma ila hanielewagi,
Siku hizi shule ni kujua kiingereza na sio kuwa na maarifa,nina mfano hai wa wanafunzi wa st.patrick kiboriloni (moshi)
Ile shule si kayumba ila wanafunzi wake wanachojua kidogo ni lugha tu ila akili ni 0,
Mtoto wa ndugu yangu amesoma pale yani kichwa ni cheupe ,kaambulia tu kujua kiingereza basi

Shule za serikali ni nzuri na ziboreshwe,mazingira ya waalimu yaboreshwe

Umeongelea swala la jf,
Mtu akiomba ushauri zinafuata dharau,kejeli na matusi
Na mtu wa aina hii hakuelewa kilishoandikwa na mtoa mada(sijui nini kifanyike angalau tukikosa elimu nzuri bas uelewa na uwezo wa kusikia,kuona na kujibu hoja uwe mzuri.
 
Mie nimeshangaa sana nimetembelea na bint wa shemeji yangu kamaliza form four mwaka jana kitu anajua ni kupika chai na uji tu ila kuna siku katupikia maharage hakuna mtu alikuwa ilibidi tukanunue chips nikawa najiuliza bint kama huyu hajui kupika , kupika pasi vizuri hajui nikawa najiuliza sie enzi zetu darasa la tatu tena mtoto wa kiume unajua kupika karibu kila kitu kasoro pilau tu,unajua kupiga pasi unajua kufua na kazi nyingine kama kupiga deki na vitu vingi kupitia Somo la Sayansi Kimu ila sasa unaweza kukutata Binti wa form four anatoa harufu yaani hata kujisafisha tu mwenyewe hawezi.
 
Naitetea serikali na wabunge unaowanyooshea kidole,hicho unachopigania wawe na daftari tatu ndicho kilichopo mashuleni toka 2014 tulipobadili mtaala.
Tuna Somo la kusoma,kuandika na kuhesabu.
Pia tuna Afya na Mazingira na Sanaa(haya masomo yanafundishwa kwa vitendo).
Kwa siku wanasoma masomo matatu tu na daftari tatu tu.
USHAURI;Beba hayo madaftari nane nenda kwa mwalimu mkuu atamwita mwalimu wa darasa akupe maelezo ya kutosha
Hicho nilichoongea sio masihara kama ulivyolichukulia wewe. Tulijaribu kwenda kwa waalimu tulikuwa watu watatu wenye watoto hapo. Ni hizi shule English medium za serikali. Tulichojibiwa hapa shuleni kwanza tuna watoto wengi. Kama huridhiki na kinachoendelea hapa,tutashukuru ukimchukulia uhamisho. Tena tulijibiwa na mkuu wa shule. Mkuu mwenyewe anapenda rushwa hatari. Hizi shule English medium za serikali
 
Acha kabisa mimi mwanangu yupo la nne masomo kumi madaftari wanatumia makaunta tena kwaya mbili yan ule mzigo wa begi anaobeba ni huruma tupu bado ujachanganya darasan wanaingia saa kumi na mbili asubuhi na kutoka saa kumi na mbili jioni
Umeona?. Halafu kuna mtu anabisha huku chini eti nenda kwa mwalimu mkuu na daftari 3. Wanakuambia mhamishe mtoto wako sisi tumepewa mitaala ya namna hiyo. Lazima kuwe na mjadala mpana kuhusu hili tunaweza kuanzia humu
 
Umeona?. Halafu kuna mtu anabisha huku chini eti nenda kwa mwalimu mkuu na daftari 3. Wanakuambia mhamishe mtoto wako sisi tumepewa mitaala ya namna hiyo. Lazima kuwe na mjadala mpana kuhusu hili tunaweza kuanzia humu
Kabla ya mijadala naona wazazi wakipata athari kwa watoto wao ndio wanaweza elewa hivi hivi zinakua kelele tu. Niliwahi kuhoji swala la mtoto kua darasa na saa kumi na mbili kamili na kutoka saa kumi na mbili kamili hapi ujaweka muda wa kumuamsha mtoto na kumuandaa na mda wa kufika nyumbani yani mtoto yupo busy zaidi ya muajiriwa wazazi wengine wakajibu wao wapo tayari hata watoto wakiambiwa na Jumapili waende sasa sielewi ni hawana huruma na watoto au watoto ni ghasia kwao wakiwa nyumbani. Hivyo kwa fahari tuonayo mtaani nasomesha mtoto english medium huku akishushwa home na gari na mbegi mkubwa naonekana kueka fahari mtaani kumbe mtoto anateseka.
 
Wazazi wanakimbia malezi mapema sana kwa kigezo cha kutafuta hela..

Mtoto akili atazitoa wapi
 
Kipindi cha nyuma Elimu haikuwa bora kipindi hiko ila sisi ndio tulikuwa bora kwani hatukuwa tumechanjwa chanjo yoyote na uwezo wetu wa kufikiria ulikuwa mkubwa kuliko kizazi hiki cha chanjo. Wana IQ ndogo sana. Angalia tu hata humu JF ya 2000's na uilinganishe na ya sasa ya 2020"s utaona wanaongelea na kutukanana kuhusu kutoana marinda tu. Mungu awasaidie kwa kweli.
Nani anasimamia elimu yetu? Unaweza kujianzishia shule yako ukaamua masomo gani uongeze nje ya yale ya msingi yanayotambuliwa.
 
Kabla ya mijadala naona wazazi wakipata athari kwa watoto wao ndo wanaweza elewa hivi hivi zinakua kelele tu. Niliwahi kuhoji swala la mtoto kua darasana saa kumi na mbili kamili na kutoka saa kumi na mbili kamili hapi ujaweka muda wa kumuamsha mtoto na kumuandaa na mda wa kufika nyumbani yani mtoto yupo busy zaidi ya muajiriwa wazazi wengine wakajibu wao wapo tayari hata watoto wakiambiwa na jumapili waende sasa sielewi ni hawana huruma na watoto au watoto ni ghasia kwao wakiwa nyumbani. Hivyo kwa fahari tuonayo mtaani nasomesha mtoto english medium huku akishushwa home na gari na mbegi mkubwa naonekana kueka fahari mtaani kumbe mtoto anateseka.
Duuh...! Yaani mimi hili swala linanichanganya kwa kweli. Watoto wameingizwa utumwani kabisa
 
Back
Top Bottom