Shule kongwe kuchemka matokeo kidato cha 6 ni matokeo ya wakuu Shule kusimamia maslahi ya mamlaka za uteuzi badala ya taaluma

Tozo

Member
Aug 23, 2021
76
154
Unaweza usiamini ukiangalia shule zetu kongwe zinavyoburuzwa na sekondari za kata zenye miundombinu isiyo rafiki kwa wanafunzi, hazina chakula cha mchana, watoto wanatembea umbali mrefu hata ruzuku inayotolewa kwa shule hizi haitoshi.

Ukilinganisha na shule kongwe nchini ukiacha zile za vipaji. Pugu sekondari ni ya 44 kati 44 mkoa wa Dar es salaam na ya 627 kati ya 644 kitaifa, Jangwani ni ya 608, Bwiru boys 595, Ifakala girls 555, Korongwe Girls 540, Tambaza 556, Kisutu 520, Tanga Tech 503, Morogoro Sec. 468, Loleza 492, Iyunga 570, Ifunda Tech 522, Dodoma Sec 443, Minaki 445, Bukoba 512.

Karibu shule zote kongwe hata zile ambazo sijaorodhesha zimeshindwa kuzidi hata nusu ya Shule zote 644 zilizofanya mithani hii.

Serikali imezifanyaia ukarabati wa mamilioni ya pesa na bado inapeleka ruzuku kubwa sana kwa shule hizi pamoja na kuzipangia wanafunzi wenye ufaulu mzuri kidato cha 4 ukilinganisha na shule za kata ambazo zimeanza kupangiwa wanafunzi wa kidato cha 5.

Ukiangalia shule hizi zimeendelea kuwa na matokeo mabovu kwa miaka mingi mfululizo na wasimamzi wake yaani wakuu wa Shule hizi wakiwa walewale wanaorudisha mgao wa ruzuku kwa mamraka za uteuzi (mabosi wa Tamisemi).

Hatua ifike sasa shule hizi zipangiwe mwisho wa nafasi kwenye mithani hii.

Kwa mfano kwa kuwawekewa mwisho wa nafasi ya ufaulu na wakuu wa Shule wasipopata nafasi hizo basi wakuu hao wanyanganye madaraka.

Kwa mfano shule Kongwe itakayoshika nafasi ya zaidi 200 kati ya 644 basi Mkuu avuliwe madaraka, hii itasaidia wakuu wa Shule kushirikiana vizuri na walimu kusimamia taaluma.
 
Kwa mfano kwa kuwawekewa mwisho wa nafasi ya ufaulu na wakuu wa Shule wasipopata nafasi hizo basi wakuu hao wanyanganye madaraka.
Itasababisha wizi wa mitihani, rushwa na uzandiki kuibuka.

Matokeo mabovu ni mkusanyiko wa Mambo mengi sana. Siyo uongozi wa shule peke yake
 
Wakuu wa Shule kongwe wanapesa kuliko maafisa Elimu wao wa wilaya. Bajeti ya Shule ni kubwa kuliko ya Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri. Na wanaogopwa na maafisa Elimu kwani wao wanamtandao mpaka Tamisemi. Shule kongwe hufadhiri uendeshaji wa ofisi za maafisa Elimu kwa stationaries, pesa ya mafuta ya gari na vitafunwa na vinywaji vya vikao. Mkuu wa Shule akitaka kukomolewa hupewa uafisa elimu taaluma wilaya.
 
Sikubaliani na wazo la kuzipangia nafasi kitaifa. Badala yake wapangiwe % ya Div. I, II, III, IV, na 0.
 
Wakuu wa Shule kongwe wanapesa kuliko maafisa Elimu wao wa wilaya. Bajeti ya Shule ni kubwa kuliko ya Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri. Na wanaogopwa na maafisa Elimu kwani wao wanamtandao mpaka Tamisemi. Shule kongwe hufadhiri uendeshaji wa ofisi za maafisa Elimu kwa stationaries, pesa ya mafuta ya gari na vitafunwa na vinywaji vya vikao. Mkuu wa Shule akitaka kukomolewa hupewa uafisa elimu taaluma wilaya.
Niliwahi kukutana Morogoro na Headmaster wa zamani wa Kwiro sec na baadae Tabora Boys nadhani. Kaunda suti ilikuwa imepauka na ngozi yake imesinyaa nikamuuliza uko wapi siku hizi akaniambia ni afisa Elimu taaluma Manispaa Fulani. Mwanzo I nilidhani amepata maradhi kumbe njaa.
 
Unaweza usiamini ukiangalia shule zetu kongwe zinavyoburuzwa na sekondari za kata zenye miundombinu isiyo rafiki kwa wanafunzi, hazina chakula cha mchana, watoto wanatembea umbali mrefu hata ruzuku inayotolewa kwa shule hizi haitoshi.

Ukilinganisha na shule kongwe nchini ukiacha zile za vipaji. Pugu sekondari ni ya 44 kati 44 mkoa wa Dar es salaam na ya 627 kati ya 644 kitaifa, Jangwani ni ya 608, Bwiru boys 595, Ifakala girls 555, Korongwe Girls 540, Tambaza 556, Kisutu 520, Tanga Tech 503, Morogoro Sec. 468, Loleza 492, Iyunga 570, Ifunda Tech 522, Dodoma Sec 443, Minaki 445, Bukoba 512.

Karibu shule zote kongwe hata zile ambazo sijaorodhesha zimeshindwa kuzidi hata nusu ya Shule zote 644 zilizofanya mithani hii.

Serikali imezifanyaia ukarabati wa mamilioni ya pesa na bado inapeleka ruzuku kubwa sana kwa shule hizi pamoja na kuzipangia wanafunzi wenye ufaulu mzuri kidato cha 4 ukilinganisha na shule za kata ambazo zimeanza kupangiwa wanafunzi wa kidato cha 5.

Ukiangalia shule hizi zimeendelea kuwa na matokeo mabovu kwa miaka mingi mfululizo na wasimamzi wake yaani wakuu wa Shule hizi wakiwa walewale wanaorudisha mgao wa ruzuku kwa mamraka za uteuzi (mabosi wa Tamisemi).

Hatua ifike sasa shule hizi zipangiwe mwisho wa nafasi kwenye mithani hii.

Kwa mfano kwa kuwawekewa mwisho wa nafasi ya ufaulu na wakuu wa Shule wasipopata nafasi hizo basi wakuu hao wanyanganye madaraka.

Kwa mfano shule Kongwe itakayoshika nafasi ya zaidi 200 kati ya 644 basi Mkuu avuliwe madaraka, hii itasaidia wakuu wa Shule kushirikiana vizuri na walimu kusimamia taaluma.
kwa dar, usafiri ni changamoto sana. Ndiyo sababu wazazi wengi wa dar wenye vipato na wanaoamua kujinyima watoto wao wakipangiwa shule za hapa hawawapeleki watoto wao. Shule binafsi za mkoa wa pwani zinazong'ara watoto wanaosoma huko si wakazi wa pwani ni wakazi wa dar
 
Unaweza usiamini ukiangalia shule zetu kongwe zinavyoburuzwa na sekondari za kata zenye miundombinu isiyo rafiki kwa wanafunzi, hazina chakula cha mchana, watoto wanatembea umbali mrefu hata ruzuku inayotolewa kwa shule hizi haitoshi.

Ukilinganisha na shule kongwe nchini ukiacha zile za vipaji. Pugu sekondari ni ya 44 kati 44 mkoa wa Dar es salaam na ya 627 kati ya 644 kitaifa, Jangwani ni ya 608, Bwiru boys 595, Ifakala girls 555, Korongwe Girls 540, Tambaza 556, Kisutu 520, Tanga Tech 503, Morogoro Sec. 468, Loleza 492, Iyunga 570, Ifunda Tech 522, Dodoma Sec 443, Minaki 445, Bukoba 512.

Karibu shule zote kongwe hata zile ambazo sijaorodhesha zimeshindwa kuzidi hata nusu ya Shule zote 644 zilizofanya mithani hii.

Serikali imezifanyaia ukarabati wa mamilioni ya pesa na bado inapeleka ruzuku kubwa sana kwa shule hizi pamoja na kuzipangia wanafunzi wenye ufaulu mzuri kidato cha 4 ukilinganisha na shule za kata ambazo zimeanza kupangiwa wanafunzi wa kidato cha 5.

Ukiangalia shule hizi zimeendelea kuwa na matokeo mabovu kwa miaka mingi mfululizo na wasimamzi wake yaani wakuu wa Shule hizi wakiwa walewale wanaorudisha mgao wa ruzuku kwa mamraka za uteuzi (mabosi wa Tamisemi).

Hatua ifike sasa shule hizi zipangiwe mwisho wa nafasi kwenye mithani hii.

Kwa mfano kwa kuwawekewa mwisho wa nafasi ya ufaulu na wakuu wa Shule wasipopata nafasi hizo basi wakuu hao wanyanganye madaraka.

Kwa mfano shule Kongwe itakayoshika nafasi ya zaidi 200 kati ya 644 basi Mkuu avuliwe madaraka, hii itasaidia wakuu wa Shule kushirikiana vizuri na walimu kusimamia taaluma.
Huu ni ujinga unataka kuanziasha ndiyo utakua mwanzo wa kuiba mitihan
Na kutoa rushwa
Huu ushetan ukemewe haswa
Acha watu wapambane wote ni watanzania kama ni kilaza atajua mwenyewe
 
Kipindi cha mwenda kuzimu hata Chato ilikuwa ina toa wanafunzi bora.
Hii nchi ni ya ajabu sana. Siasa hata kwenye elimu?? Are we serious??
 
Kama hivyo basi kuna idadi kubwa ya wanafunzi magenius .

Ila kumbuka kwa A-level shule kuwa nafasi za chini haimaanishi wanafunzi wamefeli bali nafasi ya ufaulu kitaifa inategemea na idadi ya wanafunzi mfano Tambaza hapo inawanafunzi wengi sana lakini hawana zero hata moja na div 4 chache sana.
 
Kama hivyo basi kuna idadi kubwa ya wanafunzi magenius .

Ila kumbuka kwa A-level shule kuwa nafasi za chini haimaanishi wanafunzi wamefeli bali nafasi ya ufaulu kitaifa inategemea na idadi ya wanafunzi mfano Tambaza hapo inawanafunzi wengi sana lakini hawana zero hata moja na div 4 chache sana.
Tambaza hata comb za arts zimeshindwa kuwabeba wamezidiwa na Kilangalanga sec. ya Mlandizi miundo mbinu mibovu, madarasa kama vibanda vya kufugia kuku Kipunguni Ukonga combination zao PCB na PCM tu lakini hawana Div 4. Wanafunzi wengi kama Tambaza tu nafasi 306 kati 644. Wengi wa wanafunzi ndiyo iwe wa 600 huko?
 
kwa dar, usafiri ni changamoto sana. Ndiyo sababu wazazi wengi wa dar wenye vipato na wanaoamua kujinyima watoto wao wakipangiwa shule za hapa hawawapeleki watoto wao. Shule binafsi za mkoa wa pwani zinazong'ara watoto wanaosoma huko si wakazi wa pwani ni wakazi wa dar
Inacurrate research.
 
Afisa elimu taaluma wa wilaya,anakua na njaa?
Labda hajui namna ya kula.
Niliwahi kukutana Morogoro na Headmaster wa zamani wa Kwiro sec na baadae Tabora Boys nadhani. Kaunda suti ilikuwa imepauka na ngozi yake imesinyaa nikamuuliza uko wapi siku hizi akaniambia ni afisa Elimu taaluma Manispaa Fulani. Mwanzo I nilidhani amepata maradhi kumbe njaa.
 
Back
Top Bottom